Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 397
- 993
Mbunge Abdulhafar Juma akichangia kwenye miswada ya sheria uchaguzi ametoa pendekezo la kuongeza kipengele cha kutoa elimu namna ya kupokea matokeo.
Akisema, "Kushindwa kwa baadhi ya viongozi katika uchaguzi ndio kunaleta kitahalani katika taifa. Kumbe labda tu kwasababu hawana elimu.
"Nadhani kiwekwe kabisa kipengele katika mswada huu, moja ya majukumu ya tume ni kuwafunza wanasiasa kupokea matokeo. Wakishindwa wajue huyu ameshindwa.
"Mimi Chama changu Cha Mapinduzi ni wazoefu wakubwa wa kupokea matokeo ya kushinda na kushindwa. Nadhani sisi ndani ya chama chetu tumefundishwa sana, pale tunaposhindwa tunahimili, tunasubiri miaka mitano tunaendelea.
"Nina wasiwasi na vyama vingine vya upinzani kama kwao wanapeana elimu ya kupokea matokeo ya uchaguzi, Sasa nataka nione tume ya uchaguzi ina wajibu wa kisheria wa kuwafundisha kuwa ukishindwa kubali, tulia, unga mkono tujenge taifa letu."
Akisema, "Kushindwa kwa baadhi ya viongozi katika uchaguzi ndio kunaleta kitahalani katika taifa. Kumbe labda tu kwasababu hawana elimu.
"Nadhani kiwekwe kabisa kipengele katika mswada huu, moja ya majukumu ya tume ni kuwafunza wanasiasa kupokea matokeo. Wakishindwa wajue huyu ameshindwa.
"Mimi Chama changu Cha Mapinduzi ni wazoefu wakubwa wa kupokea matokeo ya kushinda na kushindwa. Nadhani sisi ndani ya chama chetu tumefundishwa sana, pale tunaposhindwa tunahimili, tunasubiri miaka mitano tunaendelea.
"Nina wasiwasi na vyama vingine vya upinzani kama kwao wanapeana elimu ya kupokea matokeo ya uchaguzi, Sasa nataka nione tume ya uchaguzi ina wajibu wa kisheria wa kuwafundisha kuwa ukishindwa kubali, tulia, unga mkono tujenge taifa letu."