Dr. Tslaa alijibu vizuri juu ya tuhuma hizi. Alisema kwamba, kama hali aliyosema Mukama ni kweli, basi huo ni udhaifu wa kiulinzi na usalama wa serikali iliyo chini ya CCM; kwani imeonyesha CHADEMA wana mbinu bora zaidi za kiusalama ambazo zimewafanya waweze kupenyeza makomandoo wao hadi Igunga bila vyombo vya usalama vilivyo chini ya utawala wa CCM kugundua. Ama kweli Tslaa ni mwanafilosofia; kwa majibu hayo sidhani kama Mukama na wanaCCM wengine wameweza kumuelewa.Kama Mkama anakiamini hicho alichokisema, sasa aonyeshe mfano! Amshinikize waziri wa Mambo ya ndani ajiuzuru mara moja kwa kuruhusu makomandoo hao kuingia nchini kinyume cha sheria! Kisha na yeye ajiuzuru kwa kuwa chama chake kinaongoza serikali isiyowajibika. Chadema ungeni mkono hoja ya Mkama mara moja! ... kwamba ni kweli kuna makomandoo na kisha ashinikizwe kujiuzuru!
hivi mzee anaechukua wake wa ndoa wa watu na kauli zilizotolewa ni yupi anaonekana kichaa na hana hekima na busara!
isue hapo ni ushahidi na si ushabiki yasije yakawa ya madawa yakulevya ya viongozi wa dini na jakaya then baada ya ushahidi wakaloa