Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Kwa masikitiko makubwa naomba niseme kuwa Yusuf Makamba alikuwa bora kuliko huyu Mukama. Mambo aliyoongea Mukama ni aibu tupu kwa CCM, Ikulu na Waziri Membe.
Mukama anasema makomando walipata mafunzo Libya 1990. Sijui kama anaugua ugonjwa wa kusahau lakini labda tumkumbushe huyu mzee kuwa vyama vingi vya siasa vilianza baada ya 1990 na hivyo kama kuna mafunzo ya makomando yaliyofanyika 1990 basi yatakuwa ya CCM maana kipindi hicho nchi ilikuwa chini ya chama kimoja (ccm). Na ufahamu wangu hadi 1990 uhusiano wa Tanzania na Libya haukuwa mzuri kihivyo. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere bado alikuwa hai na asingeruhusu mahusiano ya karibu na Libya nchi iliyotupiga mabomu wakati wa vita ya Uganda. Mukama hajatulia!
Pili, madai kwamba CHADEMA wanaleta makomando toka nje ya nchi kama ni kweli basi CCM hawana sifa hata chembe ya kuongoza nchi hii tena. Nasema hivyo kwa sababu kwa serikali ya ccm kukaa kimya huku ikiwa na taarifa ya kuingia nchini watu wanaotishia usalama wa raia wake (Igunga na pengine popote nchini) ni usaliti wa hali ya juu. Na swali ambalo Mukama na serikali ya ccm wanatakiwa kujibu ni hili, usalama wetu sisi raia ukoje? Tayari tumeshakumbwa na milipuko ya mabomu, na pia ndege za kivita toka nchi nyingine (Qartar) zimekuwa zinatuwa kwenye viwanja vyetu vya ndege na kuchukuwa wanyama kupeleka kwao na serikali hii ya wakina Mukama ikikaa kimya! How safe are we under ccm government?
Juzi Mukama huyu huyu alitembelea nyumba wanayodai imechomwa moto na wafuasi wa CHADEMA huko Igunga. Kwa mshango nyumba imeungua isipokuwa karatasi linataja jina la CHADEMA! Narudia, nyumba imengua lakini karatasi yenye maneno 'CHADEMA si wanajidai wajanja' haikuungua. Pengine wanasayansi wanaweza kutuasaidia hapa kwamba inakuwaje karatasi hii haikuungua? Haya ndio mambo ya kitoto na ni fedheha kwa watanzania kuwa na viongozi wenye uwezo mdogo wa kufikiri kama huyu Mukama.
Mwisho, badala ya Mukama kuhuburi hizi siasa za mwaka 1947 ni vizuri atoe maelezo kwa nini tunafanya uchaguzi Igunga leo hii? Kwa nini Rostam Aziz aliachia nafasi yake ya ubunge kwa madai ya kuchoshwa na siasa uchwara? Na je Mukama kama mtendaji mkuu wa ccm ana mkakati gani wa kuiepeusha CCM na siasa uchwara? Hii mipasho ya mafunzo ya makomando amwachie Hadija Kopa na Kapteni Komba. Mukama asitupotezee air-time tena.
You can simply call mukama the hopless ccm secretary general.