Mbowe kuunda baraza la Chadema pekee

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,488
14,355
Send to a friend Thursday, 10 February 2011 21:23

KIONGOZI wa upinzani Bungeni, Freeman Mbowe amesema ataunda baraza za Mawaziri kivuli
litakalojumuisha wabunge wa Chadema pekee.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi ofisini kwake jana, Mbowe alisema atatangaza baraza hilo wiki ijayo huku akifafanua kuwa itakuwa unafiki kwake kuunda baraza kivuli la mseto katika kipindi ambapo kuna kejeli na matusi miongoni mwa vyama vya
upinzani.

"Majeraha yote haya ni mengi, yanahitaji muda kupona, katika hatua ya sasa nitaunda Baraza la Mawaziri Kivuli
ambalo litakuwa la Chadema pekee," alisema Mbowe.

Alifafanua kuwa muda huo aliosema ni wa kutibu majeraha, ni fursa ya kuona maendeleo ya vyama vingine tofauti na Chadema katika utendaji ili kutibu na kuondoa tofauti baina yao.

Hata hivyo alisema kama ilivyo Bunge hudumu miaka mitano na Baraza la Mawaziri Kivuli pia hudumu miaka
mitano hivyo linaweza kubadilika.

"Ni matumaini yangu tutatibu majeraha yetu, kupata amani na kuwaingiza wenzetu katika Baraza la Mawaziri Kivuli.
Tupende, tusipende tuna mawasiliano ya kibunge, pengine tutagundua tuna makosa au wenzetu watagundua wao
walikosea, msimamo wetu ni ule ule kwa kanuni ile iliyobadilishwa, lakini sifungi uwezekano wa kuunda baraza
la mawaziri shirikishi," alisema Mbowe.

Mbowe ambaye ni mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro alisema kuwa anaamini busara zitarejea kwa vyama vya
upinzani na matendo yataashiria utulivu utakaowawezesha kurekebisha tofauti zao.

Akizungumzia kuchelewa kuunda baraza hilo kivuli, Mbowe alisema ni kutokana na sintofahamu utaratibu utakaotumika
kuunda baraza hilo, kutokuwepo kwa kamati za kibunge za kisekta na kwamba yupo katika hatua za mwisho kukamilisha hilo kabla ya kulitangaza wiki ijayo.

Katika hatua nyingine Mbowe alisema Chadema inaheshimu na itawapa ushirikiano wabunge wa upinzani
waliochaguliwa kuwa wenyeviti wa kamati za Bunge.

"Kuna mambo matatu yaliyopo nataka niweke wazi, kanuni tayari, chaguzi za kamati tayari, binafsi naheshimu wabunge
wenzangu, wote wana uwezo mzuri. Naheshimu waliochaguliwa uenyeviti wa kamati walio upande wa CCM
hata upinzani, Chadema tutawapa ushirikiano kipekee walio
nje ya CCM," alisema Mbowe na kuongeza:

"Tutawasaidia kwa kila linalowezekana, pamoja na kuwa tulitofautiana na bado tunatofautiana kuhusu kanuni, wana
jukumu kubwa kwa Watanzania, tutwasaidia, Cheyo, Mrema na Zitto waweze kufanya kazi kwa ufanisi."

Alisema kimsingi Zitto, Cheyo na Mrema wanatakiwa kuwa polisi kwa CCM na serikali, lakini bahati mbaya wapinzani
wamewapa CCM fursa ya kutekeleza mkakati wa kuwagawa na kuwatawala na wamefanikiwa azma hiyo.

Awali Mbowe alieleza kuwa tangu kampeni hata baada ya uchaguzi kumekuwa na hali ya sitofahamu baina ya vyama vya upinzani hali iliyoutikisa upinzani.

Alisema hali hiyo ya wapinzani kutetereka, imeipa CCM nguvu ya kuwa 'broker' (dalali) wa kuwachagulia namna ya kufanya mambo yao.

"Katika mtiririko huo, tumeifanya CCM broker, broker anapokuwa adui yenu atawapa mkakati wa kuwekana sawa
ili mumkosoe?," alihoji.


Source: Mwananchi
 
Send to a friend Thursday, 10 February 2011 21:23

KIONGOZI wa upinzani Bungeni, Freeman Mbowe amesema ataunda baraza za Mawaziri kivuli
litakalojumuisha wabunge wa Chadema pekee.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Mwananchi ofisini kwake jana, Mbowe alisema atatangaza baraza hilo wiki ijayo huku akifafanua kuwa itakuwa unafiki kwake kuunda baraza kivuli la mseto katika kipindi ambapo kuna kejeli na matusi miongoni mwa vyama vya
upinzani.

"Majeraha yote haya ni mengi, yanahitaji muda kupona, katika hatua ya sasa nitaunda Baraza la Mawaziri Kivuli
ambalo litakuwa la Chadema pekee," alisema Mbowe.

Alifafanua kuwa muda huo aliosema ni wa kutibu majeraha, ni fursa ya kuona maendeleo ya vyama vingine tofauti na Chadema katika utendaji ili kutibu na kuondoa tofauti baina yao.

Hata hivyo alisema kama ilivyo Bunge hudumu miaka mitano na Baraza la Mawaziri Kivuli pia hudumu miaka
mitano hivyo linaweza kubadilika.

"Ni matumaini yangu tutatibu majeraha yetu, kupata amani na kuwaingiza wenzetu katika Baraza la Mawaziri Kivuli.
Tupende, tusipende tuna mawasiliano ya kibunge, pengine tutagundua tuna makosa au wenzetu watagundua wao
walikosea, msimamo wetu ni ule ule kwa kanuni ile iliyobadilishwa, lakini sifungi uwezekano wa kuunda baraza
la mawaziri shirikishi," alisema Mbowe.

Mbowe ambaye ni mbunge wa Hai mkoani Kilimanjaro alisema kuwa anaamini busara zitarejea kwa vyama vya
upinzani na matendo yataashiria utulivu utakaowawezesha kurekebisha tofauti zao.

Akizungumzia kuchelewa kuunda baraza hilo kivuli, Mbowe alisema ni kutokana na sintofahamu utaratibu utakaotumika
kuunda baraza hilo, kutokuwepo kwa kamati za kibunge za kisekta na kwamba yupo katika hatua za mwisho kukamilisha hilo kabla ya kulitangaza wiki ijayo.

Katika hatua nyingine Mbowe alisema Chadema inaheshimu na itawapa ushirikiano wabunge wa upinzani
waliochaguliwa kuwa wenyeviti wa kamati za Bunge.

"Kuna mambo matatu yaliyopo nataka niweke wazi, kanuni tayari, chaguzi za kamati tayari, binafsi naheshimu wabunge
wenzangu, wote wana uwezo mzuri. Naheshimu waliochaguliwa uenyeviti wa kamati walio upande wa CCM
hata upinzani, Chadema tutawapa ushirikiano kipekee walio
nje ya CCM," alisema Mbowe na kuongeza:

"Tutawasaidia kwa kila linalowezekana, pamoja na kuwa tulitofautiana na bado tunatofautiana kuhusu kanuni, wana
jukumu kubwa kwa Watanzania, tutwasaidia, Cheyo, Mrema na Zitto waweze kufanya kazi kwa ufanisi."

Alisema kimsingi Zitto, Cheyo na Mrema wanatakiwa kuwa polisi kwa CCM na serikali, lakini bahati mbaya wapinzani
wamewapa CCM fursa ya kutekeleza mkakati wa kuwagawa na kuwatawala na wamefanikiwa azma hiyo.

Awali Mbowe alieleza kuwa tangu kampeni hata baada ya uchaguzi kumekuwa na hali ya sitofahamu baina ya vyama vya upinzani hali iliyoutikisa upinzani.

Alisema hali hiyo ya wapinzani kutetereka, imeipa CCM nguvu ya kuwa 'broker' (dalali) wa kuwachagulia namna ya kufanya mambo yao.

"Katika mtiririko huo, tumeifanya CCM broker, broker anapokuwa adui yenu atawapa mkakati wa kuwekana sawa
ili mumkosoe?," alihoji.


Source: Mwananchi

Hamadi Rashidi na Kafulila watakua polisi wanani? maana pamoja na kupiga debe ili wapate japo kamati moja hawajafanikiwa, CUF na NCCR hakuna chama kilichopata kamati dah! hii ni noma sijui yule mama Makinda alishawajua hawa jamaa ni wanafiki.... namshauri Mbowe awakaange asiwape kabisa uwaziri kivuli
 
The current power struggle within the opposition camp does not augur well with our nascent multi-party democracy
 
Our multi party democracy is not even nascent. It is actually a single "state" party system with a few opposition parties allowed to appease donors and other foreign powers. True democracy stems from the regulatory framework in place (i.e. constitution and laws governing politics). Am afraid the single "state" party system in Tanzania is entrenched in our legal framework. Unless we change it there won't be true democracy in Tanzania.
 
Back
Top Bottom