Slave
JF-Expert Member
- Dec 6, 2010
- 5,314
- 2,635
Ndg zangu wapendwa kumekuwepo na malalamiko mengi sana kuhusiana na wizi katika zap account na m-pesa. Katika utafiti wangu usio rasmi nimegundua kwamba kuna makosa yanayo fanywa na wamiliki kwakuto kuwa makini katika utunzaji wa namba zao za siri hivyo kuwarahisishia hao wezi kuiba pesa. Kuna mbinu nyingi wanazo zitumia hawa wezi hapa nitataja baadhi. 1.ni ile ya mtu kuomba simu yako aione. hapo mwizi hupata muda wa kusoma msg hasa zile za m pesa hapo hujua moja kwa moja kama unapesa hau hauna. akijua unazo anaanza kuleta vijimidala vya kuhusu vitamburisho, kwa kutumia hila zake anaweza akakumbia jambo ambalo linaweza kukulazimisha utoe kitambulisho chako, mfano anaweza akakuambia,yaani sura yako inaonyesha wewe unamiaka 80.na kwa kuwa wewe najua hauna hiyo miaka unaweza ukabisha na mwisho kabisa unaweza uka mdhibitishia kwa kumuonesha kitamburisho chako.hilo ni kosa kubwa sana kwani atakariri mwaka wako wa kuzaliwa,namba ya kitamburisho,na mahala pa kuzaliwa.siku hiyo anaweza akakuacha akakuvizia siku ingine ambapo anaweza akakuomba umuazime tena simu ili akuibie sasa. 2.njia ingine ni mtu kufanya kukuazima simu,kisha anabeep kwenye namba yake ikiwa lengo ni kuipata namba yako ya simu.kisha kukufanyia hla za kupata kitamburisho chako na baada ya mwizi humpigia mwizi mwenzie wa mbali kabisa na kumtajia namba ya line na za kitamburisho ili ai swap huko huko mikoani.na kisha kutoa pesa zako zote.hapo ukiwapigia simu voda wanaweza wakakushangaza mno.pale utakapowaambia wewe umeibiwa ili hali inaonyesha japo wewe upo dar ila pesa zako kuna mtu kachukua akiwa bukoba. NITARUDI ...