Mbeya: Mwandishi wa Habari afariki baada ya kujifungua

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
388a6093-ae51-4392-9544-e5d24119d375.jpg

Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya (MBPC) kimepata pigo baada ya kuondokewa na mwanachama wake wa muda mrefu, Hannerole Mrosso aliyefariki baada ya kujifungua katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kitengo cha Wazazi Meta Jijini Mbeya tarehe Mei 13, 2022.

Akitoa taarifa mume wa marehemu, Baraka Kasubiri ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii amesema mkewe alifanyiwa upasuaji na kujifungua mtoto wa kike na muda mfupi baada ya kujifungua alipoteza maisha akimuacha mtoto ambaye anaendelea vizuri.

Taratibu za mazishi zinafanywa eneo la Sokomatola Jijini Mbeya ambapo mwili umesafirishwa kwenda Namtumbo Mkoani Ruvuma kwa maziko yanayotarajiwa kufanyika tarehe leo Mei 15, 2022.

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya, Joseph Mwaisango amesema marehemu alikuwa ni mwanachama ambaye alikuwa na mchango mkubwa kwa tasnia ya habari pia alikuwa na ushirikiano na kila mtu.

Naye, Mwenyekiti wa Jukwaa la Uchumi kwa Wanahabari (MJEF), Kakuru Msimu amesema msiba huu umewaumiza hasa pale ambapo wanapompoteza mwenzao ambaye walitegemea kujikwamua kiuchumi.

Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi Wanahabari Wanawake, Esther Macha amesema wamepata pigo kwani wamempoteza mwanachama wao ambaye alikuwa na mchango mkubwa tangu kuanzishwa chama chao.

Sambo amesema marehemu ambaye pia alikuwa mwanachama chama cha kusaidiana wanahabari (Amani) amefariki wakati chama chao kikiwa kichanga na marehemu alikuwa mshiriki mwaminifu.

"Ni vigumu kuamini kuwa Hannerole ametuacha kwani upole wake na ucheshi wake ulikuwa ni faraja katika kikundi," amesema Martha.

Naye mwandishi mwandamizi Felix Mwakyembe amesema tasnia imeondokewa na mwandishi ambaye alipenda kujifunza na kujiendeleza kielimu ambapo hadi umauti alikuwa akisoma Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji(TEKU) Mbeya.

Mmoja wa wanafunzi wa TEKU, Shaban Nassoro Kisilwa amesema ndoto za mwenzao zimezimika ghafla kwani walitarajia kuhitimu naye mwaka huu.

Shughuli zote za msiba zinaratibiwa na Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya, Kenneth Mwakandyali ambapo amewataka waandishi kushirikiana katika kumsindikiza mwenzao katika safari yake ya mwisho.

Enzi za uhai wake marehemu amewahi kuhudumu kituo cha Radio cha Generation Fm na Baraka Fm akiwa masomoni.

Marehemu ameacha watoto watatu wawili wakiwa ni mapacha Bwana alitoa Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe.

Chanzo: Mwanahalisi
 
Nimekumbuka pia mwezi uliopita yule mbunge aliejifungua kwa OP nakufariki so Sad
wanawake wengi OP zimekuwa nyingi kuliko njia za kawaida Je shida ni njia ndogo au Ndiyo kuzuia kuongezeka kwa maumbile baada ya kujifungua ??
 
View attachment 2225156
Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya (MBPC) kimepata pigo baada ya kuondokewa na mwanachama wake wa muda mrefu, Hannerole Mrosso aliyefariki baada ya kujifungua katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kitengo cha Wazazi Meta Jijini Mbeya tarehe Mei 13, 2022.

Akitoa taarifa mume wa marehemu, Baraka Kasubiri ambaye ni Afisa Ustawi wa Jamii amesema mkewe alifanyiwa upasuaji na kujifungua mtoto wa kike na muda mfupi baada ya kujifungua alipoteza maisha akimuacha mtoto ambaye anaendelea vizuri.

Taratibu za mazishi zinafanywa eneo la Sokomatola Jijini Mbeya ambapo mwili umesafirishwa kwenda Namtumbo Mkoani Ruvuma kwa maziko yanayotarajiwa kufanyika tarehe leo Mei 15, 2022.

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya, Joseph Mwaisango amesema marehemu alikuwa ni mwanachama ambaye alikuwa na mchango mkubwa kwa tasnia ya habari pia alikuwa na ushirikiano na kila mtu.

Naye, Mwenyekiti wa Jukwaa la Uchumi kwa Wanahabari (MJEF), Kakuru Msimu amesema msiba huu umewaumiza hasa pale ambapo wanapompoteza mwenzao ambaye walitegemea kujikwamua kiuchumi.

Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi Wanahabari Wanawake, Esther Macha amesema wamepata pigo kwani wamempoteza mwanachama wao ambaye alikuwa na mchango mkubwa tangu kuanzishwa chama chao.

Sambo amesema marehemu ambaye pia alikuwa mwanachama chama cha kusaidiana wanahabari (Amani) amefariki wakati chama chao kikiwa kichanga na marehemu alikuwa mshiriki mwaminifu.

"Ni vigumu kuamini kuwa Hannerole ametuacha kwani upole wake na ucheshi wake ulikuwa ni faraja katika kikundi," amesema Martha.

Naye mwandishi mwandamizi Felix Mwakyembe amesema tasnia imeondokewa na mwandishi ambaye alipenda kujifunza na kujiendeleza kielimu ambapo hadi umauti alikuwa akisoma Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji(TEKU) Mbeya.

Mmoja wa wanafunzi wa TEKU, Shaban Nassoro Kisilwa amesema ndoto za mwenzao zimezimika ghafla kwani walitarajia kuhitimu naye mwaka huu.

Shughuli zote za msiba zinaratibiwa na Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya, Kenneth Mwakandyali ambapo amewataka waandishi kushirikiana katika kumsindikiza mwenzao katika safari yake ya mwisho.

Enzi za uhai wake marehemu amewahi kuhudumu kituo cha Radio cha Generation Fm na Baraka Fm akiwa masomoni.

Marehemu ameacha watoto watatu wawili wakiwa ni mapacha Bwana alitoa Bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe.

Chanzo: Mwanahalisi
Poleni sana wafiwa operesheni zimekuwa kaa la moto kwa kina mama wengi wanaojifungua kwa njia hiyo
 
Back
Top Bottom