Mbadala wa matumizi ya "shikamoo" wenye heshima ile ile

Rwaz

JF-Expert Member
May 3, 2013
1,967
3,316
binafsi huwa sipendi kusalimiwa au kusalimia SHIKAMOO. sababu kubwa ni historia ya neno lenyewe kuwa la enzi za utumwa "NIKO CHINI YA MIGUU YAKO" lakin ningependa kumsalimia kwa adabu anayestahili. sasa wataalam wa lugha na maadili mnisaidie mbadala wa matumizi ya neno hilo na maana na adabu ibaki palepale. nilipokuwa Pemba nilifurahia matumizi ya asalaam aleikhum kwa rika zote. lakin kwa huku mikoani ni salaam yenye tafsiri ya dini ya uislam. huwez kuitumia pote ukaeleweka.
 
Habari yako...... kwangu mim ni salam sahihi kwa mtu wa rika lolote
sawa. lakin kwa upana wa lugha ya kiswahili hamna salaam nyingne badala ya neno "shikamoo"? sababu za kutoipenda nimeshazisema. namkumbuka baba yangu alikuwa anatulazimisha kumsalimia kwa kilugha kuliko kutumia shikamoo.
 
Kipi bora utoe salamu ya kitumwa shikamoo au utoe salama ya kawaida ambayo itamjulia hali mtu wa rika lolote lile
Mim sion utafauti kimantiki kati ya asalam aleykum na habari yako... mtamo tu ndugu
 
Mimi sipokeo shikamoo. Ila natoa tu.
kuna mtangazaj wa cloud kipind cha dini mr. Temu aliwai kusema ukitaka mkosane vibaya msalimie shikamoo. nikagundua tuko wengi.sema mr Julius hakunielewa niliposema neno "asalaam aleikhum" niliona zanzibar na ukanda wa pwani unamaliza tatzo la shikamoo lakin kwa wa mikoan weng halikubalik kwa wote hasa kama sio muislam. tupanue kiswahili kwa hili.
 
Kwa iyo, mr lengo ni kutoa salam itakayomridhisha mtu na salam atakayoikubali msalimiwa.? Kama lengo ni mbadala wa shikamoo naamin mibadala ipo
 
wengi hawajui maana ya shikamoo
Shikamoo natoa kwa watu wazima sana
Vijana flani hivi mid age,za sa hizi,za asubuhi,habari yako nk
 
mbadala wa shikamoo ni Heshima yako tatizo haina itikio maalum kila mtu anaitikia kivyake,mimi ukinisalimia kwa kuniambia Heshima yako nakujibu IMEFIKA MAHALA PAKE!!
 
Mie nadhani wewe tuu unavyoona.

Mie nikikutana Na wazazi Na ndugu wa kikristu rika yoyote salamu yetu ni ya kumsifu Bwana wa Mabwana, Mfalme wa wafalme, Mungu Kweli Kwa Mungu Kweli

Tumsifu Yesu Kristo. Milele Amina.

Nikikutana Na mwisilamu namwambia Tumsifu nabii ISA.
MF. Faizafoxy Tumsifu Nabii Isa.
 
Jambo! Jambo bwana!!

Wakati niko jeshini nilimsalimia Afande shikamoo!! Alimind huyoo..akanijibu shikamoo kamsalimie Baba yako nyumbani huku Jeshini salamu yetu ni Jambo afande!!..akaniuliza lwa ukali.. wazi!! Kwa utii nikajibu wazi afaaaaandeee!!!

Mpaka leo najiuliza maantiki ya kusisitizwa salamu ya jambo afaaande!! Kwenye majeshii..bado nascratch...!
 
Kuna huyu mama hapokei shikamoo yangu hapa job cjui anamaana gani, na anatabasam muda wote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom