OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 227
Ndiyo Wakuu , heshima kwenu ! Awali ya yote naomba nianze na nukuu ifuatayo :- " TAIFA LETU,TAIFA LOLOTE NI ZURI NA MAHALI PAZURI PA KUISHI KAMA RAIA WAKE WATALIFANYA LIWE HIVYO .UONGOZI WAKE UNAWEZA KUWA MZURI,MBAYA AU USIOJALI LAKINI KAMA WATU WAKE WAMEAMKA KIELIMU NA WANAJITAMBUA, HAITACHUKUA MUDA MREFU KUWAKILISHA MTAZAMO WA JAMII NA KUBADILI MAWAZO NA MATUMAINI YA TAIFA ." BY MWL NYERERE 1922-1999 . Baada ya nukuu hiyo , naomba turejee kwenye mada yetu. Katika kuelekea hitimisho la kampeini za uchaguzi wa madiwani i.e kesho tarehe 16.6.2013 hapa wilayani Sengerema ,hali si nzuri upande wa ccm. Ikumbukwe kuwa kuna jumla ya kata mbili ambazo ni Nyampulukano na Lugata ambapo madiwani wake walijivua magamba chini ya kamanda Lema na kuamua kujiunga na jeshi la ukombozi cdm . Siku za mwanzo alifika Nape Mnauye ambapo ali ambulia aibu kubwa sana baada ya kuzomewa na umati wa wananchi hapa sengerema wakati akiendeleza siasa zake za maji taka. Baadae pia alifika Ngereja ambaye ni mbunge wa jimbo hili, nae vilevile tangu amefika hapa sengerema amekuwa akizomewa na wapiga kura wake ambapo hali hii imewafanya washindwe kufanya mikutano ya kumunadi mgombea wao. Jana mchana ccm wamekurupushwa maeneo ya uwanja wa ndege wakigawa chumvi na kununua shahada ambapo ktk purukushani hiyo kioo cha gari la cdm kilipasuliwa kwa mawe huku kamanda mmoja cdm akijeruhiwa. Kada wa ccm alikamatwa kwa kusababisha uharibifu huo na hatimae kupelekwa polisi. Kama hiyo haitoshi, usiku wa kuamkia leo makamanda cdm chini ya Mawazo walipata taarifa za kugawa chumvi na kununua shahada maeneo ya Nyamazugo road na Migombani ambapo waliweza kuwakurupusha na kutokomea mbali. Kwa ufupi, hiyo ndo njia sahihi ccm wameamua kutumia ili kuendelea kutawala huku wakivunja ahadi ya 4 ya MwanaTANU inayosomeka "RUSHWA NI ADUI WA HAKI.SITAPOKEA WALA KUTOA RUSHWA." Leo Wenje, Dkt Mbasa na Mawazo watahitimisha wakati Waziri Wasira atahitimisha upande wa ccm . My take :- " SIKU MJINGA AKIJITAMBUA ,MWEREVU YUPO MATATANI ."