Mawakili wa Gwajima wamwandikia Kova barua

Kuna kosa la uhujumu na Pesa chafu pia niweza pelekea kuombwa vitu hivyo KWA ajili ya Usalama wa nchi
 
Ignorance and stupidity at its best level,hivi kweli tutaendelea kwa kua na type ya watu kama wewe?Think outside the box.

Tehee. .tehee...tihii ! Hakuna haja ya box kuwepo, liondoe kabisa ili ufikirie huru. Gwajey kakanyaga mavi lazima aruke ruke tuu.
 
Gwajima asiishi katika material world, material life, aishi kwa vitendo katika spiritual world, spiritual life apambane kiroho kwa maombi sala na toba, aachane na mawakili ni kumkaribisha shetani
Kama kweli yeye ni mteule mtenda miujiza na anayeamini katika roho na kweli, asimame na Mungu sasa na kuonyesha kwa vitendo kile anachohubiri na kukiamini
Aachane na craving katika vitu na pesa, ada za mawakili azipeleke kuwasaidia wahitaji, afunge na kujitenga na ulimwengu wa sheria za mwanadamu ataona miujiza ikitendeka,. Asichanganye Mungu na dunia
 
It is true what you say ndugu yangu...Sorry, This was part of my response to Gefu
 
...yupo sawa hupaswi kuogopa taasisi zilizowekwa kwaajili ya kutenda haki. Kwanini ziogopwe kwani zimekuwa magaidi ? Kimsingi hata rais anapaswa kuheshimiwa na sio kuogopwa...

It is true what you say ndugu yangu, uko sawa na yeye yupo sawa. hata mimi nikiitwa na Polisi huwa naenda tu, nikijua ni mahali pa haki. Nikiambiwa nipeleke document yoyote kama cheti cha kuzaliwa, lesseni ya udereva, hati a nyumba, napeleka tu, maana najua ni mahali pa haki, wala siwezi kutetemeka, kutokwa jasho, au kuzimia kwasababu ya kuhojiwa na Polisi, wala siwezi kutafuta wakili katika hatua za awali za mahojiano. Na HASA kama najijua ni msafi. Kama nitapatikana na hatia ya kutakiwa kufikishwa mahakamani, naweza kutafuta msaada wa wakili . HOPE UNANIELEWA ndugu yangu. sijatofautiana nae, na pia nakubaliana na wewe, najaribu kusema alichosema siku anatukana na wakati anaomba watu wachukue CHA KUREKODIA NA WAMREKODI, MAANA YEYE HAOGOPI POLISI WALA MAHAKAMA WALA BUNGE. That is what he said.
 
Nyaraka alizoatakiwa apeleke ziba uhusiano gani na shutuma za kimsingi?

Apeleke nyaraka kwa kifungu kipi cha sheria?

Nyinyi ndio hata polisi wakikohoa tu mnazimia, mwishowe watawamuru muwape wake zenu ebo!

Mwambie asipekeke maana yeye kidume! Pia asiende akiitwa maana hakuna sheria! Hao wanaozitaka wana maana nazo. Wewe ni mshabiki tu
 
Ukishindana na police wa tanzania utaumia tu hakuna aliewahi kuwashinda,,,,kwa wale wanaokumbuka kesi ya zombe
 
Mwambie asipekeke maana yeye kidume! Pia asiende akiitwa maana hakuna sheria! Hao wanaozitaka wana maana nazo. Wewe ni mshabiki tu

Nilikuwa nasoma pia hayo maswali ya ukali ya Twilumba. Kama mtu ni msafi, tena ni mtumishi wa Mungu, anaogopa nini kupeleka documents ? Jamani,documents tu ? Atoe photocopy, aende na wakili wake pale Polisi, wathibitishe kuwa zile copy zinatokana na zile originals. Polisi watazikagua, Then ataruhusiwa kuondoka na original documents zake. Mbona katika audio moja anasema kuwa ana ushirikiano mzuri sana na Polisi kiasi cha kufadhili baadi ya kazi za Polisi, sasa HAPA KWENYE NYARAKA anarudisha mikono nyuma KUNA NINI ?
 
Waliwahi kuja kwangu kunifanyia upekuzi bila warrant wamevaa kiraia hawana vitambulisho nikakataa kusachiwa kihuni mmoja kasema Ngoja nikachukue warrant alipofika kwa mkuu wake kamweleza jamaa nijeuri amekataa kupekuliwa zilikuja gari mbili zimejaa police hapo kipigo na wageni nilikua nao pia wakachezea kipigo,baada ya upekuzi hawajakuta chochote ili kunitia adabu wakanibeba mm na mgeni wangu na mke wangu bila kujali alikua na kichanga cha week moja tena kajifungua kwa operation wote kituoni na hatukutoka bure💵💶💷
 
Akipeleka hizo nyaraka ataambiwa apeleke tena nyaraka zinazohusu mahari aliyotoa wakati anaoa! Ni afadhali waseme wanahitaji nyaraka hizo kwa mujibu wa Sheria gani ili tuhuma zieleweke! Pia awe anaitwa kwa barua na sio kujipeleka tu kwa kusikia tu kwenye vyombo vya habari!

Mh !, we Buchaman, Gwajima alipoenda Polisi tarehe 27 March alikuwa na hiari ya kwenda au kuacha. Polisi walisema " … ajisalimishe Polisi haraka sana kabla hawajamtafuta…" alikuwa na hiari ya kuacha kwenda ili ATAFUTWE. Hata kuhusu nyaraka, I am sure hajalazimishwa, ameombwa apeleke kwa hiari yake. Pia ana hiari ya kukataa, ili asubiri hayo maandishi. Yeye amechambua, ameona mbali sana, anajua aina ya nyaraka alizonazo ( Mimi na wewe hatujui). Ameona atafute msaada utakaopelekea yeye kutotoa nyaraka hizo. I pray for him, walau awe na nyaraka hizo na ziwe sahihi, ili mwisho wa safari aweze kuthibitishia umma wa watanzania kwamba nyaraka hizo zipo. Lingine tukumbuke kuwa Polisi hawaendeshi kesi, hivyo wakili hawezi kuwa na msaada mkubwa sana katika hatua za awali. Polisi watamwomba wakili huyo awasubiri wamalize kazi yao ya kipolisi, kisha wakili huyo akamsaidie mteja wake mahakamani, ili kuuthibitishia umma kuwa tuhuma kwa mteja wake zote ni za uwongo. Kwa sasa, polisi wanakusanya taarifa tu. Sasa mtu akitafuta wakili katika hatua za kukusanya taarifa, nadhani anawahi mno na huenda anawaongezea Polisi mashaka zaidi. Haya ni maoni yangu tu.
 
Kova na team yake uzee unawajia vibaya,nasi wawaandikie barua kina kakobe,lusekelo,mwingira,nabii flora na mwakasege wapeleke nao vielelzo hivyo.

Gwajima yy kiburi, haogopi jeshi la polisi, mahakama wala bunge, na anasema hivyo wakati anajua ana mambo yake nyuma ya pazia akidhani polisi hawajui, sasa polisi wamepata pa kuanzia kufichua maovu yake...
 
Watanzania is this all you can think? Mmekuwa obsessed to that extent na udini kiasi hamuoni mantiki ya usawa kisheria? Angekuwa baba yako, au ndugu yako ananyanyaswa kisheria ungeshabikia kuasi hiki.
 
Gwajima yy kiburi, haogopi jeshi la polisi, mahakama wala bunge, na anasema hivyo wakati anajua ana mambo yake nyuma ya pazia akidhani polisi hawajui, sasa polisi wamepata pa kuanzia kufichua maovu yake...

Kwani hajuhi vya kaizari anapewa kaizari? sasa anaogopa nini kupeleka vile alivyoombwa kama anavyo mbona sie tukiombwa upelekaa? alafu yeye anajiita mtu wa Mungu lakini hana heshima na mamlaka na amejaa kiburi hivi si ipo siku atakuja kuwaambia wafuasi wake wasilipe kodi? lakini mbona bwana Yesu aliwaambia wayahudi vya kaizari mpeni kwa maana zitii mamlaka za dunia iweje nabii anapinga utii wa mamlaka? maandiko mbona yanasema tuchunge sana ndimi zetu lakini nabii mzima anauacha ulimi wake unautia mwili wake chachu,kwanini anajivuna na kutoa matusi wakati imesemwa mkiombwa shavu la kulia wapeni na la kushoto yeye anasita nini kumwachia Mungu kazi ili amtetee badala take anatumia pesa ambayo haileti utukufu mbele za anayemtumikia ( Mungu) ama ameshindwa kuliishi neno lilivyoandikwa? anatia mashaka sana na ndo maana anamiliki bunduki badala ya kuomba ulinzi wa roho mtakatifu
 
Yeye SIO DOLA, that is why baada ya kutukanwa amekaa kimya. Gwajima kwa mdomo wake alisema haogopi DOLA: haogopi Polisi, haogopi mahakama na wala haogopi Bunge...That is what he said, kumbe wakili wa nini ?
Hakuna bosi anayeweza kuogopa vyombo alivyounda mwenyewe vimtumikie; hivi ni kifungu gani cha katiba kinachosema raia waogope polisi, mahakama na bunge au dola kwa mfumo wowote?
 
why why why / shame shame ahame to ......../ makanisa na misikiti yote ianze kupeleka nyaraka za mali zao PLICE STATIONS haraka
 
Back
Top Bottom