Mauaji ya visasi

Aisee roho ya jamaa italala kuzimu sasa na damu yake itatulia
Mfanyabiashara Hemed Ally amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa kukusudia Farihani Maluni.

Habari inaeleza Farihani alimpa milioni 30 Hemed amuagizie lori aina ya fuso na baada ya muda mrefu kupita bila ya lori kufika na mdai kulidai, Ally alimuita Farihani nyumbani kwake alipopanga eneo la Sharif Shamba, Ilala.

Hamjat Nassoro wakati akitoa ushahidi wake ambae ndie mmiliki wa nyumba hiyo alisema Ally hakumaliza kodi yake ya mwaka wa pili na alikaa miezi mitano pekee akidai amenunua nyumba Magomeni hivyo anahama.

Hamjat amesema wakati Ally akiishi kwenye nyumba hiyo alimuomba ruhusa aende kwa mjumbe ili achimbe shimo nje ya nyumba atapishe maji kutokana na shimo kujaa majitaka hata hivyo mjumbe hakutoa ruhusa.

Ally alirudi kwa Hamjat akimwomba amruhusu achimbe shimo kwa ndani ya uzio wa nyumba ambapo alimruhusu kwa maelekezo afukie vizuri kama kulivyokuwa, shimo hilo lilitumika kumfukia marehemu Juni 12, 2014.

Februari 9, 2015 Hamjat alipokea simu kutoka kwa polisi wakimtaka aende katika nyumba yake kuna tukio mshtakiwa alilifanya naye akaenda na baada ya kufukua walikuta mabaki ya mwili wa Farihani ukiwa umefungwa kamba mikononi na plasta maeneo ya fuvu(Daktari alihisi ilitumika kumziba mdomo na kumsababishia akose pumzi).

VIDEO 2015
View attachment 2390814

 
IMG-20221024-WA0245.jpg
 

Ukishindwa kusamehe lipa kisasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Ukishindwa kusamehe lipa kisasi

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii niliipitisha kwa 100%
 
Mahakamani Kuu Kanda ya Iringa ambayo imefanya kikao mkoani Njombe imemuhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa Katekista wa Kanisa katoliki jimbo la Makambako Daniel Philipo Mwelango mwenye umri wa miaka 43 kwa kosa la mauaji baada ya kukutwa na hatia.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Februari 8, 2022 kwa kumuua Daniel Elias Myamba mwenye umri wa miaka 43 mkazi wa mtaa wa Kahawa Makambako kesi Na MC 74/2022 katika mtaa wa Bwawani mjini Makamabako.

Hukumu hiyo imetolewa mbele ya Jaji Mhe. Said Kalunde.

Akisoma hukumu hiyo Jaji wa Mahakama kuu Kanda ya Iringa amesema Mahakama imefikia uamuzi huo baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa pasipo shaka yoyote kwamba mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo.

Jaji Kalunde amesema siku ya tukio mshitakiwa alifanya maandalizi kwa kuandaa Panga,Chuma pamoja na mifuko minne ya Kinga njaa,mifuko miwili ilikuwa kwa ajili ya kuzuia damu isisambe na miwili mingine kwa ajili kuhifadhi mwili wa marehemu.

Baada ya hapo akampiga na chuma kwenye kisogo baada ya kuona ameanguka chini na kufariki alimkata vipande viwili na kuvipaki katika mifuko ya kinganjaa ili iwe rahisi kubeba mwili huo na kwenda kuutupa mbali,baada ya kuona mke wa marehemu anapiga simu mara kwa mara kwenye simu ya Maherehemu pamoja mwenyekiti wa kigango alishindwa kuubeba mwili huo na kuamua kuondoka huku akiwa amelibeba panga na kwenda kulitumbukiza katika shimo la choo cha shule ya msingi Makambako na chuma alichotumia kumpiga nacho alikificha kwenye gata karibu na duka na yeye kutorokea Dar es Saalam.
 

Attachments

  • FB_IMG_1702369992032.jpg
    FB_IMG_1702369992032.jpg
    47.7 KB · Views: 3
Mahakamani Kuu Kanda ya Iringa ambayo imefanya kikao mkoani Njombe imemuhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa Katekista wa Kanisa katoliki jimbo la Makambako Daniel Philipo Mwelango mwenye umri wa miaka 43 kwa kosa la mauaji baada ya kukutwa na hatia.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Februari 8, 2022 kwa kumuua Daniel Elias Myamba mwenye umri wa miaka 43 mkazi wa mtaa wa Kahawa Makambako kesi Na MC 74/2022 katika mtaa wa Bwawani mjini Makamabako.

Hukumu hiyo imetolewa mbele ya Jaji Mhe. Said Kalunde.

Akisoma hukumu hiyo Jaji wa Mahakama kuu Kanda ya Iringa amesema Mahakama imefikia uamuzi huo baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa pasipo shaka yoyote kwamba mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo.

Jaji Kalunde amesema siku ya tukio mshitakiwa alifanya maandalizi kwa kuandaa Panga,Chuma pamoja na mifuko minne ya Kinga njaa,mifuko miwili ilikuwa kwa ajili ya kuzuia damu isisambe na miwili mingine kwa ajili kuhifadhi mwili wa marehemu.

Baada ya hapo akampiga na chuma kwenye kisogo baada ya kuona ameanguka chini na kufariki alimkata vipande viwili na kuvipaki katika mifuko ya kinganjaa ili iwe rahisi kubeba mwili huo na kwenda kuutupa mbali,baada ya kuona mke wa marehemu anapiga simu mara kwa mara kwenye simu ya Maherehemu pamoja mwenyekiti wa kigango alishindwa kuubeba mwili huo na kuamua kuondoka huku akiwa amelibeba panga na kwenda kulitumbukiza katika shimo la choo cha shule ya msingi Makambako na chuma alichotumia kumpiga nacho alikificha kwenye gata karibu na duka na yeye kutorokea Dar es Saalam.
du!!!!........aisee!!! sasa nimwamini nani????......huyu katekista atakuwa kasomea CUBA!!!!!"very proffsional killer jamaa!!!!........hamna raia wa kawaida anaweza ku2mia mbinu kali namna hii!!!...yaani kama mauaji ya kashogi????
 
Mauaji ya visasi (kulipa kisasi) ni dhambi ya tatu kuzaliwa duniani
Dhambi ya kwanza ngono na usaliti pale Eden, lakini hii ina mazonge mengi kwakuwa uongo na kutotii maagizo vyote vinaingia hapo! Ni dhambi yenye vipengele A, B C na D

Dhambi ya tatu ni mauaji, ambayo asili yake ni choyo na wivu, pale Kaini alipofanya uchoyo wa kutoa sadaka iliyonona na matokeo yake ikakataliwa.. Ya mdogo wake Abel ilipokelewa na ndipo roho ya chuki ilipomuingia Kaini na kuamua kumuua mdogo wake kwa mama. Adam hakuwa babayake wa damu.

Tangu hapo mkeka wa mauaji ya visasi uliasisiwa ulimwenguni.. Tangia hapo maelfu kwa maelfu wameuawa kwa mauaji ya visasi. Nimekisoma kisa cha kijana wa Songwe aliyeuwawa mbele ya mkewe na mwanae na wauaji wakaondoka bila kuchukua chochote! Visa hivi ni vingi mno na nitasimulia baadhi kadiri ya kumbukumbu zangu, nakukaribisha nawe uungane nami kama kuna chako unakikumbuka!

Maisha haya hutukutanisha na wengi lakini pia na mengi, kuna watu kwa sababu zozote zile wanajiona ya kwamba wao ndio wao na wengine si kitu.

Wao ndio wanastahili kupata
Wao ndio wanastahili maisha mazuri
Wao ndio wanaijua pesa kuliko wengine
Wao ndio wanastahili maisha na vitu vizuri kuliko wengine

Visa hivi vya mauaji ya visasi vina asili moja! Wauaji hawachukui chochote! Visa hivi vyanzo vyake ni
Usaliti wa kibiashara/dili
Usaliti kwenye mapenzi/mahusiano
Harakati za kisiasa na madaraka
Wivu wa maendeleo/kupata kwa wengine
Dhuluma
Utemi
Ubabe nk nk
Kwenye hili kuna wauaji wa kukodi ama baadhi hutekeleza mauaji wenyewe tena kwa taarifa kabla ya kutekeleza mauaji.

Sometimes kwenye haya mambo ukishindwa kusamehe lipa kisasi! Haikuongezei kitu lakini inakupunguzia maumivu! Ila usiijaribu hii njia imejaa mabaya!

Mnamkumbuka yule traffic aliyeuliwa kwa risasi pale sayansi? Jamaa alikuja na boda akamuuliza Afande unanikumbuka? Jamaa akajibu ndio.

Jibu hilo lilitosha kummininia risasi zilizoondoka na uhai wake
Nitakuja na visa vingine.
Kisasi ni haki kwa wale wanaodhulumiwa.

"Kuua ni Dhambi, lakini kumuua mtu Muuaji au Mtu-dhulumati siyo dhambi na wala siyo kosa kisheria, bali ni kitendo cha kishujaa cha kujihami dhidi ya adui hatari."
 
Kisasi ni haki kwa wale wanaodhulumiwa.

"Kuua ni Dhambi, lakini kumuua mtu Muuaji au Mtu-dhulumati siyo dhambi na wala siyo kosa kisheria, bali ni kitendo cha kishujaa cha kujihami dhidi ya adui hatari."
Kuna kitu kinaitwa karma unakijua? Karma haiangalii kama uliua kwa manufaa ama kwa hasara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dhambi ya kwanza ni husda ya kiumbe wa kuitwa Ibilisi. Husda ilipelekea dhambi ya pili ya kutotii agizo la kumuangukia Adamu (kumsujudia) kwa elimu kubwa aliyopewa na Muumba wake, ndipo ukafuata uongo (dhambi ya tatu)
Husda ilikuja kujirudia kwa Kaini na Abeli, ikapelekea mauaji.
 
Kuna kitu kinaitwa karma unakijua? Karma haiangalii kama uliua kwa manufaa ama kwa hasara

Sent using Jamii Forums mobile app
KRMA ni noma jamaa!!! "KARMA is a real GANSTAR ever".....kuna jamaa alikuwa rafiki yangu sana na tumetoka mkoa mmoja,,,na tunaishi jirani,kimaendeleo ya kidunia na kielimu nilikuwa nimemuacha sana,ofisi ze2 zilikuwa jirani,,sasa ikawa asubui nampitia na motokaa yangu tunaenda wote kazini,jioni namstua tunaondoka wote,tunapita sehem 2nalamba wote MASANGA na nyama za hapa na pale,,kumbe jamaa alikuwa ananionea wivu!!!sasa ili kubalance situation akaone anichafue sababu tukikaa pamoja sehem yeye anaonekana kama mpambe wangu ivi,,,bsi akaanza kutangaza kwamba mimi mishe zangu ni jambazi na muuza unga,na kwenye gari natembea na mguu wa kuku,,akaenda mpaka serikali za mtaa,na serikali za mtaa wakaripoti ngazi za juu,,,sasa kwa vile kila sehemu nilikuwa nae jamii iliaminikwa sababu ni friend wangu,,,mimi sijui ili wala lile siku moja namfuata twen"zetu job jamaa akaniambia anajisikia vibaya kumbe kuna ambush ilipangwa bhana!!!.....basi nimefika maeneo ya mtava nikapigwa stop, na askari,kusachi kweli nina moto,,wakaniuliza unamiliki kihalali? nikawaonyesha kitabu,,,basi haoo mpaka centro,,wakaniuliza nafanya kazi gani nikaenda nao mpaka ofisini kwangu bahati nzuri kuna askari wawili pale nilisoma nao A-LEVEL!!!!.......,,,kutoka ofisini nikaenda nao hadi home na sniff dog,,kusachi hamna ngada,,,wakaomba vyeti vya shule na vyou nikawapa na walibutwaa sana!!,,,wakaniambia nifungue kesi ya kuchafuliwa nikakataa nikasema sina muda wa kupoteza kwa ajili ya m2 mwenye akili ndogo,,,basi wakaniambia watajua cha kufanya{hawakunitajia huyo jamaa}..kumbe baada ya siku kadhaa wakatia ofisini kwa huyo jamaa{mimi nilikuwa sijui kinachoendelea} walimtimbia ka watano hivi......kufika pale wakati wanamhoji,akatokea bosi wake{ jamaa alikuwa anapiga issue za wakala wa forodha}...bosi akauliza kuna nini??? wana usalama wakampa issue nzima,,,,,kilichotokea pale,,,jamaa yuko mtaani anakaanga chips,kwani bosi wake alimfukuza baada ya mwezi mmoja,,na kumwambia"wewe ni m2 mmbaya sana,unaweza kunchoma mimi na issue zangu nikaishia vibaya,,,sasa kwa vile jamaa kaishia kidato cha nne,,,ndo ivo yupo kiaa anapigika kiboya....akiniona anajificha......nilikuja kubaini ni yeye baada ya kuambiwa na jirani yake!!!!"KARMA NOMA"
 
KRMA ni noma jamaa!!! "KARMA is a real GANSTAR ever".....kuna jamaa alikuwa rafiki yangu sana na tumetoka mkoa mmoja,,,na tunaishi jirani,kimaendeleo ya kidunia na kielimu nilikuwa nimemuacha sana,ofisi ze2 zilikuwa jirani,,sasa ikawa asubui nampitia na motokaa yangu tunaenda wote kazini,jioni namstua tunaondoka wote,tunapita sehem 2nalamba wote MASANGA na nyama za hapa na pale,,kumbe jamaa alikuwa ananionea wivu!!!sasa ili kubalance situation akaone anichafue sababu tukikaa pamoja sehem yeye anaonekana kama mpambe wangu ivi,,,bsi akaanza kutangaza kwamba mimi mishe zangu ni jambazi na muuza unga,na kwenye gari natembea na mguu wa kuku,,akaenda mpaka serikali za mtaa,na serikali za mtaa wakaripoti ngazi za juu,,,sasa kwa vile kila sehemu nilikuwa nae jamii iliaminikwa sababu ni friend wangu,,,mimi sijui ili wala lile siku moja namfuata twen"zetu job jamaa akaniambia anajisikia vibaya kumbe kuna ambush ilipangwa bhana!!!.....basi nimefika maeneo ya mtava nikapigwa stop, na askari,kusachi kweli nina moto,,wakaniuliza unamiliki kihalali? nikawaonyesha kitabu,,,basi haoo mpaka centro,,wakaniuliza nafanya kazi gani nikaenda nao mpaka ofisini kwangu bahati nzuri kuna askari wawili pale nilisoma nao A-LEVEL!!!!.......,,,kutoka ofisini nikaenda nao hadi home na sniff dog,,kusachi hamna ngada,,,wakaomba vyeti vya shule na vyou nikawapa na walibutwaa sana!!,,,wakaniambia nifungue kesi ya kuchafuliwa nikakataa nikasema sina muda wa kupoteza kwa ajili ya m2 mwenye akili ndogo,,,basi wakaniambia watajua cha kufanya{hawakunitajia huyo jamaa}..kumbe baada ya siku kadhaa wakatia ofisini kwa huyo jamaa{mimi nilikuwa sijui kinachoendelea} walimtimbia ka watano hivi......kufika pale wakati wanamhoji,akatokea bosi wake{ jamaa alikuwa anapiga issue za wakala wa forodha}...bosi akauliza kuna nini??? wana usalama wakampa issue nzima,,,,,kilichotokea pale,,,jamaa yuko mtaani anakaanga chips,kwani bosi wake alimfukuza baada ya mwezi mmoja,,na kumwambia"wewe ni m2 mmbaya sana,unaweza kunchoma mimi na issue zangu nikaishia vibaya,,,sasa kwa vile jamaa kaishia kidato cha nne,,,ndo ivo yupo kiaa anapigika kiboya....akiniona anajificha......nilikuja kubaini ni yeye baada ya kuambiwa na jirani yake!!!!"KARMA NOMA"
FB_IMG_1702355601682.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom