msafiri.razaro
JF-Expert Member
- Oct 12, 2010
- 1,239
- 731
Mangula > Makamba > Mkama > Future Part Secretary inaashilia ushindi for the Peoples
Matukio haya kuchoma nyumba,kumwagia watu tindikali imebainika yanapangwa na katibu mkuu wa CCM Wilson Mkama ili kuipa CDM taswira Mbaya mbele ya jamii , wanayapanga wao wenyewe CCM chini ya uratibu wa Mkama akishirikiana na komba… kama ni kuchomanyumba wameichoma wenyewe ni mpango wao huo
Tuhuma za tindikali zinazoelekezwa kwa Chadema ni mipango iliyosukwa makusudi na CCM na kwamba kama ni watu wenye tindikali, basi CCM ndiyo walionazo.Propaganda hizi zilizopitwa na Wakati anazotumia Mkama haziwapendezi viongozi wa CCM Mkoa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa Wakasubi na Katibu wa CCM Mkoa Ahmed wamenukuliwa wakisema Mukana anawaaribia ''Tatizo la mkama anatumia propaganda za kizamama as if bado tupo kwenye siasa za kijamaa''
nenda igunga. Kuna muujiza huko. Kuku wanakufa lakini binadamu anabaki kwa mto uliomteketeza kuku na nyumba
Tujikumbushe miaka ile Omary Mahitah akiuonyesha umma visu vya CUF vilivyoingizwa kwa ajiri ya kuvunja amani na mpaka leo tunasubiri waliongiza hivyo visu wapelekwe mahakamani. Tatizo lao walizoea kuwahadaa wananchi kwamba Vyama vingi vitaleta ya Rwanda na Burundi na watu walikuwa wanaamini, wamesahau kabisa kwamba watu wanabadirika kifikra, Unaweza ukawadanganya watu wote kwa wakati mmoja lakini huwezi ukawadanganya watu wote kwa wakati wote, Sasa hivi wanaweza kumdanganya bibi yangu aliyepo Kasuru Kigoma lakini hawawezi kumdanganya na mjukuu wake kijana kama mimi, ninaamini vijana woote wameujua ukweli kuhusu CCM ila wana maslahi binafsi ambayo yanatofautiana kutoka mtu mmoja na mtu mwingine, kwa mfano mpaka sasa kuna vijana ambao ujanja wa kununua Tshirt na Kofia hawana wao inatosha sana kuwahonga Tshirt na Kofia, pia wapo
wale ambao wanafanya biashara visivyo halali ili wawe salama wanalazimika kujifanya wao ni CCM damudamu mfano halisi ni maeneo mengi ya pembeni mwa barabara yenye vibustani vya kuuzia miti na maua, utakuta mtu yupo eneo lisilo ruhusiwa kibiashara ili kujihami anapeperusha bendera ya CCM au kufungua katawi ka wakereketwa wa CCM akiamini watu kama polisi na City hawatambuguzi kwa kujua ni mtu wao. CCM badirikeni Watu wamebadirika sana.
Mkuu hiyo mbinu walikuwa nayo kwa namna tofauti, ilikuwa imepangwa hivi: siku ya kurejesha fomu C.U.F waanzishe vurugu ktk vurugu hilo waichukue fomu ya mgombea wa cdm waichane chane na kuipoteza, ccm ndo ilivokuwa imepanga kutimiza hilo kupitia cuf.kama utakumbuka tukio hilo, tulokuwepo kwnye tukio kiongozi wa cuf aliamuru dereva aingize gari barabaran punde tu cdm walipoanza kuondoka, dereva alikataa huku akisema barabara imejaa watu ngoja wapite, waliendelea kubishana hadi kiongozi huyo alipo amuru aachiwe usukani ndipo dereva alipo liingiza gari kwa barabara, ukatokea mtafaaruku kidogo baadaye cdm wakarudi pembeni na ikawa ndiyo ponapona ya cdm siku hiyo, mpango ulikuwa umesukwa na kufadhiliwa na ccm mtekelezaji akiwa ni CUF nilishangaa sana kuwaona cuf wakilalamika kwny vyombo vya habari kuwa wamefanyiwa fujo wakati wao ndo walowafanyia cdm! Ova!CDM Mshukuruni Mungu zaidi kuna mbinu nyingine wameikosea timing tu. MBINU YA KUTEKA MTU NYARA. Inatumika sana hiyo kwenye harakati za kurudisha fomu. MAGAMBA ni Mafia wale
They dont give a sh.t watu wangapi wanapata ulemavu, wanapoteza maisha, mali kiasi gani zinaharibiwa.Ukiwa mwizi unnaweza ukajikuta unajiibia mwenyewe, sasa kumuharibu mtu sura yake kwa tindikali na kusingizia CHADEMA ili wanyimwe kura hizo si ni akili mbovu.
Kumchomea mtu banda lake la kuku na kusingizia CHADEMA ili upate huruma ya kura huo si unyama, CCM inabidi wajitazame upya kuliko kuendeleza unya wanaoufanya!!1
Kwa jimbo moja tu ccm wanakuwa makatili hivyo.!
Inawezekana tu kwenye mazingaombwe ya wakongo na wanaijeria.Kuku na nyumba vinaungua lakini karatasi ya ushahidi inabaki