petro faustine
Member
- Oct 2, 2014
- 74
- 6
WANAFUNZI CHUO KIKUU ST.JOSEPH ARUSHA WAWEKA MGOMO Wanafunzi wa chuo kikuu cha ST.JOSEPH kilichopo Kisongo mkoani Arusha wameitaka serikali kutoa tamko kwa chuo hicho kwamba ni cha halali ama sio cha cha halali kwani hawatendewi haki ya kimasomo kama ilivyo vyuo vingine. Wakizungumza na waandishi wa blog hii wanafunzi hao ambao wameweka mgomo na kukataa kusoma katika chuo hicho wamedai chanzo ni baada ya kauli aliyotoa bungeni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dk.Shukuru Kawambwa kuwa chuo hicho kinatoa masomo ngazi ya Diploma na sio Degree hali ambayo imepelekea wanafunzi hao kufanya mgomo ili kutaka kujua hatma yao katika chuo hicho kwani wengi wao wanasoma degree.
Wamesema wanaiomba serikali kulitumia macho suala hilo kwani wanashindwa kuwa na imani na chuo hicho kutokana na jinsi ambavyo wanapata mafunzo kupitia walimu ambao hawana uzoefu ulio bora wa kuwafundisha. Naye Raisi wa chuo hicho ndg.Jumanne Maryogo amesema hawaoni muelekeo mzuri katika chuo chao ikiwemo mfumo ambao wanatumiwa kufundishiwa kwani wanabadilishiwa walimu mara kwa mara hali ambayo imesababisha kutokuwa na utaala uliobora kwa wanafunzi hao.
Blog hii imelezimika kumtafuta mkuu wa chuo hicho ili aweze kuzungumzia mgogoro huo ambapo Makamu mkuu wa chuo hicho bwn.Siles Balasink amesema wanafunzi wamefanya mgomo huo baada ya kusikia kauli ya waziri lakini pia amedai chuo hicho kina usajili uliokamilika wa TCU hivyo amewataka wanafunzi warudi chuoni ili waweze kupata suluhu ya mgogoro huo. Hata hivyo wanafunzi hao walikuwa na jazba kutokana na kudai haki zao wanedai kwenda mpaka katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma ili wapeleke malalamiko yao na hatimaye waweze kutatuliwa
Wamesema wanaiomba serikali kulitumia macho suala hilo kwani wanashindwa kuwa na imani na chuo hicho kutokana na jinsi ambavyo wanapata mafunzo kupitia walimu ambao hawana uzoefu ulio bora wa kuwafundisha. Naye Raisi wa chuo hicho ndg.Jumanne Maryogo amesema hawaoni muelekeo mzuri katika chuo chao ikiwemo mfumo ambao wanatumiwa kufundishiwa kwani wanabadilishiwa walimu mara kwa mara hali ambayo imesababisha kutokuwa na utaala uliobora kwa wanafunzi hao.
Blog hii imelezimika kumtafuta mkuu wa chuo hicho ili aweze kuzungumzia mgogoro huo ambapo Makamu mkuu wa chuo hicho bwn.Siles Balasink amesema wanafunzi wamefanya mgomo huo baada ya kusikia kauli ya waziri lakini pia amedai chuo hicho kina usajili uliokamilika wa TCU hivyo amewataka wanafunzi warudi chuoni ili waweze kupata suluhu ya mgogoro huo. Hata hivyo wanafunzi hao walikuwa na jazba kutokana na kudai haki zao wanedai kwenda mpaka katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma ili wapeleke malalamiko yao na hatimaye waweze kutatuliwa