B.G TANTAWI
JF-Expert Member
- Jul 3, 2013
- 495
- 375
Mh. Henry Matata wiki iliyopita alinusurika kipigo kutoka kwa vijana alowapa kazi ya kupakua mizigo yake kutoka kwnye mitumbwi eneo la Mwaloni jijini Mwanza.
Sekeseke hilo lilikuwa hivi, baada ya mitumbwi kutia nanga aliwachukua vijana kuwa waende wateremshe mizigo kwa makubaliano kuwa atawalipa baada ya kazi. Vijana wale wakatii, baada ya kumaliza kazi vijana walimwambia Mh. kuwa tayari wamemaliza kazi so awape chao.
Mh. alikuja kuakiki kama ni kweli kazi imeisha, baada ya kuridhika kuwa kazi yake imeisha Matata akawaambia "ok, asanteni" akaanza kuondoka, ndipo vijana wale waliokuwa zaidi ya 50 wakamzunguka, Mh. kuona vile akatoa bastora yake, bahati nzuri au pengine mbaya, rafiki yake matata alimuona Mh. akitoa Bastola akasikika akisema "Matata rudisha bastola watakuua" mara moja Mh. akarudisha bastola mfukoni na kuanza kutii maagizo ya vijana wale, kwanza alikarishwa chini ya ulinzi na akaamriwa awape pesa zao, Mh. akatoa pesa mfukoni na kuanza kuwalipa, zilipungua, ndipo akapiga simu kwa mtu asiye fahamika mara moja na baada ya muda mfupi mtu huyo akaja na pesa zingine ili kuwamalizia vijana.
source: Nilikuwepo mimi.
Sekeseke hilo lilikuwa hivi, baada ya mitumbwi kutia nanga aliwachukua vijana kuwa waende wateremshe mizigo kwa makubaliano kuwa atawalipa baada ya kazi. Vijana wale wakatii, baada ya kumaliza kazi vijana walimwambia Mh. kuwa tayari wamemaliza kazi so awape chao.
Mh. alikuja kuakiki kama ni kweli kazi imeisha, baada ya kuridhika kuwa kazi yake imeisha Matata akawaambia "ok, asanteni" akaanza kuondoka, ndipo vijana wale waliokuwa zaidi ya 50 wakamzunguka, Mh. kuona vile akatoa bastora yake, bahati nzuri au pengine mbaya, rafiki yake matata alimuona Mh. akitoa Bastola akasikika akisema "Matata rudisha bastola watakuua" mara moja Mh. akarudisha bastola mfukoni na kuanza kutii maagizo ya vijana wale, kwanza alikarishwa chini ya ulinzi na akaamriwa awape pesa zao, Mh. akatoa pesa mfukoni na kuanza kuwalipa, zilipungua, ndipo akapiga simu kwa mtu asiye fahamika mara moja na baada ya muda mfupi mtu huyo akaja na pesa zingine ili kuwamalizia vijana.
source: Nilikuwepo mimi.