Bramo
JF-Expert Member
- Oct 21, 2009
- 13,160
- 10,007
By Ansebert Ngurumo
SWALI kuu la wiki hii ni hili: Kwa nini Rais Jakaya Kikwete ameogopa kuwatumia wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), badala yake akawatumia wanafamilia kutafuta wadhamini ili aidhinishwe kugombea tena urais mwaka huu? Tafsiri zimekuwa nyingi. Lakini kubwa kuliko zote ni kwamba Rais Kikwete hana imani na wanachama wenzake. Anawaogopa, nao wanamtilia shaka. Anaona ni vema kutumia wanafamilia mkewe na mwanaye katika harakati za kurejea Ikulu.
Maana yake nini? Miaka mitano Ikulu haikuwa neema kwake na chama chake. Uhusiano wake na wapambe wake wa msingi umedorora. Chama kimejaa makundi yasiyoaminiana, yanayofitiniana.
Kwa hiyo, wakati anajitapa kuwa amedumisha umoja na mshikamano, na kusema kwamba hili ni moja ya mafanikio yake yanayomfanya agombee tena urais; kitendo cha kuwakwepa wana CCM wenzake na kuwatumia wanafamilia kinaonyesha kwamba wana CCM hawana umoja wala mshikamano unaotosha kumwezesha yeye kupata wadhamini wanaoaminika.
Baada ya siasa za wapambe na mtandao, sasa tumerudi kwenye siasa za baba, mama, mtoto na mama mkwe.
Ukweli unabaki kuwa kwamba upepo wa kisiasa katika wiki mbili zilizopita unaonyesha kwamba JK wa mwaka 2005 si huyu wa mwaka 2010.
Wana CCM wamesema pembeni na hadharani. Wapambe wamejadili, na vyombo vya habari vimeandika. Utetezi na ufafanuzi wa chama na Ikulu vimetolewa. Lakini tunapotazama na kutafakari, tunaona kwamba hata zile shamrashamra za mwaka 2005 hazipo tena.
Hazikuwapo siku alipotangaza kuchukua fomu. Kule kujiamini alikokuwa nako mwaka 2005 aliposisitiza kwamba hafikirii kushindwa hakupo tena.
Sasa kuna hofu kwamba JK anaweza kushindwa; na kama atashinda itakuwa kwa asilimia ndogo.
Nakumbuka baadhi ya mashushushu wake waliowahi kunisihi nipunguze makali, walikiri kwamba iwapo wananchi wataelimika na kuhamasika vya kutosha, rais anaweza kushinda kwa kura chache tu, jambo ambalo linaweza kuleta mzozo, kwani wananchi wanaweza kukataa matokeo ya kura; wakaandamana na kuleta zogo na kuifanya nchi isitawalike.
Na wakasisitiza kwamba iwapo hilo litatokea, mimi nitakuwa nimechangia kuleta vurugu nchini jambo ambalo niliwaomba walitafakari kwa kina.
Ukweli huo umesemekana kuwa ulimfanya naye afikirie mara mbili, kama achukue fomu au aachie ngazi hadi alipohakikishiwa na kushawishiwa na watu wake kwamba hawatampinga.
Alijua, na alihofia, kwamba iwapo angejitokeza mgombea mwingine ndani ya chama, lolote lingeweza kutokea; kwani kuna wajumbe wa vyombo vikuu vya uamuzi ndani ya CCM ambao wana nguvu kubwa sana kuliko ya mwenyekiti wao.
Alijua pia kwamba hata wanachama wa kawaida, kama wangepata mbadala, na kushawishiwa vilivyo, wangeweza kuandika historia kama ya chama cha ANC cha Afrika Kusini, ambacho kilimtosa rais aliyekuwa madarakani (Thabo Mbeki) kikamchagua Jacob Zuma.
Hofu hii ndiyo ilimfanya asiruhusu maswali ya wananchi na waandishi wa habari, alipochukua fomu Dodoma, Jumatatu wiki hii. Alijua kuna maswali mengi yasiyojibika.
Na hofu hii ndiyo inawafanya baadhi ya watu wake kusema kwa kujiamini kwamba hata kama utaitishwa mdahalo wa kisiasa kwa wagombea urais mwaka huu, JK hatashiriki. Anaogopa maswali.
Kama mwaka 2005 aliogopa kushiriki akiwa mpya na mweupe, atawezaje kukubali akiwa ameshachafuka kwa matope ya miaka mitano ya utendaji usioridhisha?
Vyovyote itakavyokuwa, na ingawa hadi sasa JK anaonekana mgombea pekee wa urais kutoka CCM, yeye hana amani kwamba hatapingwa. Inawezekana naye anajua moyoni, ingawa mdomoni anasema atashinda, kwamba anaweza kupita kwa nguvu ya dola au kwa ushindi wa asilimia ndogo sana isiyokubalika kwa wananchi.
Na yeye binafsi angependa kujua kama hadi mwisho wa mwezi huu hatajitokeza mtu mwingine (asiyeogopa utabiri wa Sheikh Yahya Hussein) wa kumpinga; na kama vyama vya upinzani havitaweza kumpata mgombea anayekubalika anayeweza kuleta tumaini la Watanzania kuondokana na ombwe la uongozi.
Hakika, miaka mingine mitano chini ya ombwe ni laana isiyokubalika kwa taifa la watu wanaozidi milioni 40. Na ndiyo maana nimekuwa nawauliza wana CCM wanaoogopa kugombea na JK: Hivi Tanzania imeishiwa na watu wema, wenye uwezo na upeo, wanaoweza kuwa viongozi bora?
Tungepata waandishi kumi kama Ngurumo,walah Wa Tanzania woote wangeamka kutoka usingizini.
SWALI kuu la wiki hii ni hili: Kwa nini Rais Jakaya Kikwete ameogopa kuwatumia wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), badala yake akawatumia wanafamilia kutafuta wadhamini ili aidhinishwe kugombea tena urais mwaka huu? Tafsiri zimekuwa nyingi. Lakini kubwa kuliko zote ni kwamba Rais Kikwete hana imani na wanachama wenzake. Anawaogopa, nao wanamtilia shaka. Anaona ni vema kutumia wanafamilia mkewe na mwanaye katika harakati za kurejea Ikulu.
Maana yake nini? Miaka mitano Ikulu haikuwa neema kwake na chama chake. Uhusiano wake na wapambe wake wa msingi umedorora. Chama kimejaa makundi yasiyoaminiana, yanayofitiniana.
Kwa hiyo, wakati anajitapa kuwa amedumisha umoja na mshikamano, na kusema kwamba hili ni moja ya mafanikio yake yanayomfanya agombee tena urais; kitendo cha kuwakwepa wana CCM wenzake na kuwatumia wanafamilia kinaonyesha kwamba wana CCM hawana umoja wala mshikamano unaotosha kumwezesha yeye kupata wadhamini wanaoaminika.
Baada ya siasa za wapambe na mtandao, sasa tumerudi kwenye siasa za baba, mama, mtoto na mama mkwe.
Ukweli unabaki kuwa kwamba upepo wa kisiasa katika wiki mbili zilizopita unaonyesha kwamba JK wa mwaka 2005 si huyu wa mwaka 2010.
Wana CCM wamesema pembeni na hadharani. Wapambe wamejadili, na vyombo vya habari vimeandika. Utetezi na ufafanuzi wa chama na Ikulu vimetolewa. Lakini tunapotazama na kutafakari, tunaona kwamba hata zile shamrashamra za mwaka 2005 hazipo tena.
Hazikuwapo siku alipotangaza kuchukua fomu. Kule kujiamini alikokuwa nako mwaka 2005 aliposisitiza kwamba hafikirii kushindwa hakupo tena.
Sasa kuna hofu kwamba JK anaweza kushindwa; na kama atashinda itakuwa kwa asilimia ndogo.
Nakumbuka baadhi ya mashushushu wake waliowahi kunisihi nipunguze makali, walikiri kwamba iwapo wananchi wataelimika na kuhamasika vya kutosha, rais anaweza kushinda kwa kura chache tu, jambo ambalo linaweza kuleta mzozo, kwani wananchi wanaweza kukataa matokeo ya kura; wakaandamana na kuleta zogo na kuifanya nchi isitawalike.
Na wakasisitiza kwamba iwapo hilo litatokea, mimi nitakuwa nimechangia kuleta vurugu nchini jambo ambalo niliwaomba walitafakari kwa kina.
Ukweli huo umesemekana kuwa ulimfanya naye afikirie mara mbili, kama achukue fomu au aachie ngazi hadi alipohakikishiwa na kushawishiwa na watu wake kwamba hawatampinga.
Alijua, na alihofia, kwamba iwapo angejitokeza mgombea mwingine ndani ya chama, lolote lingeweza kutokea; kwani kuna wajumbe wa vyombo vikuu vya uamuzi ndani ya CCM ambao wana nguvu kubwa sana kuliko ya mwenyekiti wao.
Alijua pia kwamba hata wanachama wa kawaida, kama wangepata mbadala, na kushawishiwa vilivyo, wangeweza kuandika historia kama ya chama cha ANC cha Afrika Kusini, ambacho kilimtosa rais aliyekuwa madarakani (Thabo Mbeki) kikamchagua Jacob Zuma.
Hofu hii ndiyo ilimfanya asiruhusu maswali ya wananchi na waandishi wa habari, alipochukua fomu Dodoma, Jumatatu wiki hii. Alijua kuna maswali mengi yasiyojibika.
Na hofu hii ndiyo inawafanya baadhi ya watu wake kusema kwa kujiamini kwamba hata kama utaitishwa mdahalo wa kisiasa kwa wagombea urais mwaka huu, JK hatashiriki. Anaogopa maswali.
Kama mwaka 2005 aliogopa kushiriki akiwa mpya na mweupe, atawezaje kukubali akiwa ameshachafuka kwa matope ya miaka mitano ya utendaji usioridhisha?
Vyovyote itakavyokuwa, na ingawa hadi sasa JK anaonekana mgombea pekee wa urais kutoka CCM, yeye hana amani kwamba hatapingwa. Inawezekana naye anajua moyoni, ingawa mdomoni anasema atashinda, kwamba anaweza kupita kwa nguvu ya dola au kwa ushindi wa asilimia ndogo sana isiyokubalika kwa wananchi.
Na yeye binafsi angependa kujua kama hadi mwisho wa mwezi huu hatajitokeza mtu mwingine (asiyeogopa utabiri wa Sheikh Yahya Hussein) wa kumpinga; na kama vyama vya upinzani havitaweza kumpata mgombea anayekubalika anayeweza kuleta tumaini la Watanzania kuondokana na ombwe la uongozi.
Hakika, miaka mingine mitano chini ya ombwe ni laana isiyokubalika kwa taifa la watu wanaozidi milioni 40. Na ndiyo maana nimekuwa nawauliza wana CCM wanaoogopa kugombea na JK: Hivi Tanzania imeishiwa na watu wema, wenye uwezo na upeo, wanaoweza kuwa viongozi bora?
Tungepata waandishi kumi kama Ngurumo,walah Wa Tanzania woote wangeamka kutoka usingizini.