Marufuku Kumuoa hata kama ana mimba

Mghoshingwa

JF-Expert Member
Jul 9, 2011
305
73
Wana Jf, poleni kwa majukumu! Najitokeza kwa mara ya kwanza kuomba ushauri!
Nina mpenzi kwa miaka 4 hivi na tuna pendana sana. Kwa muda wote huu tulikuwa boy friend na girl friend. Mwez uliopita (september) bint alipata Ujauzito. Kimsing tulifurah sana. Niliamua kutuma wazaz wangu wapeleke posa. Jambo la kushangaza POSA ILIKATALIWA KWA KUWA MIMI NA HUYU BINT TUNASALI MADHEHEBU TOFAUTI. Yeye ni MSABATO NA MIMI NI MLUTHERI. Wazazi wake hawataki kusikia lolote kuhusu ndoa japo wanajua binti yao ni MJAMZITO. Bint ananipenda na mimi nampenda pia. NAOMBENI USHAURI WADAU.
 
teana ishu ya dini na mapenzi. naona vijana sasa inabidi niwape somo.

jambo la kwanza jamani wakati mnachagua galfrend hakikisha vigezo vyote ambavyo ungependa future wife awe navyo anavyo. usijidanganye oh hapa namega K na kusepa ...oh hao hao ma galfrend ndio wanakuwa wake.

kwa kipengele cha dini najua kuwa watu wengi siku hizi hatutilii umuhimu hii kitu lakini mwisho wa siku lazima uliangalie maana mnapendana nyie lakini mwisho wa siku lazima mtarudi kwa wazazi ambao wao dini ni kitu important sana. Wanaume tuwe wenye hekima basi na kutopuuzia hili swala. kama wewe sio mtu wa dini basi hakikisha huyo demu ni yule atakayekubali kwenda kufunga ndoa bomani.
 
Just cool down, itafahamika tu....Chunga mimba wasiitoe, lakini ongea na huyo girl friend wako asije akadanganywa akaitoa mimba hata siku moja, wakizingua zaidi unajipanga unamhamishia nyumbani...saa zingine naona watanzania wamekuwa wakididimizwa na dini, ndoa za watu zimevunjika kwa sababu ya dini, IKIWA SISI KAMA VIJANA HATUTAWEZA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO VIZURI TUTAKUJA KUZIJUTIA BAADAYE vijana wa nchi nyingine wanashindana kwa maendeleo lakini Tanzania Vijana wengi wanakusanywa ktk DINI, sikatazi kuabudu ila tukumbuke mambo mazuri ya kesho yanatengenezwa leo...ndugu wala usihangaike nao sana cha msingi hakikisha mimba haitolewi
 
Wana Jf, poleni kwa majukumu! Najitokeza kwa mara ya kwanza kuomba ushauri!
Nina mpenzi kwa miaka 4 hivi na tuna pendana sana. Kwa muda wote huu tulikuwa boy friend na girl friend. Mwez uliopita (september) bint alipata Ujauzito. Kimsing tulifurah sana. Niliamua kutuma wazaz wangu wapeleke posa. Jambo la kushangaza POSA ILIKATALIWA KWA KUWA MIMI NA HUYU BINT TUNASALI MADHEHEBU TOFAUTI. Yeye ni [colour=blue]MABATO[/colour] NA MIMI NI MLUTHERI. Wazazi wake hawataki kusikia lolote kuhusu ndoa japo wanajua binti yao ni MJAMZITO. Bint ananipenda na mimi nampenda pia. NAOMBENI USHAURI WADAU.

hapo kwenye blue ndio dini gani vile.
 
mabato au sabato? dhehebu si kegezo bana ,watu wanaoana dini tofauti we unaongelea dhehebu
 
hapa ndipo dini zinapokiuka misingi ya kiutu mbona hayo madhehebu hayakuizuia mimba isitunge,mkuu kausha baba kama wako wako tu mzee.ila hizi dini zenu za kitumwa zitawaua hizi.
 
Mambo ya kizamani sana hayo
LUtheran na Sababto ndio iwe kigezo
Sidhani kama hao wazazi wanajua wanalolifanya
Jipange tuu na msichana wako na kama ameandikiwa kuwa mke wako atakuwa mke wako no matter what
Sabato na Lutheran sio kigezo cha kukufanya wewe uachane na mtu ambaye mmeshapanga kuwa pamoja
Jaribu kuwatuma wazee wenye uelewa na hata wachungaji wako wakaongee na wazazi wa binti maana yote ni ya kikristo so sioni tatizo na after all hujamlazimisha mkeo kufuata la kwako wala wewe kufuata ya kwake
Mbona hata walio dini tofauti wanaoana bana
 
Kama unampenda na yeye anakupenda ongeza mtoto mwingine wakuleee!
 
Kosa ulilolifanya ni kumpa mimba kabla ya kuoana, maana sasa unalazimika kutaka kumwoa hata kama hujajipanga sawasawa!!!

Siku zote kumbuka kuwa ndoa ni suala la MAPENZI, IMANI, JAMII, SHERIA na UCHUMI. Huwezi kukwepa kitu na ukijaribu tu kukwepa tegemea kupambana na matatizo mbele ya safari.

Tatizo hapo kwako ni JAMII(Wazazi na ndugu) na wala sio IMANI, nakushauri kufanya haya;

1/Jitahidi kuwashawishi zaidi wazazi ili wakuelewe(Tumia hata wazee wenye busara wenye ukaribu na wazazi
wake)

2/Angalia uwezekano wa kubadilisha dhehebu(Kama unahisi wazazi wako watapenda na wewe kama unapenda!!)

3/Tulia mpaka mchumba ajifungue halafu uanze mchakato upya(Huenda wazazi watakuja kukubali)

*Yote hayo yakishindikana basi na LIWALO NA LIWE, ama kumwoa au kutokumwoa kabisa, hilo unaamua mwenyewe pasipo kujali mtu!!!
 
mimi ni msabato nacho jua mara nyingi wasabato huwa wanamtenga mwanao juu ya lile alilolifanya kiimani lakini ushauri mkubwa huwa ni kwamba yeye arudi kwenye darasa la ubatizo ajifunze upya na kubatizwa na mara ingine kama biti ataruhusiwa kuolewa na mwanaume mwenye dini tofauti ushauri mkubwa huwa ni kwamba mshauri mume wakawe msabato mfunge ndoa na akikataa basi alazimishwa
 
mimi ni msabato nacho jua mara nyingi wasabato huwa wanamtenga mwanao juu ya lile alilolifanya kiimani lakini ushauri mkubwa huwa ni kwamba yeye arudi kwenye darasa la ubatizo ajifunze upya na kubatizwa na mara ingine kama biti ataruhusiwa kuolewa na mwanaume mwenye dini tofauti ushauri mkubwa huwa ni kwamba mshauri mume wakawe msabato mfunge ndoa na akikataa basi alazimishwa

Maisha yawaumize kichwa, Dini nazo ziwatese......sishauri kubadili dini kwani wote ni wakristo wametofautiana siku za kuabudu na misingi ya kanisa....vema wakae na wazazi wawaruhusu, wakikataza basi kama kutengwa na watengwe, binadamu akikuchukia Mungu si upamoja naye

(Joshua1:9)[SUP]9 [/SUP]Have not I commanded you? Be strong, vigorous, and very courageous. Be not afraid, neither be dismayed, for the Lord your God is with you wherever you go
 
Maisha yawaumize kichwa, Dini nazo ziwatese......sishauri kubadili dini kwani wote ni wakristo wametofautiana siku za kuabudu na misingi ya kanisa....vema wakae na wazazi wawaruhusu, wakikataza basi kama kutengwa na watengwe, binadamu akikuchukia Mungu si upamoja naye

(Joshua1:9)[SUP]9 [/SUP]Have not I commanded you? Be strong, vigorous, and very courageous. Be not afraid, neither be dismayed, for the Lord your God is with you wherever you go

Asante kaka.
 
Huyo binti mwambie asome kwenye kanuni za kanisa la wasabato wameandikaje kuhusu ndoa,hizo kanuni zimenukuliwa kutoka kwenye biblia ambapo inasema msioe wasio na imani moja na nyie.
Wasabato hufuata Amri kumi za Mungu ambazo hazijawa altered,hufuata biblia yote agano jipya na la kale,etc kuoana hapo itakuwa ngumu jombaa

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Tusiquote biblia vibaya anza kusoma tokea mwanzo,kuna mtu kasema yeye ni msabato swali unajua kanuni imeandikaje kuhusu ndo?

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Kosa ulilolifanya ni kumpa mimba kabla ya kuoana, maana sasa unalazimika kutaka kumwoa hata kama hujajipanga sawasawa!!!

Siku zote kumbuka kuwa ndoa ni suala la MAPENZI, IMANI, JAMII, SHERIA na UCHUMI. Huwezi kukwepa kitu na ukijaribu tu kukwepa tegemea kupambana na matatizo mbele ya safari.

Tatizo hapo kwako ni JAMII(Wazazi na ndugu) na wala sio IMANI, nakushauri kufanya haya;

1/Jitahidi kuwashawishi zaidi wazazi ili wakuelewe(Tumia hata wazee wenye busara wenye ukaribu na wazazi
wake)

2/Angalia uwezekano wa kubadilisha dhehebu(Kama unahisi wazazi wako watapenda na wewe kama unapenda!!)

3/Tulia mpaka mchumba ajifungue halafu uanze mchakato upya(Huenda wazazi watakuja kukubali)

*Yote hayo yakishindikana basi na LIWALO NA LIWE, ama kumwoa au kutokumwoa kabisa, hilo unaamua mwenyewe pasipo kujali mtu!!!

Asante ndugu, ila dini siwezi kubadili coz ninasali kwa mungu sio kwa dhehebu. Asante kwa ushauri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom