Sanctus Mtsimbe
R I P
- Jul 14, 2008
- 1,820
- 1,031
Mtsimbe cheki PM yako mkuu.
Mkuu nimekupata, asante. Fungua barua pepe yako.
Mtsimbe cheki PM yako mkuu.
Sanctus Mtsimbe,
Mkuu samahani sana, nitakuomba uandike maelezo yako kwa lugha yetu ya Kiswahili ili wengi wasomaji wpate kukuelewa.
Mkuu Mkandara, nitajitahidi kufanya hivyo. Unajua kilichotokea ni coincidence ya mawazo yangu na Plan ya Rev. Kishoka. Issue ya Elimu na Kilimo nimekuwa nikivifanyia kazi muda mrefu na nilikuwa nimeviandika kwa kiingereza katika kumbukumbu zangu kwa sababu za kiutendaji na hivyo ilikuwa rahisi kwa mimi kutoa mawazo yangu katika lugha hiyo.
Bila ya shaka nitajitahidi kuzingatia ushauri wako
Tatizo mimi ninaloona ni kua sisi wengi wetu ni kujaribu fikiri matatizo yetu ni kutokana na muono mbovu ama ufupi wa uelewa wa viongozi wetu kuhusu matatizo ya nchi yetu na kujaribu kutumia nguvu nyingi kuwapa plan B na namna ambayo ingefaa kuchukuliwa.
Ukweli ni kwamba hawa viongozi wana uelewa mkuu juu namna mbinu na mikakati ya kututoa ktk umasikini. Sasa basi kwanini hawafanyi hivyo?
Ni jaribio hatari kwao na falme zao za kimwinyi kujaribu kumletea masikini maisha bora,kwao ktk hali hiyo ya umasikini ni Bora zaidi ya mara mia kuliko kuwaendeleza wananchi na hatimaye utawala wao kupeana vijiti kua ktk hali tete.
Yani kwao kumuendeleza masikini ni sawa na kumpa adui yako silaha makini na mbinu maridadi.
Wao wana endekeza mfumo huo ili wapokezane madaraka watoto wajukuu,vitukuu,vining'ina.
Na ukitaka kuangalia kwa makini na kuunganisha nukta ni kwa nini bodi ya mkopo pale wanataka lazimisha mtoto wa masikini lazima asome Engineering?? Maana akisoma masomo mengine ama asipate kabisa mkopo ama wampe 50% sasa hizo zingine atatoa wapi??.
Tatizo la TZ sio mipango wala sera ,tatizo ni patriotism tupiganieni patriotism kwanza..
Mchungaji,
Napata shida sana kwani watu kama wewe wenye mitazamo mizuri hampati nafasi ktk utawala wa taifa letu, nchi yetu sasa inarithishwa kwa watoto waviongozi na si vinginevyo.
Mchungaji hapo nyuma ktk thread yangu( Mbowe jiuzulu ukinusulu chama) nimeshauri kuwa tupate kiongozi mwingine anayeweza kuendeleza kazi njema aliyoianzisha, la kushangaza wewe na vigogo wengine ktk forum hii mmekaa kimya, ama mmeiona ni mada hiyo ni tete au vipi.
Mchungaji
Mchango wako bado unaitajika ktk taifa letu
Mungu ibariki Tanzania
Nimefarijika kuona Rev. Kishoka umetumia muda wako na kushusha mipango, hata kama ina dosari hapa na pale lakini kuna starting point na ni mwanzo mzuri kwa mjadala mkubwa. Kila mmoja wetu akishusha kwa mtindo huu wa uwazi na mkamilifu, tunaweza tukagundua matatizo yetu yako wapi! Hongera sana Rev. Kishokainaendelea...
Viwanda, Mashirika, Huduma na Biashara
Makosa ya Azimio la Arusha ni sawa na yale mapinduzi ya viwanda ambayo yalifanywa na Stalin kule Urusi na hata Mao wa China na ile sera ya Great Leap Forward. Aidha makosa ya wakati wa kubinafsisha viwanda miaka ya 1990-2008 ili kuachana na kuendesha viwanda kutokana na ufanisi mdogo na kuingia hasara hayatarudiwa.
Tumejifunza kuwa tunataka kuwa na viwanda, lakini kilichotushinda hapo awali ni kukosekana utaalamu, motisha, ubunifu na tija katika kuendesha viwanda hivi. Viwanda kama Machine Tools, Mgololo, Ufi, Mwatex na vinginevyo havikustahili kufa.
Makosa ya kuzubaa na kuendelea kuvikamua na kutumia mapato ya viwanda hivi kwa kazi nyingine ambazo hazihusiani na shughuli za uzalishaji mali wa viwanda hivi kama kujijenga kisiasa na vyama vya siasa, ulisababisha kwa kiwango kikubwa kuanguka kwa viwanda vyetu. Makosa ya kubebesha Mashirika na Viwanda mzigo wa Public Welfare, haukuwa mzuri. Ni mfumo huo ambao ulisababisha mapato ya wafanyakazi kudumaa na hivyo kuchochea vitendo vichafu ambavyo viliua moyo wa uchapa kazi, uwajibikaji na uadilifu.
Mpango wa Mchungaji ni kurejesha viwanda vya kusindika mazao ya chakula na biashara, viwanda vya mchecheto (processing) mazao kama katani, pamba, viwanda vya bidhaa za matumizi ya nyumbani na viwanda na yote haya ni katika jitihada za kupunguza uagizaji wa bidhaa za matumizi kutoka nje. Motisha utatolewa kwa viwanda vya zana za kilimo na ujenzi.
Msukumo wa kujijenga kiviwanda utalenga kujenga na kuimarisha viwanda kutokana na rasilimali tulizonazo zikiwa ni pamoja na kilimo na chakula, mifugo, uvuvi, misitu, madini, ngozi, nguo, madawa, mbolea, na kama tutakuwa na uwezo, viwanda vya teknolojia kama vifaa vya umeme.
Kwa kuwa tutakuwa tumeweka nguvu katika nishati, kuwepo kwa umeme wa kutosha kutakuwa ni motisha kukaribisha viwanda vya wawekezaji wa kimataifa ambao hukimbia nchi zao kutokana na gharama kubwa za uzalishaji na kutafuta gharama rahisi za kuzalisha mali. Kukaribisha wawekezaji hawa, hakuna maana kuwa Tanzania itakubali wafanyakazi wake wanyonywe au kudhalilishwa kwa kuwa ni cheap labor. Serikali itahakikisha kuwa sheria za kazi za nchi na kimataifa zinafuatwa ikiwa ni pamoja na kanuni za usalama viwandani.
Mashirika kama SIDO na NDC, yatapewa msukumo wa kuchocha ukuaji wa viwanda na taaluma za ndani. Wahitimu kutoka vyuo vya VETA , watapewa miongozo na usimamizi na kusaidiwa shughuli zao kupitia SIDO. NDC itarudishwa kuwa nguvu iliyoleta maendeleo ya viwanda kabla ya zoezi ka kuuza mashirika.
Kama Taifa, tumejijenga kwa kuwa na biashara ndogo ndogo na si biashara kubwa. Tumejenga utamaduni wa kukimbila biashara za bidhaa dhaifu na zisizo na ubora na kutokana na mtazamo duni, tunashindwa kukabili ushindani wa kibiashara kutoka kwa wageni.
Elimu ya biashara, utunzaji mahesabu, bajeti, masoko na matangazo ya biashara, yatasaidia sana kuhakisha sekta hii ya biashara na viwanda inakuwa kwa ushindani na umahiri. Tukiangalia wenzetu Wakenyana hata Rwanda, mipango yao ya maendeleo ni shirikishi katika kuelimisha wafanyabiashara wao mbinu bora za kufanya biashara.
Bodi kama BET na BIT zinabidi ziungane na TCCIA kuwa na mikakati bora ya kuimarisha viwanda na biashara.
Pendekezo moja ambalo litasaidia jamii na wafanyakazi katika nyanja hii na hasa katika Viwanda na Mashirika ya Biashara na Huduma ya umma ni kuanza kuwashirikisha wafanyakazi katika umiliki wa vyombo hivi kwa kutoa hisa za mashirika haya kwa wafanyakazi wake, ili nao wanufaike na mgawanyo wa riba za mapato. Hii itakuwa ni motisha na kichocheo kikubwa cha kujenga Uwajibikaji, Uaminifu, Tija na Utii (loyalty).
Katika kila nyanja ya uzalishaji mali, huduma na kuwa na malengo bora ni kiini cha mafanikio. Waliosema kuwa mteja ni mfalme hawakukosea. Viwanda, Mashirika na Wafanyabiashara wetu wanabidi kujizatiti na kukabili ushindani kwa kuwa na huduma na bidhaa bora, kuwa watangazaji wa bidhaa za ndani ili kuongeza mapato ya ndani
itaendelea...
Nimefarijika kuona Rev. Kishoka umetumia muda wako na kushusha mipango, hata kama ina dosari hapa na pale lakini kuna starting point na ni mwanzo mzuri kwa mjadala mkubwa. Kila mmoja wetu akishusha kwa mtindo huu wa uwazi na mkamilifu, tunaweza tukagundua matatizo yetu yako wapi! Hongera sana Rev. Kishoka
Rev Sijaona hiyo attachment!? au ni mimi tuu?Kwa wale ambao walikuwa wanahitaji nakala ya Waraka wa mchungaji, mkibonyeza hichoo kitufe chenye kuonyesha attachment, mtaipata nakala kamili ikiwa katika word document format.
Rev Sijaona hiyo attachment!? au ni mimi tuu?
Inaendelea...
Uchumi utaanza kujengeka kwa kuanza kujenga misingi bora ya maarifa na hii ni kupitia sekta ya Elimu.
Elimu
Mfumo wa elimu wa Tanzania unabidi kubadilika na kuhakikisha kuwa tunajenga mfumo wa elimu ambao unachochea ubunifu, unarahisisha uzalishaji mali na unawiana na maendeleo yetu. Kuna haja ya kuachana na mfumo wa Elimu ya kufaulu na kuhakikisha kuwa kinachofundishwa kinaeleweka na kinaweza kutumika ipaswavyo na wanafunzi wote, kuanzia chekechea, shule ya msingi, sekondari, vyuo vya fani stadi na hata elimu ya juu.
Mpango wa Rev. Kishoka kuboresha Elimu ni kuhakikisha kuwa mitaala na silabasi za kufundishia zinalingana na mahitaji ya jamii. Kipaumbele kitakuwa si kuongeza shule ili kuongeza maarifa na taifa la walioelimika, bali ni kuwa na elimu ya kiwango cha juu, elimu ambayo itafundishika kwa urahisi na kuweza kutumika kwa vitendo kadri wanafunzi wanavyoendelea kujifunza.
Mkazo utakuwa ni kuwa na walimu wenye uwezo wa kufundisha na wenye mapenzi katika fani ya ualimu. Waalimu watapewa kila nyenzo zinazohitajika kuhakikisha kuwa kazi zao zinafanyika kwa ufanisi na mafanikio na matunda ya kazi zao yanaonwa na kupokewa na jamii nzima.
Katika mpango wangu, kila Wilaya itapaswa kuwa na Shule si chini ya mbili za Sekondari na chuo cha ufundi ambazo zitakuwa chini ya mamlaka za Tamisemi. Kila mkoa utapaswa kuwa na shule za sekondari ya elimu ya juu si chini ya 4, Vyuo vya ualimu, uuguzi na utabibu, kilimo, uvuvi na mifugo, , biashara na uhasibu, ufundi (mithili ya Dar Tec), sanaa utamaduni na michezo.
Katika elimu ya juu ya kiwango cha Chuo kikuu, msukumo utakuwa wa kuwa na chuo kikuu kwa kila mkoa ifikapo mwaka 2050. Katika hili, uchochezi wa kupanuka kwa sekta ya kilimo utajumuisha watu binafsi, taasisi za kidini na jumuiya za maendeleo za mikoa.
Jukumu la Serikali kuu litakuwa ni kuratibu mfumo wa elimu na si kuendesha kila kitu kuhusiana na Elimu. Chini ya mpango huu, Serikali Kuu itasaidia kwa kipindi cha miaka minne kwa shule na vyuo kujijenga na uendeshaji wake na baada ya hapo, jukumu litakuwa katika Serikali ya mitaa na jamii kuhakikisha kuwa wajibu wa kuziendesha shule na vyuo hivi havitegemei Serikali kuu pekee.
Serikali kuu itakuwa tayari kutoa msaada na ushauri. Serikali kuu itajenga mfuko na mfumo mpya wa mikopo ya Wanafunzi na kuachana na bodi ya mikopo ya Wanafunzi iliyoko sasa hivi ambayo ni kero kwa wananchi na wanafunzi.
Matarajio ya mpango huu wa elimu ni kuwa kwa kusogeza mchakato mzima wa elimu kwa mamlaka za mikoa, zitasaidia ile dhamira ya kusukuma madaraka mikoani, wananchi wa mikoa na wilaya watapata fursa sawa na wale walioko katika mikoa mingene ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikinufaika kwa kuwepo kwa kila aina ya shule na vyuo.
Msisitizo utakuwa katika elimu ambayo itazalisha watu ambao wako tayari kufanya kazi. Fani kama uhunzi, uashi, useremala, ufundi mchundo, bwana shamba, bwana maji, fundi umeme, magari, na ujenzi zitaongeza idadi ya watu wenye ujuzi si wa asili na kuvumbua binafsi, bali kwa kupata mafunzo na nyenzo za kuboresha vipaji asili katika fani hizo.
Tutakapoweza kuwa na msingi bora wa elimu ambayo utaongeza maarifa na kuchochea juhudi za kila mmoja wetu na kuhakikisha kuna ushiriki wa kila mmoja na kila mmoja ana nafasi ya kuwa bingwa katika fani yake, masuala kama ukosefu wa ajira au kukosekana kwa walio na utaalamu katika fani mbali mbali utapungua.
Lakini hatutaweza kufanikisha azma ya kuwa na mfumo na elimu bora ikiwa maslahi na vitendea kazi vya waalimu na shule zetu vitaendendelea kuwa duni na dhaifu, huku Serikali ikifumbia macho na kusukuma wajibu huo kwa Wananchi, Waalimu na uongozi wa shule na vyuo hivi. Suala la maslahi ya waalimu nitaliongelea kwa mapana na marefu katika kipengele cha Ujira, Mishaharana maslahi ya Wafanyakazi.
itaendelea...
Mch. Ningependa uongezee kipengele cha LUGHA katika sehemu ya ELIMU. Hii nikutokana na ukweli kwamba lugha ndio inatumika kuhifadhi au kubeba ufahamu (knowledge) kutoka sehemu moja kwenda nyingine. mfano kutoka kwa mwalimu kwenda kwa mwanafunzi na kinyume, kutoka kwenye vitabu kwenda kwa mwalimu au mwanfunzi. n.k
Kwa mantiki hiyo, lugha inabidi ipewe msisitizo MAALAMU katika sera ya elimu. Kwa maoni yangu, Tanzania ni Lazima tujifunze na kujua kwa ufasaha angalau lugha mbili, kiswahili na kingeereza. Hii itawawezesha waTanzania kuchota ufahamu mwingi ambao tayari upo katika lugha ya kiingereza bila kutegemea wakalimani nk na wakati huo huo kuendelea kuwa na identity yetu kupitia lugha ya Kiswahili.
kwa mtazamo wangu, tatizo la lugha Tanzania ni KUBWA na lenye mizizi mirefu ndani ya jamii, kuliko watuwengi wanavyo dhani, na suluhisho lake linahitajika haraka!
Asante.
Selemala.
Selemala,
Kirutubisho kikubwa ambacho tumekipuuza na sikukiweka kwa makusudi hapa n ihiki ulichokileta cha lugha.
Ubaya mmoja ambao unaleta mgawanyiko ni ile hisia kwa ili Tanzania iendelee na kufana katika nyanja za kimataifa, ni lazima kila kitu kifanywe na kufundishwa kwa lugha ya Kiingereza.
Najiuliza iweje Mchina, Mjapan, Msweden, Mrusi, Mjerumani, Mturuki, Muajemi wa Iran, Mkorea, Mgiriki, Muargentina na wenginewe, waendelee mbele kwa kujifunza mambo kwa kutumia lugha zao kuu za asili na si lugha ya pili?
Iweje sisi Watanzania na hata Waafrika wengine kwa ujumla, tuhenyee na kuhemea kwa kuongea Kiingereza, Kifaransa, Kiarabu na Kireno ambazo ni lugha za pili na si mama ili tuwe na mwamko wa kutoa elimu na mafunzo?
Kiingereza ni lugha ya pili ukiondoa Kiswahili ambacho tumekifanya kuwa ni lugha kuu na kila Mtanzania anakielewa na ana uwezo wa kusoma na kuandika.
Kwa nini hatufanyi mapinduzi ya nguvu ya kujivunia tulichonacho na kukimbilia kudai ni lazima tujue kukoroga yai na kuongea ung'eng'e na umombo ili tuonekane tuna uwezo katika nyanja za kimataifa?
Laiti Watanzania na viongozi wao wangejua kuwa tungemfundisha mwanafunzi wa Tanzania masomo ya sayansi, biashara, utawala, sanaa na mengineyo kwa kutumia Lugha aliyo na uwezo nao na mamlaka nayo, tungekuwa tumepiga hatua sana kuleta jamii inayojitegemea na bunifu.