Marekani yasema hakuna kusitisha vita. Nchi za kiarabu zasema hakuna kuhama. Wapalestina wasema bora kufa ndani ya majumba yao. Safari hii ni tofauti

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,551
11,607
Mpaka jana (tarehe 23 Oktoba) raisi Joe Biden wa Marekani ameendelea na msimamo wake kwamba hataki mashambulizi ya Israel yasimamishwe huku madhambulizi hayo yakizidi kuongezeka na kuzidi kuuwa watu.

======

'Then we can talk': Biden says no ceasefire in Israel-Hamas war until hostages released

Kwa upande wao nchi za kiarabu kwa sauti moja zimesema hakuna kuhama kwa wapalestina kutoka ardhi zao.Wamekumbusha kuwa tayari kuna maazimio ya kuundwa kwa taifa la wapalestina.Hilo taifa litaundwa na nani na wapi kama wapalestina watahamishwa kutoka ardhi zao.

Arab states say Palestinians must stay on their land as war escalates

Hayo yakitokea wapalestina waliowahi kutiii agizo la kuhama maeneo ya kaskazini ya Gaza ili kwenda kusini wameamua kurudi walikotoka wakitoa matamko kuwa ni bora kufa kuliko dhiki wanazozipata huko walikokwenda.Mashambulizi yamewafuata huko huko na wamejikuta wameishiwa na mahitaji yote.Kwa hali hiyo wameona warudi walikotoka ili kufukua visima vya maji japo yenye chumvi wanavyovikumbuka .

Upande wa jeshi la Israel kumeonekana kuwepo kwa msuguano mkubwa baina ya waziri mkuu,Benjamin Netanyahu na waziri wa ulinzi uliopelekea hapo jana kujitokeza kwa pamoja kukanusha habari hizo.Waziri wa ulinzi,Gallant amehimiza jeshi liingie Gaza kwa haraka kwani vijana wameanza kuchoka kusubiri na hamasa zao zimeanza kupomoroka.Waziri mkuu kwa mbinu zake za kivita anasema kuingia Gaza kutafungua lango jengine la mapigano upande wa kaskazini kutoka kwa Hizbulah.

Israel’s military push for Gaza invasion in apparent rift with Netanyahu


1698122442013.png
 
Saizi lazima wapate suluhisho la kudumu, ila sahizi nimependa umoja wa waarabu, wamegoma kutumika kipuuzi, na hio ndio imefanya mambo yawe magumu kwa USA na Israel
Huwezi kutumia mbinu hiyo hiyo ya ukandamizaji miaka nenda rudi.Lazima itagundulika na ndicho kimeitia kizunguzungu Israel.
Haya sasa Misri hafungui mpaka kuhama wapalestina wala kuwaokoa wenye uraia wa Marekani. Wapalestina nao wanarudi makwao.Watauwa kwa mabomu mpaka lini.Huko nje kila nchi kuna upinzani kwa kianchofanywa na Israel
 
Mtu Muhimu sana ni King Hassan wa Jordan kakataa Palestina wasiondoke pamoja na Misri, Saudia haya mataifa Marekani na Israel wanayaogopa sana.
Ni mfalme Abdalla mtoto wa king Hussein.Alitayarishwa zamani awe kibaraka daima.Sasa anaanza kuwageuka baada ya ubinadadamu kumrudia.
Huyu ni muhimu sana kwao.Akisema basi ndio itakuwa basi.
 
Back
Top Bottom