Marafiki wa kweli ni wa utotoni

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,902
Usiumizwe sana na marafiki wa ukubwani
Usiwaamini sana marafiki wa ukubwani
Wachache sana huwa wakweli na wasio na agenda kificho
Marafiki wa kukutana high school
Marafiki wa kukutana vyuoni
Marafiki wa kukutana makazini
Marafiki wa kukutana ukubwani kwenye biashara, uchumba nknk.. Si marafiki halisi bali ni marafiki kwa sababu fulani

Hawa ni mpaka mkae muda mrefu sana pamoja kwenye hali zote shida na raha, kukosa na kupata, kuumia na kuumizwa! Wengi wao rangi zao halisi hujifunua huku!

Rafiki uliyekua naye mkasoma wote shule ya msingi, mkacheza pamoja, mkachunga pamoja,mkalima pamoja mkatembeleana, mkacheka pamoja mkalia pamoja, familia zenu zinafahamiana ndugu zenu wanafahamiana.. Hawa ndio huwa marafiki wa kweli kwakuwa bond wanayoijenga huwa na vyanzo vingi.. Hawadahauliani na ni vigumu mno kusalitiana!

Tunakutana na watu wapya kila siku, wema na wabaya! Na wabaya waliojificha kwenye joho la wema! Sio dhambi kuwa na marafiki wapya! Maisha ni watu bila watu hakuna maisha ama maisha yanakuwa hayana maana!

Rai tangu ni hii kuwa makini sana unapochagua marafiki wa ukubwani.. Wengi ni marafiki wa agenda.. Wengi ni marafiki kwa sababu . Agenda ikiisha/ikifa ama sababu ikikoma na urafiki nao hufika tamati

Ninao marafiki wengi na ninawaamini sana ila baadhi wameniachia makovu .. Siumii kwakuwa natambua marafiki wa kweli ni wale wa utotoni

648a99c703d1bd428c291d6eaf56de1d.jpg
 
Usiumizwe sana na marafiki wa ukubwani
Usiwaamini sana marafiki wa ukubwani
Wachache sana huwa wakweli na wasio na agenda kificho
Marafiki wa kukutana high school
Marafiki wa kukutana vyuoni
Marafiki wa kukutana makazini
Marafiki wa kukutana ukubwani kwenye biashara, uchumba nknk.. Si marafiki halisi bali ni marafiki kwa sababu fulani

Hawa ni mpaka mkae muda mrefu sana pamoja kwenye hali zote shida na raha, kukosa na kupata, kuumia na kuumizwa! Wengi wao rangi zao halisi hujifunua huku!

Rafiki uliyekua naye mkasoma wote shule ya msingi, mkacheza pamoja, mkatembeleana, mkacheka pamoja mkalia pamoja, familia zenu zinafahamiana ndugu zenu wanafahamiana.. Hawa ndio huwa marafiki wa kweli kwakuwa bond wanayoijenga huwa na vyanzo vingi.. Hawadahauliani na ni vigumu mno kusalitiana!

Tunakutana na watu wapya kila siku, wema na wabaya! Na wabaya waliojificha kwenye joho la wema! Sio dhambi kuwa na marafiki wapya! Maisha ni watu bila watu hakuna maisha ama maisha yanakuwa hayana maana!

Rai tangu ni hii kuwa makini sana unapochagua marafiki wa ukubwani.. Wengi ni marafiki wa agenda.. Wengi ni marafiki kwa sababu . Agenda ikiisha/ikifa ama sababu ikikoma na urafiki nao hufika tamati

Ninao marafiki wengi na ninawaamini sana ila baadhi wameniachia makovu .. Siumii kwakuwa natambua marafiki wa kweli ni wale wa utotoniView attachment 2519891
Sisi wa geti kali tusemeje sasa 🌬️🤣🤣

Ila una point nxuri
 
Mna marafiki pia kwa rank yenu
Duuuh mimi nilipokulia hamna aseee ni mtoto pekee kwenye familia mkuuu sina rafiki yeyote wa utotoni sijui kucheza michexo ya kombolela sijui makaraa hiyo naisikiaga tu kwa watu mm ni midoli na magari ya kitoto tu ndo ninayoijua nina rafiki 1 tu wa kweli nimesoma nae from form 1 to form 6 basi combi sawa kila kitu sawa chuo tu ndo tumepotezana yupo mbeya mi nipo dar yeye pekee ndio ninaeweza kumchuja hapa tumetoka mbali sana kwenye maisha ya shule mawasiliano hayakauki
 
Duuuh mimi nilipokulia hamna aseee ni mtoto pekee kwenye familia mkuuu sina rafiki yeyote wa utotoni sijui kucheza michexo ya kombolela sijui makaraa hiyo naisikiaga tu kwa watu mm ni midoli na magari ya kitoto tu ndo ninayoijua nina rafiki 1 tu wa kweli nimesoma nae from form 1 to form 6 basi combi sawa kila kitu sawa chuo tu ndo tumepotezana yupo mbeya mi nipo dar yeye pekee ndio ninaeweza kumchuja hapa tumetoka mbali sana kwenye maisha ya shule mawasiliano hayakauki
You have a stolen past
af04ede45ec5df2dc9e9fd4821ac790b.jpg
a9d9adf8ceb05ce11ae3cc8d04661feb.jpg
 
Ambae hajawahi kuchezea mvua daaah utoto kazi kweli kweli

Nakumbuka pale Mkapa Export kabla hapajawekwa ukuta kulikua na minara ya mawasiliano sasa ukipita km unaenda Mabibo hostel kulikua na vichaka kulikua na matunda poli fulani hivi enzi hizo tupo watoto watoto tulikua tunayafuata matamu kishenzi daah sasa hivi hakuna poli pale 😂
 
Ambae hajawahi kuchezea mvua daaah utoto kazi kweli kweli

Nakumbuka pale Mkapa Export kabla hapajawekwa ukuta kulikua na minara ya mawasiliano sasa ukipita km unaenda Mabibo hostel kulikua na vichaka kulikua na matunda poli fulani hivi enzi hizo tupo watoto watoto tulikua tunayafuata matamu kishenzi daah sasa hivi hakuna poli pale
Zilipo Mabibo hostel yalikuwa ni mashamba ya mpunga
 
Kwa sisi wa vijijini, ni raha ilioje unaporudi Kijijini na kukutana na marafiki wa utotoni.
Yaani mkikutana jioni kwenye moja moto moja baridi hapo pesa huwaga haina thamani tena.
Ni furaha stori na vicheko kwenda mbele.

Poleni sana mliokulia kwanye mageti.
Laiti wakati ungekuwa na rivasi... Muda ungerufunulia mengi tuliyopitia yakatujengea bond isiyokatika.. If i could turn back the time!
 
Umenena vyema mkuu..."mchizi wa kweli unamfaham ndani ya mboni,macho hayafichi ukweli ni kama skendo mtaan mob" (mabovu)...

Nimesoma na wengi,
Nimejuana na wengi
Wengi ni wanafiki hata njia zao naziona..

Nimerudi home ndo nagundua wa kweli ni wapi?
 
Rafiki ndio ndugu unabidi kuhakikisha unapata wa kweli mmoja ,wawili au watatu na wanne ..


Mimi nilipata rafiki Chuoni niseme huyu Jamaa namkubali Sana kuzidi Hadi ndugu zangu wote wa ukoo mzima achilia mbali wazazi



Huyo Mwamba ni rafiki yangu wa ukubwani ukitoa JF anafata yeye.
 
Back
Top Bottom