Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,634
- 697,902
Usiumizwe sana na marafiki wa ukubwani
Usiwaamini sana marafiki wa ukubwani
Wachache sana huwa wakweli na wasio na agenda kificho
Marafiki wa kukutana high school
Marafiki wa kukutana vyuoni
Marafiki wa kukutana makazini
Marafiki wa kukutana ukubwani kwenye biashara, uchumba nknk.. Si marafiki halisi bali ni marafiki kwa sababu fulani
Hawa ni mpaka mkae muda mrefu sana pamoja kwenye hali zote shida na raha, kukosa na kupata, kuumia na kuumizwa! Wengi wao rangi zao halisi hujifunua huku!
Rafiki uliyekua naye mkasoma wote shule ya msingi, mkacheza pamoja, mkachunga pamoja,mkalima pamoja mkatembeleana, mkacheka pamoja mkalia pamoja, familia zenu zinafahamiana ndugu zenu wanafahamiana.. Hawa ndio huwa marafiki wa kweli kwakuwa bond wanayoijenga huwa na vyanzo vingi.. Hawadahauliani na ni vigumu mno kusalitiana!
Tunakutana na watu wapya kila siku, wema na wabaya! Na wabaya waliojificha kwenye joho la wema! Sio dhambi kuwa na marafiki wapya! Maisha ni watu bila watu hakuna maisha ama maisha yanakuwa hayana maana!
Rai tangu ni hii kuwa makini sana unapochagua marafiki wa ukubwani.. Wengi ni marafiki wa agenda.. Wengi ni marafiki kwa sababu . Agenda ikiisha/ikifa ama sababu ikikoma na urafiki nao hufika tamati
Ninao marafiki wengi na ninawaamini sana ila baadhi wameniachia makovu .. Siumii kwakuwa natambua marafiki wa kweli ni wale wa utotoni
Usiwaamini sana marafiki wa ukubwani
Wachache sana huwa wakweli na wasio na agenda kificho
Marafiki wa kukutana high school
Marafiki wa kukutana vyuoni
Marafiki wa kukutana makazini
Marafiki wa kukutana ukubwani kwenye biashara, uchumba nknk.. Si marafiki halisi bali ni marafiki kwa sababu fulani
Hawa ni mpaka mkae muda mrefu sana pamoja kwenye hali zote shida na raha, kukosa na kupata, kuumia na kuumizwa! Wengi wao rangi zao halisi hujifunua huku!
Rafiki uliyekua naye mkasoma wote shule ya msingi, mkacheza pamoja, mkachunga pamoja,mkalima pamoja mkatembeleana, mkacheka pamoja mkalia pamoja, familia zenu zinafahamiana ndugu zenu wanafahamiana.. Hawa ndio huwa marafiki wa kweli kwakuwa bond wanayoijenga huwa na vyanzo vingi.. Hawadahauliani na ni vigumu mno kusalitiana!
Tunakutana na watu wapya kila siku, wema na wabaya! Na wabaya waliojificha kwenye joho la wema! Sio dhambi kuwa na marafiki wapya! Maisha ni watu bila watu hakuna maisha ama maisha yanakuwa hayana maana!
Rai tangu ni hii kuwa makini sana unapochagua marafiki wa ukubwani.. Wengi ni marafiki wa agenda.. Wengi ni marafiki kwa sababu . Agenda ikiisha/ikifa ama sababu ikikoma na urafiki nao hufika tamati
Ninao marafiki wengi na ninawaamini sana ila baadhi wameniachia makovu .. Siumii kwakuwa natambua marafiki wa kweli ni wale wa utotoni