Maoni ya wanasheria kuhusu tukio la Makonda

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
TUNDU LISSU

Mwanasehria Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, alisema mkuu wa wilaya ana mamlaka ya kuamuru mtu aliyefanyakosa mahali ambako hakuna polisi akamatwe.

Kama kuna polisi kwenye eneo la kosa hayo mamlaka hawezi kuwa nayo, na kama akitoa amri hiyo atakuwa anawajibika kutoa maelezo na sababu za kumkamata mtu huyo kwa hakimu wa wilaya.

"Alichokifanya DC wa Kinondoni ni uvunjaji wa sheria na tutamshughulikia hadi ataikimbia hiyo wilaya," alisema Lissu.

KIBATALA

Akizungumzia kuhusu mamlaka ya mkuu wa wilaya kutoa amri ya kukamatwa mbunge, mwanasheria Peter Kibatala alisema amefurahi kutokea kwa kesi hiyo na anaomba suala hilo kwenda mahakamani kama shtaka la jinai.

Alisema kesi hiyo itasaidia kuhoji mamlaka ya mkuu wa wilaya na namna ambavyo anayatekeleza.

"Vyovyote iwavyo lazima tuhakikishe tunawasilisha malalamiko kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ili kupata uamuzi wa nini hasa mipaka kati ya serikali na maafisa wake na wabunge hasa wa upinzani," alisema Kibatala.

FREDERICK KIHWELO

Kwa upande wake mwanasheria wa mbunge huyo, Frederick Kihwelo alisema jambo la msingi katika suala hilo ni kuhakikisha cheo hicho kinaondolewa ili kiweze kuwaacha polisi wafanye kazi zao kwa uhuru.

"Inasikitisha kuona mkuu wa wilaya ni kada wa CCM, mjumbe wa siasa wa wilaya wa CCM na ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hivyo ni bosi wa OCD na ofisa usalama wa wilaya," alisema.

Aliwataka wale waliopewa mamlaka hayo kuhakikisha wanatumia mamlaka hayo kwa busara badala ya kutumia nguvu na jeuri.
 
Yangu ni macho na masikio kuona nini kitatokea kuhusu huyu DC dictetor
 
TUNDU LISSU

Mwanasehria Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, alisema mkuu wa wilaya ana mamlaka ya kuamuru mtu aliyefanyakosa mahali ambako hakuna polisi akamatwe.

Kama kuna polisi kwenye eneo la kosa hayo mamlaka hawezi kuwa nayo, na kama akitoa amri hiyo atakuwa anawajibika kutoa maelezo na sababu za kumkamata mtu huyo kwa hakimu wa wilaya.

"Alichokifanya DC wa Kinondoni ni uvunjaji wa sheria na tutamshughulikia hadi ataikimbia hiyo wilaya," alisema Lissu.

KIBATALA

Akizungumzia kuhusu mamlaka ya mkuu wa wilaya kutoa amri ya kukamatwa mbunge, mwanasheria Peter Kibatala alisema amefurahi kutokea kwa kesi hiyo na anaomba suala hilo kwenda mahakamani kama shtaka la jinai.

Alisema kesi hiyo itasaidia kuhoji mamlaka ya mkuu wa wilaya na namna ambavyo anayatekeleza.

"Vyovyote iwavyo lazima tuhakikishe tunawasilisha malalamiko kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ili kupata uamuzi wa nini hasa mipaka kati ya serikali na maafisa wake na wabunge hasa wa upinzani," alisema Kibatala.

FREDERICK KIHWELO

Kwa upande wake mwanasheria wa mbunge huyo, Frederick Kihwelo alisema jambo la msingi katika suala hilo ni kuhakikisha cheo hicho kinaondolewa ili kiweze kuwaacha polisi wafanye kazi zao kwa uhuru.

"Inasikitisha kuona mkuu wa wilaya ni kada wa CCM, mjumbe wa siasa wa wilaya wa CCM na ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hivyo ni bosi wa OCD na ofisa usalama wa wilaya," alisema.

Aliwataka wale waliopewa mamlaka hayo kuhakikisha wanatumia mamlaka hayo kwa busara badala ya kutumia nguvu na jeuri.

huyu DC tutamgawana tu
 
"Inasikitisha kuona mkuu wa wilaya ni kada wa CCM, mjumbe wa siasa wa wilaya wa CCM na ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hivyo ni bosi wa OCD na ofisa usalama wa wilaya," alisema.

.
Mfumo wa chama kimoja - wakati tunajivuna eti tuna mfumo wa vyama vingi toka 1992.
 
Naona Tundu Lissu na wenzake wana wadanganya...! Matusi ya kubenea yalikuwa yanataka kuhatarisha amani na kuleta vurugu hivyo Paul Makonda alitumia busara ya hali ya juu kumuweka ndani(kumpumzisha) hata Lissu akileta ngebe atapumzishwa..!

Kubenea anapaswa kufunzwa jinsi ya kufanya kazi na serikali na kujua mipaka yake....
 
Last edited by a moderator:
Naona Tundu Lissu na wenzake wana wadanganya...! Matusi ya kubenea yalikuwa yanataka kuhatarisha amani na kuleta vurugu hivyo Paul Makonda alitumia busara ya hali ya juu kumuweka ndani(kumpumzisha) hata Lissu akileta ngebe atapumzishwa..!

Kubenea anapaswa kufunzwa jinsi ya kufanya kazi na serikali na kujua mipaka yake....
Umeoza na uCCM hata ufahamu wa kawaida huna/ eti mwanasheria? Huko huko Lumumba Tumeona maDR wa kichina toka Lumumba utakuwa wewe?
 
Nilitegemea kuona wanasheria tofauti tofaut. Ungewachukua hata wanasheria wa vyama vingine wazungumzie swala hilo. We need to understand one thing every side will defend accordingly so as to prove it is or was not their or his or her fault. Naomba mleta mada jaribu ku consult and other lawyers wanasemaje kuhusu hilo maana wapo wengi sio hao tu.
 
Naona Tundu Lissu na wenzake wana wadanganya...! Matusi ya kubenea yalikuwa yanataka kuhatarisha amani na kuleta vurugu hivyo Paul Makonda alitumia busara ya hali ya juu kumuweka ndani(kumpumzisha) hata Lissu akileta ngebe atapumzishwa..!

Kubenea anapaswa kufunzwa jinsi ya kufanya kazi na serikali na kujua mipaka yake....

Mpumbavu,mtu amekaa kutatua mgogoro toka asubuhi halafu eti aje kuhatarisha amani?Amani ya nani?Mbona wafanyakazi walikuwa watulivu?mahaba yako na ccm yatakuua kwa kushindwa kuona ukweli!
 
Last edited by a moderator:
TUNDU LISSU

Mwanasehria Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu, alisema mkuu wa wilaya ana mamlaka ya kuamuru mtu aliyefanyakosa mahali ambako hakuna polisi akamatwe.

Kama kuna polisi kwenye eneo la kosa hayo mamlaka hawezi kuwa nayo, na kama akitoa amri hiyo atakuwa anawajibika kutoa maelezo na sababu za kumkamata mtu huyo kwa hakimu wa wilaya.

"Alichokifanya DC wa Kinondoni ni uvunjaji wa sheria na tutamshughulikia hadi ataikimbia hiyo wilaya," alisema Lissu.

KIBATALA

Akizungumzia kuhusu mamlaka ya mkuu wa wilaya kutoa amri ya kukamatwa mbunge, mwanasheria Peter Kibatala alisema amefurahi kutokea kwa kesi hiyo na anaomba suala hilo kwenda mahakamani kama shtaka la jinai.

Alisema kesi hiyo itasaidia kuhoji mamlaka ya mkuu wa wilaya na namna ambavyo anayatekeleza.

"Vyovyote iwavyo lazima tuhakikishe tunawasilisha malalamiko kwa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ili kupata uamuzi wa nini hasa mipaka kati ya serikali na maafisa wake na wabunge hasa wa upinzani," alisema Kibatala.

FREDERICK KIHWELO

Kwa upande wake mwanasheria wa mbunge huyo, Frederick Kihwelo alisema jambo la msingi katika suala hilo ni kuhakikisha cheo hicho kinaondolewa ili kiweze kuwaacha polisi wafanye kazi zao kwa uhuru.

"Inasikitisha kuona mkuu wa wilaya ni kada wa CCM, mjumbe wa siasa wa wilaya wa CCM na ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hivyo ni bosi wa OCD na ofisa usalama wa wilaya," alisema.

Aliwataka wale waliopewa mamlaka hayo kuhakikisha wanatumia mamlaka hayo kwa busara badala ya kutumia nguvu na jeuri.

mbona kama haya maoni yote yametolewa na wanasheria wenye itikadi za vyama pinzani? mmpata na maoni ya wanasheria wa chama tawala na wasio na vyama?
 
Mfumo wetu ni mbovu, huu mfumo una faa kwneye nchi ambazo hazina vyama vingi, mfumo wetu unatakiwa ufumuliwe, kama tunahitaji wakuu wa Mikoa na wilaya basi kazi zao zitambulike na wasitumike kama manamba wa chama tawala au upinzani. Pili waondolewe kwenye kamati au ujumbe katika chama chochote, wao wabaki kuwa ni watendaji na wasimamizi wakuu katika wilaya au mikoa yao, hapo itakuwa rahisi kufanya kazi na chama tawala au upinzani. Kuna hatari kama ikiwa mkuu wa wilaya akifanya kazi za siasa, maana yeye ana chama, atafanya kila njia kufutini mbunge wa jimbo fulani , maana kila aendapo atakuwa amezungukwa na police, na tanzania yetu aliyezungukwa na police ndo huonekana mchap kazi, nyuma ya mkuu wa wilaya kuna mkuu wa mkoa-mwanasiasa, kuna waziri-mwanasiasa, kuna raisi-mwanasiasa, kuna mkuu wa police-manamba wa chama, Kwa mfumo huu wabunge hao tuliowachagua mnatarajia watatuletea maendeleo kweli?
 
Kesi hii imekuja wakati muafaka na naimani majukumu ya mkuu wa wilaya yatatafsiriwa kimahakama nakila mtu atajua wajibu wake.

Ikitokea kubenea kashindwa kesi na kuhukumiwa jela hatima yake ya ubunge itakuwaje?
 
Mpumbavu,mtu amekaa kutatua mgogoro toka asubuhi halafu eti aje kuhatarisha amani?Amani ya nani?Mbona wafanyakazi walikuwa watulivu?mahaba yako na ccm yatakuua kwa kushindwa kuona ukweli!
Nyau wewe, mbunge na mkuu wa wilaya, wajua tofauti zao kimamlaka?? Mpumbavu na lofa mkubwa wewe. Huyo Kubenea atakula uongo na matusi yake. Bahati yake Makonda ni mstaarabu na mwenye huruma sana, huyo mbunge alitakiwa ale kipondo cha haja kabla ya kuswekwa upango
 
Back
Top Bottom