MAONI: Shule za kata zifikiriwe upya

Pamoja na changamoto nyingi za vifaa na walimu, wanafunz hawasomi wanajamvi. Wako busy na simu na upuuz wa kila aina. Tunapaswa kwanza kuwaelimisha nidhamu ya kusoma. Ni disaster
 
Ndugu wanajamvi salaam,

Nimengi yamezungumzwa kuhusiana na shule za kata,
Shule ambazo serikali na ya sasa na chama chake imekuwa ikijinasibu kuwa imefanikiwa
kuleta mapinduzi makubwa ya kielimu kwa kujenga shule hizo kila kata,huku suala la walimu na nyumba zao likibaki kuwa halina ufumbuzi wa wazi.

Mwisho wa juma hili nilipanda daladala kwenda kimbiji,tuliondoka feri saa tatu na nusu,
Ndani ya dala dala kulikuwa na wanafunzi pia wa shule ya sekondari somangira,nikajiuliza hawa kwa muda huu wataenda kusoma nini?
Tulifika kama saa tano hivi wanafunzi walikuwa hoi,wamesweti njia nzima walikuwa wamesimama,mmoja alikuwa amevaa fulana imeandikwa "education for positive change" nikajiuliza which positive change????????????

Nikatafakari hivi watawala wetu na wanasiasa wanajua hatari inayolinyemelea taifa letu kwa kuendelea kuwa na shule hizi?nikawa na majibu mchanganyiko,nikaendelea na safari yangu,mwanafunzi wa mwisho alishuka kimbiji toka feri umbali wa kama saa moja na nusu au mawili.

Wakati narudi ilikuwa saa nane na nusu niliwakuta kituoni wanafunzi hao tena,wakapanda daladala lililokuwa limejaa wakasimama,nikajiuliza tena hii hali mpaka lini?nilimwuliza mmoja wao kuwa anakaa wapi akaniambia tandika,pia akasema wapo wanafunzi wengi wanakaa mjini,nikasema MUNGU WANGU!

Niliuliza tena mwaka jana f4 matokeo yalikuwaje?akasema hakukuwa na one wala div two,kati ya wanafunzi zaidi ya 100 three hazikuzidi tano wliobaki wachache 4 na wengi ziro.

Kwa ufupi hii ndo hali halisi ya shule zetu za kata,nimezunguka hata ktk shule nyingine mikoa mbalimbali hali haiko tofauti.

Nimetafakari sana nikajaribu kulingaisha na shule za wenzetu,ambazo kama si bording,basi watoto wanapelekwa na kurudishwa wakila na kunywa wanachotaka.
Watoto zaidi ya sitini kupata sifuri ni hatari kwa ustawi wa Taifa,
CCM itaondoka lkn Tanzania itabaki,

Wanajamvi na watanzania hili Taifa ndo ccm inataka kutuachia ikishaondoka madarakani?Au ndo inalijenga ikiendelea kuwa madarakani?
Vyama mbadala mpo?mnaiona nchi inavyo uliwa?

Tafadhari nawaomba waungwana tuisaidie hii roho ya nchi,wanasiasa hawa ndo wapiga kura wenu wa kesho,hawa ndo tutawatumia kuondoka na umaskini lkn wamepoteza miaka 4 na kutoka bila kitu kichwani.

Pia rafiki zetu wanaojiandaa kufungua matawi ya ccm NYC,nao tunaomba msaada wao wa kimawazo.Suala la elimu si lakungoja mtoto akishamaliza f4 nikazi kubwa tena kumrudisha aanze upya tunapoteza rasilimali kubwa ya Taifa,tunaua vipaji jambo ambalo ni hatari kubwa kwa ustawi wa nchi yetu

Ebu tutoe maoni kwakuwa serikali sikivu inapita humu inaweza ikayafanyia kazi,watoto wa walala hoi wanaenda shule kukua na wanatoka f4 mikono mitupu.

Naomba kuwasilisha.
 
Kama kweli una malengo mazuri ya mtoto wako, kuliko umpeleke shule ya kata bra ukae nae nyumbani, umsomeshe mwenyewe na aende shule kufanya mitihani tu, maana atafaulu zaidi kuliko akaenda hapo toka asubuhi akila na kuuza ubuyu wa mwalimu, wakishinda kufagia majengo hayo yaliyochakaa kabla ya muda, maana kifupo hakuna kusoma.

hebu angalia matokeo yao ya kidato cha nne, ndio utapata jibu la kuwepo kwa hizo shule za ccm (shule za kata), lengo lao kubwa ni kuhakikisha watoto wa masikini wanabaki kuwa masikini, hawafanikiwi katika elimu so hawatofanikiwa katika maisha. kama kweli wangelikuwa na lengo la kuwainua watoto wa masikini katika hizo shule za kata, wangeweka kila kitu muhimu, na wangewapeleka watoto wao wasome huku kama mfano.............
 
Afadhali umeliona hili.
Kuna wakati niliwahi kuandika kwa mtazamo tofauti kidogo. Mimi nilisema kuwa shule za kata ni jela kwa watoto wa mkulima.
Huo mfano ni wa huko mjini ambako tunatarajia kuna kila kitu. Sasa kumbe hata huko hamna kitu.
Embu fikiria mtoto aliyezaliwa pale kijijini, akaanza shule ya awali ya pale pale kijijini kwao. Kama ana bahati sana atakuwa amesoma nursery ya kanisa ambayo anagalao wanaweza hata kupewa uji pale! Anaanza shule darasa la kwanza pale pale kwao! anamaliza anajiunga na shule ya kata palepale kwao. Hajawahi hata siku moja kufika kunakoitwa mjini wala hajui huko ni wapi! Sanasana akiugua ndo ataenda mbali kwenye zahanati ya kijiji cha jirani kupata tiba na kurudi. Afadhali na siku hizi wamerudisha sera ya michezo labda wanaweza kutoka kucheza na shule ya jirani! Akimaliza hapo ashukuru kama atachaguliwa kwenda high school mbali na hapo (kama yupo atakayefaulu) vinginevyo sasa wengine wanajiandaa kufungua vyuo vya kata ili watoto wao waende pale! Huyo ndiye mtaalamu tunayemtegemea! Aliyekulia kwao pale na sasa anaondoka kwenda kutafuta kazi baada ya kutumikia nusu ya maisha yake pale kijijini kwao! Unamtegemea kweli huyu! Yeye kwake computer anafananisha na TV! Akipanda basi anataapika maana hajawahi hata siku moja kupanda gari liendalo kasi!
Pamoja na sera nyingine mbovu za baba wa Taifa hili lakini nasifu sana sera yake ya kuwapeleka wanafunzi sehemu mbalimbali za Tanzania. nakumbuka unamaliza darasa la saba unapelekwa Songea boys toka Kilimanjaro! na utafika! Kule utakutanza na Msukuma na mhaya na mwingine. Then mnacreate network fulani. Ukienda Iringa unakutana na kijana uliyesoama naye pale Old Moshi secondary! Maisha yanaenda, unakuwa sio mgeni sana! Angalao unajua wahaya wanaishi hivi. Sasa hata mmasai wa Longido hajui Mwarusha anaishi vipi!
Mimi nalzimika kuamini kuwa nafasi ya mtoto wa mkulima haipo tena kuridhi kazi yoyote hapa Tanzania. Kama kwa sasa tu nafasi nyetu kwenye idara nyeti zenye mishahara nyeti ni kwa watoto wa wakubwa tu ambao wengi wao ni mbumbumbu wa kutupwa! unategemea nini kwa hawa watoto wa shule za kata ambao wafundishwa na waalimu wawili wakizidi ni watatu!
Hizi ndizo JELA za watoto wa wakulima! Wasije huku watoto wao waliko wakachafue hali ya hewa! Angalia kwa mfano aliyeshika nafasi ya kwanza form 6 ni mtoto wa mkulima mwenye ngombe 2 tu wa maziwa. Kama tukiwathamini hawa watoto wa wakulima naamini kuna vipaji vingi sana vimefukiwa kijijini ambavyo vingeweza kuliinua taifa hili.
Kuna binti mmoja nilikutana naye kule kijijini, alikuwa hajui kuwa chuo kikuu lazima uende ukaupload forms kenye computer then ujaze, uombe mkopo nk,nk. Yeye akawa anasubiri aitwe chuo kikuu. By the time anakuja kugundua it was too late. Hana hiyo elimu! Ilibidi tumpatie ajira ya kufundisha mwaka ulofata ndo akaomba chuo!
Amini msiamini watakaotoka huku sekondari za kata ni wawili kati ya mia na hawa ni kama msamaha wa rais!
Tunaitaka serekali ibadilishe mfumo huu wa sasa!
 
Naungana na muleta hoja na wachangiaji wote kuwa shule za kata ni tatizo. Naomba nitoe angalizo kuwa tusiwe na mtazamo hasi tu bali tuzione kuwa zinaweza kuwa ni nyenzo nzuri ya kutusogeza mbeme. Tusisahau tulikotoka: kumbuka azimio la UPE, ktk azimio hili wale waliokuwa wamemaliza drs laa 7 waliitwa kufundisha shule za msingi na wanavijiji walihizwa kujenga madarasa- naskumbuka nulisoma drs la 1 kwenye jengo la udongo lililoezekwa kwa nyasi na hivi sasa ni degree2. Kule india wamefanya maendeleo makubwa ktk elimu kwa kuwa na shule km hizi za kata, wao hawakuishia hapo bali walifanya hivihivi hata kwa taasis za elimu ya juu. Kwa maoni yangu huu ni wakati muafaka kupendekezza nini kifanyike na si kubeza tu kwani sehemu kubwa ya hawa wanaoenda shule za kata hawana option nyingine.
 
Ndo mana nasema kama jamvi la watu wenye fikira pevu,
tushauri watawala wasijetuachia taifa la mazumbukuku.

Natunawaomba wenzetu walioko nje mfano rafiki yetu anaye
taka kufungua tawi NYC,nakumwalika Kikwete kwenda kulifungua,
ajue huku nyumbani mambo ni mabaya,hiyo pesa ya msafara
aitume isaidie kujenga nyumba angalau mbili za walimu.

Lakini pia ilikuwa vyema kuziunganisha hizi shule
ili angalau ktk tarafa kuwe na shule ya bweni.

OLE WENU WANASIASA MNAOANGAMIZA TAIFA LETU.
 
Gama unapotaka kufanya biashara ama shughuli yoyote lazima ufanye kitu inaitwa visible study! Kwanza tunasema hawa lengo lao halikuwa baya bali walikurupika! Walocpy mahala na wakapaste hapa! Unafungua shule huna manpower unaita shule! Umeandaa walimu wa kutosha! Matokeo wakaleta walimu vodafasta!
Pamoja na kutaka watoto wa wakulima wapate elimu! Walitakiwa waweke nayo mazingira ya kusoma yawe ya uhakika.
Hata hawa wazazi wakihamasishwa kujenga mabweni wanaweza kuitikia wito na wakajenga lakini hawawezi kupata waalimu!
Wanapeleka waalimu watoto ambao akisimama na mwalimu hakuna nidhamu maana vijana hawa kutongozana sio ajabu! Yaani walikuwa nao juzi tu kamaliza kapelekwa vodafasta anarudi anataka kumfundisha huyu reproduction! Wakati ashakum sio matusi weshavuliana nguo!
Mimi sina hiyana sana ila serikali nayo itimize wajibu wake. Ipeleke walimu wa kutosha huku kwenye kata na pia tuhamasishe mazingira mazuri ya kusoma na kwa walimu wapewe mazingira ya kufanya kazi. Kuna walimu najua wanaka over 35km na wanaenda na kurudi kwao kila siku. Atafundisha saa ngapi huyu! Unamkuta saa tatu na nusu mpaka saa nne ndo anatokwa na mijasho anawahi kipindi! Atafundisha kweli! ama atapiga blah blah siku iende akakamue ngombe ya mwenzawazimu mwisho wa mwezi!
 
Naungana na muleta hoja na wachangiaji wote kuwa shule za kata ni tatizo. Naomba nitoe angalizo kuwa tusiwe na mtazamo hasi tu bali tuzione kuwa zinaweza kuwa ni nyenzo nzuri ya kutusogeza mbeme. Tusisahau tulikotoka: kumbuka azimio la UPE, ktk azimio hili wale waliokuwa wamemaliza drs laa 7 waliitwa kufundisha shule za msingi na wanavijiji walihizwa kujenga madarasa- naskumbuka nulisoma drs la 1 kwenye jengo la udongo lililoezekwa kwa nyasi na hivi sasa ni degree2. Kule india wamefanya maendeleo makubwa ktk elimu kwa kuwa na shule km hizi za kata, wao hawakuishia hapo bali walifanya hivihivi hata kwa taasis za elimu ya juu. Kwa maoni yangu huu ni wakati muafaka kupendekezza nini kifanyike na si kubeza tu kwani sehemu kubwa ya hawa wanaoenda shule za kata hawana option nyingine.

Mkuu Gama nikweli kabisa hatutakiwi kuwa na mtizamo hasi,na ksudi si kubeza.
Jambo ambalo tunatakiwa tulitambue nikuwa suala la elimu sila majaribio,
Mfano unapoanzisha masomo ya sayansi lazima uhakikishe una maabara na walimu wa kutosha,
Kitu cha kwanza ni walimu,huwenzi kuanza na wanafunzi then walim,
Mwanafunzi akianza masomo ndo kaanza,akifika f2 huwezi kumrudisha tena asome masomo ya
F1 wakati huohuo anasoma masomo ya f2.

Hatukatai kuanza na kuboresha bdy,tunachokataa ni kuanza bila maandalizi
Wenzetu watoto wao wakilalamikia matatizo ktk shule wanazosoma wanawahamisha mara moja
Lakini maskini walala hoi wa kata hata pale wakiomba wahamie shule zilizo karibu na wanakoishi wanawekewa
vikwazo kibao.

Kama shule binafsi wanatakiwa kufanya maandalizi yote kabla ya kufungua shule,
Basi na serikali ionyeshe mfano.
 
mimi ni mwl ktk hzo shule za kata ktk manispaa flani mambo yaliyoko huko acha tu nyingi zina miaka mitano lakini tayari madarasani ni vumbi sakafu zishaharibika hamna milango. Kwa upande wa walimu shule hazina vifaa vya kufundishia hata vitabu tunaazima ili tutoe photocopy huwezi linganisha na shule tulizosoma miaka ya tisini mwishoni kama umbwe, usagara ,pugu na za/aina hiyo serikali imezitosa kabisa shule za kata. Pia walimu wachache waliopo wanatumia muda mwingi ktk ofisi za halmashauri kudai stahili zao na hii inatokana na uzembe wa serikali.
Kutokana na uwepo wangu kama mwalimu ktk shule za kata nimegundua haya:-
Wanafunzi ktk shule za kata wengi ni watoto wa maskini na watu wa hali ya chini ada ya elfu 20 kwa mwaka wazazi wengi inawapa tabu kulipa so capitation fund inakuwa ndogo, wazazi wengi wameshindwa kuwanunulia watoto wao madawati au mchango wa madawati elfu 40 so wengine wamekuja na stuli au wanakaa chini kwa sababu shule hazina madawati na hiyo hali ya kukaa chini inafanya zoezi la kutoa elimu kuwa gumu na inaencourage utoro, pia wazazi wameshindwa kuwanunulia watoto wao vitabu wanabakia kumtegemea mwalimu ambaye na yeye ashachoshwa na hali yake ya maisha ashachukia kazi yake hence perfomance inakuwa chini.
Kuna ulaji mkubwa wa pesa kidogo zinazotengwa na halmashauri na zile za serikali kuu almost sehemu kubwa ya nchi kumekuwa na mtandao wa ulaji wa pesa kati ya maafisa elimu na wakuu wa shule so kuna walimu ambao hawana uwezo wa kuongoza wamepewa shule sababu ya maslahi binafsi ya maafisa elimu hela ya capitation haitumiki ipasavyo, ktk hizi shule hamna wataalamu wa masuala ya fedha waliojariwa so ni walimu wenyewe wanafanya hhiyo kazi hesabu haziandaliwi ipasavyo na pesa kidogo ambayo inapatikana haileti maendeleo ila inaishia kwa wajanja wachache.
Suala la nidhamu ktk shule za kata ni tatizo nidhamu iko chini saana na bila nidhamu kufundishika ni vigumu na ukosefu wa nidhamu shuleni na madarasani unasababishwa na siasa kuingizwa ktk elimu mfano. ni vigumu kuwaadhibu wachelewaji sababu watakuambia wanatoka mbali na sio kosa la bali serikali ndo imewapanga mbali au wajenge mabweni, udhibiti wa proper school uniform ni tatizo coz kwa kuwa wazazi hawana hela ya kununua uniform so wanapewa mda na baadhi yao wanatake advantage na lingine ni suala la madiwani na viongozi wa siasa kuingilia maamuzi ya walumu na bodi ya shule mfano ktk shule niliyopo kuna wanafunzi walifukuzwa kwa utovu wa nidhamu ila wakarudi kwa nguvu ya madiwani waliomshinikiza mkurugenzi sasa wanafunzi hawaogopi coz wanajua walimu hawana mamlaka yani kitu kidogo tu washakimbia kwa madiwani na wao huwa hawasikilizi upande wa walimu.
Pia wingi wa wanafunzi darasani ni tatizo kubwa saana pia tatizo lingine linaoriginate kutoka katka shule za msingi watoto wanakuja sekondari hawawezi kuongea hata sentensi moja ya kiingereza na wengine hawajui kusoma wala kuandika ila ukiangalia matatizo yote chanzo chake ni serikali na anayeumia ni yule mtanzania maskini ambae hana uwezo wa kumpeleka mtoto wake private, kumnunulia vitabu au kumlipia remedial classes kwa sababu zipo ktk shule za kata.
lingine la maana kutoka shule za kata japo ni baya kwa serikali ni hili wimbi la walimu vijana toka vyuo vikuu na diploma wamekuwa wakiaambia black and white ubaya wa serikali na kuwapa elimu ya uraia ambayo ni muhimu sana kwao ka next voters na wanapata kamwanga so ni vigumu kuuza utu wao kwa t shirt, kofia na khanga na hali halisi ya mazingira yao ya shule ukilinganisha na private schools.
Ni hayo tu kwa leo anyway kuna paper naandika iko tittled ''poor education given by public schools , its sources and solution'' pindi ntakapoimaliza tu ntaiweka humu jamvini wadau muidadavue before sijaipresent inakotakiwa
 
Asante Pukudu kwa mchanganuo mzuri,ungetumegea kidogo kwenye solution
Hatuwezi kuacha hiki kizazi kipotee hivihivi.

Mwalimu mmoja aliniambia kuwa katika shule anayofundisha(chinja chinja ya kitaaluma)
Jirani yake kunashule ya msingi,ambayo mwalimu mkuu naye amepigwa mkwara
na afisa elimu afaulishe,afisa elimu naye amepigwa mkwara na DC,Na kuendelea hadi juu,kwahiyo kinachotokea hapo watoto wanaoneshwa majibu na hivyo darasa zima linafaulu.
Darasa hilo linaenda lote f1 shule ya kata,anasema kuna vioja
kuna wanafunzi hawajui hata kusoma,na alizidi kuniambia kuwa
kwasababu wao kazi yao si kufundisha kusoma na kuandika hawahangaiki nao,
na kwakuwa serikali imechakachua mtihani wa f2,baadhi ya watoto wanahitimu
kidato cha nne hawajui kusoma wala kuandika but who cares.
Watawala wakisimama kwenye majukwaa yao wanajipiga kifua
kuwa wamefanya jitihada kubwa,
Inaumaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!

Ndiyo nchi yetu imepita milima na mabonde ya kitaaluma
lkn tofauti ya zamani na sasa,zamani shule za chini ya mti walimu walitoa elimu bora.

Wanajamvi tutoe michango labda watawala wetu watazibuka masikio.
 
Gama unapotaka kufanya biashara ama shughuli yoyote lazima ufanye kitu inaitwa visible study! Kwanza tunasema hawa lengo lao halikuwa baya bali walikurupika! Walocpy mahala na wakapaste hapa! Unafungua shule huna manpower unaita shule! Umeandaa walimu wa kutosha! Matokeo wakaleta walimu vodafasta!
Pamoja na kutaka watoto wa wakulima wapate elimu! Walitakiwa waweke nayo mazingira ya kusoma yawe ya uhakika.
Hata hawa wazazi wakihamasishwa kujenga mabweni wanaweza kuitikia wito na wakajenga lakini hawawezi kupata waalimu!
Wanapeleka waalimu watoto ambao akisimama na mwalimu hakuna nidhamu maana vijana hawa kutongozana sio ajabu! Yaani walikuwa nao juzi tu kamaliza kapelekwa vodafasta anarudi anataka kumfundisha huyu reproduction! Wakati ashakum sio matusi weshavuliana nguo!
Mimi sina hiyana sana ila serikali nayo itimize wajibu wake. Ipeleke walimu wa kutosha huku kwenye kata na pia tuhamasishe mazingira mazuri ya kusoma na kwa walimu wapewe mazingira ya kufanya kazi. Kuna walimu najua wanaka over 35km na wanaenda na kurudi kwao kila siku. Atafundisha saa ngapi huyu! Unamkuta saa tatu na nusu mpaka saa nne ndo anatokwa na mijasho anawahi kipindi! Atafundisha kweli! ama atapiga blah blah siku iende akakamue ngombe ya mwenzawazimu mwisho wa mwezi!

AM, kuna tatizo gani jwenye vodafasta?. Tuna mifano mizuri ya shule moja maaufu hapa nchini ambayo iliajiri waalim wengi kutoka kenya ambao hawakuwahi kuingia drs la ualimu na ilikuwa maarufu with very high schoool fee. Unakumbuka jinsi azimio la UPE lilivyo punguza kiwango cha kutojua kusoma na kuandika?,pendekeza, unafikiri shule hizi zisingejengwa watoto hawa wangekuwa wapi?
 
sirikali ilaumiwe! make haijali mazingira maticha wanayokuwa nayo, hainiingii akilin mwalim unakuta nyumba mboov anayoishi, kanyeshewa usiku kucha anakatiza maporini akipishana na wanyama mwitu afu umbali wa kutosha ili afike kwenye shule ya kata,kisha mshahara aupate KIMAGUMASHGUMASHI kisha utegemee atafundisha mtoto wa mtu aelewe wamekata tamaa,wanaishiaga vilabuni na mambo kama hayo
 
AM, kuna tatizo gani jwenye vodafasta?. Tuna mifano mizuri ya shule moja maaufu hapa nchini ambayo iliajiri waalim wengi kutoka kenya ambao hawakuwahi kuingia drs la ualimu na ilikuwa maarufu with very high schoool fee. Unakumbuka jinsi azimio la UPE lilivyo punguza kiwango cha kutojua kusoma na kuandika?,pendekeza, unafikiri shule hizi zisingejengwa watoto hawa wangekuwa wapi?

Hatukatai Mkuu,binafsi nilifundishwa tution na mwalimu ambaye hakusoma ualimu
lakini alikuwa mwalimu mzuri sana,mimi pia nilifundisha tution na sikusomea ualimu
na wanafunzi walipenda sana somo langu.

Tofauti iliyopo kati ya vodafasta na walimu wa private ni kwamba
walimu wa private wanafanyiwa mchujo mkali,wanafunzi pia wanaweza mkataa mwalim
kama ufundishaji wake si mzuri,lakini maskini wanafunzi wa kata hawana uhuru huo
wao mwalim afundishe asifundishe ni sawa,awe hajui kufundisha hewala.

Mwisho nitofautiane nawe mkuu,shule za kata hazijajengwa kama kijiwe cha watoto
ambao hawana pa kwenda,bali ni kwa ajili ya kupata elimu.

Asante.
 
AM, kuna tatizo gani jwenye vodafasta?. Tuna mifano mizuri ya shule moja maaufu hapa nchini ambayo iliajiri waalim wengi kutoka kenya ambao hawakuwahi kuingia drs la ualimu na ilikuwa maarufu with very high schoool fee. Unakumbuka jinsi azimio la UPE lilivyo punguza kiwango cha kutojua kusoma na kuandika?,pendekeza, unafikiri shule hizi zisingejengwa watoto hawa wangekuwa wapi?

Usilinganishe voda za kenya na tz mkuu. Angalao wenzetu walitutangulia kwenye kilugha. Kama wewe unaona hili ni sawa haya huna uchungu na watoto wa wakulim a wenzetu!
 
Lengo la hizo shule ni zuri lakini utekelezaji ovyoo. Nimeona Shule moja ya sekondari ya kata yenye wanafunzi around 300 walimu waili tu!!
My take: Bora wazifunge ASAP
 
Serikali inakitu cha kufanya,kama itadhamiria kwa dhati inaweza kabisa kuondoa
kero ktk shule za kata.Maandalizi mazuri ikiwa ni pamoja na nyumba za walimu vifaa vya kufundishia,itasaidia sana.
 
ccm wanajitengenezea mabomu na muda si mrefu yatawalipukia acha yajazane kwa miaka mitatu mfululizo halafu matokea yake watayaona tu kupitia hao wanaomaliza kidato cha nne na sita wakiwa na ziro huku wakiachwa bila msaada wowote.
 
Baada tu ya Mh J. K kuingia madarakani alikuja na mpango wa shule za sekondari maaruf kama SHULE ZA KATA na mwaka 2006 shule hz zilijengwa kwa kasi ya ajabu na hatimae kuanza tena nyingine zilichelewa kuanza mpk mwez March. Tujaribu kufanya tathmin kidogo
Juzi bungen aliwatambulisha wanafunz 20 bora ktk mtihan wa kidato cha sita, kati ya hao aliwataja wanafunz 7 kuwa ni zao la shule za kata. Nimejaribu kufanya mahesabu yaliyonichanganya kidogo, nikaanza
form 1 mwaka 2006- form 4 mwaka 2009. Form 5 mwaka 2010- form 6 mwaka 2012 feb. Sasa hawa waliopongezwa walisoma ktk shule za kata kweli?, walianza shule mwaka gan?, je wakati huo shule za kata zilikua tayari?.
TAFAKARI
 
Hawa hawatoki shule za kata za kiwete. Ni zile shule za kata za awali. Mbona wengine tumesoma shule hizo hizo. Japo umaarufu wa jina hili umekuja kipindi cha huyu mbayuwayu. Zilikuwa zinajitahidi sana. Lakini sasa huwezi kuzitofautisha na hizi za sasa. Hali zake ni mbaya sana.
 
Hawa hawatoki shule za kata za kiwete. Ni zile shule za kata za awali. Mbona wengine tumesoma shule hizo hizo. Japo umaarufu wa jina hili umekuja kipindi cha huyu mbayuwayu. Zilikuwa zinajitahidi sana. Lakini sasa huwezi kuzitofautisha na hizi za sasa. Hali zake ni mbaya sana.
sikuwah kulisikia neno shule za kata b4 2006 na kati ya shule zilizotajwa na mimi nayoifahamu KIKUYU SEC iliyopo Dodoma huwez kuiita shule ya kata hata coz haikuwa ktk mpango huo.
 
Back
Top Bottom