Mandela hastahili heshima ya juu hivi kupita makubwa yaliyofanywa na akina Nyerere

View attachment 125976 Julus Nyerere VS Nelson Mandela View attachment 125977

Sijaridhika bado na uzito wa Nelson Mandela ukilinganisha na baadhi ya viongozi wengine wambao wamefanya makubwa katika ukombozi wa bara la Afrika na baadhi ya mambo muhimu ulimwenguni. Jambo la pekee kwa Mandela ni kufungwa kwa miaka 26, na baada ya kufunguliwa makubaliano ya ANC ni kumpa nafasi ya kuongoza nchi ambapo alidumu kwa awamu moja na kuamua kuachia ngazi pengine sababu ya matatizo ya kiafya ndio alitaka upweke asibughudhiwe. Zaidi ya kupigania haki za Waafrika huku kusini hakuna tofauti na wapigania uhuru wengine katika bara hili.

Kwa kulinganisha na mmoja ambaye amekuwa katika vichwa vya waafrika wengi
Julius Nyerere naona kwa mtazamo wangu Nyerere yuko juu zaidi kwa juhudi kubwa alizofanya kupigania ukombozi wa bara la Afrika, kwani alijitolea bila hofu na hata umoja wa Afrika kuweka makao makuu ya ukombozi nchini Tanzania. Hata vyama vya wapigania ukombozi makao yao yalikuwa Tanzania, hali kadhalika ANC maskani yao yalikuwa Tanzania, karibu na mji kasoro bahari (Morogoro) ambako sasa ni chuo kikuu cha kilimo (Sokoine University).

Naweza kutafsiri kama mataifa ya magharibi yamefanya jitihada kubwa kumkuza zaidi kwa kile kinachoonekana kujaribu kufunika yale yaliyofanywa nao kipindi cha ubaguzi kwa vile walikuwa ni wazungu wenzao. Lakini kupima kwa vigezo halisi binafsi naona Nyerere yuko juu zaidi ya Mandela, na tena kuna wengine wengi tu wenye kustahili heshima zaidi yake hapa Afrika kuliko yeye. Mataifa ya magharibi yametuteka nasi tumefuata wayatakayo.

nami nakuunga mkono,mpaka sasa sijaona anayeweza kumfunika NYERERE
 
View attachment 125976 Julus Nyerere VS Nelson Mandela View attachment 125977

Sijaridhika bado na uzito wa Nelson Mandela ukilinganisha na baadhi ya viongozi wengine wambao wamefanya makubwa katika ukombozi wa bara la Afrika na baadhi ya mambo muhimu ulimwenguni. Jambo la pekee kwa Mandela ni kufungwa kwa miaka 26, na baada ya kufunguliwa makubaliano ya ANC ni kumpa nafasi ya kuongoza nchi ambapo alidumu kwa awamu moja na kuamua kuachia ngazi pengine sababu ya matatizo ya kiafya ndio alitaka upweke asibughudhiwe. Zaidi ya kupigania haki za Waafrika huku kusini hakuna tofauti na wapigania uhuru wengine katika bara hili.

Kwa kulinganisha na mmoja ambaye amekuwa katika vichwa vya waafrika wengi
Julius Nyerere naona kwa mtazamo wangu Nyerere yuko juu zaidi kwa juhudi kubwa alizofanya kupigania ukombozi wa bara la Afrika, kwani alijitolea bila hofu na hata umoja wa Afrika kuweka makao makuu ya ukombozi nchini Tanzania. Hata vyama vya wapigania ukombozi makao yao yalikuwa Tanzania, hali kadhalika ANC maskani yao yalikuwa Tanzania, karibu na mji kasoro bahari (Morogoro) ambako sasa ni chuo kikuu cha kilimo (Sokoine University).

Naweza kutafsiri kama mataifa ya magharibi yamefanya jitihada kubwa kumkuza zaidi kwa kile kinachoonekana kujaribu kufunika yale yaliyofanywa nao kipindi cha ubaguzi kwa vile walikuwa ni wazungu wenzao. Lakini kupima kwa vigezo halisi binafsi naona Nyerere yuko juu zaidi ya Mandela, na tena kuna wengine wengi tu wenye kustahili heshima zaidi yake hapa Afrika kuliko yeye. Mataifa ya magharibi yametuteka nasi tumefuata wayatakayo.


Candid Scope,
Mimi pia naamini kuwa Nyerere amelifanyia bara Afrika mengi kuliko Mandela, lakini pia naamini kuwa Mandela an astahili sifa alizomwagiwa na ulimwengu. Wakati mmoja baada ya Afrika kusini kupata uhhuru Mugabe alisikika akilalamika kuwa kwa nini Mandela anatukuzwa kuliko yeye (Mugabe) wakati Zimbabwe imechangia sana kuikomboa Afrika kusini. Siku moja mjini New York nikapata bahati ya kuzunguza na Mwalimu. Nikamtajia malalamiko hayo ya Mugabe. Alinijibu philosophically kwamba "history has assigned the role of greatness to Mandela." Kwa hiyo hata Mugabe akilalamika namna gani, hata kama Mugabe alimsaidia Mandela kupata uhuru, historia imetoa jukumu la kusifika kwa Mandela. Kwa maneno hayo nina hakika Mwalimu would have been very comfortable to watch his friend Mandela receive world accolades.
 
Ulikiwapo itawala wa nyerere au ndo imesifiwa tu huko shule?
Kama mwinyi alikua kichuguu kwa nyerere basi naye nyerere na mandela ni mbingu na ardhi
Chukulia mambo haya then linganisha
Haki za binadamu
Uhuru wa habari
Democrasy
Uchumi
Uhusiano wa nje
Ama kulinganisha kuwa alosaidia ukombozi ukweli budget yote ikitoka njee yeye alikia mpiga debe sanaa
Unyanganyi wa mali za watu ni dhulma nyengine
Kusamehe jamaa mpaka anakata roho hakuomba msamaha hata kawawa aliomba msamaha
Nyerere na mandela ni watu yofauti
 
Kwa kweli Mandela anastahili sifa kubwa na Nampa heshima zote kwa kwa kila alichofanya lakini pia nakubaliana na mleta mada kuwa kuna wengi katika Afrika ambao wamechangia vikubwa katika ukombozi wa Afrika. Kitu ni kuwa nchi za Magharibi na vyombo vyao vya habari vinachangia katika kumpigia debe Mandela sababu ya maslahi yao hayakuharibika katika Afrika Kusini - nchi yenye uchumi mkubwa Afrika. Tusisaha kuawa hizi nchi za magharibi na vyombo vyao vya habari mpaka miaka ya karibuni walikua wana sapoti utawala wa kibaguzi na wakina Mandela na wengine walikuwa ni magaidi. Kwa hiyo hadi leo ukoloni haujaisha mapaka mashujaa wetu wanatuchagulia
 
Miaka 27 aliyofungwa Mandela na sababu ya kufungwa ni kivutio tosha cha umaarufu; watoto walizaliwa wakakua wanasikia kuna mtu anaitwa Mandela alifungwa na anateswa; baadae akafunguliwa akasema yamekwishaa....!!? ni binadam wa ajabu huyu (uzee au dini).! Wazungu wanampenda kwa vile aliwasamehe na kwa kuogopa kuangusha uchumi hakuchukua mali za WEUPE kuwapa WEUSI kama yalivyokuwa makubaliano ya ANC morogoro leo ina wakati mgumu weusi wanasafa kilio cha Malema; source BBC leo (weusi mpaka leo wanalalamika ndo Maana walimshangila mugabe; na Mwl aliwambia kwenye otuba ya 1997 bungeni wakacheka); then weupe wakampa tuzo ya Nobel, sanam huko Uingereza na promo kwenye vyombo vyao n.k wakati huo wakajitahidiviongoz wengne waonekane sio wa maana nasi tukakubali...! Mfano Mandela anaonekana kuwazidi mbali akina Sisulu, Biko, Tambo, Lumumba, Nkomo, Mugabe, Sekou Toure, Mondlane, Samora, Amica Cabro, Fanon, Azikiwe, Nasser, Haile Silase, Nkrumah, Kaunda, Nyerere na wengne humshtuki?? kuna kitu hapa...! Mbona hawasifii waliowaua?? Hawa walikuwa miiba kwa wazungu na walikuwa wajamaa; ni ngumu kupata kitabu kinatoka west kinawasifu hawa..! as well Mahatma Gandh, Mao, Lenin, Marx, Castro, Chaves and the like..! Nyrere alihost wapigania uhuru toka nchi 5+ bila kinyongo; katoa ardhi na askari wetu wakaenda kupigana huko na weupe au vibaraka wao..! Hii ni hatari kuliko mapambano ya mandela make maadui alitengeneza weng; alikataa matendo yao wazi na akaweka msimamo..! East ndo waliona jitihada za Mwl wakampa Tuzo ya amani ya Lenin na si Nobel ya wanafiki..! Kati ya hao hata kama wengefanyaje wasingepata umaarufu.., ndo maana wanapenda wa sasa. Sisi wenyewe hatujashtuka tumeishia kuwalaumu wazee wetu kama wazungu wanavotaka tufanye...! (wamefanikiwa) Sidhani hata wasouth kama wanatambua mchango wa nchi nyingine za Africa kukomboa nchi yao (hata Mugabe hakupewa nafasi kuongea jana) wao ni Mandela tuuu...! Africa needs AZIMIO LA ARUSHA than ever.R. I. P Mwl Nyerere.
 
Ulikiwapo itawala wa nyerere au ndo imesifiwa tu huko shule?
Kama mwinyi alikua kichuguu kwa nyerere basi naye nyerere na mandela ni mbingu na ardhi
Chukulia mambo haya then linganisha
Haki za binadamu
Uhuru wa habari
Democrasy
Uchumi
Uhusiano wa nje
Ama kulinganisha kuwa alosaidia ukombozi ukweli budget yote ikitoka njee yeye alikia mpiga debe sanaa
Unyanganyi wa mali za watu ni dhulma nyengine
Kusamehe jamaa mpaka anakata roho hakuomba msamaha hata kawawa aliomba msamaha
Nyerere na mandela ni watu yofauti

Laiti ungejua hata nchi zinazojitangaza kuwa demokrasi ndio nyumbani, na pia tunavyoaminishwa na kuamini kwamba kwao huko Marekani demokrasi ndiko kwa kujifunza kumbe tunawazidi kwa hatua nyingi kuliko wao walioanza hiyo demokrasi zaidi ya karne tatu.

Nchini Marekani huwezi kuona watu wanajadili mambo yahusuyo taifa lao na haki zao iwe kazini au majumbani na vijiweni kama tufanyavyo Tanzania na nchi nyingine za kiafrika kwa sababu ya kujengewa woga wa kuogopa mbwa wao aka secret services, ambao kila anayeituhumu au kuisema serikali juu ya maovu ni mateso ya siri kwa kwenda mbele. Watu ni waoga we basi.

Hawa wazungu kinachowafanya wampambe mandela ni kwa kile kinachoeleweka kutowanyoshea kidole mabaya na kuwa mwazi kwa baadhi ya mambo yasiyoenda sawa alivyofanya Mandela. Katu ukiwanyooshea kidole wazungu kwa mabaya wanayosema hata ardhi yako viongozi wao hawakuja kuikanyaga.

Umeona Kikwete anavyowapamba tu Tanzania imekuwa nyumbani kwao, hata kama kuna madhaifu aliyo nayo wazungu hawaoni shida kwa vile kwao huyu si tatizo.
 
Candid Scope,
Mimi pia naamini kuwa Nyerere amelifanyia bara Afrika mengi kuliko Mandela, lakini pia naamini kuwa Mandela an astahili sifa alizomwagiwa na ulimwengu. Wakati mmoja baada ya Afrika kusini kupata uhhuru Mugabe alisikika akilalamika kuwa kwa nini Mandela anatukuzwa kuliko yeye (Mugabe) wakati Zimbabwe imechangia sana kuikomboa Afrika kusini. Siku moja mjini New York nikapata bahati ya kuzunguza na Mwalimu. Nikamtajia malalamiko hayo ya Mugabe. Alinijibu philosophically kwamba "history has assigned the role of greatness to Mandela." Kwa hiyo hata Mugabe akilalamika namna gani, hata kama Mugabe alimsaidia Mandela kupata uhuru, historia imetoa jukumu la kusifika kwa Mandela. Kwa maneno hayo nina hakika Mwalimu would have been very comfortable to watch his friend Mandela receive world accolades.

Kinachofanywa na wazungu kumwenzi Mandela kwa upeo wa juu zaidi ni kwa sababu baada ya kutoka Kifungoni hajawahi kuongelea mabaya yo yote ya wazungu katika utawala wake. Je, hii ni kwali hakuna mabaya yaliyotendeka?

Naweza kusima Mandela amekuwa raisi wa huko kusini lakini hajawahi kuongelea msimamo wa mambo ya kimataifa na kutikisa hayo mataifa makubwa kama walivyofanya akina Nyerere, Mugabe na wengineo, hicho ndicho kinachowafanya wazungu wampambe. Ole wako uwadokolee macho na kuwasema maovu yao wazungu unakuwa adui wao mkubwa na kuwekwa kwenye list kama alivyowekwa Mandela akiwa gerezani.

Ukitaka urafiki wka wazungu we sikiliza wanachokuambia, chekacheka na kutabasamu, itikia mialiko ya hata wakutembeze kwanya magari yao ya kifahari ya kukokotwa na farasi, hapo watafurahi wanajisikiwa wamekuweka sawa, hata siku moja hawatakubughudhi hata ufanya mambo yaliyo kinyume cha haki za binadamu kwa vile we si tatizo kwao.
 
Mi sijui sana jamani, mi naona our NyererE ni bora kuliko Mandela,Nyerere alisaidia kuleta uhuru kwa nchi kadhaa za africa, alikuwa mpatanishi na msuluhishi wa migogoro kwa nci mbali mbali za africa.
Msinipige mawe, mie sio mwanasiasa ni mawazo yangu tu

Bora umeona hili, nini cha pekee alichofanya Mandela baada ya kushika dola Afrika Kusini? Kama ni uchumi aliukuta umeshatengamaa ulioendeshwa na wazungu, na hangeweza kuwafukuza kwa sababu wazungu ni wazawa wa miaka mingi huko ni kwao. Ni hili la kusameheana yaliyopita na kuanza upya jambo ambalo nyuma ya pazia ni kutoka kwa mpigania haki za binadamu Afrika Kusini Askofu Mkuu Desmon Tutu, lakini amevishwa kilemba hicho Mandela kwa vile aliridhia ushauri huo wa Tutu.

Nyerere na wengineo walifanya mengi kimataifa na pengine kutingisha hayo mataifa makubwa, lakini sijaona la pekee ambalo Mandelea alifanya hata la Kukumbukwa kwa taifa zima la Afrika isipokuwa ndani ya mipaka ya Afrika kusini.

Tusisahau wakati wanapigania hayo kuna waliokuwa nyuma yao na kuwapa hifadhi na ulinzi ndio Tanzania.
 
  • Thanks
Reactions: ram
"Waziri wa fedha tangu tupate huru hadi miaka ya 70 alikuwa mzungu nadhani alikuwa anaitwa Jennings kama sijachanganya jina lake ambaye sasa ni marehemu, alikuwa Mwingereza. Pia miaka ya nyuma kipindi cha Nyerere aliweza kumpokea mkimbizi mmarekani ambaye alikuwa na itikadi za kijamaa akawa anaishi Arusha. Mji wa Morogoro kwa miaka kadhaa katika awamu ya kwanza walikuwa na mbunge mwanamke mhindi"


Nakumbuka jina la waziri wa fedha mzungu enzi ya MUSSA lilikuwa ERNEST VASSEY!!!!



 
Wewe wapi zamani?

mandela-moroka-obi_2588613b.jpg
Hata Mandela ni wa zamani hayupo tena duniani
 
Upo sahihi. Jina lake kamili lilikuwa Sir Ernest Albert Vassey. Alishika wadhifa huo tangia 1961-62.

Waziri wa fedha utawala wa Nyerere mpaka miaka ya 70 alikuwa mzungu, ingawa sina kumbukumbu nzuri ya jina lake kamili, lakini kama sijakosea kama nilivyosema awali akikuwa Jennings, ambaye kwa sasa ni marehemu, na alipofariki Tanzania alikumbukwa sana na kutangazwa na vyombo vya habari.
 
Waziri wa fedha utawala wa Nyerere mpaka miaka ya 70 alikuwa mzungu, ingawa sina kumbukumbu nzuri ya jina lake kamili, lakini kama sijakosea kama nilivyosema awali akikuwa Jennings, ambaye kwa sasa ni marehemu, na alipofariki Tanzania alikumbukwa sana na kutangazwa na vyombo vya habari.
Hilo jina ni sahihi. Jaribu kufanya utafiti kidogo na utagundua hilo!
 
Hilo jina ni sahihi. Jaribu kufanya utafiti kidogo na utagundua hilo!

View attachment 126259 Hili nia baraza la Mawaziri tulipopata uhuru lililoundwa na Nyerere waona kuna mhindi na mzungu, ukitaka kuona vizuri picha hii just double click kuikuza uone vizuri zaidi.

The multi-racial first cabinet of newly independent Tanganyika. While this sort of thing was seen as strange in other newly independent African countries, for Nyerere this was a matter of course. People were appointed on merit, based on their ability and commitment to the cause. The issue of skin colour did not feature. Amir Jamal (far right, seated), the first of many Tanzanians of Asian origin to serve in Nyerere's cabinet was a long-serving member, for many years holding the powerful portfolio of Finance Minister. He continued to hold high office beyond Nyerere's own retirement, including a five year stint as Tanzania's ambassador to the United Nations in Geneva from 1988 to 1993. His close working relationship with retired President Nyerere continued as he became his personal representative when Mwalimu Nyerere was Chairman of the South Commission and then on the South Centre, and the Dag Hammarskjold Foundation of Uppsala, Sweden. Amir Jamal was continually re-elected to Parliament by his Morogoro constituency with ever greater margins. This is despite the fact that members of his racial group comprised less than 1% of the population, testament to Mwalimu's success in making his country a truly non-racial society. Mr Jamal died in March 1995 aged 74.

CC;
hekimatele
 
View attachment 126259 Hili nia baraza la Mawaziri tulipopata uhuru lililoundwa na Nyerere waona kuna mhindi na mzungu, ukitaka kuona vizuri picha hii just double click kuikuza uone vizuri zaidi.

The multi-racial first cabinet of newly independent Tanganyika. While this sort of thing was seen as strange in other newly independent African countries, for Nyerere this was a matter of course. People were appointed on merit, based on their ability and commitment to the cause. The issue of skin colour did not feature. Amir Jamal (far right, seated), the first of many Tanzanians of Asian origin to serve in Nyerere's cabinet was a long-serving member, for many years holding the powerful portfolio of Finance Minister. He continued to hold high office beyond Nyerere's own retirement, including a five year stint as Tanzania's ambassador to the United Nations in Geneva from 1988 to 1993. His close working relationship with retired President Nyerere continued as he became his personal representative when Mwalimu Nyerere was Chairman of the South Commission and then on the South Centre, and the Dag Hammarskjold Foundation of Uppsala, Sweden. Amir Jamal was continually re-elected to Parliament by his Morogoro constituency with ever greater margins. This is despite the fact that members of his racial group comprised less than 1% of the population, testament to Mwalimu's success in making his country a truly non-racial society. Mr Jamal died in March 1995 aged 74.

CC;
hekimatele
Aisee acha ubishi. Waziri wa Fedha kati ya kipindi cha 1961-62 alikuwa Sir Ernest Vassey. Hata jamaa wa global hilo wanalijua. Ushauri wa bure: ni vizuri kusoma historia ya nchi yako kwa kina!
 
Aisee acha ubishi. Waziri wa Fedha kati ya kipindi cha 1961-62 alikuwa Sir Ernest Vassey. Hata jamaa wa global hilo wanalijua. Ushauri wa bure: ni vizuri kusoma historia ya nchi yako kwa kina!

Nadhani tuko pamoja, ila tu hatujaweza kukaa sana katika kuliweka sawa hili. Nakubaliana na Waziri huyo kuwepo kwenye cabinet ya Nyerere, pengine aliyefutata baada ya huyo ndiye ninayemsema mimi ambaye alidumu kipindi kirefu zaidi akiwa mzungu pekee katika baraza la mawaziri wa Tanzania ambaye ni Jennings. Huyo unayesema sipingani nawe kwani sina kumbukumbu vizuri ya cabinet ya kwanza miaka ya 61-62
 
Waziri wa fedha utawala wa Nyerere mpaka miaka ya 70 alikuwa mzungu, ingawa sina kumbukumbu nzuri ya jina lake kamili, lakini kama sijakosea kama nilivyosema awali akikuwa Jennings, ambaye kwa sasa ni marehemu, na alipofariki Tanzania alikumbukwa sana na kutangazwa na vyombo vya habari.
Nadhani unamchanganya na Derek Bryceson. Huyo Jennings sikuwahi kumsikia enzi hizo.
 
Back
Top Bottom