Mandela hastahili heshima ya juu hivi kupita makubwa yaliyofanywa na akina Nyerere

Unataka kusema Nelson Mandela amekuza uchumi wa S.Afrika?

Hulujui hilo??
Ulishasoma statistics za economy ya South Africa pre and post Mandela?
Halafu linganisha na pre Nyerere na post Nyerere??
Unafikiri mzee Rukhsa alipataje nickname yake??
Nyerere alibana kila kitu mpaka wananchi kupumua walikuwa hawawezi.. Ikawa Mwinyi anatoa "rukhsa" kwa kila kitu....
Inawezekana ni kati wanaojichanja kwenye "viwanja" vya maraha, lakini alipoondoka Nyerere, hata soda au juice huwezi kupata baa! Nyama bucha hakuna, ukikamatwa na sabuni ya kuogea ni kosa la jinai..... Yaaani maisha yalikuwa balaa tupu!!
Nyie picha mnayopewa ya Nyerere ni ilyopigwa msasa na CCM... Ina mapotofu na mapungufu mengi saaana!
I lived it... I KNOW IT, sijafundishwa darasani.
 
Nadhani ulinganifu sahihi kati ya hawa viongozi ni mchango wao ktk kuikomboa afrika na hapo ndio Nyerere atabaki kuws mtu wa pekee.

Nadhani uchambuzi wetu utakuwa na maana zaidi kama tutaanza na uchambuzi yakinifu wa Mandela mwenyewe kwanza, kisha tumchambue Nyerere, na baada ya hapo pengine tunaweza kufanya hiyo "comparative analysis".

mleta uzi ana mashaka na "umaarufu" anaopewa Mandela. tukumbuke kwamba huo "umaarufu" umejengwa hasa na vyombo vya Magharibi, ambao nyuma ya pazia, wao ndio wagomvi wakubwa wa Mandela, ndio walimfunga na kumtesa. na ni hao ndio alikuwa anapambana nao hasa maana wao ndio wamiliki wakuu wa makampuni makubwa ya huko Afrika ya Kusini. Wasiwasi wao mkubwa ulikuwa ni ile "Nationalisation" ambayo Mandela aliahidi mwanzoni kwamba lazima ifanyike. lakini katika kile ambacho kimeitwa "FAUSTIAN MOMENT", Mandela aliafikiana na Magharibi, wakati ambao kipindi chote cha 1991 -1996 kilikuwa ni "the battle for the soul of the ANC" [soma How the ANC's Faustian pact sold out South Africa's poorest], na hiyo iliwawezesha Magharibi kuendelea kuhodhi uchumi wa Afrika ya kusini. Asemavyo Mbeki, Afrika ya kusini ni nchi mbili katika nchi moja: nchi ya weupe wenye utajiri mkubwa, na waafrika wachache, wakiwemo viongozi wa ANC. nyingine ni ya wasionacho, Waafrika masikini, na ANC yao "Asilia".

Hawa, kama ilivyokuwa Shaperville, wanaendela kuuawa kama ilivyokuwa katika MARIKANA. wazungu wanayo sababu nzuri ya kumsifu Mandela, kwa kuwa kahakikisha kwamba wanabaki na mali za Waafrika walizonyonya na wataendelea kunyonya. Tukitaka kuelewa vizuri suala la Afrika ya kusini na Mandela, tuachane na hizi porojo za akina Obama - Obama anawakilisha mfumo wa kibeberu wa kidunia, na ndio Rais wa kwanza mwenye asili ya Afrika huko Marekani - na amewapa wazungu zawadi ya pekee - maana wakati Reagan alimshambulia tu Gaddafi, yeye amemwondoa kabisa madarakani - done under Obama's watch. of course Obama lazima ampige vijembe Mugabe, mtu aliyediriki kupambana uso kwa uso na mifumo ya kibeberu ya kidunia.

Tukitaka kuelewa vizuri, na kujua nini tufanye, tuangalie mapambano yanayoendelea in the background, ambayo hata hapa kwetu Tanzania hali ni hiyo hiyo. tuangalie mapambano ya kitabaka huko Afrika ya kusini, mchango wa Mandela katika mapambano hayo, na kile alichokiacha. hapo tutajua mbivu na mbichi ni zipi na tufanye nini
 
This document tells us a lot about these friends of ours how close they are to Nyerere.
 
Mi sijui sana jamani, mi naona our NyererE ni bora kuliko Mandela,Nyerere alisaidia kuleta uhuru kwa nchi kadhaa za africa, alikuwa mpatanishi na msuluhishi wa migogoro kwa nci mbali mbali za africa.
Msinipige mawe, mie sio mwanasiasa ni mawazo yangu tu


Anastahili mandela kuheshimiwa alifungwa miaka 26 kwa ajili ya kupinga ubaguzi wa rangi ili kuwakomboa waafrica weusi africa ya kusini, aliwasamehe waliomfunga nani anaweza? Wazazi wake walimuomba kuachana na harakati za siasa lakini mandela alisimamia msimamo wake anatisha, maisha yake ya ujana yameishia gerezani hakupata muda wa kukaa na familia na kuwatunza wazazi wake kama mtoto anavyotakiwa kufanya kwa wazazi rest in peace mandela dunia inakila sababu ya kukukumbuka uliletwa na mungu kwa kusudi malumu
 
Sikuwahi kusikia hii!

komaa kiakili ndugu yangu, unapotumia muda wako kuandikia mambo finyu namna hiyo utajichelewesha sana. Typo ndogo kama hizo siyo jambo la kushanganza na kukufanya usielewe maana ya post nzima. Iwapo kwenye post hiyo. hayo maneno mawili tu ndiyo uliyoelewa basi inabidi ujitahidi sana kukomaza akili zako kuweza kuona mengine.
 
This document tells us a lot about these friends of ours how close they are to Nyerere.
Kwanza, kuwalinganisha viongozi uliowataja na Nyerere ni makosa. Nyerere hawezi kulinganishwa na yeyote kwa kuwa wakati wake ulikuwa na changamoto zake ambazo haziwezi tena kuwepo sasa. Pili, waraka ulioambatanishwa hapa is a poor work of art . Nilipinga barua pepe iliyosambazwa siku za nyuma ikimhusisha Naibu Katibu Mkuu wa CCM na Waziri wa Mambo ya Ndani......this too doesn't worth a penny!
 
komaa kiakili ndugu yangu, unapotumia muda wako kuandikia mambo finyu namna hiyo utajichelewesha sana. Typo ndogo kama hizo siyo jambo la kushanganza na kukufanya usielewe maana ya post nzima. Iwapo kwenye post hiyo. hayo maneno mawili tu ndiyo uliyoelewa basi inabidi ujitahidi sana kukomaza akili zako kuweza kuona mengine.
Umedandia gari kwa mbele mjomba, lengo langu nilikuwa nauliza kama nyerere alifungwa Jela? acha kudandia issue zilizokupita umri!
 
Mie nakuunga mkono asilimia mia kwa mia, ukweli huyu marehemu hastahili sifa kubwa kiasi hicho kumzidi baba wa taifa letu. Yawezekana hamegeuka baada ya kumuita gaidi na sasa kumfanya shujaa baada ya kutekeleza matakwa (masharti waliyompa) yao ya kutowaingilia kiuchumi wazungu waliopo huko Afrika Kusini basi. NYERERE yupo juu na tunamuombea kwa Mungu milele na milele. Amina.
 
View attachment 125976 Julus Nyerere VS Nelson Mandela View attachment 125977

Sijaridhika bado na uzito wa Nelson Mandela ukilinganisha na baadhi ya viongozi wengine wambao wamefanya makubwa katika ukombozi wa bara la Afrika na baadhi ya mambo muhimu ulimwenguni. Jambo la pekee kwa Mandela ni kufungwa kwa miaka 26, na baada ya kufunguliwa makubaliano ya ANC ni kumpa nafasi ya kuongoza nchi ambapo alidumu kwa awamu moja na kuamua kuachia ngazi pengine sababu ya matatizo ya kiafya ndio alitaka upweke asibughudhiwe. Zaidi ya kupigania haki za Waafrika huku kusini hakuna tofauti na wapigania uhuru wengine katika bara hili.

Kwa kulinganisha na mmoja ambaye amekuwa katika vichwa vya waafrika wengi
Julius Nyerere naona kwa mtazamo wangu Nyerere yuko juu zaidi kwa juhudi kubwa alizofanya kupigania ukombozi wa bara la Afrika, kwani alijitolea bila hofu na hata umoja wa Afrika kuweka makao makuu ya ukombozi nchini Tanzania. Hata vyama vya wapigania ukombozi makao yao yalikuwa Tanzania, hali kadhalika ANC maskani yao yalikuwa Tanzania, karibu na mji kasoro bahari (Morogoro) ambako sasa ni chuo kikuu cha kilimo (Sokoine University).

Naweza kutafsiri kama mataifa ya magharibi yamefanya jitihada kubwa kumkuza zaidi kwa kile kinachoonekana kujaribu kufunika yale yaliyofanywa nao kipindi cha ubaguzi kwa vile walikuwa ni wazungu wenzao. Lakini kupima kwa vigezo halisi binafsi naona Nyerere yuko juu zaidi ya Mandela, na tena kuna wengine wengi tu wenye kustahili heshima zaidi yake hapa Afrika kuliko yeye. Mataifa ya magharibi yametuteka nasi tumefuata wayatakayo.



Wanafiki wakubwa! Alikuwa kwenye listi yao ya magaidi hadi mwaka 2008, lakini leo wanamtukuza kama malaika!!
 
Mandela aliyepigania usalama wa wazungu ni mtu muhimu kwa mataifa ya magharibi, lakini Mugabe anayepigania haki za waafrika walio wengi ni mtu hatari kwa nchi za magharibi, hii ndio hali halisi na ndicho kinachoendelea katika sakata hilo la kuenziwa Mandela ambaye inaonekana kama mdau mmoja alivyosema ni kuongeza mafuta kwenye utambi.
nakubaliana na wewe ila nashukuru mungu waafrika tunaelewa ukwewli na hatukubali kupelekwa kibubusa na western media
 
Mugabe tu anampita mandela kwa ushujaa kwa kuwapokonya ardhi wazungu na kuirudisha kwa waafrika. Nyerere ndio engine ya ukombozi afrika. Hakuna kiongozi wa ukombozi afrika ambaye hapakua na mkono wa nyerere kumtengeneza; kuanzia kina mondlane, samora, augustino neto, sam nujoma, oliver tambo hadi mandela mwenyewe. Msisahau oliver tambo ndiye kiongozi aliyeongoza anc miaka yote mandela akiwa jela nakufariki dunia kabla ya ukombozi wa SA. Muhimu kila kiongozi amecheza role yake na kwa wakati wake. Ila historia ikitendewa haki, nyerere ndie baba wa ukombozi afrika.

Mandela kawa maarufu kwa sababu ya kutolipiza kisasi. Nafikiri alipima pia kuwa wakati anapata madaraka, all security institutions were still under whites. Na weupe wenyewe hawakuwa wachache kama ilivyokuwa zimbabwe. Kule south walikuwa karibu 5m by then, angelipiza kisasi angeishia kupigania a losing battle.
kwa mchango wa ukombozi, mandela hawezi linganishwa na kina Oliver Tambo, sembuse kumlinganisha na Nyerere. Tatizo kubwa lililompata Nyerere ni kuwa muumini wa dini fulani ambayo kuna manazi hapa hapa Tanzania wanaihusisha na matatizo yao. Ni manazi hao hao ndio wapo tayari kutoa mapovu ilimradi tu Nyerere aonekane si lolote wala si chochote.
 
kwani ule mchakato wenu wa kanis katoliki wa kamfanya Nyerere kuwa mtakatifu w kanisa katolii umeishia wapi? Mtu anayepewa utakatifu na kanisa lake kwa kazi mzuri aliyolifanyia kanisa lake kwa kulipenelea unawezaje kumfananisha na mandela aliyeamini binadamu wote ni sawa akaishi hivyo!
 
Jambo la kawaida kujadili matukio ya wakati kwa kuwa yanatufanya kama kioo kujitazama tulikotoka, tulipo na tunakoenda, wakati wenzetu wanajadili haya mambo katika vyombo mbalimbali ya kimataifa sisi tunasema wanaoleta mada za kujadili wana wivu. Tutafika kwa mwendo huu?
haya bwana we subiri kuabudiwa

Hii ni nafsi kwetu kujifunza namna wenzetu walivyofanikiwa kumjengea mazingira Madiba kuabudiwa hivyo wakati sisi tuhahangaika kutafuta kasoro kadhaa kuwadhalilisha viongozi wetu ambao wamefanya makubwa si kwa nchi yetu tu ila kwa bara zima la Afrika na dunia.
haya bwana we subiri kuabudiwa, wakati wenzio wana fanya kazi, ukifanya vizuri watu wata sema tu, sio kwa kupiga kampeni au magazeti, China walifanya kazi wakafikia hapo walipo, vivyo hivyo kwa wajerumani, leo hii kenya tunasema wana strong economy eac nk walifanya kazi hawakutumia mitandao au magazeti kufikia hapo
 
Back
Top Bottom