Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
[h=2]Mambo 5 ambayo Watanzania wanayakataa na hawatovulimia tena chini ya CCM[/h] Na. M. M. Mwanakijiji
Nimejaribu kutafakari kwanini kuna wimbi la watu kuikataa CCM na serikali yake kwa nguvu zaidi wakati huu kama ilivyokuwa mwaka 1995. Miaka mingi imepita lakini wakati mwaka 1995 ilikuwa kwa kiasi kikubwa ni kutumia uhuru wa kujiunga na chama kingine zaidi ya CCM safari hii kuna kitu tofauti kinajionesha wazi. Watanzania kwa maelefu mijini na vijijini, wazee kwa vijana, wake kwa waume wameamua kuiambia CCM Bye Bye na kujiunga kwa mbwembwe kwenye CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO. Nilipotafakari zaidi mangamuzi haya mapya yanayoendelea nimejikuta nikirudi nyuma zaidi karibu miaka hamsini iliyopita.
Vitu vile vile vilivyowafanya Watanganyika na Waafrika kwa ujumla kuukataa ukoloni na serikali yake vimeanza kukataliwa tena na safari hii si dhidi ya ukoloni bali dhidi ya utawala ambao umegeuka na wenyewe na mwelekeo wa ukoloni usiopingika. Mambo haya matano manne kati yake yanajulikana sana kwani yamekuwepo katika tangazo la Azimio la Arusha la mwaka 1967 na ambalo ukweli wake bado unasimama.
Katika Azimio la Arusha tulitangaza hivi: Tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kututosha, tumenyanyaswa kiasi cha kutosha na tumepuuzwa kiasi cha kutosha Ni unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe, tunyonywe, tunyanyaswe na tupuuzwe. Sasa tunataka mapinduzi ili tusionewe, tusinyanyaswe na tusipuuzwe tena! Hivyo mambo manne ya kwanza ambayo Watanzania wanayakataa ni kuonewa, kunyonywa, kunyanyaswa na kupuuzwa. Tuyaangalie haya kidogo:
SOMA HAPA NA MWAMBIE MWINGINE