Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Nimesikia katika vichwa vya habari kwenye mojawapo ya magezeti yaliyosomwa leo redioni kwamba Hazina (Treasury -- i.e. Wizara ya Fedha) imesema haina hela sasa hivi kuilipa Dowans mabilioni hayo.
Na ni bora isiwe nazo kabisa hizo hela -- kwani itafanya ukatili mkubwa sana ikiwalipa hawa Dowans kwanza kabla ya mamia (bila shaka) ya wananchi wengine wanaodai malipo yao kutoka serikalini -- wengine kutokana na amri za mahakama halali za humu kwetu ndani -- siyo mahakama uchwara inayoketi katika sitting room ya RA.
Treasury iwasaidie wananchi, iweke madai hayo ya Dowans katika foleni, mwisho kabisa, yatangulie yale yaliyokuja mwanzi, hata ni kama ya miaka kumi iliyopita. Dowans ina haraka gani? Inataka ilipwe kabla Bunge kukutana, na ambalo RA na genge lake la wezi linahofu linaweza kupiga kura kusitisha malipo hayo?
Na ni bora isiwe nazo kabisa hizo hela -- kwani itafanya ukatili mkubwa sana ikiwalipa hawa Dowans kwanza kabla ya mamia (bila shaka) ya wananchi wengine wanaodai malipo yao kutoka serikalini -- wengine kutokana na amri za mahakama halali za humu kwetu ndani -- siyo mahakama uchwara inayoketi katika sitting room ya RA.
Treasury iwasaidie wananchi, iweke madai hayo ya Dowans katika foleni, mwisho kabisa, yatangulie yale yaliyokuja mwanzi, hata ni kama ya miaka kumi iliyopita. Dowans ina haraka gani? Inataka ilipwe kabla Bunge kukutana, na ambalo RA na genge lake la wezi linahofu linaweza kupiga kura kusitisha malipo hayo?