Fungu la kukosa
Member
- Jun 16, 2009
- 64
- 0
CCM ni Chama cha Mafisadi, na ambaye anaupinga ufisadi basi huyo si Mwana CCM halisi.Huu ndiyo ukweli wenyewe na wala haupingiki. Wapo baadhi ya wana CCM wachache ambao wanaokerwa sana na tabia hii mbaya ya ufisadi wa mali za umma, lakini wanakosa platform ya kuzungumzia kero zao kwa kuhofia kufanyiwa yale waliyo fanyiwa marehem Hores Kolimba na Prof Kighoma Malima. Baada ya ukweli kudhihiri na uwongo kujitenga, Malima alijitoa ndani ya CCM na kuanzisha kambi yake ya upinzani dhidi ya CCM. Alipokwenda nchini Uingreza kwa ziara binafi(inasemekana alikwenda tafuta misaada ya kisiasa), makachero wa CCM nawo wakapanda ndege na kufuatilia nyendo zake na walipowasili huko walijifanya ni waandishi wa habari na hivyo kumfuata mojakwamoja hotelini alikofikia na kumuhoji mahojiano bandia huku wakijua walichokuwa wamedhamilia kukifanya zidi ya uhai wake. Baada ya masaa machache tu kupita Prof Mlima aliripotiwa kuwa amefariki kwa ugonjwa wa pressure ya moyo. Kwa upande wake Kolimba, mambo ni karibu sawa na yaleyale aliofanyiwa mwenzake. Akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge huko Dodoma, alianguka chini na kufariki dunia baada ya nukta chache tu za kukamata kipaza sauti kinachodawi kuwa kilikuwqa kimeandaliwa rasmi kwa yeye Kolimba kukitumia wakati wa kujitetea kwake pale aliposhutumiwa kwa kusema CCM ilikuwa imepoteza muelekeo wa kisiasa. Kwahivyo, kwa mifano hiyo michache, yatosha kuwa ni vikwazo halisi kwa wana CCM wapenda haki kueleza bayana dukuduku zao dhidi ya wenziwao wasiopenda haki na usawa katika nchi hii ya Tanzania. Kila mtu anazingatia ule msemo maarufu wa kiswahili usemao YARAABI NAFSI!!!!!!!!!!! nahivyo kuifanya agenda nzima ya ufisadi kuwa ni swala nyeti na la siri ndani ya CCM. MPO HAPO WA BONGO!!!!!!!!!!!!!!? HUU NDIO UKWELI HALISI NA SABABU HASWA YA USIRI WA UFISADI NDANI YA CCM.
Last edited: