Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Serikali ya Malawi Malawi inajiandaa Kuhalalisha Uhakaba Monday, October 26, 2009 8:37 AM
Serikali ya Malawi inajiandaa kupitisha sheria itakayohalalisha biashara ya ukahaba nchini humo kwa kuwaruhusu makahaba wafanye ukahaba kwenye majumba yao badala ya kusimama barabarani. hatua hiyo ya serikali ya Malawi inakusudia kuwalinda wanawake wanaojiuza barabarani kutokana na manyanyaso wanayopata kutoka kwa wateja wao.
Waziri wa masuala ya jamii na maendeleo wa Malawi, bi Patricia Kaliati akiongea na shirika la habari la Reuters alisema kwamba muswada wa kuruhusu biashara ya ukahaba majumbani nchini humo uko kwenye hatua za mwisho kupelekwa bungeni ili upitishwe uwe sheria.
"Tunataka watoke mitaani wakafurahie tendo la ngono kwenye majumba yao na hivyo kuepukana na kunyanyaswa kijinsia au kubakwa na wateja wao na hivyo kuwalinda na gonjwa la ukimwi", alisema Kaliati.
Ugonjwa wa ukimwi nchini Malawi yenye idadi ya watu milioni 13 umeishaua zaidi ya watu laki nane tangia ulipoingia nchini humo mwaka 1985.
Jitihada za kuwaelimisha watu kujikinga na ugonjwa huo zimesaidia kupunguza idadi ya waathirika toka asilimia 14 hadi 13. Madawa mengi yanayotolewa bure kwa waathirika yamesaidia kupunguza idadi ya vifo vya waathirika kwa asilimia 70.
Hata hivyo muswada huo wa kuhalalisha ukahaba tayari umeishakumbwa na upinzani toka taasisi mbali mbali.
"Malawi ni nchi ambayo raia wake ni waumini wa dini zinazokataza ukahaba kwa njia yoyote ile, hivyo lazima tusisahau kuzingatia mila zetu na imani zetu za kiroho", alisema Mavuto Bamusi, mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu.
Waziri Kaliati aliutetea muswada huo kwa kusema lengo lake kubwa si kuhalalisha ukahaba bali kuwalinda wanawake wanaofanya ukahaba.
Miji mikubwa ya Malawi imekuwa na ongezeko la madada poa katika miaka ya hivi karibuni na miongoni mwa wasichana wanaojiuza wengine wana umri mdogo kuanzia miaka 12. http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=3413526&&Cat=2