Makwaiya na je tutafika? Anaichambua ccm sasa ivi chanel ten

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,499
86,037
Dear Members! kama mtaweza angalieni chanel ten nimeipenda sana motion ambayo ni mwendelezo wa kipindi cha wiki iliyobaki! mjumbe mmoja anauliza kuhusu wapi iliishia tume ya Mzee Mwinyi kuhusu wabunge waliokuwa wanalumbana? Sabato sijaomuona bado
 
Anaeongea sasa ivi ni Bashiru Ally sijui ni nani lakini anazungumzia jinsi CCM walipokosea kuwa mwanzoni CCM ilikua chama cha wanyonge lakini sasa kimegeuka na kuwa chama cha wachache, juhudi zilizofanywa ni pamoja na zile za SOKOINE ambaye pia alitoweka ghafla....anadai kilichokosekana leo ni ile sera ya ujamaa na kujitegemea na kuletwa sera ambazo hazitekelezeki kama zile za NYARUBANJA...Unamiliki ardhi ambayo si yako mfano madini ni yetu lakini hatuyamiliki...
 
Bashiru Ally ni lecturer UDSM! Anauliza nani mswahili anaemiliki madini kama sio kuishia kwenye vijiwe vya gahawa, anadai hakuna mjadala wenye muelekeo na iliyepo ni ile inayoongozwa na miiko ya do this and not that... viongozi serikalini ni walanguzi na wajasiriamali wanaojilimbikizia mali na ndio source ya makundi CCM
 
Mkono aliwahi kuomba kuongezwa alama ya tatu juu ya jembe na nyundo.....kuwakilisha wajasiriamali...sijui nembo ingeonekanaje
 
Makwaia anauliza kwanini wafanyakazi hata wale wa kawaida wanatoka nje ya nchi na sio hapa? Bashiru anajibu nae kwa kuuliza kuwa hao wawekezaji ni akina nani? mtaji wao ni upi? uwekezaji ni ulimbikizaji na kitendo hicho hakipo Tanzania: Mzee Kitine naye yupo! Makwaiya na mwana CCM alieasi??? simuelewi na sasa anamuuliza Miraji kuwa CCM ilikua na uwezo wa kuangalia mbali zaidi lakini je leo yapo? jibu! hayapo na mara ya mwisho ilitolewa 1987 hadi sasa hakuna program ya chama tena iliowahi kutolewa
 
Kuna ombwe CCM na sasa mtu mmoja anakuwa mjumbe wa kamati kuu, mbunge, waziri, n.k , ni uroho wa madaraka na waliowengi wanafanya kazi kwa mazoea kama ilivyo sekretarieti ya ccm ya sasa!!!
 
NEC haina nafasi tena ya kukosolewa na kilichobaki ni kusifiana tu! mfano unajenga daraja la milioni tano na kuanza kusifiana yaani umetumia nyundo kubwa kuua panya mdogo! halmashauri kuu ya CCM ni heri ikawa kama bodi kuliko kuruhusu kila mtu aingie... na sasa ni Mzee Kitine anaulizwa kuwa vikao vya chama vimekaakaaje? na kwamba mzee kitine nae alishawahi kushughulikiwa baada ya kutoa mawazo yako!!!
 
Naona Mze Kitine nae kaanza kwa kujielezea profile yake kuwa alishika uongozi akiwa na umri chini ya miaka 30 NA kwamba alikua pia katika idara ya usalama wa Taifa!! vikao vilivyokuwa vikiongozwa na Nyerere vilikua vimejaa challanges ambazo zililenga kujenga chama kama Mzee Mtandika-Pwani, Mzee Kaaya - Arusha kuwa waliwahi kumkosoa Nyerere na Nyerere alikubali kukosolewa! utamaduni huo sasa umetoweka!!
 
Mzee Kitine sasa anamfagilia Dr. Slaa na kwamba sasa CCM imepoteza mwelekeo, anadai vikao vya CCM vimejaa fitna, majungu, maneno na kugombana na kwamba sio chama tena cha wakulima!!! ni chama cha WAFANYABIASHARA!!!
 
Kuna ombwe CCM na sasa mtu mmoja anakuwa mjumbe wa kamati kuu, mbunge, waziri, n.k , ni uroho wa madaraka na waliowengi wanafanya kazi kwa mazoea kama ilivyo sekretarieti ya ccm ya sasa!!!

Na bado akataka ubunge wa SADC bila kujua hiyo SADC kirefu chake ni nini(Sophia Simba)
 
Nyerere hakuteuwa mtu bila kuwa-consult usalama wa taifa... sasa mambo yanaenda hovyo tu na kwamba sasa kuna makatibu wakuu ni wezi na viongozi wengine ni wezi, naona anakazia kwenye makatibu wakuu kwenye wizara ingawa hajawataja!! Makwaiya kampiga stoop kidogo tu mzee kitine awataje majina!!!
 
SWALI: Kazi ya chama inaishia wapi? Miraji anajibu, kazi za chama ndani ya chama zilifanywa na vijana including itikadi ya chama, vijana wengi sasa hawana hio na kwamba wameokotwa okotwa tu!!! sasa hawa vijana wa sasa hawakilindi bali wanakibomoa! yaani vijana wenyewe wanajipigia debe waingie madarakani pamoja na kutumiwa na baadhi ya wazee
 
Vijana wa sasa wanauza majengo! umetolewa mfano wa jengo lililopo Morogoro limekodishwa na bado wenyewe hawafaidiki!! Ex-Officials wamewaacha na kuruhusu baadhi ya viongozi kama speaker na mawaziri but wakati huohuo wanaingia kwenye CC hivyo hata kama ataachishwa uwaziri bado ataendelea na wadhifa wake kwenye NEC...
 
Tanzania chama cha siasa ni kuwapiginia watu walioonewa na kunyanyaswa na wakoloni...
 
Je baada ya uchaguzi hakuna mikutano tena ya siasa? au hadi uchaguzi? Mzee Kitine anajibu; chama cha watu ni lazima wajue katiba na wajibu wao kila wakati na sio kusubiri wakati wa chaguzi!! vingenevyo kazi ya chama haitakuwa na manufaa kwa mtu!! CCM imekua chama cha wenye cash huna cash basi na ujamaa haupo tena!!! ujamaa maana yake ni kwamba; mali zote za nchi zitumike kuboresha maslahi ya wananchi wake! kuna kazi kubwa ya kukirudisha CCM kwenye misingi yake inangawa uwezekano huo haupo!! kauwa huyu mzee
 
Kikwete karithi matatizo kutoka awamu zilizopita, lakini kapata fursa ya kurekebisha. Chama kikimfia, historia itamhukumu-Miraji
 
Haki na dhuluma haviwezi kukaa pamoja-Dr. Kitine's closing remarks
 
Maneno ya malumbano ndani ya CCM yanasaidiaje chama? Bashiru anasema JK amepata fursa ya kubadilisha mambo asipoitumia hio fursa basi historia itamhukumu! CCM itakufa ila Tanzania kwanza na lazima kupinga ufisadi na rushwa! Mzee Kitine anamalizia kuwa HAKI haiwezi hata siku moja ika CO-EXIST na dhuluma ila ili kuweza hilo ni kuwa na moyo mkubwa wa kuchange mambo...Makwaiya kamkatiza tena huyu dingi...alitaka amwage sumu! haya usiku mwema kipindi kimeisha
 
Back
Top Bottom