Makinda aunda tume ya bunge kwenda Mtwara

Spika Anna Makinda kwa mara nyingine tena amewafunga midomo wabunge kwa kukataa hoja yoyote binafsi ambayo ilikuwa inataka kujadili swala la gesi ya Mtwara eti kwa kisingizio kwamba kuwa ni zito na nyeti, linalopaswa kujadiliwa kwa hekima kubwa na busara ya kutosha ili kupata muafaka wa kweli.

Swali ni kwamba wabunge waliochaguliwa na watanzania hawana busara za kutosha kujadili maswala la kitaifa???? na nina anapaswa ajadili maswala yetu??

Huu ni muendelezo mwengine wa kubananga demokrasia.

Kwa hili nadhani spika ameamua vyema. Ukweli ni kuwa mara nyingi huwa nahoji busara ya wabunge wetu wengi na iwapo kweli wananchi tunapata value for money kwenye huu mchakato wa bunge. Nadhani wengi wa wabunge wanatumia vichwa vyao kufugia nywele na si kutafakari mustakabali wa nchi yetu.
 
yaani anatuaminisha watanzania wawakilishi wetu tuliowachagua hapo bungeni watuwakilishe tulichagua mabolizozo ambayo hayajui a wala z ya unyeti wa taifa hili na rasilimali zake. Wabunge wetu hawana akili na busara ya kujadili masuala nyeti ya kitaifa mbona hii ni kashifa nzito kwa bunge na uongozi wake. Nadhani amepotoka au alikusudia ili kuwalidhisha wakubwa wake waliomweka hapo

Hajapotoka ndugu yangu huo ndio ukwelu wenyewe. Hata uwepo wake kwenye uspika ni ushahidi tosha wa hali ilivyo ndani ya bunge.
 
Ndg yangu makinda amefanya vema ameshajua bunge letu halina maana tena,halina maamuzi,ni bunge la watu wasio na uwezo wa kujadili mambo ya maana,limebaki kama kijiwe cha kupiga soga na kungonoana tu.

vema??????????? kwa hiyo kuzuia hoja za msingi zisisemwe ama kujadiliwa ndio kuwa vyema? au kuficha madudu yasizungumzwe ni kufanya vema?
hii nayo unaiona busara?
 
Kwa hili nadhani spika ameamua vyema. Ukweli ni kuwa mara nyingi huwa nahoji busara ya wabunge wetu wengi na iwapo kweli wananchi tunapata value for money kwenye huu mchakato wa bunge. Nadhani wengi wa wabunge wanatumia vichwa vyao kufugia nywele na si kutafakari mustakabali wa nchi yetu.
Na hapo ndipo busara na uimara wa uongozi wa Bunge unapotakiwa kuonekana. Kama kiongozi wa mhimili wa utawala, Spika alikuwa na mamlaka (uwezo) wa kuinglia suala hili tangu mapema, lakini hakufanya hivyo mpaka pale alipoanza kupokea hoja (shinikizo) kutoka kwa wabunge hao hao ambao baadhio yao tunawatuhumu kwa kukosa busara.
Kwangu mimi, udhaifu wa wabunge ni kielelezo cha udhaifu wa uongozi wa Bunge. kama tungekuwa na uongozi wa Bunge imara, wabunge dhaifu wasingepata nafasi ya kuonyesha udhaifu wao
 
So Mbumbumbu wamejaa pale????
Asanteeeeee(in madam spikaz voice)
 
Na hapo ndipo busara na uimara wa uongozi wa Bunge unapotakiwa kuonekana. Kama kiongozi wa mhimili wa utawala, Spika alikuwa na mamlaka (uwezo) wa kuinglia suala hili tangu mapema, lakini hakufanya hivyo mpaka pale alipoanza kupokea hoja (shinikizo) kutoka kwa wabunge hao hao ambao baadhio yao tunawatuhumu kwa kukosa busara.
Kwangu mimi, udhaifu wa wabunge ni kielelezo cha udhaifu wa uongozi wa Bunge. kama tungekuwa na uongozi wa Bunge imara, wabunge dhaifu wasingepata nafasi ya kuonyesha udhaifu wao

Unafurahisha unavyojaribu kutenganisha uwezo wa wabunge na wa viongozi wao.
 
ndo maana baadhi yao wanasubiri kuwezeshwa ili kuropoka wanavyojisikia. wabunge c wanawakilisha wanachi au anataka sote tuingie humo ndo watuchuje wenye busara wp na wasio ni wp.
 
Heshima mkuu.kwa mtazamo wangu hili ni tusi baya sana kwa wazazi wetu wote na sio kwa huyu bibi tu kwani ukimshutumu mtu kwaajili ya kitu ambacho ni relating to or concerning nature. hapo ebu jaribu kumfikria mtu mwingine amwambie hivyo mama yako mzazi utajisikiaje? hata kama tunaichukui ccm pamoja na watu wake lakini tujaribu kuwasilisha hisia zetu kwa namna ambayo inaweza kuwa sio matusi. uliposema hivyo nimemwona mama yangu na nikajihisi vibaya sana


Absolutely
 
Nawashangaa kweli, Kwani alilokosea huyu mama ni lipi? Yaani utitiri wa wabunge wale wote ambao hawawezi kukataa hata pale wanapoambiwa nchi yenye watu milioni 45 inaungana na nchi yenye watu milioni 1.5 halafu kila kitu kitakuwa sawa kuanzia uwakilishi kwa masuala nyeti kama vile kumteua mgombea urais, bajeti, n.k wao ni sawa tu bila kuhoji lolote utasema wanahekima hao.?

WABUNGE WA SASA UKIONDOA WACHACHE SANA HASA WA VYAMA VYA UPINZANI NA KAMA 3 TU WA CCM, NDIYO WANA HADHI YA KUONGELEA MASUALA YA NCHI. SASA MTU KAMA NCHEMBA AU YULE WA DODOMA ALIYETUKANA KULE ARUSHA NI WABUNGE NAO ETI! SHHEET!
 
Absolutely


WEDNESDAY, 30 JANUARY 2013
Imetumwa kwenye Jamii
Imesomwa mara: 3
Tuma Maoni
http://www.fullshangweblog.com/2013...limo-na-kukagua-miradi-kigoma-vijijini/5-137/
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana CCM, UVCCM Bw. Martin Shigela akishiriki katika kupalilia shamba la Karanga katika kijiji cha Nkungwe Tarafa ya Mabembe Wilaya ya Kigoma Vijijini wakati alipotembelea na kujionea shughuli mbalimbali na kukagua miradi inayotekelezwa na wananchi kwa pamoja na Serikali


 
Heshima mkuu.kwa mtazamo wangu hili ni tusi baya sana kwa wazazi wetu wote na sio kwa huyu bibi tu kwani ukimshutumu mtu kwaajili ya kitu ambacho ni relating to or concerning nature. hapo ebu jaribu kumfikria mtu mwingine amwambie hivyo mama yako mzazi utajisikiaje? hata kama tunaichukui ccm pamoja na watu wake lakini tujaribu kuwasilisha hisia zetu kwa namna ambayo inaweza kuwa sio matusi. uliposema hivyo nimemwona mama yangu na nikajihisi vibaya sana
Yeye maamuzi yake ni zaidi ya matusi kwasababu athari yake nikubwa kwa maisha yetu lakini hilo unalosema ni tusi halimuadhiri kwa chochote
 
Yeye maamuzi yake ni zaidi ya matusi kwasababu athari yake nikubwa kwa maisha yetu lakini hilo unalosema ni tusi halimuadhiri kwa chochote

Unajua kila mmoja ana mtazamo wake kwenye mambo kwa namna ya tofauti.
Je iwapi busara ya mtu aliyetukanwa naye akarudisha tusi?
 
Huenda akawaudh tena watu,,,,maana mambo yooote yanayotokea huwa anayazima,lakin jamani me nahis ni AMRI TOKA KWA WALOMUWEKA,MSIMLAUMU
 
Maccm bwana? Cdm hawajatoka nje?maana wakikubali basi wote hawana busara

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Tume ya nini? kwa gharama za nani?
Ni Ripoti ngapi amefungia vitumbua mpaka sasa? Kama anataka Tume basi amshauri JK waunde Tume ya Kimahakama kuchunguza mauaji holela ya raia nchini.

Kamanda Lissu alikuwa sahihi "another silly session"
 
hapo wanachofanya ni kuwapooza wa tz kwani wanajuwa kuwa wa tz ni wasahaulifu/ wepesi kusahau na wazito kufatilia mambo
 
Back
Top Bottom