Spika Anna Makinda kwa mara nyingine tena amewafunga midomo wabunge kwa kukataa hoja yoyote binafsi ambayo ilikuwa inataka kujadili swala la gesi ya Mtwara eti kwa kisingizio kwamba kuwa ni zito na nyeti, linalopaswa kujadiliwa kwa hekima kubwa na busara ya kutosha ili kupata muafaka wa kweli.
Swali ni kwamba wabunge waliochaguliwa na watanzania hawana busara za kutosha kujadili maswala la kitaifa???? na nina anapaswa ajadili maswala yetu??
Huu ni muendelezo mwengine wa kubananga demokrasia.
Kwa hili nadhani spika ameamua vyema. Ukweli ni kuwa mara nyingi huwa nahoji busara ya wabunge wetu wengi na iwapo kweli wananchi tunapata value for money kwenye huu mchakato wa bunge. Nadhani wengi wa wabunge wanatumia vichwa vyao kufugia nywele na si kutafakari mustakabali wa nchi yetu.