Majina ya Waliopendekezwa Viti Maalum na hoja za Leticia Musore

MWENYEKITI WA BARAZA LA WANAWAKE TAIFA (BAWACHA)...... SAWA NA U.W.T...AHAMIA N.C.C.R-MAGEUZI.......hii ndiyo habari
 
Aliongeza kwamba katika uchaguzi wa Bawacha, yeye alishika nafasi ya tano kwa kura zaidi ya 60 za wanawake wa chama hicho huku Suzan Lyimo akipata kura sita, Grace Kiwelo mbili na Halima Mdee saba, lakini hakuteuliwa katika uchaguzi wao wa wabunge 25 jambo ambalo si la kidemokrasia.

Dr Kitila Mkumbo kama sikosei wewe ulikuwa ni consultant katika kutafuta nani aingie kwenye ubunge wa viti maalumu wa Chadema. Kwa kuzingatia vigezo ulivyoweka na points walizopata wale wote walioomba nafasi ya ubunge wa viti maalum kupitia chadema, je waweza tueleza hayo aliyoyasema huyo mama yana ukweli kiasi gani????
 
Pole sana Urassa najua lazima utampinga huyu mama hata kama ana hoja za msingi ni vizuri unge declear interest zako (kabila) halafu ungemshambulia mama musori. Mimi binafsi sikupenda chama kumteua Mwanaume kuwateulia wanawake wawakilishi wa viti maalum mie kwangu hilo halijakaa sawa otherwise kama ndio katiba ya chama ipo hivyo na tuiheshimu.
Walipewa nafasi ya kujichagua waka shindwa na yeye akiwa kiongozi ulitegemea nini?
 
Dr Kitila Mkumbo kama sikosei wewe ulikuwa ni consultant katika kutafuta nani aingie kwenye ubunge wa viti maalumu wa Chadema. Kwa kuzingatia vigezo ulivyoweka na points walizopata wale wote walioomba nafasi ya ubunge wa viti maalum kupitia chadema, je waweza tueleza nani alipata nini??? Maana huyo mama analalamika kuwa kwa vigezo vya points vilivyowekwa alipata points 60 na alishika nafasi ya tano akiwa juu ya watu kama Lucy Owenya, na Halima Mdee. Je hayo aliyoyasema huyo mama yana ukweli kiasi gani???? Isijekuwa ana msingi mzuri wa kulalamika na hasa ukizingatia nafasi aliyokuwa nayo ndani ya Chadema
 
MOSHI unaoendelea kufuka ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) unaonekana kuficha moto.

Baada ya uchaguzi mkuu mwaka huu, hali ndani ya chama hicho inaonekana kutokuwa shwari hasa kutokana na mgawanyiko wa wazi unaojitokeza sasa.

Chachu zaidi ilijitokeza hivi karibuni baada ya Katibu Mkuu wa Chama hicho ambaye pia alikuwa mgombea urais, Dk. Willibrod Slaa, kukataa kutambua matokeo yaliyompa ushindi Rais Jakaya Kikwete, aliyekuwa akigombea kwa tiketi ya CCM.

Hali hiyo ndiyo iliyofanya baadhi ya wabunge wa chama hicho kususia pia hotuba ya Rais Kikwete, alipokuwa akizindua Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Novemba 18, Dodoma.

Tukio hilo lilitanguliwa na la kutohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kulikofuatiwa usiku na hafla ya kupongeza wabunge, ambapo baadhi ya wabunge wa chama hicho walihudhuria.

Hatua hiyo ilisababisha mgawanyiko wa wazi, kwa baadhi ya wabunge kutoshiriki ususiaji huo na kutoa sababu zao walizoona ni za msingi.

Lakini, kana kwamba hiyo haitoshi, juzi Mwenyekiti wa Chama hicho wa Mkoa wa Mbeya, Sambwee Shitambala akatangaza kujiuzulu wadhifa huo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizoelekezwa kwake.

Shitambala aliwambia waandishi wa habari kuwa uongozi wa chama hicho kitaifa unamtuhumu kuhongwa Sh milioni 600 ili ahujumu chama chake na kushindwa kutwaa jimbo la Mbeya Vijijini.

Wakati hayo yanaendelea, huku uongozi wa juu ukikataa kuyazungumzia kuchelea majibizano, jana Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Leticia Musori, alitangaza kukihama chama hicho na kujiunga rasmi na NCCR-Mageuzi. Kiini cha hatua hiyo ni uteuzi wa wabunge wa viti maalumu katika chama hicho.

Musori aliwambia waandishi wa habari jana kuwa hakushirikishwa katika uamuzi wa kuteua wabunge hao na kudai kuwa waliteuliwa kwa kufuata uhusiano na vigogo wa chama hicho.

Akizungumza wakati anakabidhiwa rasmi kadi ya NCCR-Mageuzi na Mwenyekiti wa Chama hicho, James Mbatia, Musori alisema uamuzi wake unatokana na wanawake kukosa haki na mfumo dume kuendekezwa ndani ya chama hicho kwa kutoshirikisha wanawake katika vikao vya uamuzi.

Alisema kitendo cha chama hicho kuendeleza uozo na udikteta katika kufanya uamuzi, huku pia kikiendeshwa kama kampuni ya wakubwa katika kufikia uamuzi mbalimbali.

Musori alisema uchaguzi halali wa Bawacha ulivurugwa na viongozi wa juu wa chama hicho, ili kutoa nafasi kutoa viti maalumu kwa wanaowataka badala ya kuachia vikao vya wanawake wa chama hicho kuamua kama zinavyoelekeza kanuni za Bawacha.

Musori alisema jambo lingine ni kutokubali utumwa wa Mwenyekiti Mbowe ambaye alidai hataki kupingwa katika uamuzi wake.

"Mimi nilikuwa nikipingana na Mbowe katika hoja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupinga utaratibu wa Chadema ambao Mwenyekiti anakuwa mtia saini ilhali yeye ndiye Mwenyekiti wa vikao vya Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, ambavyo kimsingi ndio vyenye mamlaka ya kusimamia Sekretarieti ya chama," alisema.

Aliongeza kwamba katika uchaguzi wa Bawacha, yeye alishika nafasi ya tano kwa kura zaidi ya 60 za wanawake wa chama hicho huku Suzan Lyimo akipata kura sita, Grace Kiwelo mbili na Halima Mdee saba, lakini hakuteuliwa katika uchaguzi wao wa wabunge 25 jambo ambalo si la kidemokrasia.

Alisema kutokana na uamuzi huo wa vigogo wa Chadema kuwanyima haki wanawake waliochaguliwa na wenzao, wengi watahama chama hicho ambacho alidai kipo kwa ajili ya maslahi ya wachache na hakina demokrasia.

Aliendelea kudai kwamba akiwa na cheo hicho cha Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mjumbe wa Baraza Kuu la Chadema na Mweka Hazina wa Umoja wa Madiwani wa Chadema na kukidhi vigezo vilivyowekwa na viongozi hao, bado hakuteuliwa kuwa mbunge wa viti maalumu kutokana na kumpinga Mbowe.

Alisema amechukua uamuzi wa kuhamia NCCR - Mageuzi ili aendeleze mageuzi baada ya kufanya utafiti na kuona kuwa chama hicho ndicho kinamfaa na kusisitiza kuwa tatizo si kupata uongozi kwani alikuwa na vyeo vingi ndani ya Chadema.

Akimpokea mwanachama huyo na kumkabidhi kadi, Mbatia alitoa rai kwa wanasiasa kuzingatia haki kwa kila mmoja, kwani bila kutoa haki Taifa haliwezi kwenda vizuri, na alitaka haki ianzie kwenye familia hadi Taifa.

Septemba mwaka jana, kutokana na kilichoonekana ni mchezo mbaya ndani ya Chadema katika kutafuta uongozi wa Baraza la Vijana (Bavicha), kulitokea kutoelewana kambi, moja ikiwa ya Mwenyekiti Freeman Mbowe na nyingine ya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe.

Mvutano huo ulisababisha uchaguzi kufutwa na Baraza la Wazee na hivyo aliyekuwa akiwania nafasi ya uenyekiti, David Kafulila wa kambi ya Zitto, kuhama chama na kujiunga na NCCR-Mageuzi na sasa ni Mbunge wa Kigoma Kusini kupitia chama hicho.


Huu ni wakati wa kuwajua wanachadema wa kweli na mapandikizi,Chadema kamwe haitayumba.Mapandikizi wote tutawajua watatoka na cream itabaki.
Mwenyekiti wa bawacha was just there and she had no impact,watu kama nyie ambao mnataka kushuhudia anguko la chadema halitatokea.
 
Mkuu hii habari iko hapa tangu juzi, next time check kama kuna stori inayofanana na ile unayotaka kupost kabla hujaposti ya kwako kuturahisishia na sisi wachangiaji na wasomaji.


Asante kwa ushauri, inshallah nitaufanyia kazi.
 
mkuu, sidhani kama chadema inaongozwa na kuwa moerated na JF... and i am worried kama ulichouliza ndio utaratibu wa kupata details...

ninachoona ni kuishi kama tulivyozoea wengi, kubwabwaja, kutokufuata utaratibu wa kujua jambo na kudandia terni kwa mbele. if one reads what you have written, atabaki na maswali yafuatayo

  1. hivi huyu wa wapi hajui taratibu za kupata taarifa za kuitendaji hasa chamani?
  2. katumwa na huyo mama?
  3. au ndiye huyo mama?
  4. vipi kamuandikia kitila kwenye public forum wakati tuna pm options?

Ushauri wangu, unaweza kuwa na swali la msingi, lakini jaribu kufuata njia za msingi... otherwise swali lako la msingi linaweza kuwa kama kauli za vijiwe vya kahawa na konyagi

thanks

acid
 
Aliongeza kwamba katika uchaguzi wa Bawacha, yeye alishika nafasi ya tano kwa kura zaidi ya 60 za wanawake wa chama hicho huku Suzan Lyimo akipata kura sita, Grace Kiwelo mbili na Halima Mdee saba, lakini hakuteuliwa katika uchaguzi wao wa wabunge 25 jambo ambalo si la kidemokrasia.

Dr Kitila Mkumbo kama sikosei wewe ulikuwa ni consultant katika kutafuta nani aingie kwenye ubunge wa viti maalumu wa Chadema. Kwa kuzingatia vigezo ulivyoweka na points walizopata wale wote walioomba nafasi ya ubunge wa viti maalum kupitia chadema, je waweza tueleza hayo aliyoyasema huyo mama yana ukweli kiasi gani????

baada ya akina mama kushindwa lupitisha utalatibu wa kuwapata, consultant alifanya kazi hiyo, kwa list tuliyopewa jana na iliyokwenda NEC huyo mama alikuwa 29, mbona akulalamika mapema?
 
Hivi ni kweli kuwa wanaozunguka katika vyama nia yao ni kupata vyeo tu??? Kama kweli Katibu Mkuu wa CHADEMA kasema hivyo, sasa naanza kuelewa. Vipi Shibuda, Lema na wengineo. Kumbe Slaa uko sahihi, wote hao shida yao ni vyeo, hivyo huyo mama Musori naye asilaumiwe hata kidogo naye pia anazunguka kutafuta cheo. Hata Dr. Slaa haukuanzia Chadema, mbona yeye hajisemi mwenyewe???? Jibu sasa kama wewe mwanaume.
 
mkuu, sidhani kama chadema inaongozwa na kuwa moerated na JF... and i am worried kama ulichouliza ndio utaratibu wa kupata details...

ninachoona ni kuishi kama tulivyozoea wengi, kubwabwaja, kutokufuata utaratibu wa kujua jambo na kudandia terni kwa mbele. if one reads what you have written, atabaki na maswali yafuatayo

  1. hivi huyu wa wapi hajui taratibu za kupata taarifa za kuitendaji hasa chamani?
  2. katumwa na huyo mama?
  3. au ndiye huyo mama?
  4. vipi kamuandikia kitila kwenye public forum wakati tuna pm options?

Ushauri wangu, unaweza kuwa na swali la msingi, lakini jaribu kufuata njia za msingi... otherwise swali lako la msingi linaweza kuwa kama kauli za vijiwe vya kahawa na konyagi

thanks

acid

Kwa ushauri zaidi, kuna website ya chama pia: Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), angeweza kuitumia hiyo kutoa dukuduku zake kama si kupata email za viongozi wa kuu wa CHADEMA ambao wanaweza kumsaidia kueleza hizo dukuduku zake.
 
Naema hivi.............kama hujipendi, hebu thubutu kutangaza nia ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA, weeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!! kamuulize Zitto kama hukuipata fresh. Chama kina wenyewe babu weeeee....... wengine wapiga debe tu.
 
Mama Msori katika rank ulikua No 29 ndiyo ulideserve kulingana na vigezo vilivyowekwa na kama wachakachuaji wasingechakachua majimbo ya Shinyanga mjini, Kibaha mjini, Karagwe , Tarime, Segerea etc lazima ungekuwa mmoja wa wabunge wa Chadema, embu nikuulize swali kama ungepata ubunge bado ungejiuzulu?
 
Chadema wanatakiwa kuwa imara kukabiliana na wimbi ambalo CCM kwa kushirikiana na NCCR wataliunda ili kuwashusha hadhi mbele ya jamii,wanatakiwa na wao watumie njia zote za haki ya msingi kuuhabarisha umma ukweli ni upi,wanaotaka kuondoka waache waende na kama kuna wanawake wengine wanaotaka kwenda naye leticia NCCR wamfuate tuu hakuna shida,Chadema ni taasisi itapambana na mfumo kandamizi unaosisitizwa na CCM kwa msaada wa vyama pandikizi kama NCCR.Wananchi sasa hivi tunajua kupembua pumba na mchele kwa hiyo mwisho wa siku tutajua nani yupo kwa manufaa ya nchi yetu sio kwa manyufaa ya kutumikia mabwana wa CCM,Chadema kazeni buti wote waliochoka na kuendeleza mapambano ili kurudisha utawala wa sheria hapa nchini kwetu
 
Mkuu Sokomoko,

Pamoja na hoja zako za kumtetea huyu mama, lakini mimi ninadhani Mama ana mapungufu. Akiwa kama Mwenyekiti wa BAWACHA alitakiwa asimamie kuandaa utaratibu wa kuwapata wabunge na mawadiwani wa viti maalum.

Mara baada ya Uchaguzi wa 2005, kulikuwa na mjadala mkali sana wa jinsi wabunge wa Viti Maalum walivyopatikana, baada ya kuona kasoro hizo she was supposed kuitisha vikao vya BAWACHA ili waweke utaratibu wa kuwapata wabunge wa viti maalum. Lakini cha kusikitisha ni kwamba mpaka sasa hakuna utaratibu maalum wa kidemokrasia wa kuwapata wabunge na madiwani wa Viti Maalum. Nani alaumiwe na ilihali huyo Mama ndio alikuwa Mwenyekiti wa BAWACHA?

Kunapokuwa hakuna utaratibu uliowekwa ndipo nepotism inapoingia, maana watu watajiwekea vigezo vyao. Kwa maneno mengine, Mama nae alitarajia kwamba angependelewa kwa kuwa ni Mwenyekiti wa BAWACHA, baada ya kutupwa ndipo anaanza kulia.

Kwa sababu alishindwa kuandaa utaratibu wa kuwapata wabunge wa viti maalum, nadhani hakuwa na uwezo wa uongozi. Uongozi ni pamoja na kunyoosha mambo yote yaliyopinda au kuwekwa chini ya uvungu. Sasa kama nae alishiriki kuweka mambo uvunguni basi imekula kwake. Mwenyekiti atakayefuata anatakiwa kufanyia kazi swala hilo ili kuondoa dhana ya nepotism.

Angekuja na ushahidi kwamba katika kipindi alichokuwa Mwenyekiti alijaribu kuandaa utaratibu wa kuwapata wabunge wa Viti Maalum lakini hakupata support kutoka Uongozi wa Juu wa Chama na Kamati Kuu, hapo ningeweza kumwelewa. Je, anaweza kutuambia alifanya nini ili kuondoa dhana ya upendeleo wa kupata wabunge wa viti maalum?
 
Suala la watoto/ wake /ndugu/ mashemeji na wakwe wa vigogo kuteuliwa kuwa wabunge wa chadema (viti vya upendeleo) ulilishughulikiaje? Je, inawezekana kuwa ile orodha ya kwanza ambayo wakubwa wa Chama waliitolea macho huenda haikujumuisha majina ya watu wao? Kurudisha majina ya watu walewale ambao walikwepo awali tena kulihitaji mshauri mtaalamu kuendesha zoezi lile?
 
Dr Kitila Mkumbo kama sikosei wewe ulikuwa ni consultant katika kutafuta nani aingie kwenye ubunge wa viti maalumu wa Chadema. Kwa kuzingatia vigezo ulivyoweka na points walizopata wale wote walioomba nafasi ya ubunge wa viti maalum kupitia chadema, je waweza tueleza nani alipata nini??? Maana huyo mama analalamika kuwa kwa vigezo vya points vilivyowekwa alipata points 60 na alishika nafasi ya tano akiwa juu ya watu kama Lucy Owenya, na Halima Mdee. Je hayo aliyoyasema huyo mama yana ukweli kiasi gani???? Isijekuwa ana msingi mzuri wa kulalamika na hasa ukizingatia nafasi aliyokuwa nayo ndani ya Chadema

Ofisi za CHADEMA ZIKO KINONDONI, ni vizuri ukapeleke kero zako uko
 
Naema hivi.............kama hujipendi, hebu thubutu kutangaza nia ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA, weeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!! kamuulize Zitto kama hukuipata fresh. Chama kina wenyewe babu weeeee....... wengine wapiga debe tu.

kamuuliza na Masauni pia, au Wajua ugomvi wa Marehemu Anina chifupa na akina Nchimbi pale UVCCM?
 
Naema hivi.............kama hujipendi, hebu thubutu kutangaza nia ya kugombea uenyekiti wa CHADEMA, weeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!! kamuulize Zitto kama hukuipata fresh. Chama kina wenyewe babu weeeee....... wengine wapiga debe tu.

Zitto angehitaji haki ya kutaka kugombea angepiatia vikao vya chama sio kukurupuka kwenye magezeti mbona Shibuda aliadhibiwa kwa kusema tu nia yake ya kugombea uraisi mbona walitaka kumuuua kisiasa tafadhali sana tumeyaaona ya sita na wakurugenzi wote waliopewa demotion na makamanda wa polisi waliopelekwa mikoa njaa tu kwa kuwa na misimamo ya uzalendo zitto ananafasi ya kusema atakacho ndani ya chadema kitu ambacho CCM hairuhusu kabisa muulize Sitta yaliyompata na SHibuda
 
Kila siku CHADEMA CHADEMA CHADEMA HII IKOJE,MAANA YAKE NINI?HAYA NI MAELEZO MAFUPI;

  • Ni chama mbadala wa ccm
  • Ni chama kilichokuwa na wabunge wengi zaidi wa upinzani katikati bunge la JMT
  • Ni chama kilichoshika kasi ya aina yake kwa ukuaji wa Democrasia Tanzania
  • Ni chama chenye msimamo kisichoyumba mpaka sasa
  • Ni chama kinachoongozwa kwa mujibu wa katiba na sheria za Nchi
  • Ni chama chenye itikadi ya kisiasa
  • Ni chama kilichoenea sehemu zote Tanzania pamoja na mapungufu ya bajeti yake
  • Ni chama pekee kilichodiriki kuyakataa matokeo ya urais waziwazi bila kuficha
  • Ni chama kilichodhihirisha ulimwengu kuwa rais aliyeingia madarakani kaingia kwa wizi wa kura kwa kutoka nje ya bunge wakati alipotaka kuanza kuhutubia bunge.
  • Ni chama kitakachosimamia uundaji wa katiba mpya mpaka sasa.
  • Ni chama kilichoonesha UPINZANI wa kweli ndani na nje ya bunge.

Wapiga debe huwa siyo abiria, wao hubaki kituoni. Kenyawabisabisa oburwere ekerero keremobora. NCCR wako wapi, TLP nao wako wapi???
Ukipuuzia jambo dogo ujue makubwa yatakupata. Msilewe na ushindi huo kiduchu.
 
Back
Top Bottom