Majina ya Waliopendekezwa Viti Maalum na hoja za Leticia Musore

Sokomoko, Huyu mama Naomi Kaihula, yuko kwenye siasa tangu muda mrefu, ni mwanaharakati wa siku nyingi, wewe umemjulia CBE, sisi ametufundisha Tambaza, enzi hizo akiwa kasichana fulani.

Hoja yako ya msingi ambayo nakubaliana nayo, kama Chadema, ingepata kiti kimoja tuu cha ubunge wea upendeleo, then mtu stahiki kukikalia, alitakiwa awe ni Mwenyekiti wa BAWACHA, no one else!, sasa imepata vitu lukuki na bado hayupo, then kuna jambo.

Hakuna ubishi kuwa Chadema, kimeshaonyesha njia, kimesimama kuhesabiwa na hesabu zimeshaanza kuleta bajibu ya vema, na zinategemea kubalance mwaka 2015. Kwenye mada yangu kule nyuma, nilisema, Chadema, hawajajipanga, ili hesabu zibalance vizuri, nilisema nina matumaini watautumia muda huu kujijenga na kujipanga ili hesabu zao zibalance vizuri 2015.

Ili mtu fulani yoyote kupata sifa za kuchaguliwa kuiwakilisha Chadema kwenye ubunge wa viti maalum, lazima kuna sifa na vigezo valivyotumia, wengine walishakuweko huko miaka 5 iliyotangulia, walifanya nini mle mjengoni kustahili kuendelea?. Uchaguzi wa wabunge hao, umeendelea kukybikwa la ile ile dhana inayoitafuna Chadema, huku viongozi wa Chadema wakiendelea kuikanusha, Chadema can't survive in denial!, ni kama kansa, inakula ndani kwa ndani!.

Kwa maoni yangu binafsi mimi kama Pasco wa JF ambaye sio mwanachama wa chama chochote cha siasa bali ni mshabiki wa demokrasia ya kweli ndani ya bunge, Chadema, hawakumtendea haki Mwenyekiti wao wa Bawacha kunyima Ubunge mteremko, lakini pia huyo Mwenyekiti, ameonyesha udhaifu mkubwa kuihama Chadema ambayo sasa ni more promising na more prospective opposition na kujiunga na chama kinacho chechemea!.

Mimi nimekutana na huyu mama mwaka 2003 nilipaanza diploma yangu pale CBE na mpaka namaliza Advance yangu mwaka 2008 nimemuacha ni kweli huyu mama ni mwanaharakati wa TNGP na ninafahamiana vizuri sana na kwakwe huwa namtembelea ni kama mama yangu sina ubaya nae wowote wala chuki na huyu musori simjui na wala hanijui ila kama mpenda haki sijaridhika na chama kuchagua "mwanaume awachague wanawake wakawawakilishe wanawake"
 
amehamia nccr mageuzi kwa sasa baada ya kukosa viti maalumu ndani ya chadema huku akitoa shutuma za udini,ukabila na kila aina ya ubaguzi ambao anadai upo ndani ya chadema.
kwa umri wake hakupaswa kusema hayo yote,hivi muda wote wa utumishi wake ndani ya chadema hakuyaona hayo anayoshutumu kwa sasa?
Amejikwaa,amepotea njia,amekuwa mfa maji na sasa anatapatapa,akumbuke utu uzima dawa,akae kimya kama amegundua kuna uozo chadema na aelekee kule anakokuona kwake ni sahihi.chadema si yeye bali ni taasisi ya watu wenye mapenzi mema,wapenda mabadiliko,wazalendo na wanaharakkati wa kweli

Huyu mama inaonekana ameondoka kwa hasira tu ya kukosa ubunge, angepata asingehama. Labda NCCR wamemuahidi atapata ubunge. Mi naona kama amepishana na mafanikio. Yaani mafanikio yanapatikana yeye anaondoka. Hata huko NCCR wakimnyima ataondoka. Mi namshauri aende CCM akaozee huko. Yeye hatofautiani na yule dada aliyekuwa katibu wa Chadema Mwanza ambaye anajuta kukitosa chama. wengine wanaojuta ni Mr./Mrs. Politician dada Nakaya. Hawa wataaibika milele.
 
Mi najiuliza, mtu kukaa kwenye chama kwa muda nrefu ndio kigezo cha kupewa ubunge/uongozi?

Kama ni hivyo, Kingunge Ngombale Mwiru angekuwa rais wa nchi hii badala ya JK.

Huyu mama kapambwa sana kwenye magazeti leo lakini kesho hatutasikia tena habari zake ameamua kujizika huko NCCR
 
Chadema itawashangaza wengi; ni chama makini na kinaona mbali huwezi kumpatia ubunge mtu asiyekuwa na ndoto ya kuchukua jimbo kama akina Rose Kamili, Regia, Leticia Nyerere, na wengineo lazima tumpatie ubunge mtu anaweza kuchukua jimbo baada ya miaka mitano.

Huyu mama katumia demokarisia yake na ana uhuru wa kuondoka tutaweka mtu mwingine pale mchapa kazi na atakayeendeleza mazuri aliyofanya huyu mama aliyetimkia nccr -tunafurahi kwamba ameamua kwenda kuendeleza kasi ya ukombozi nccr ili tujue vyema mbatia anapata kiasi gani kutoka ccm. Chadema inaongozwa na watu makini saaaaana na wenye kuona mbali imekamilika idara zote.

Sokomoko hisia zako tunaziruhusu chadema na mwazo yako tunayaona majibu alishayatoa dr slaa siku nyingi lakini kama bado hujaelewa waruhusu wana jf wakusaidie siyo kulalama ukichoka nenda ccm watakupokea au basi cuf
 
[SIZE=4 said:
urasa[/SIZE];1294197]amehamia nccr mageuzi kwa sasa baada ya kukosa viti maalumu ndani ya chadema huku akitoa shutuma za udini,ukabila na kila aina ya ubaguzi ambao anadai upo ndani ya chadema.
kwa umri wake hakupaswa kusema hayo yote,hivi muda wote wa utumishi wake ndani ya chadema hakuyaona hayo anayoshutumu kwa sasa?
Amejikwaa,amepotea njia,amekuwa mfa maji na sasa anatapatapa,akumbuke utu uzima dawa,akae kimya kama amegundua kuna uozo chadema na aelekee kule anakokuona kwake ni sahihi.chadema si yeye bali ni taasisi ya watu wenye mapenzi mema,wapenda mabadiliko,wazalendo na wanaharakkati wa kweli

Pole sana Urassa najua lazima utampinga huyu mama hata kama ana hoja za msingi ni vizuri unge declear interest zako (kabila) halafu ungemshambulia mama musori. Mimi binafsi sikupenda chama kumteua Mwanaume kuwateulia wanawake wawakilishi wa viti maalum mie kwangu hilo halijakaa sawa otherwise kama ndio katiba ya chama ipo hivyo na tuiheshimu.
 
Shida yetu sisi tumekariri siasa...
Sio lazim amwenyekiti wa wanawake wa chama awe mbunge kwa sasa huo sio mfume wa CHADEMA. Kama vyama vingine vinafanya hivyo let it be. Huyu mama anapanic bure mbona naona ana kazi kubwa kuliko hata ya ubunge? Kazi ya kitaifa ya kuwaunganisha na kuwaongoza wanawake wana CHADEMA kitaifa si kazi ndogo kama una malengo. Jamani uongozi ni utumishi. Sasa bungeni anataka akafanye nini?

Unasema BUNGENI akafanye nini? Je hao viongozi waliopeleka wake, wakwe, mahawara, na binti zao jengoni hujapata tu jawabu kuwa hapa hakuna cha Uongonzi wala utetezi bali kazi ni MOJA kujaza mamifuko yao. Milioni SABA kwa mwezi ndio kiini cha kila mtu kutaka kuingia jengoni na siyo maslahi ya Taifa.
Chadema hakuna demokrasi yeyote bali ni maslahi kama vyama vyote ya siasa.
icon13.png
 
wangeingia Ikulu inaonekana Kamili na mwenzie wangekuwa kama Janeth Museveni..lol Power corrupts, and absolute power corrupts absolutely... I guess 49 seats too corrupt. Haijapita ata wiki vijimambo vimeshaanza kujitokeza.
 
Chadema Imeanza kuoza
Na wanaanza kutuonyesha kuwa hata Dk W. Slaa alikuwa ni chambo tuu kwenye kugombania urais
Hakika kama wangepata basi baada ya miaka mitano wangemtoa na kumsimamisha mmoja wao kati ya wana ndugu na mashemeji
Hii imenipa wasiawai sanaaa
Naimani hata Zitto Atang'atuka Chadema ifikapo au ikaribiapo 2015
Chadema siyo Chaguo la MUNGU

Huyu mama asikusumbue kichwa bwana Kitila. Yeye inaonekana azma yake haijatimia ndani ya Chadema. Mwacheni akaozee NCCR. Labda tu jiulize kwa nini hawa jamaa wanachomokea NCCR. Je ni mamluki?
 
Chadema wameshaanza kujichanganya na mpaka 2015 hawatakuwa na nguvu waliyonayo
Kweli ukabila umo na ushemeji
Hata Hayati Chacha Wangwe alisema haya
Na wengine wameyaona
Mbio za sakafuni

Na kwa bahati nzuri alieshtakiwa kwa kosa la kusababisha Chacha Wangwe kufa kwenye ajali kwa kosa la kuendesha gari bila ya leseni ni mwajiriwa wa Chadema kuna vitu vingi mimi vinanichanganya sio siri..................
 
Chadema itawashangaza wengi; ni chama makini na kinaona mbali huwezi kumpatia ubunge mtu asiyekuwa na ndoto ya kuchukua jimbo kama akina Rose Kamili, Regia, Leticia Nyerere, na wengineo lazima tumpatie ubunge mtu anaweza kuchukua jimbo baada ya miaka mitano.

Huyu mama katumia demokarisia yake na ana uhuru wa kuondoka tutaweka mtu mwingine pale mchapa kazi na atakayeendeleza mazuri aliyofanya huyu mama aliyetimkia nccr -tunafurahi kwamba ameamua kwenda kuendeleza kasi ya ukombozi nccr ili tujue vyema mbatia anapata kiasi gani kutoka ccm. Chadema inaongozwa na watu makini saaaaana na wenye kuona mbali imekamilika idara zote.

Sokomoko hisia zako tunaziruhusu chadema na mwazo yako tunayaona majibu alishayatoa dr slaa siku nyingi lakini kama bado hujaelewa waruhusu wana jf wakusaidie siyo kulalama ukichoka nenda ccm watakupokea au basi cuf

Lucy Fidelis Owenya
Grace Sindato Kiwelu

Hawa hawajafikisha miaka mitano mjengoni? Nadhani hapa watu wengi hawaoni tatizo mie pengine nina matatizo ya kufikiri nashindwa kukubali utaribu wa chama iwe CCJ au hata CDM kuteua "MWANAUME" ili wataeulie "WANAWAKE" wa kuwawakilisha bungeni "WANAWAKE" kupitia viti maalumu. Mie hapo tu! ila kama katiba inasema hivyo basi tuiheshimu na kama ina mapungufu tuibadili sambamba na kudai katiba mpya ya Tanzania...
 
Unasema BUNGENI akafanye nini? Je hao viongozi waliopeleka wake, wakwe, mahawara, na binti zao jengoni hujapata tu jawabu kuwa hapa hakuna cha Uongonzi wala utetezi bali kazi ni MOJA kujaza mamifuko yao. Milioni SABA kwa mwezi ndio kiini cha kila mtu kutaka kuingia jengoni na siyo maslahi ya Taifa.
Chadema hakuna demokrasi yeyote bali ni maslahi kama vyama vyote ya siasa.
icon13.png
Ndio nimeuuliza hivyo kwasababu
1. Kwa mtazamo wangu kazi yake yeye nikuwapika wanawake wa CHADEMA aidha anaenda bungeni au haendi. Siasa haipo bungeni tu
2. Ni lazima awe na upeo mkubwa ambao naona amaeonyesha dhahiri hana. Mbona Dr Slaa hakung'ng'ania arudi bungeni?
3.Mama anatamani kwenda bungeni kwa migongo ya wanawake wenzie kama huko kwingine. Sio CHADEMA...angetafuta jimbo aongeze idadi ya kura labda according to the criteria angefikiwa.
4. Nini mchango wa hao wenyeviti wa kinamama wengine wa vyama walioenda bungeni? Hamna.Yaani ni kubweteka tu na kusubiri vya bure.
5. Sasa hiv nilitegemea mama awe amekuja ni mikakati ya kupata wanawake wengi wa kugombea majimboni na udiwani sio yeye kulilia kwenda bungeni. Hajakomaa kisiasa.

Tuache ushabiki haina maana wanawake wakichagua wenyewe ndio demokrasia au watu sahihi wamechaguliwa. Dkt. Mkumbo amesema ametumia vigezo vingi.
 
Haku-meet vigezo. Kwani hata ukiwa ndani ya chama miaka kibao lakini vigezo vingine hauna ndio upewe nafasi?
 
MOSHI unaoendelea kufuka ndani ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) unaonekana kuficha moto.

Baada ya uchaguzi mkuu mwaka huu, hali ndani ya chama hicho inaonekana kutokuwa shwari hasa kutokana na mgawanyiko wa wazi unaojitokeza sasa.

Chachu zaidi ilijitokeza hivi karibuni baada ya Katibu Mkuu wa Chama hicho ambaye pia alikuwa mgombea urais, Dk. Willibrod Slaa, kukataa kutambua matokeo yaliyompa ushindi Rais Jakaya Kikwete, aliyekuwa akigombea kwa tiketi ya CCM.

Hali hiyo ndiyo iliyofanya baadhi ya wabunge wa chama hicho kususia pia hotuba ya Rais Kikwete, alipokuwa akizindua Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Novemba 18, Dodoma.

Tukio hilo lilitanguliwa na la kutohudhuria sherehe za kuapishwa kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kulikofuatiwa usiku na hafla ya kupongeza wabunge, ambapo baadhi ya wabunge wa chama hicho walihudhuria.

Hatua hiyo ilisababisha mgawanyiko wa wazi, kwa baadhi ya wabunge kutoshiriki ususiaji huo na kutoa sababu zao walizoona ni za msingi.

Lakini, kana kwamba hiyo haitoshi, juzi Mwenyekiti wa Chama hicho wa Mkoa wa Mbeya, Sambwee Shitambala akatangaza kujiuzulu wadhifa huo ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizoelekezwa kwake.

Shitambala aliwambia waandishi wa habari kuwa uongozi wa chama hicho kitaifa unamtuhumu kuhongwa Sh milioni 600 ili ahujumu chama chake na kushindwa kutwaa jimbo la Mbeya Vijijini.

Wakati hayo yanaendelea, huku uongozi wa juu ukikataa kuyazungumzia kuchelea majibizano, jana Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Leticia Musori, alitangaza kukihama chama hicho na kujiunga rasmi na NCCR-Mageuzi. Kiini cha hatua hiyo ni uteuzi wa wabunge wa viti maalumu katika chama hicho.

Musori aliwambia waandishi wa habari jana kuwa hakushirikishwa katika uamuzi wa kuteua wabunge hao na kudai kuwa waliteuliwa kwa kufuata uhusiano na vigogo wa chama hicho.

Akizungumza wakati anakabidhiwa rasmi kadi ya NCCR-Mageuzi na Mwenyekiti wa Chama hicho, James Mbatia, Musori alisema uamuzi wake unatokana na wanawake kukosa haki na mfumo dume kuendekezwa ndani ya chama hicho kwa kutoshirikisha wanawake katika vikao vya uamuzi.

Alisema kitendo cha chama hicho kuendeleza uozo na udikteta katika kufanya uamuzi, huku pia kikiendeshwa kama kampuni ya wakubwa katika kufikia uamuzi mbalimbali.

Musori alisema uchaguzi halali wa Bawacha ulivurugwa na viongozi wa juu wa chama hicho, ili kutoa nafasi kutoa viti maalumu kwa wanaowataka badala ya kuachia vikao vya wanawake wa chama hicho kuamua kama zinavyoelekeza kanuni za Bawacha.

Musori alisema jambo lingine ni kutokubali utumwa wa Mwenyekiti Mbowe ambaye alidai hataki kupingwa katika uamuzi wake.

"Mimi nilikuwa nikipingana na Mbowe katika hoja mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupinga utaratibu wa Chadema ambao Mwenyekiti anakuwa mtia saini ilhali yeye ndiye Mwenyekiti wa vikao vya Kamati Kuu, Baraza Kuu na Mkutano Mkuu, ambavyo kimsingi ndio vyenye mamlaka ya kusimamia Sekretarieti ya chama," alisema.

Aliongeza kwamba katika uchaguzi wa Bawacha, yeye alishika nafasi ya tano kwa kura zaidi ya 60 za wanawake wa chama hicho huku Suzan Lyimo akipata kura sita, Grace Kiwelo mbili na Halima Mdee saba, lakini hakuteuliwa katika uchaguzi wao wa wabunge 25 jambo ambalo si la kidemokrasia.

Alisema kutokana na uamuzi huo wa vigogo wa Chadema kuwanyima haki wanawake waliochaguliwa na wenzao, wengi watahama chama hicho ambacho alidai kipo kwa ajili ya maslahi ya wachache na hakina demokrasia.

Aliendelea kudai kwamba akiwa na cheo hicho cha Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mjumbe wa Baraza Kuu la Chadema na Mweka Hazina wa Umoja wa Madiwani wa Chadema na kukidhi vigezo vilivyowekwa na viongozi hao, bado hakuteuliwa kuwa mbunge wa viti maalumu kutokana na kumpinga Mbowe.

Alisema amechukua uamuzi wa kuhamia NCCR - Mageuzi ili aendeleze mageuzi baada ya kufanya utafiti na kuona kuwa chama hicho ndicho kinamfaa na kusisitiza kuwa tatizo si kupata uongozi kwani alikuwa na vyeo vingi ndani ya Chadema.

Akimpokea mwanachama huyo na kumkabidhi kadi, Mbatia alitoa rai kwa wanasiasa kuzingatia haki kwa kila mmoja, kwani bila kutoa haki Taifa haliwezi kwenda vizuri, na alitaka haki ianzie kwenye familia hadi Taifa.

Septemba mwaka jana, kutokana na kilichoonekana ni mchezo mbaya ndani ya Chadema katika kutafuta uongozi wa Baraza la Vijana (Bavicha), kulitokea kutoelewana kambi, moja ikiwa ya Mwenyekiti Freeman Mbowe na nyingine ya Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe.

Mvutano huo ulisababisha uchaguzi kufutwa na Baraza la Wazee na hivyo aliyekuwa akiwania nafasi ya uenyekiti, David Kafulila wa kambi ya Zitto, kuhama chama na kujiunga na NCCR-Mageuzi na sasa ni Mbunge wa Kigoma Kusini kupitia chama hicho.

Source:- Habari LEO!!!!!!!!!!!
Habari Leo sio source nzuri ya habari za CDM kwani wote tunajua walikuwa au wanafanya nini kuhusu CHADEMA. Huyu mama anakili kutofautiana na M/Kiti wake hii ni sababu tosha ya kutopata UBUNGE anaoulilia. Vile Vile anajionyesha kuwa na element za ZITO ambaye tayari anaonyesha alivyomvurugaji "Entrophy" ndani ya chama. Huyu asingesubiri kuhama baada ya kutangazwa majina na aelewe kuwa hata hawa akina Mdee anaosema aliwashinda walitoka nje majimboni wakajaribu kuonyesha kuwa sio mzigo kwenye chama. Kila la kheri na si muda mrefu atakuja kubadilisha mme/chama mwisho ataishia kwa mzee wa KINUNDU maana yeyete anayeshambulia Mbowe au Chadema ni rafiki wa CCM.
Kama umesaliti chama Kama Shitambala-Mbeya, Anthony Komu-Moshi Vijijini, Phocus Rwegasira-Nkenge, nk. unategemea chama kikae kimya? na hapo ndo useme SI SWARI hapana ni upepo unapukutisha majani makavu.
 
Ndio nimeuuliza hivyo kwasababu
1. Kwa mtazamo wangu kazi yake yeye nikuwapika wanawake wa CHADEMA aidha anaenda bungeni au haendi. Siasa haipo bungeni tu
2. Ni lazima awe na upeo mkubwa ambao naona amaeonyesha dhahiri hana. Mbona Dr Slaa hakung'ng'ania arudi bungeni?
3.Mama anatamani kwenda bungeni kwa migongo ya wanawake wenzie kama huko kwingine. Sio CHADEMA...angetafuta jimbo aongeze idadi ya kura labda according to the criteria angefikiwa.
4. Nini mchango wa hao wenyeviti wa kinamama wengine wa vyama walioenda bungeni? Hamna.Yaani ni kubweteka tu na kusubiri vya bure.
5. Sasa hiv nilitegemea mama awe amekuja ni mikakati ya kupata wanawake wengi wa kugombea majimboni na udiwani sio yeye kulilia kwenda bungeni. Hajakomaa kisiasa.

Tuache ushabiki haina maana wanawake wakichagua wenyewe ndio demokrasia au watu sahihi wamechaguliwa. Dkt. Mkumbo amesema ametumia vigezo vingi.

Jukumu hilo la kuwapika Wanawake wa Chadema alikabidhiwa Mhe Kitila Mkumbo yeye ndio alie wachagua watakaowakilisha kuenda bungeni kwa kupitia viti maalumu kama Chadema wangejua jukumu la huyu mama kama mwenyekiti wa wanawake wa chama wangemwambia sikiliza mama wewe hapa jukumu lako ni kuwapika wanachama na mhe Mkumbo atashirikiana na wewe kufanya mchakato kwa wanaofaa kutuwakilisha lakini matokeo yake yeye hakushirikishwa akachaguliwa Mwanaume kuwachagulia wanawake wawakilishi wao!
 
Haku-meet vigezo. Kwani hata ukiwa ndani ya chama miaka kibao lakini vigezo vingine hauna ndio upewe nafasi?

Napinga vigezo vya nafasi za wanawake zitolewa na mwanaume bila kujali demokrasia tunaelezwa ndani baraza la wanawake kuna utaratibu wa kura na huyu mama aliwashinda hao waliopelekwa bungeni ila kwakuwa katiba ya chama hajaelezea utaratibu wa kuchagua wabunge wa viti maalumu ikaamuliwa atafutwe mwanaume awachagulie wanawake wanawake wa kuwawakilisha wanawake wenzao bungeni kupitia viti maalum...... hapo ndio kwenye tatizo otherwise sioni tatizo la chadema
 
Huyu mama asikusumbue kichwa bwana Kitila. Yeye inaonekana azma yake haijatimia ndani ya Chadema. Mwacheni akaozee NCCR. Labda tu jiulize kwa nini hawa jamaa wanachomokea NCCR. Je ni mamluki?

Swali lako ni la kufanyia kazi, zaidi sana kwanini huo umaarufu wa Zitto kule Kigoma haukuweza kuisaidia CHADEMA badala yake NCCR ndio imepata mafanikio?
 
Masikini Habari Leo mumeamua kuwa kipeperushi cha udaku hivi hivi?Yaani pamoja na kuwa uchaguzi umekwisha bado mnaendeleza upuuzi uleule.
 
Back
Top Bottom