nguvumali
JF-Expert Member
- Sep 3, 2009
- 4,923
- 1,325
siri ni kujituma katika usimamizi wa raslimali fedha, na kutumia raslimali zilizopo kwa vipaumbele sahihiHivi nini siri ya mafanio ya majimbo hayo ya CHADEMA?
siri ni kujituma katika usimamizi wa raslimali fedha, na kutumia raslimali zilizopo kwa vipaumbele sahihiHivi nini siri ya mafanio ya majimbo hayo ya CHADEMA?
brother, listi yenu inazidi kupungua kwani huko kagera kuna mgombea wenu mmoja wa chadema kajitoa sasa sijui nini kapewa any way watu kama hawa ndio wanataka kupewa ridhaa ya kuongoza ni hatari sana kwani yaliyowakuta wa zambia mwaka 1991 bado hawajayasahau baada ya kumtupa kenneth kaunda na kumpa madaraka mlokole chiluba! Matokeo yake kila mtu anayajuwa! Mlokole aliifilisi nchi na sasa kesi yake bado inaendelea!
Chadema wacheni kuhadaa wananchi uwezo uwezo na nia ya kuongoza hamna labda sababu na hiyo haitoshi kama hamna uwezo na nia ya dhati!
tukuite mnajimu au mpiga madogoli. Siku zote hakuna umasikini mbaya kama umasikini wa mawazo. Kama ni mmoja wao ama umedhurika na fikra fifi nakupa pole sana. Ccm siku zote wamekuwa wakitumia mifano ya nchi zilizoshindwa kuonesha ubaya wa vyama mbadala. Mbona zilizofanikiwa hamtumii kuonyesha uzuri wa mabadiliko (kwa kukusaidia kenya).
Na isitoshe katika darasa la mambumbumbu yupo anaekuwa wakwanza, pengine mafanikio mnayojivunia wewe na serikali yako ya ccm ni kama ya yule mbumbumbuanayeshika nafasi ya kwanza darasani. Kukuthibitishia madai yangu kamwe ccm haijivunii mafanikio ya kimaendeleo kulinganisha na nchi nyingine. Ndio maana mpaka leo tanzania ni kati ya nchi masikini sana duniani, wakati ni kati ya nchi zenye utajiri sana duniani.
Mtaji wa ujinga unatumiwa sana na ccm. Mpaka siku utakapogundua unafanywa mjinga ndipo utakapo kata shauri la kujikomboa toka katika utumwa wa kiakili.