Majibu ya Kigwangalla: Kwa Nini Sikusaini Hoja ya Mhe. Zitto Zuberi Kabwe (MB)!

kigwangala+ lusinde+nchemba = 0, hana hoja hana tofauti na lusinde ambaye hata shule hajaenda, yaani ukishakua gamba akili nayo inapotea, bora mbaki kwenye taaluma zenu kuliko kupotoka na kukosa fikra huru
 
Mh. HK uwezo wako wa kufikiri ndo umeishia hapo au ndo umeanzia hapo!! Nyie ndo mnakiangusha chama kwa hoja dhaifu ka hizo.
 
Unajaribu kujikosha ili JK akukumbuke kwenye nafasi ya uwaziri sio?. Magamba Pumzikeni tu mmeshajichokea. Wenzenu wanajichotea mali za nchi nyie mnabaki mnalalama tu, Halafu mnaogopa kukata matawi yaliyozeeka kisa eti mtadondoka wote!. mti wenyewe ni mpapai!. Hiyo ni akili ya minyoo (Giardia lumbria).
 
Hapa ndo namkumbuka makamba(katibu mstaafu) aliwakataza wabunge waccm wasishiriki mdahalo duuu angeokoa hili angekukataza dr usishiriki kwenye mitandao ya kijamii!
Ni aibu wewe ni kilaza sana ndo maana magamba wanatibiwa india!
 
una akili iliyopofuka, unafikira rojo mithiri ya ute wa yai, unatazama mambo kwa macho yaliyojazwa kiwi, una tongotongo za tamaa za madaraka kwa jasho la walalahoi wa taifa letu, anayaona mambo katika sura ya ccm kwanza, taifa baadae.

anawaza kimasikini, anajivika kilemba cha uchapakazi na kutetea vibovu, anasema anakwaza na baraza la mawaziri bila kukerwa na alieliteua baraza hilo, haiwezekani ukawa unaumizwa na rushwa halafu anaeilea rushwa akawa rafiki yako. ...huu ni unafiki, uzandiki na ubinafsi wa kiwango cha juu.
Mkuu..
Kama hawa ndio viongozi taifa letu linaelekea shimoni..

We're wretched of the Earth..

Kinachonishanagaza ni kuwa huyu bado kijana, ana uwezo wa kupiga machimbuz ya maripoti ya CAG hadi asubuhi...

Sijui na yeye ni mlamba viatu ili apate deal za kununua pamba??

Sijui hata hasomi report zinazoletwa bungeni au vipi??

Na madegree kibao sijui ya udaktari biashara etc lakini bado ni kilaza hivi!!!

Nimeshangaa sana!!
 
Hivi kweli wewe una fikra huru??

Wewe inamaana hata ukiona nchi imetafunwa na nyie mchwa utakaa kimya kwa sababu Serikali ni ya chama chako??

Vipi kuhusu vile vimisemo vyenu vya 'Taifa mbele, Chama baadaye'??

Unaelewa maana ya concept ya 'Tanzania ilikuwepo kabla ya CCM'??

Nadhani ndio maana ulibebwa kwenye kura za maoni, hufai kuwa hata balozi wa nyumba kumi!!

bit za kina Hawa Ghasia kwenye sakata la madaktari lilikuingia eh? Nilidhani una misimamo ya utaifa zaidi kumbe bure na haufai. Au unavizia uwaziri mkuu?
 
Mkuu kwanza nikupongeze kwa kuja kuleta majawabu sawia!

Ingawa siwezi kuthubutu kukuita mnafiki kutokana na ukubwa wa neno hili kwa muumba, ila naona kama kuna sehemu sijakufahamu vyema kauli yako kwamba

"Leo hii mimi niko chama kimoja tu, CCM, na nitafanya mambo yanayokubalika ndani ya CCM",

Wasiwasi wangu katika hili ni je ikiwa mambo hayo ambayo kimsingi yanakubaliwa na ccm yatakuwa yanaenda kinyume na matakwa ya wananchi itakuwaje hapo? mfano tunajua kuwa uongozi ni dhamana na ubadhirifu ni kukosa unaminifu na ni dalili ya unafiki kwa kutenda kinyume na dhamana hapo inakuwaje kaka yangu hebu nijibu tafadhari?


" Tatu, msisahau kitu kimoja cha muhimu kabisa. Kwamba, mimi ni Mbunge kutokea CCM na kama walivyo wengi wenzangu hatukusaini kwa sababu hatuwezi kuiangusha serikali ya CCM kwa hoja inayoletwa na Mbunge wa Kambi ya Upinzani! Mbunge wa Chama Tawala kuamua kuiangusha serikali ya chama chako ni sawa na kuamua kukata tawi la mti uliokalia, kwa vyovyote vile utaanguka nalo! Simple logic "


Lakini pia katika dhana hiyo hiyo ya kuungana na yatokanayo na chama chetu "CCM" na kutokubali hoja iliyotoka upande wa pili, napo ninaomba unipe ufafanuzi mzuri, naamini kabisa pamoja na sababu chafu na agenda zingine za vyama vyetu vya upinzani lakini bado kuna masuala yalio sahihi na yanayogusa maslah ya umma,

Huenda hoja iliyoanzishwa kwa upande mmoja ikapelekea kuwapa ushindi wa kisiasa wapinzani lakini swali langu kwako Mh. Ni upi msimamo wako pale hoja inapoletwa na wapinzani ikawa ina maslah makubwa kwa taifa lakini itakipunguzia nguvu chama chetu CCM, utaunga mkono hoja au kupinga? na kama ni lazima uitetee serikali yako huoni kama kwa hilo huwatendei haki wananchi?

Best
Tume ya katiba
Brother, waliopo CCM pia ni wananchi wa nchi hii hii, na ninakuhakikishia kabisa kwamba ndani ya wabunge wa CCM kuna watu wazuri sana, tena wazalendo kupita kiasi kuliko unavyotaka kufikiri, na ndiyo maana tunaendelea kuchaguliwa na wananchi. Suala la kusaini ama kutokusaini ni la kiutaratibu na kwa mfumo tulionao si sahihi kwa MB wa CCM kupiga kura ya kitu kizito kama hicho bila kuangalia msimamo wa chama chake. Kusimamia mambo ya kitaifa na hata kuunga mkono hoja za kambi ya upinzani kwenye mambo madogo madogo inakubalika lakini siyo kwenye mambo kama haya, hili la kutokuwa na imani na WM!!!! Hata kama CHADEMA wangekuwa wanatawala wasingekubali hilo...
 
a hakuwa na u-seriousness wa kutaka kweli kumuondoa wm bali ni baadhi ya mawaziri, sema alichomeka tu hiyo kauli ili kutia presha zaidi!). Zaidi ya hapo, ninaamini hoja hiyo ni nzito na kimsingi, kwa sasa, imegeuka kuwa ni mchezo wa kisiasa na media na haitofika popote! Kama mhe.

Hk.
mbona unajichanganya sana? Hueleweki mbona?!!!!
 
mwanamapinduzi wa cuba che quavar alisema i would rather die standing than living kneeling lakin mheshimiwa hovyo amekubal kuish huku amepiga magoti kwamba bado ni mtumwa kifikra,mchumia tumbo mtu ambaye anasubir chama kimfanyie nin badala yeye kufikiri ataifanyia nin Tanzania ndugu zangu samak mmoja akioza wote wataoza so leo hii sitak kujiaminisha sana kama kuna mtanzania anashabikia chama cha magamba ukamwita mzalendo wa kwel shame on u Kigwangaala and that CCM of yours
 
Najisikia kuugua ghafla baada ya kusoma unafiki huu
na nahisi nikiendelea kuusoma nitajibu ovyo na kutukana na nitaishia kupata BAN
Bora niende kwenye kjukwaa jingine kabisa


mnafiki huyu amekuja baada ya kuona humu ndani mnamtaja kuwa yumo au atakuwa katika baraza la mawaziri ndio maana akaona ak=jitokeze na kujipendekeza ili JK amsome na akiweza amtupie uwaziri wa afya baada ya kujua waziri wa afya ni mmoja wa watakao achia ngazi ama kweli unafiki ni kitu kibaya humfanya mtu apoteze utu na uhuru wa Fikra zake halisi!!!!!!!!!!!!

Hata yeye akisoma tena alichandika atajua kabisa si anachamo amini!!
 
Mimi ningekuwa wewe ningechagua kukaa kimya, i.e. kutokujibu hoja; kuliko kutoa majibu ambayo baadae nikiyafikiria nitaona aibu kujiita Mtanzania. Nawahurumia wapigakura wako waliokuweka hapo.
 
Huo ndio unafiki wenyewe, wewe unatumikia chama au wananchi?? Kumbe hadi hapo hujaona mabaya ya CCM!! Kajipange upya kujibu hoja naona ni mbabaishaji tu.

Ulikuwa kwenye majukumu ya kujenga taifa au majukumu ya kuibia taifa??
 
Bwana mdogo, asante kwa majibu yako ambayo yameweza kutuonesha watanzania wewe ni mtu wa namna gani na una nia gani na Tanzania. Kwa upande wangu naona na wewe pia ni moja kati ya uozo, uchafu na upuuzi unaoiangamiza Tanzania.

Ripoti za CAG kila mwaka zimekuwa zikionesha wizi na ufisadi wa hali ya kutisha, lakini Chama chako kimeshindwa kuwachukulia hatua mawaziri husika. Hoja ya Zitto ililenga kuwaondoa mawaziri wabadhilifu ndani ya baraza la mawaziri na hilo lilikuwa ni jukumu la waziri mkuu. Alipoona waziri mkuu hachukui hatua ndipo alipoamua kuleta hoja ya kumuondoa PM madarakani. Watanzania tumechoka kuibiwa kila kukicha na watu tuliowapa dhamana ya kulinda mali zetu. Wewe na baadhi ya wabunge wenzako ambao mnatuibia kila siku si watanzania wa kweli bali ni watanzania wachumia tumbo. Mimi ni mwanachama wa CCM lakini niliafiki azimio la zitto 110% kwani lina lengo la kulinda mali za watanzania wote bila kujali itikadi za chama. Kukishinikiza chama chako kuwajibika si jambo baya hata kidogo na wala haukiangushi chama chako bali unakikomaza na kukisafisha. Nilitegemea kabisa kwamba wewe kama kijana mwenye uelewa na upeo mpana wa hali halisi ya maisha ungesaini na kuunga mkono lile azimio la Zitto. Lakini kwa sasa umeonesha wazi kwamba wewe si mtanzania halisi kwani umeweka mbele masilahi ya chama chako na wala si Taifa. CCM tumetawala miaka mingi sana lakini lazima tukubali kwamba tumewaangusha sana watanzania. Tumefuga wezi na wabadhilifu kwa kuwakumbatia kwa gharama kubwa sana. Sina imani na wewe tena na lazima 2015 nitakuwa mstari wa mbele kuendesha kampeni za kukutoa bungeni kwa gharama yoyote.
 
Hukuweza kusaini karatasi ya Zitto kwa sababu ni 'sawa na kukata mti uliokalia'. kwa hapa ndugu nimekuelewa. Hofu ni haki ya kila mmoja na hasa linapokuja suala la kuchagua. Ulikuwa na hofu na huoni maisha nje ya baraza hili na serikali hii na kwa maana hiyo hata kelele na misimamo yako ya kutetea wananchi wa Nzega kupata faida na utajiri unaowazunguka (rejea msimamamo wako kwenye Resolute co.) ilikuwa ni kuzuga tu!

Kazi njema bwana HK, na ukweli ni kuwa pamoja na kuwa umeingia ndani, bado tunaona umekanyaga kapeti letu na viatu vyako vichafu'

Sitaki kuamini kwamba nimepoteza muda kusoma utetezi wa huyu *****!!
Yaani kwake chama kwanza,taifa baadae.

Alipokua anajidai kutetea madaktari na WM akamwambia kwamba ana
dhalilisha chama chake alikaa kimya,..........HUU NI UNAFIKI.

Anapojidai kutetea wana nzega kwenye suala la migoma kumbe ni
UNAFIKI TU.

Kwa vigezo vya dini yake alivyotoa kama vinavyo define mnafiki naona
kesha fuzu,.....

maana ALIAHIDI KUTETEA MADAKTARI LAKINI AKA WARUKA KIMANGA.
 
Kama huna utetezi ni bora kunyamaza.

Utetezi wa aina hii hauna tofauti na ule wa Nundu!!

Tawi ulilokalia sio? Mkono unaokulisha sio?
Tutang'oa mtu wote tuone utakula wapi!

Tutang'oa mti wote tuone atakula wapi!!!! hana adabu, huu utetezi naomba uhifadhiwe, tutakuja mnyonga nao iwe anataka kuhamia chama chochote au kuomba uwakilishi wowote!!!
 
Back
Top Bottom