Majibu rasmi ya BoT juu ya nyumba ya Ndulu

Reverend,

Let me be clear as I can , I still stand by everything I said and I am not going to apologize as you have requested. In fact , you are the one who should apologize for distorting my position. By the way, can you please explain to me what u' meant by :

Rufiji,

Nilitoa mfano kuwa katika BOT kufanya biashara yake kwa niaba ya Serikali, 75% ya mapato inarudi Serikalini na 25% inabakia kuwa ni yao kwa kujiendesha (let say my breakdown of percentage is accurate).

Nimeuliza kwa nini kama wao wanatumia hiyo 25% yao wanavyotaka kinatuumia nini katika maana kubwa na pana na sivyo ilivyopokelewa.

Tanzania tunadai kuwa kila kitu kilikuwa kinaingiliwa na Serikali au kudhibitiwa na Serikali (big brother) sasa kama tunataka kuwa na jamii na taasisi zinazojiendesha kwa uhuru, na hicho ndio kilio chetu kingine kwa nini Wanasiasa wanaingilia uendeshaji wa taasisi na mashirika, iweje nasi tung'ang'anie kuwa hilo fungu la BOT kujiamulia wajifanyie wanalotaka tutake nalo lidhibitiwe?

Kama unakumbuka, nilikuuliza, weye unanifahamu vizuri na ninachoandia katikati ya mstari, lakini mkanirukia kiringe na kunitusi eti najidai jiniasi!

NItaendela kukujibu hivi:

NIliuliza, je kuna mtu kafanya tathmini ya gharama za ujenzi Tanzania? NIkaendelea kuuliza kama BOT ndio wadhibiti na walinda uchumi, iweje kuwe na uholela wa gharama za ujenzi mpaka leo hii?

Sasa kama nilitamka kuwa BOT wajiamulie wanalotaka halafu nikahoji suala la uholela wa gharama za ujenzi, huoni ninachoainisha kuwa kuna Tatizo kubwa sana la kiutendaji Tanzania na hata ubovu BOT ambayo ndiyo inapaswa kuwalinda Watanzania? Tena nikaongeza kwa kuuliza, kama BOT waliafiki kununua kiwanja au kulipa gharama hizo za ujenzi, ina maana kuwa Tanzania katika sekta ya nyumba, ardhi na ujenzi, gharma hizo ni halali na hazihitaji kuangaliwa?

NItaendela kufafanua kauli zangu.

Nikaendelea na kuhoji, ikiwa BOT leo hii wanajukumu la kuratibu shughuli za ujenzi wa nyumba boa na nafuu, Tanzania, je walitumia kwa kiasi gani ujuzi wa wajibu wao katika kujijengea nyumba hizi? Zaidi nikauliza, je nyumba za Wafanyakazi wengine ziwe pale Dar, Arusha, Mwanza, Mbeya au Zanzibar, nazo zinakarabatiwa kama zilivyofanyiwa hizi nyumba?

Sasa kwa kuwa hukuelewa nilichokuwa na lenga, basi ilikuwa ni rahisi kwako kuainisha kuwa nilichosema kuwa nahalalisha matumizi ya kodi ya wananchi. JokaKuu akaamua kuangalia Act na Charter ya BOT akakutakuwa Mwenyekiti wa Bodi ni Gavana na hao manaibu Gavana nao wako kwenye bodi, hivyo wao wana sauti katika upigaji kura.

Je ilikuwa ni lazima niandike kuwa hili lian walakini? Ni kila kitu watu warahisishiwe? Ndio maana nikaghadhibika na kuuliza je kuna mwenye kuchukua muda kusoma na kuangalia facts nba si kutumia emotions?

Sasa kwa nyongeza ya maswali yangu matatu ya awali ambayo umeamua kuniita mnafiki, nina mengine ya ziada, kwa BOT na kwa faida ya wengine. Ni uamuzi wako na msomaji yeyote kama utaamua kuendelea kuamini kuwa ama nimeamua kubadilika au sikueleweka hapo awali na kupokelewa kwa utata kwa kuwa sikujibu hoja kwa hisia bali kwa kupima hali halisi ya Tanzania.

Maswali yangu yanayofuatia ni hayal

Je nyumba hizi zimejengwa kuwa kutumia malighafi na Rasilimali ambazo zinazalishwa Tanzania? Kama sivyo, ni kwa nini BOT ambayo inatakiwa kuchochea uzalishaji wa mali na kukuza uchumi wetu ilikubali mkandarasi alieagiza mbao kutoka Malaysia, huku tuna mbao nyingi kule Mufindi? Je udongo ulaya, misumari, fito, madirisha, samani, nyaya na hata udongo vilitoka nje ya nchi na hivyo kuongeza gharama za ujenzi?

Je Benki Kuu pamoja na kuwa hizi pesa zilitengwa awali, je kulikuwa na ulazima wa kuingia gharama na kuzijenga nyumba hizi wakati huu ambao Uchumi si wa Tanzania tuu bali wa Dunia ni mbaya na hivyo matumizi haya yalifanyiwa maamuzi na kuidhinishwa bila kutumia busara? Je Ndulu na wenzake walikuwa wanakaa wapi kabla ya kuwa Gavana wa Benki?

Je, Serikali na Mkaguzi Mkuu walikuwa wapi kuhoji matumizi haya? Nyumba hizi zimejengwa kwa Bajeti ya BOT ya 2007-2008/2009. je hakuna hata mtu mmoja ambaye alipitia mahesabu ya BOT hasa Wizara ya Fedha na kuwauliza BOT mantiki ya wao kutumia fedha nyingi kiasi hicho hata kama kiko ndani ya uwezo wa wa kutumia wakati huu ambapo BOT imeshakumbwa na kashfa nyingi za uhujumu na ufujaji mali?

La mwisho, ni mfumo wa BOT wa kujiendesha na maamuzi yake. Ikiwa Bodi na Menejimenti ya BOT viliamua kutokutumia busara katika matumizi haya, hata kutumia vigezo vya kiuchumi kama Taaluma na hasa kulinda mfumuko wa Bei na thamani ya sarafu yetu, je leo hii kama Wangetumia robo ya fedha hizi, kujijengea nyumab hizi, kungeleta mwamko ulioko leo hii wa kulalamika? Hapa nikiwa na maana ya kusema ikiwa Ndulu, Reli, na wenzao wawili wana kura nne ndani ya Bodi na wao ndio wakubwa wa Bodi, Serikali haioni kuwa kuna makosa makubwa kuwa maamuzi makubwa yaliyotuletea EPA na Minara ya BOT yalifanywa katika mazingira haya haya ambayo yanatokana na mfumo mbovu wa kiutawala?

Nilipouliza iweje CCM wajinunulie magari 200, kuna mtu akanijibu BOT ni mali ya umma, na CCM ni Chama cha Kisiasa. Lakini CCM nayo si inategemea Ruzuku ambayo ni kodi yetu na zaidi ni kuwa CCM imekuwa ikijiendesha na kutumia kodi zetu hata bila idhini yetu?

Sasa leo iweje tuone la BOT kuwa ni kubwa zaidi an tukasirike kuwa hizi ni kodi zetu, ilhali CCM wanadai kuwa Serikali ni yao na wanatumia mamlaka na dola ya Jamhuri ya Tanzania kwa Manufaa yao binafsi na si kwa manufaa ya Taifa?

I hope mlioko Tanzania ambao mtapata nafasi ya kuongea na Ndulu, Mkulo au kiongozi yyote hata kama ni Pinda na Kikwete, mtapata nafasi ya kuwauliza ninachouliza hapa na kuonyesha udhaifu na ubovu wa mfumo wetu wa uongozi na kukosekana kwa busara na hata soni kwa waliochaguliwa na kuteuliwa kulitumikia Taifa letu (kama Taifa na Serikali ni bado zetu!)!
 
Ningependa kuuliza kaswali kama kuna wajenzi humu ukumbini. Hivi leo nikitaka kujenga nyumba ya kisasa pale Tanzania, yenye vyumba vitano, sebule mbili, jiko ya kisasa, ikiwa na air conditioning na matenki ya maji safi itanigharimu kiasi gani? Achilia mbali bwawa la kuogelea kwa sababu tupo karibu na pwani nitaogelea pale Coco Beach. Tuseme viwanja Oyster Bay na Masaki havipatikani, basi kule Boko.

Jasusi,

Katik gharama, wamesema genereta la umeme, swali langu ni kwanini wawakutumia Dola Elfu 30 wakanunua Solar Panel System ambayo ina faida kubwa kuliko lijenereta na pesa za mafuta kila mwezi?

Kama wao wamejihami na kujinunulia Jenereta kwa kila nymba, je wantuambia nini Watanzania kuhusu suala la umeme? Je BOT haina dhamira ya kuisukuma Serikali ya Tanzania ipatie ufumbuzi wa kudumu tatizo la nishati ya umeme?

Then Tanzania tutapigaje hatua kiuchumi ikiwa hatuna umeme na wenye uwezo wa ushawishi kuishauri Serikali itatue suala la Umeme, wao wanakuwa wa kwanza kujipendelea na kujiwekea "kinga" ya jenereta?
 
Maswali ya kujiuliza,

1. Kwa nini bado tuna utamaduni wa mashirika, taasisi na Serikali kujengea wafanyakazi nyumba? Kwa nini wasijihudumie wao wenyewe kwa kutumia mishahara yao?

2. Kwa nini Benki Kuu kama mdhibiti wa Uchumi wa Tanzania ilikubali kujengewa nyumba kwa gharama za juu kiasi hiki, ukizingatia kuwa sekta ya Ujenzi inajipangia bei zake kiholelea na hakuna udhibiti wa mfumuko wa bei za viwanja na malighafi (vifaa vya ujenzi) unaofanyiwa uratibu na Serikali?

3. Kama Benki kuu inaazimia kuwa bei hizi ni sawa (si kwa sababu ya bajeti) kutokana na hali halisi ya sekta ya ujenzi na nyumba Tanzania, je Uchumi wa Tanzania na safari ya Watanzania kuwezakujitegemea na kujijengea nyumba bora itafanikiwa vipi ikiwa kila siku kuna mfumuko wa bei za viwanja, hakuna sheria madhubuti za ardhi, na gharama za vifaa vya ujenzi na wajenzi ni kubwa kuliko sehemu nyingi duniani na ukipima uwiano wa umahiri wa Sarafu yetu?

Mkuu Rev Only In Tanzania, Kiongozi analipwa Mshahara Mkubwa, anapewa House allowance, Transport allowance na bado anaishi katika Nyumba ya Serikali, anatumia gari la Serikali
 
Mojawapo ya majibu ambayo bado nafikiria maana yake ni hili la kutuambioa kuwa:

Makampuni yote hayo yamesajiliwa Tanzania.


Hapa nikakumbuka... Dowans, Richmond, n.k.... Ningependa kujua kweli haya makampuni ni ya nani hasa?
 
Sijui, Mkuu! Sina uhakika kama hivyo vyumba vya wageni vya ziada vipo. Ninachokusudia kusema ni kuwa taarifa yao haijitoshelezi. Kutokana na taarifa yao kuna majengo ya nje ya ziada kuliko yatayayohifadhi watumishi ndiyo maana nikakisia kuwa kuna nyumba ya wageni, kwa lugha yenu mlioenda shule, guest wing!

Amandla......

Fundi Mchundo,

Kama walijenga nyumba kwa mkao wa Kimarekani, basi Ndulu angejuwa hakuna ulazima wa kuwa na vyumba vitano! Watoto wake ni wakubwa wanazidi miaka 18, hivyo wanapaswa wajitegemee!
 
Tunashukuru Reverend kwa kurudi kundini, maana tulivyo kuwa tunakemea/kupinga toka mwanzo ni kutokana vitu hivi hivi unavyo viongelea.

August,

Alikuwambia nani kuwa nilikuwa nimepotea kwenye zizi au kulikimbia kundi?
 
Jamani, naomba tumuulize Ndulu swali hili, Thamani ya kweli ya Shilingi ya Tanzania!

Maana isijekuwa tayari sarafu yetu ni karatasi ya ch oo ni kama ile Zim Dollar au Faranga za Zaire wakati wa Mobutu-Kabila War!
 
Hizo ni nyumba mbili tu! je hawa wawili waliobaki inakuwaje maana kuna Gavana na Manaibu Gavana watatu!!!
 
Ningependa kuuliza kaswali kama kuna wajenzi humu ukumbini. Hivi leo nikitaka kujenga nyumba ya kisasa pale Tanzania, yenye vyumba vitano, sebule mbili, jiko ya kisasa, ikiwa na air conditioning na matenki ya maji safi itanigharimu kiasi gani? Achilia mbali bwawa la kuogelea kwa sababu tupo karibu na pwani nitaogelea pale Coco Beach. Tuseme viwanja Oyster Bay na Masaki havipatikani, basi kule Boko.

Itategemea na size, kitu ambachi kinaweza kutupa uwiano wa ukweli wa gharama ni gharama kwa mita ya mraba. hii italinganisha na ukubwa wa nyumba pia. kwa Tanzania wastani wa gharama za nyumba kwa mita ya mraba zinajulikana. Ndio maana walisema twin tower gharama yake kwa mita ya mraba haijawahi onekana TZ wala Marekani
 
Mimi hapa ndipo ninaposhindwa kuelewa. Nyumba ya $450,000 kweli unawakatia waliokutayarishia michoro, mahesabu ya nguzo n.k ka measly $5,000? Yaani hawa jamaa gharama yao ni sawa na jokofu na pungufu ya mlango wa gereji! Bila shaka mafundi walilamba zaidi ya hii maana naona watalamu wa kazi tamu uliwaachia zaidi ya $20,000!

Inasikitisha lakini ndivyo ilivyo. Wataalamu wanaothaminiwa bongo ni madaktari (ukifanya mchezo unaondoka) na mawakili ( ukifanya mchezo utajisaidia kwenye ndoo.) tuu!

BTW Tanzania GDP per capita (2007) ilikuwa ni $369.7. ref:

http://data.un.org/CountryProfile.aspx?crName=United%20Republic%20of%20Tanzania

$ 2000 hatujawahi kugusa. GDP per capit (PPP) ni kama $1,300 tu!

Amandla......
Yani kwenye ujenzi bongo kuna Vioja vingi sana,one them is architects and building consultants are mostly bypassed or ignored.Ndio haya ya ujenzi kuwa $1M bila mtu yoyote kustuka.
 
Mimi siamini eti Ndugu Mukulo alikuwa hajui BOT kutumia fedha nyingi kiasi hicho hadi juzi ndipo kafahamu hivyo. Mbona wanalazimisha sisi wananchi kutuaminisha kwamba Serikali inafanya mambo kama maigizo hivi? Inakuwaje Waziri anayesimamia fedha za umma asijue tena Wakala wa Serikali aliye chini yake (Agency-BOT) ametumia fedha hizo pasipo ulazima wowote wa kufanya hivyo? Hivi Mukulo anapotuambia kwamba Serikali imeshangazwa kusikia matumizi hayo ya fedha anataka tuamini nini? Anaposema anafanya uchunguzi wa uhalali wa matumizi hayo ya fedha za umma, je anafikiri ni halali kutumia sh. bilioni 1.3 kujenga nyumba moja ya kuishi mtumishi wa umma, kiasi cha yeye kusema tu anaangalia uhalali wa matumimizi hayo. Hapo haihitaji hata uchunguzi, maana Kama waziri wa fedha anao uzoefu wa kutosha kabisa kuhusiana na ujenzi wa miradi ya nyumba nchini. Sasa hapo achunguze nini? Ama ni kwenda kujiandaa kuja kudanganya umma ili unyamazie ufujaji wa mali za umma wa namna hiyo?

Hayo ni maswali ya nyongeza kwenye maswali yaliyotangulia kuulizwa na mtoa thread hii! Tusubiri majibu na nyongeza ya maswali ya wadau wa JF!!!

Echonza,

Swali lako hili ni la msingi sana. Mwaka 1989 nilipata bahati ya kufika nyumbani (Ifakara) kwa wazazi wake Professor Benno Ndulu. Ni maisha ya kawaida aliyokulia Gavana Ndulu.
 
Sidhani kama ni fair jamani kumhukumu mlongu wangu ndullu katika hili, sirikali inafahamu gharama halisi na fact zile za b.o.t ni ukweli wa mambo ila kuna mjinga mmoja anajifanya kushangaa yanayoendelea nyumbani kwake. Ndullu siyo mwizo ila ana deal na technical facts zinazoletwa kwake na wataalam wa serikali hii, iweje waziri aanze kumtemea pumba gavana wakati yeye ndie mtetezi wa bajeti nzima ya nchi??

Nadhani wenye nguvu hawamtaki mndamba mwenzangu pale gharani wameanza kumsukia zengwe la kumng'oa hapo kwakweli. Prof. Ndullu komaa nao hawa wajinga wasikuchafue kabisa.

Lakini nao ni unyonge na uaminifu wetu wana ulanga-kilombero, tunawatendea mema sana watz wenzetu lakini tunaponyanyaswa na manyang'au tunadharirishwa na umma wote halafu baadae ukweli unaonekana kuwa siyo kweli lakini tayari tushajeruhiwa sana.
Enough is enough, wakuu tuwe fair na shutuma hizi dhidi ya ndullu
 
Wakuu hili imenilazimu kutoa maoni kama mzawa maana orodha ya wahanga wanaotokea huko kwetu imekuwa ikiongezeka kila kukicha mbaya zaidi wanatumiwa hawa majirani zetu humohumo morogoro. Inaonyesha wana mtu wao wanataka kumpa u-gavana, wafanye hivyo na si kumchafua innocent man
 
Ndulu anajua kuwa nyumba inayojengwa ni kuishi Gavana (yeye), anajua gharama za mradi, anajua hali ya uchumi na Tanzania na watanzania wake. Amebariki matumizi ya kiasi hicho fedha kwa raha zake.Nakubali kwamba kwa hadhi yake anastahili kuishi nyumba nzuri lakini siyo ya kifahari. Kwa kweli kwa maoni yangu, 1 bilioni vyovyote iwavyo ni kikubwa sana. Jamani tuone huruma wenzenu
 
Ndulu anajua kuwa nyumba inayojengwa ni kuishi Gavana (yeye), anajua gharama za mradi, anajua hali ya uchumi na Tanzania na watanzania wake. Amebariki matumizi ya kiasi hicho fedha kwa raha zake.Nakubali kwamba kwa hadhi yake anastahili kuishi nyumba nzuri lakini siyo ya kifahari. Kwa kweli kwa maoni yangu, 1 bilioni vyovyote iwavyo ni kikubwa sana. Jamani tuone huruma wenzenu

Hili liko wazi ni kwamba muonapo yeye Ndulu kagaramikia hako kajumba kwa hizo pesa basi mjue kuna makubwa zaidi ya hayo, Maana Ndulu hashtuki ni kuwa wanatushaangaaa watanzania ati. Ndulu nadhani hawezi akawa na nguvu za kufanya mambo kama hayo kama hakuna source ya kitu kuna wakubwa nao wanajichumia kupita maelezo nae akaona hapo ndipo kuna kamwanya kwa kufanyia nae mambo yake. Lazima Tujiulize kama yeye ni gavana na anajua uchumi wa nchi ukoje na hali ya wadanganyika ikoje, how yeye akajenge kajumba kama kale kwa thamani ile?? kuna kitu behind pale Bank Kuuu, Chunguzeni sana mtabaini

 
Sidhani kama ni fair jamani kumhukumu mlongu wangu ndullu katika hili, sirikali inafahamu gharama halisi na fact zile za b.o.t ni ukweli wa mambo ila kuna mjinga mmoja anajifanya kushangaa yanayoendelea nyumbani kwake. Ndullu siyo mwizo ila ana deal na technical facts zinazoletwa kwake na wataalam wa serikali hii, iweje waziri aanze kumtemea pumba gavana wakati yeye ndie mtetezi wa bajeti nzima ya nchi??

Nadhani wenye nguvu hawamtaki mndamba mwenzangu pale gharani wameanza kumsukia zengwe la kumng'oa hapo kwakweli. Prof. Ndullu komaa nao hawa wajinga wasikuchafue kabisa.

Lakini nao ni unyonge na uaminifu wetu wana ulanga-kilombero, tunawatendea mema sana watz wenzetu lakini tunaponyanyaswa na manyang'au tunadharirishwa na umma wote halafu baadae ukweli unaonekana kuwa siyo kweli lakini tayari tushajeruhiwa sana.
Enough is enough, wakuu tuwe fair na shutuma hizi dhidi ya ndullu

Wewe usitufanye sie hatujui uongozi let alone kuelewa Bot inafanya kazi vp.

Kama wewe unaletewa facts and figures mezani kwako uzipitishie maamuzi hulazimishwi na mtu yeyote kuzikubali hata Kama ni rais ndio maana kukawa na neno linaitwa accountability baba we are accountable for the action we take!. Usimtetee bure unataka Gavana ameshindwa kucross check hizo figure na independent surveyor!

Basi ok tuseme hana muda yuko verry busy ameshindwa kukaa katika ofisi yake akagoogle ( which is the worstcase scenario) ajue nchi maskini wenzie wanakaaje magavana wake!!! Acha kumtetea kaka hapa kidogo kablew up 2.4 billion for houses hata mwemdawazimu atang'aka tuna uchungu na hela zetu enzi za ujamaa zimeisha sasani ubepari kwenda mbele tutahoji kila kituhata viatu unavyovaa kwani tumekuteua usimamie na sio utumie pesa zetu
 
Sidhani kama ni fair jamani kumhukumu mlongu wangu ndullu katika hili, sirikali inafahamu gharama halisi na fact zile za b.o.t ni ukweli wa mambo ila kuna mjinga mmoja anajifanya kushangaa yanayoendelea nyumbani kwake. Ndullu siyo mwizo ila ana deal na technical facts zinazoletwa kwake na wataalam wa serikali hii, iweje waziri aanze kumtemea pumba gavana wakati yeye ndie mtetezi wa bajeti nzima ya nchi??

Nadhani wenye nguvu hawamtaki mndamba mwenzangu pale gharani wameanza kumsukia zengwe la kumng'oa hapo kwakweli. Prof. Ndullu komaa nao hawa wajinga wasikuchafue kabisa.

Lakini nao ni unyonge na uaminifu wetu wana ulanga-kilombero, tunawatendea mema sana watz wenzetu lakini tunaponyanyaswa na manyang'au tunadharirishwa na umma wote halafu baadae ukweli unaonekana kuwa siyo kweli lakini tayari tushajeruhiwa sana.
Enough is enough, wakuu tuwe fair na shutuma hizi dhidi ya ndullu

Unataka kutwambia Mkulo akae chini aanze kusoma budget za idara za zilizotumia mwaka mzima kuziandaa nchi itafika hivyo???? Acha kutafuta sababu za kumtetea Professor Ndulu. Kuhusu competence jamaa ni mzuri but inawezekana njaa ikamharibia reputation kwa vijana wake sie aliotufundisha. Kwani Professor Mahalu ikoje????
 
Wakuu hili imenilazimu kutoa maoni kama mzawa maana orodha ya wahanga wanaotokea huko kwetu imekuwa ikiongezeka kila kukicha mbaya zaidi wanatumiwa hawa majirani zetu humohumo morogoro. Inaonyesha wana mtu wao wanataka kumpa u-gavana, wafanye hivyo na si kumchafua innocent man

Ngoja tukisaidie mzee usije kuona tunamuonea gele mzee wako na ukadhani tunamuonea wivu ni hivi fatilia mtiririko huu hapa chini nakusaidia.
According to Bloomberg Ben Benarke mnene mwenzie alinunua nyumba Capitol Hill in May 2004 kwa thamani ya $839,000. Mwaka 2005 ilipanda kufikia karibu $1.1 million according to S&P/Schiller Index (mahesabu waambie jamaa zako wa BOT wakusaidia sina muda huo).

2006 Ikashuka thamani kuwa $840,000 . According to Federal Housing Oversight the median value of house ya sasa in Capitol Hill is about $545,000 ambapo bwana Ben benarke anakaa.

Sasa tuje katika mahesabu ya nyumba ya Ben mwenyewe tukitumia S&P/Schiller Index tuassume price ya mnene Ben ni 840,000 discount na index inayosema imedecline
by 16.3% -07
by 16.6%-08
by 20.3%-09

Unakuta

2007 - Bei ilishuka to 722,270

2008 - Bei imeshuka to 619,442

2009- Bei imeshuka to 514,914.38

Tutie na vikorokoro vya usalama wake na familia yake sidhani kama vinazidi 30,000 kwa state of the art security.

Unakutana na round figure ya 544,914.38 weka na contingencies 549,000

Usifikiri hapa jamii forum watu wana wivu na mtu mzee tunataka umakini wa vitu tu hamna zaidi.
 
Back
Top Bottom