SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 43,707
- 60,760
Lingine la Makamba ni kuwa mwaka 1974 akiwa mkuu wa wilaya ya Tanga, Makamba aliwahi kuwaamuru askari FFU wampige mzee mmja kwa kosa la kukatiza barabara karibu ya TANU Hall wakati akisubiriwa makamu wa rais Mzee Aboud Jumbe kuja kufungua mnara kuashiria kufungua sherehe za sabasaba ambazo kwa mara ya kwanza zilifanyka nje ya Dar es salaam. Kitendo hicho kiliwahuzunisha wote walioshuhudia mzee wa watu akigarazwa huku Makamba akichekelea ukatili ule. Siku hiyo hiyo habari zilimfikia Rais Nyerere, naye kwa kukerwa na ubazazi wa Makamba akampa uhamisho kwenda Kibondo, kiasi kwamba hata hizo sherehe ambazo alishiriki kwa kiasi kikubwa kuziandaa hakuziona. Rejea hii ni kwa taarifa ya wale ambao hawamjui huyu mzee, ni katili, ni jeuri, dikteta,fedhuli,na sifa nyingine zinazo fanana na hizo. Nashauri mtu huyu apuuzwe, akili yake si nzuri