TWIZAMALLYA
JF-Expert Member
- Oct 1, 2011
- 397
- 81
Wanajamiiforums nimesikia kuwa serikali imepeleka mahindi ya msaada Arumeru Mashariki.Swali najiuliza kama kweli kuna haja kihivyo kupeleka msaada Arumeru Mashariki, kwa nini wakati huu wa uchaguzi?.Je serikali imeshindwa vipi kuchelewesha kidogo kupeleka mahindi Arumeru mashariki mpaka uchaguzi upite?.Na je Ni Arumeru mashariki tu ndio kwenye njaa hapa Tanzania?,sehemu kama majirani zao wa Arumeru magharibi hawana shida ya chakula.Mwenye kuweza kuninyoshea haya anisaidie kwani naweza nikawa nimesikia vibaya.Nimesikia kwenye uchambuzi wa magazeti asubuhi ya leo kupitia MAGIC FM.