MTZ 255Dar
JF-Expert Member
- Sep 25, 2018
- 1,114
- 3,768
Kumekuwa na maoni mbalimbali hasa ya wale wanaoongozwa na Hisia kusema kwamba Israel imeshindwa vita dhidi ya Hamas. Sababu kuu ni kwamba wanadai malengo ya Israel ya kuivamia Gaza ilikuwa kuwaokoa mateka jambo ambalo limeshindikana na hivyo Israel imeshindwa vita.
Tukienda kwa Mkitadha huo basi na Urusi imeshindwa vita dhidi ya Ukraine. Kwasababu zifuatazo:
Malengo makuu ya Urusi kuivamia Ukraine yalikuwa yafuatayo;
(i) Kuondoa wanazi ambao wanatawala pale Ukraine(Denazification)
(ii) Kuharibu Silaha zote za Ukraine na kuifanya Ukraine isiwe na uwezo tena kijeshi(Demilitarization)
(iii) Kuyakomboa majimbo yote matatu(Dotnesk, Luhansk na Kherson) kutoka kwenye utawala wa Ukraine.
Matokeo yake
(i) Lengo la kwanza la kuwaondoa wanazi pale Ukraine limefeli. Kwanini? Mwanzo wa Vita Putin na Waziri wake wa Mambo ya nje Sergei Lavrov waliweka wazi kwamba Ukraine inatawaliwa na Wanazi ambao wanachochea mauaji ya watu wanaozungumza Kirusi kule mashariki mwa Ukraine, hapa maana yake kuanzia Rais Zelensk, na Mawaziri wake walio wengi ni Manazi ambao wanatakiwa kuuawa au kuondolewa madarakani. Mpaka leo sote ni mashahidi, huu ni mwaka wa pili, hakuna kiongozi yoyote yule wa ngazi za juu wa Ukraine ambaye alishauawa hasa viongozi wa kisiasa. Kwahiyo lengo la kuwaondoa Manazi kwa mjibu wa Putin nalo limefeli pakubwa make ndio kwanza kabisa Warusi wanachukiwa zaidi nchini Ukraine na hata nchi jirani za Baltics(Estonia, Latvia na Lithuania) kuliko kabla ya vita hivyo.
(ii) Lengo la Pili la Kuharibu uwezo wa kijeshi wa Ukrane limefeli tena sana. Mwanzo wa vita Urusi iliweka ushahidi wa maneno na madai lukuki kwamba Ukraine inatumiwa na nchi za Magharibi kwa maandalizi ya kuivamia Urusi kupitia jimbo la Crimea. Wakati huo, Ukraine ilikuwa haijawhi kurusha hata jiwe moja kuelekea nchini Urusi. Sasa leo hii mwaka wa pili wa oparesheni ya kuharibu uwezo wa kijeshi wa Ukraine tunashuhudia Ukraine ikipata uwezo wa Kijeshi wa Kurusha ndege zisizo na rubani mpaka sio tu mji mkuu wa Moscow bali mpaka kwenye makazi ya rais wa Urus pale Kremlin. Tumeshuhudia manowari ya kijeshi(Flagship) ya Urusi kwa jina MOSKVA ikizamishwa na makombora ya NEPTUNE ya Ukraine. Je, Is Ukraine Stronger or weak after the War?
(iii) Lengo la tatu la Kuyateka majimbo matatu ya Ukraine nalo limefanikiwa kisiasa lakini kijeshi bado kabisa. Ukweli ni kwamba, mpaka tunavyozungumza hivi sasa, Urusi imefanikiwa kuteka vipande tu vya majimbo yafuatayo kule mashariki na kusini mwa Ukraine, kwenye mabano ni % ya eneo lilotekwa na Urusi kwenye jimbo husika.
Majimbo ya Dotnesk la Luhansk hata kabla ya vita tayari yalikuwa yanatawaliwa na waasi wa DPR na LPR ambao wanaungwa mkono na Urusi. Licha ya Urusi kutoyadhibiti majimbo hayo kijeshi kwa 100% basi iliamua kujichukulia ushindi wa kisiasa zaidi ya kuamlu upigaji wa kura ya maoni wa vipande vya majimbo hayo kujiunga na Urusi. Ikumbukwe kuwa miji mikuu ya majimbo hayo iko chini ya udhibiti wa Ukraine mpaka sasa.
Mwisho
Licha ya wengi kuwa na madai kwamba Ukraine inapata msaada wa Silaha kutoka nchi za Magharibi, lakini wakumbuke kuwa Silaha bila Molare ya vita lazima ushindwe. Licha ya kupewa silaha za kutosha na mafunzo kede wa kede, Serikali ya Ashraf Ghan wa Afghanistan iliangushwa na Wapiganaji wa Taaliban masaa 48 tu baada ya Wanajeshi wa Marekani kuondolewa nchini humo.
NB
Kama kushinda vita ni kufikia malengo ya Vita, basi Urusi na Israel wameshindwa Vita kwa Mkitadha huo.
Tukienda kwa Mkitadha huo basi na Urusi imeshindwa vita dhidi ya Ukraine. Kwasababu zifuatazo:
Malengo makuu ya Urusi kuivamia Ukraine yalikuwa yafuatayo;
(i) Kuondoa wanazi ambao wanatawala pale Ukraine(Denazification)
(ii) Kuharibu Silaha zote za Ukraine na kuifanya Ukraine isiwe na uwezo tena kijeshi(Demilitarization)
(iii) Kuyakomboa majimbo yote matatu(Dotnesk, Luhansk na Kherson) kutoka kwenye utawala wa Ukraine.
Matokeo yake
(i) Lengo la kwanza la kuwaondoa wanazi pale Ukraine limefeli. Kwanini? Mwanzo wa Vita Putin na Waziri wake wa Mambo ya nje Sergei Lavrov waliweka wazi kwamba Ukraine inatawaliwa na Wanazi ambao wanachochea mauaji ya watu wanaozungumza Kirusi kule mashariki mwa Ukraine, hapa maana yake kuanzia Rais Zelensk, na Mawaziri wake walio wengi ni Manazi ambao wanatakiwa kuuawa au kuondolewa madarakani. Mpaka leo sote ni mashahidi, huu ni mwaka wa pili, hakuna kiongozi yoyote yule wa ngazi za juu wa Ukraine ambaye alishauawa hasa viongozi wa kisiasa. Kwahiyo lengo la kuwaondoa Manazi kwa mjibu wa Putin nalo limefeli pakubwa make ndio kwanza kabisa Warusi wanachukiwa zaidi nchini Ukraine na hata nchi jirani za Baltics(Estonia, Latvia na Lithuania) kuliko kabla ya vita hivyo.
(ii) Lengo la Pili la Kuharibu uwezo wa kijeshi wa Ukrane limefeli tena sana. Mwanzo wa vita Urusi iliweka ushahidi wa maneno na madai lukuki kwamba Ukraine inatumiwa na nchi za Magharibi kwa maandalizi ya kuivamia Urusi kupitia jimbo la Crimea. Wakati huo, Ukraine ilikuwa haijawhi kurusha hata jiwe moja kuelekea nchini Urusi. Sasa leo hii mwaka wa pili wa oparesheni ya kuharibu uwezo wa kijeshi wa Ukraine tunashuhudia Ukraine ikipata uwezo wa Kijeshi wa Kurusha ndege zisizo na rubani mpaka sio tu mji mkuu wa Moscow bali mpaka kwenye makazi ya rais wa Urus pale Kremlin. Tumeshuhudia manowari ya kijeshi(Flagship) ya Urusi kwa jina MOSKVA ikizamishwa na makombora ya NEPTUNE ya Ukraine. Je, Is Ukraine Stronger or weak after the War?
(iii) Lengo la tatu la Kuyateka majimbo matatu ya Ukraine nalo limefanikiwa kisiasa lakini kijeshi bado kabisa. Ukweli ni kwamba, mpaka tunavyozungumza hivi sasa, Urusi imefanikiwa kuteka vipande tu vya majimbo yafuatayo kule mashariki na kusini mwa Ukraine, kwenye mabano ni % ya eneo lilotekwa na Urusi kwenye jimbo husika.
- Kharkiv(12%)
- Dotnesk (70%)
- Luhansk(85%)
- Kherson(60%)
- Zhaporizhia(40%)
Majimbo ya Dotnesk la Luhansk hata kabla ya vita tayari yalikuwa yanatawaliwa na waasi wa DPR na LPR ambao wanaungwa mkono na Urusi. Licha ya Urusi kutoyadhibiti majimbo hayo kijeshi kwa 100% basi iliamua kujichukulia ushindi wa kisiasa zaidi ya kuamlu upigaji wa kura ya maoni wa vipande vya majimbo hayo kujiunga na Urusi. Ikumbukwe kuwa miji mikuu ya majimbo hayo iko chini ya udhibiti wa Ukraine mpaka sasa.
Mwisho
Licha ya wengi kuwa na madai kwamba Ukraine inapata msaada wa Silaha kutoka nchi za Magharibi, lakini wakumbuke kuwa Silaha bila Molare ya vita lazima ushindwe. Licha ya kupewa silaha za kutosha na mafunzo kede wa kede, Serikali ya Ashraf Ghan wa Afghanistan iliangushwa na Wapiganaji wa Taaliban masaa 48 tu baada ya Wanajeshi wa Marekani kuondolewa nchini humo.
NB
Kama kushinda vita ni kufikia malengo ya Vita, basi Urusi na Israel wameshindwa Vita kwa Mkitadha huo.