OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,336
: Mahanga alikamatwa na masanduku ya kura | Send to a friend |
SHAHIDI wa tisa katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge katika Jimbo la Segerea, Aziza Masoud (25) ameieleza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kuwa mbunge wa jimbo hilo, Dk Makongoro Mahanga alikamatwa na masanduku ya kura. Masoud ambaye ni Mwandishi wa Habari wa gazeti la Mwananchi, alidai hayo jana kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wakati akitoa ushahidi wake katika kesi hiyo inayosikilizwa na Jaji Profesa Ibrahim Juma, akiongozwa na wakili Peter Kibatala anayemtetea Mpendazoe. Kesi namba 98 ya mwaka 2011, ilifunguliwa na Mpendazoe aliyekuwa mgombea wa nafasi hiyo kwa tiketi ya Chadema, akipinga ushindi wa Dk Mahanga katika uchaguzi mkuu mwaka 2010. Katika ushahidi wake jana Masoud alidai kuwa Dk Mahanga alikamatwa wakati akiwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Segerea na walipata taarifa za kukamatwa kwake kupitia kwa baadhi ya mawakala waliokuwa wakishiriki katika uchaguzi huo katika jimbo hilo. Alidai kuwa Novemba Mosi mwaka 2010 Msimaizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo katika Manispaa ya Ialala, Gabriel Fuime alithibitisha kukamatwa kwa mgombea huyo na kwamba tayari alishapeleka taarifa hizo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). "Katika mkutano wa wandishi wa habari ulioitishwa na Fuime kuna mwandishi aliomuuliza kuhusu suala hili, Fuime alikiri kuwa na taarifa hizo na alisema kwamba yeye hawezi kulishughulikia suala hilo bali atalipeleka NEC na atatoa majibu kwa wagomea,"alidai Masoud. Aliendelea kudai kuwa baada ya msimamizi huyo wa uchaguizi kukiri kupata taarifa hizo aliandika habari iliyotoka katika gazeti la Mwananchi Novemba 2, 2010. Hata hivyo Maosud alidai kuwa katika habari hiyo, hakumtaja kwa jina mgombe huyo aliyekamatwa na masanduku wala cheo chake licha ya kutajiwa na vyanzo vya vyake vya habari. Alidai kuwa kuandika taarifa hiyo hakukumletea matatizo ama vitisho ingawa aliwahi kusikia ofisini kwake kuwa kuna baadhi ya watu waliopiga simu kuhoji kuhusu habari hiyo. Aliongeza kuwa yeye binafsi wala gazeti lake hawajawahi kushtakiwa mahali popote kutokana na kuandika au kuchapisha habari hiyo. "Hatujawahi kushtakiwa au kufikishwa mahakamani kwa kum-quote (kumnukuu) Fuime katika stori hiyo, sisi tuna utaratibu wa kutoa taarifa kwa jamii , hatuogopi ikiwa habari husika ina maslahi kwa jamii,"alidai. Katika kesi hiyo Mpendazoe analalamikia mwenendo mzima wa uchaguzi katika jimbo hilo akida taratibu na sheria za uchaguzi zilikiukwa katika ukusanyaji ujumulishaji na utaratibu wa kuhesabu na utangazaji wa matokeo. Hivyo anaiomba Mahakama hiyo itengue matokeo ya ushindi wa mbunge aliyetangazwa na kuamuru ufanyike uchaguzi mdogo, au yeye atangazwea mshindi.Kesi hiyo itaendelea tena leo mahakamani hapo ambapo mashahidi wa upande wa madai wataendelea kutoa ushahidi. |