nguvumali
JF-Expert Member
- Sep 3, 2009
- 4,923
- 1,325
nimefuatilia sokomoko na Mh.Magufuli na kauli zake dhidi ya wakazi wa Kigamboni, likanikumbusha kauli zingine tata kuwahi kutolewa huko nyuma, nikadharau kuwa hayo ni malipo kwetu dhidi ya ujinga wa kuchagua wasio chagulika , wasioaminika na wasiojali usalama wa maisha yetu na ndio maana hata hakuwahi kuona aibu kugawa nyumba kwa kijana wake na kwa yule mwanamke ambae uusiano wake haujawahi kuwekwa wazi na familia yake.
Wiki iliyopita Magufuli akaibukia na Wajapani na kututangazia kuwa watarudia ujenzi wa Barabara ya Kilwa, na akajitapa kuwa watarudia bila malipo mapya na gharama yote italipwa na serikali ya Japan maana wao ndio waliomleta Mkandarasi yule alieshindwa.
Nakubaliana nae katika hilo.
lakini tujiulize, Je hawakua mainjinia wa serikali ya Jamhuri ya Muungano waliopokea hiyo barabara ya awali ikiwa na mapungufu makubwa ? Je wamechukuliwa hatua gani kwa kupokea barabara duni, dhaifu na mbovu ajabu ? Je muda wetu unaopotea wakati wa ukarabati mpya unalipwaje ? je Mkandarasi yule aliejenga barabara mbovu amechukuliwa hatua gani ? maana ni Magufuli huyuhuyu huwa anajitapa ni bingwa wa kufuta makamouni ya kitapeli , Mbona hawa Kajima ni maji mazito kwake ?
Kwatabia zake za kuwalinda watendaji waliopokea barabara hiyo namuona magufuli akielea katika bahari ileile ya wanachama wenzie dhaifu wa ccm
Wiki iliyopita Magufuli akaibukia na Wajapani na kututangazia kuwa watarudia ujenzi wa Barabara ya Kilwa, na akajitapa kuwa watarudia bila malipo mapya na gharama yote italipwa na serikali ya Japan maana wao ndio waliomleta Mkandarasi yule alieshindwa.
Nakubaliana nae katika hilo.
lakini tujiulize, Je hawakua mainjinia wa serikali ya Jamhuri ya Muungano waliopokea hiyo barabara ya awali ikiwa na mapungufu makubwa ? Je wamechukuliwa hatua gani kwa kupokea barabara duni, dhaifu na mbovu ajabu ? Je muda wetu unaopotea wakati wa ukarabati mpya unalipwaje ? je Mkandarasi yule aliejenga barabara mbovu amechukuliwa hatua gani ? maana ni Magufuli huyuhuyu huwa anajitapa ni bingwa wa kufuta makamouni ya kitapeli , Mbona hawa Kajima ni maji mazito kwake ?
Kwatabia zake za kuwalinda watendaji waliopokea barabara hiyo namuona magufuli akielea katika bahari ileile ya wanachama wenzie dhaifu wa ccm