Magufuli apiga STOP Safari za nje ya Nchi; Elimu Bure kuanza Januari 2016...

Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue, ameweka bayana kuwa hata safari ya nje ya nchi isiyogharamiwa na serikali nayo inaweza kukataliwa pia kama itaonekana haina tija kwani mtumishi awapo nje ya nchi bado serikali inamlipa mshahara wake hivyo ni lazima serikali ijiridhishe kwanza kuhusu umuhimu wa safari hiyo.

Chanzo: Channel 10.

Changamoto:Katibu Mkuu kiongozi hii kazi ya kuidhinisha safari sidhani kama ataimudu peke yake labda kazi zake zingine zisimame maana bila shaka meza yake itajaa maombi ya safari za kila siku na bado zingine zitakuwa safari za dharura.

Ushauri:Kwenye Bunge litakaloonza mwishoni mwa mwezi January mwakani,serikali ipeleke taarifa Bungeni imepokea maombi kiasi gani ya safari na ni maombi kiasi gani yamekubaliwa na yale yaliyokataliwa na pia umma upewe taarifa ni kiasi gani cha fedha serikali imeokoa.


Bado siku ya siku hii nia njema ya kuokoa pesa ni sehemu ya kutengeneza mianya ya rushwa tena kubwa kubwa itakayo husu Ofisi ya Raisi mmoja kwa Mmoja-chini ya Usimamizi wa Katibu Mkuu Kiongozi.

Nilitegemea mpaka sasa Katibu Mkuu Kiongozi angekuwa amekwisha weka wazi Vigezo vinavyotumika kufikia kutoa kibali cha kusafiri nje.
Maana itafika mahali Mfumo huu wa nyuma ya pazia ndiyo utakuwa Fimbo kwa waisopendwa kwa kuchuki binafsi au za Kisiasa,Ukabila nadani yake na mengineyo.


Everything you do in life you must do with caution!


 
Mwanzo mzuri, nyie ndio mnataka maendeleo? Unadhani maendeleo yanakuja ndani ya wiki mbili? Come on bwana, ulitaka alipoapishwa tu sement, mbao, viwanja vishuke bei...sijasomea uchumi lakini mkuu maendeleo hayaji hivyo. Ni lazima kwanza afanye kubana matumizi ya serikali, pato la taifa liongezeke, aweke vipaumbele na kuanza kuvifanyia kazi.
Tusubiri tuone,lakini mie Tomaso.Hakuna jipya kutoka CCM.Richmond,Dowans,Symbion,Escrow,Gas,Madini,Iptl,EPA,nk ashughulikie hivyo.Akiweza hivyo pamoja na Rushwa kubwa na madawa ya kulevya na ujangili then tukaenda sambamba na kubana matumizi Tanzania itakuwa Paradiso
 
WANDUGU, tujiulize, hivi magufuli kuzuia watu kusafiri nje ya nchi kuna faida au hasara?
1. manufaa yake ni yepi? kwamba wanaenda kuficha hela?

2. kwanini wote wanaoenda nje wanaenda kuficha pesa? kwanini usipige marufuku hao wakubwa tu na sisi wadogo uturuhusu bila kupitia kwako? hiki kufungo kitaendelea hadi lini? tunakos vingi.

watu wengi wanaadhibiwa kwa kuwekwa kwenye kundi moja na mafisadi wakati wao hawajawahi hata kuwa mafisadi. kwanini mafisadi watufanye tuzuiliwe safari za nje?

3. kwanini haja categorise? wafanyakazi wa ngazi za juu ndio wazuiliwe, na hawa ambao hata hawana milioni kumi kwenye account zao waruhusiwe tu kwasababu kuna wafanyakazi wa hali za chini wanaoenda kusoma na wanakosa ruhusa kutoka nje, mtu umepata scholarship hata hela ya kujilipia ulikuwa huna, serikali yako imeshindwa kukulipia, umepata scholarship ila unashindwa kwenda kwasababu rais amezuia.

4. kwanini vibali vinachelewa sana? vinacheleweshwa sana ukitaka kusafiri unaomba kibali miezi mitatu kabla?

kwanini tunaishi kama kifungoni? hivi watanzania mbona tumekuwa kama kuku wa kufugwa namna hii? tutakombolewa lini na kifungo hiki? watu wanapoteza hata scholarship, badala ya kwenda kusoma warudi watumikie taifa ati wanashindwa kutoka nje kwasababu rais amekataza wafanyakazi kutoka nje......

NAKUOMBA RAIS, jaribu kufikiria hili jambo, tunajua kuwa unataka watu wasipeleke nje hela walizoiba, lakini sio wote wana hizo hela, wengine wamedunduliza wakasome nje wamepata shule lakini hawawezi kutoka nje, na hadi kuja kupata kibali cha kusafiri hapo kwako, kutokana na volute ya vibali vingi, inachukua muda, inapoteza muda hadi dili ulilokuwa unafukuzia linayeyuka, sasa hapo kuna faida gani?

mtu kama huyo unakuwa umemsaidia vipi sasa, urais wako ataona una faida gani kama alipata shule, scholarship halafu anashindwa kwenda nje kwasababu wewe ulichaguliwa kuwa rais? Mungu akusaidie.
 
Wapi Raisi alikataza watu kusafiri kwenda nje ya nchi? Mimi nafahamu ni watumishi wa umma ndio wanatakiwa kusafiri kwa kupata kibali cha katibu mkuu na sio raia wote
 
Wapi Raisi alikataza watu kusafiri kwenda nje ya nchi? Mimi nafahamu ni watumishi wa umma ndio wanatakiwa kusafiri kwa kupata kibali cha katibu mkuu na sio raia wote
watumishi wa umma hao ndio tunaowaongelea, kuna watumishi wa umma wengine kwa mwezi wanapata laki tano mshahara kwa mfano, hajaiba, amepata scholarship anataka kwenda kusoma nje, anatakiwa kuanza kuomba kibali cha kusafiri nje, haujui kitatoka lini manake application hiyo imeenda ikulu, ....hivi hao ndio walikuwa target group ya kuwazuia wasisafiri? watumishi wa umma ni wangapi Tanzania? ni wengi sana, rais ashughulikie matatizo (hata kama anamtumia katibu mkuu kiongozi) halafu na hapohapo ashughulikie ati mtu wa chini namna hii apate au asipate kibali? hao hao watumishi wa umma wanapata scholarship wanashindwa kwenda nje kwasababu ya milolongo kama hiyo....au hao sio watu? tunaongea kwasababu tumeshuhudia madogo wakipata shida sana na huko ikulu hauna mtu wa kukusaidia kuharakisha mambo, na hauwezi kwenda ikulu ati kuwaambia wakufanyie assessment haraka. kwanini watumishi wa umma wanakuwa kifungoni namna hiyo? hao nao walimpigia kura ati?

mimi nampenda magufuli na ninamshukuru Mungu ametuletea rais wa aina yake. lakini, kitu hiki kinanikwaza sana, nahisi kuna kundi la watu linapata adhabu kutokana na mafisadi wachache ndani ya utumishi wa umma, hauwezi kufanya kitu kitakachowadhuru wote kiasi hiki. kuna watu wanadhurika kwa katazo hili hata kama watu wanakaa kimya.
 
Kwani zamani mlikua mnajiondokea tu bila kibali?
Kama unaenda kusoma wakikubania ruhusa,sepa tu
 
Kuna watu wengi wameathiliwa kwa zuio hili la rais hata wanafunzi waliopaswa kwenda masomoni msumbiji wamekataliwa
 
Hata mimi nimesumbukia kutafuta scholarship tangu mwaka 2013, mwaka huu naona kuna dalili za kupata halafu tena wanatuzuiya kwenda nje! Dah, binafsi nashindwa nifanyeje
 
Zile takwimu mabillion ya posho hukuzisikia?
Kwa taarifa yako, posho ya siku moja ni Dollar 400! Fanya hesabu za haraka hapo upate jibu
 
Airport bongo ukiwa unapita dirisha la uhamiaji to international departures wanauliza hadi kitambulisho chako cha kazi if ukiwaambia wewe sio mtumishi wa umma,so kama hauna inaweza kukuletea shida.
 
watu wengine hawaendi kule kwa kutumia hela ya serikali hii, wanaenda kule kwa scholarship na wengine wameokoteza toka kwa ndugu na marafiki, halafu ati unatakiwa uadhibiwe kwasababu serikali ina mafisadi, kwanini watu wa chini wapate kibano kwasababu ya mafisadi wasio hata na shida? hiki kibano mheshimiwa rais kimezidi, punguza au toa mwongozo mpya.
 
watu wengine hawaendi kule kwa kutumia hela ya serikali hii, wanaenda kule kwa scholarship na wengine wameokoteza toka kwa ndugu na marafiki, halafu ati unatakiwa uadhibiwe kwasababu serikali ina mafisadi, kwanini watu wa chini wapate kibano kwasababu ya mafisadi wasio hata na shida? hiki kibano mheshimiwa rais kimezidi, punguza au toa mwongozo mpya.
Upo sahihi mkuu! Ni wakati umefika sasa mheshimiwa rais alifikirie upya swala hili kwani wanyonge hawana hatia hususani kwa wanafunzi waliopata scholarship
 
Airport bongo ukiwa unapita dirisha la uhamiaji to international departures wanauliza hadi kitambulisho chako cha kazi if ukiwaambia wewe sio mtumishi wa umma,so kama hauna inaweza kukuletea shida.

Hivi watajuaje kama huyu ni mtumishi wa serikali na yule si mtumishi wa serikali,hiyo sorting inafanyika vip.
 
Watu kama wewe ni jamii ya mashetani, kwani shetani ndie asiyependa zuri lolote kwa mwanadamu.

Rais ndio kwanza ameanza kazi ,nyie mshaanza kumuombea ashindwe. Akifanikiwa matunda ni ya watanzania wote, sioni sababu ya kwanza fitina.
CCM hakuna jipya , hata JK alianzaga na mbwembwe kama hizi
 
Hivi watajuaje kama huyu ni mtumishi wa serikali na yule si mtumishi wa serikali,hiyo sorting inafanyika vip.
Kama nilivosema hapo wanauliza kitambulisho chako cha kazi,yani as if kuna sheria ukisafiri ubebe na id ya kazini,chenga sana. Unaweza sema sijaajiriwa lakini wanaweza komaa tu kizushi.
 
Leo Jumamosi, Rais Dr. Magufuli akutana na makatibu wakuu, manaibu makatibu wakuu na watendaji wakuu wa serikali leo Ikulu.

Huu ni Mkutano Maalum.

=============================

Updates;





Picha na Ikulu





nadhani issue kubwa hapa ni wale wafanyakazi wa serikali/umma ambao walikuwa wanatengeneza safari alafu masurufu yake au perdiem zake zinalipwa na serikali, na kama sijakosea ni karibu dola 4000 kwa siku kwa mtu mmoja akiwa safari ya kikazi nje ya nchi. Ila kwa mtu ambaye safari yake hailipiwi hata senti moja na pesa za serikali/umma nadhani masharti yangelegezwa kidogo.
 
Hivi watajuaje kama huyu ni mtumishi wa serikali na yule si mtumishi wa serikali,hiyo sorting inafanyika vip.
waeleze tu kwamba, watumishi wa serikali wa kada hii ndio waadhibiwe, kuanzia hao wakurugenzi, wakuu wa vitengo n.k. sasa kuna mwingine ndio ameajiriwa ana miaka miwili au mitatu anataka akajiendeleze kimasomo, naye wanambania au anaingizwa kwenye kundi la watu wanaoenda ulaya kuficha hela au kuzurura? hata kama wanasema asiyetaka kazi aache, kuna siku watu wataacha halafu serikali sijui itafanya kazi na nani. hakuna mazingira mazuri, mfanyakazi wa serikali anaonekana ni mwizi hata kama hajawahi kuiba, manyanyaso kibao mshahara mdogo, loh
 
Back
Top Bottom