Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Utangulizi
Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais J.P.Magufuli (CCM) imeanza kuwatumikia wananchi kwa kipindi cha (2015-2020) kwa mujibu wa katiba ya JMT(1977).
Vipaumbele vikuu vya serikali ya awamu ya tano ni pamoja na:
·Kurudisha nidhamu katika mfumo wa fedha za umma
·Kuziba mianya ya ukwepaji kodi na
.Kubana matumizi ya fedha za umma.
Sambamba na haya, serikali pia (kupitia waziri wa Fedha, Uchumi na Mipango, Dr. Mpango), imewasilisha sura ya bajeti ya mwaka 2016-17 pamoja na mapendekezo ya Mpango wa pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano (2016/2017 – 2020/2021).
Tutajadili matarajio ya kiuchumi chini ya Rais Magufuli na Changamoto zake kwa kipindi cha 2015-2020. Tutafanya hivyo kwa muktadha wa dhana ya “Mabadiliko” tarajiwa ya Wananchi wengi, hasa maisha yao KIUCHUMI.
Wananchi wengi (hasa maskini) wanatumaini Uchaguzi wa TANO wa Vyama Vingi (2015) katika dhana ya ''mabadiliko'' utaondoa mfumo unaoshadidia mambo YALE YALE kufanywa kwa namna ILE ILE na yenye matokeo YALE YALE kwa maisha yao kwa miaka zaidi ya Hamsini ya uhuru.
Mjadala wetu umegawanyika katika sehemu kuu SITA:
Sehemu ya Kwanza
Tutajadili Matarajio ya wananchi Kiuchumi tukiyangalia katika maeneo makuu mawili:
(1) Sura ya Bajeti ya Kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano (2016-17) na Mapendekezo ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano (2016/17-2020-2021).
(2) Tutajadili matarajio ya wananchi kwa undani juu ya yanayopaswa kuwa ‘Majukumu ya Serikali” katika Uchumi wa Taifa.
Sehemu ya Pili
Tutajadili ngazi kuu za Serikali – (i) Serikali Kuu” na (ii)Serikali za Halmahauri.
Hapa tutaangalia kwa undani mgawanyo wa majukumu wa ngazi hizi mbili za Serikali katika kuleta ufanisi na matokea chanya kisiasa (demokrasia), kiuchumi na kijamii, kwa faida ya wananchi walio wengi.
Sehemu ya Tatu
Tutajadili Mamlaka ya Kodi na Mapato [“Taxation and Revenue powers”] katika ngazi mbili kuu za serikali – Serikali Kuu na Serikali Za Halmashauri.
Tutatazama urali “Fiscal Imbalances” katika ngazi za Halmashauri na jinsi gani changamoto zake zinapaswa kutatuliwa kwa ushirikiano baina ya ngazi mbili kuu hizi za Serikali.
Pia tutaangalia aina mbalimbali za Kodi:
– Kodi zipi zinapaswa kusimamiwa na serikali kuu;
- Kodi zipi zinapaswa kusimamiwa na Serikali ngazi za halmashauri; na
- Kodi zipi zinaweza kusimamiwa kwa kushirikisha ngazi kuu mbili.
Lengo kuu hapa ni kuleta ufanisi wenye matokeo chanya kwa maisha ya wananchi walio wengi - Kijamii, Kiuchumi na Kisiasa(demokrasia)
Sehemu ya Nne
Tutajadili hali ya “Deni la Taifa” na changamoto (zitokanazo) kwa Serikali ya awamu ya Tano katika utekelezaji wa mipango yake mbalimbali ya kibajeti na kimaendeleo.
Sehemu ya Tano
Tutajadili hali ya baadae ya uchumi katika muktadha wa deni la NJE, kwa kufanya tathmini ya mwenendo wa deni la nje.
Pamoja na mengineyo, tutajadili:
· Historia fupi ya deni la nje.
· Matumizi (kisekta) ya deni la nje.
· Athari (impact) ya mikopo ya nje katika maendeleo ya uchumi na jamii.
· Hatari (risk) iliyopo mbeleni ya nchi kuingia katika mgogoro mkubwa kiuchumi na hivyo kutoweza kukopesheka. Katika hili, tutafanya tathmini ya masuala makuu mawili:
- Kwanza ni tathimini ya Mapato ya kodi kwa kuangalia iwapo katika kipindi cha 2016-2021, mapato haya yatatosha kuiwezesha serikali kulipa madeni ya nje bila ya kuathiri majukumu ya serikali ya kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi.
- Pili, ni tathmini ya Mapato ya Fedha za Kigeni kupitia mazao ya kibiashara nje ya nchi kwa kipindi cha 2016-2021, na kuangalia iwapo mapato haya yatatosha kuiwezesha serikali kulipa madeni ya nje bila ya kuathiri uwezo wake wa kuwajibika kwa wananchi.
Sehemu ya Sita
Sehemu ya Siita itakuwa ni hitimisho la mjadala.
Bandiko linalofuata litaanza na sehemu ya kwanza:
(1) Sura ya Bajeti ya Kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano (2016-17) na Mapendekezo ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano (2016/17-2020-2021).
(2) Tutajadili matarajio ya wananchi kwa undani juu ya yanayopaswa kuwa ‘Majukumu ya Serikali” katika Uchumi wa Taifa.
Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais J.P.Magufuli (CCM) imeanza kuwatumikia wananchi kwa kipindi cha (2015-2020) kwa mujibu wa katiba ya JMT(1977).
Vipaumbele vikuu vya serikali ya awamu ya tano ni pamoja na:
·Kurudisha nidhamu katika mfumo wa fedha za umma
·Kuziba mianya ya ukwepaji kodi na
.Kubana matumizi ya fedha za umma.
Sambamba na haya, serikali pia (kupitia waziri wa Fedha, Uchumi na Mipango, Dr. Mpango), imewasilisha sura ya bajeti ya mwaka 2016-17 pamoja na mapendekezo ya Mpango wa pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano (2016/2017 – 2020/2021).
Tutajadili matarajio ya kiuchumi chini ya Rais Magufuli na Changamoto zake kwa kipindi cha 2015-2020. Tutafanya hivyo kwa muktadha wa dhana ya “Mabadiliko” tarajiwa ya Wananchi wengi, hasa maisha yao KIUCHUMI.
Wananchi wengi (hasa maskini) wanatumaini Uchaguzi wa TANO wa Vyama Vingi (2015) katika dhana ya ''mabadiliko'' utaondoa mfumo unaoshadidia mambo YALE YALE kufanywa kwa namna ILE ILE na yenye matokeo YALE YALE kwa maisha yao kwa miaka zaidi ya Hamsini ya uhuru.
Mjadala wetu umegawanyika katika sehemu kuu SITA:
Sehemu ya Kwanza
Tutajadili Matarajio ya wananchi Kiuchumi tukiyangalia katika maeneo makuu mawili:
(1) Sura ya Bajeti ya Kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano (2016-17) na Mapendekezo ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano (2016/17-2020-2021).
(2) Tutajadili matarajio ya wananchi kwa undani juu ya yanayopaswa kuwa ‘Majukumu ya Serikali” katika Uchumi wa Taifa.
Sehemu ya Pili
Tutajadili ngazi kuu za Serikali – (i) Serikali Kuu” na (ii)Serikali za Halmahauri.
Hapa tutaangalia kwa undani mgawanyo wa majukumu wa ngazi hizi mbili za Serikali katika kuleta ufanisi na matokea chanya kisiasa (demokrasia), kiuchumi na kijamii, kwa faida ya wananchi walio wengi.
Sehemu ya Tatu
Tutajadili Mamlaka ya Kodi na Mapato [“Taxation and Revenue powers”] katika ngazi mbili kuu za serikali – Serikali Kuu na Serikali Za Halmashauri.
Tutatazama urali “Fiscal Imbalances” katika ngazi za Halmashauri na jinsi gani changamoto zake zinapaswa kutatuliwa kwa ushirikiano baina ya ngazi mbili kuu hizi za Serikali.
Pia tutaangalia aina mbalimbali za Kodi:
– Kodi zipi zinapaswa kusimamiwa na serikali kuu;
- Kodi zipi zinapaswa kusimamiwa na Serikali ngazi za halmashauri; na
- Kodi zipi zinaweza kusimamiwa kwa kushirikisha ngazi kuu mbili.
Lengo kuu hapa ni kuleta ufanisi wenye matokeo chanya kwa maisha ya wananchi walio wengi - Kijamii, Kiuchumi na Kisiasa(demokrasia)
Sehemu ya Nne
Tutajadili hali ya “Deni la Taifa” na changamoto (zitokanazo) kwa Serikali ya awamu ya Tano katika utekelezaji wa mipango yake mbalimbali ya kibajeti na kimaendeleo.
Sehemu ya Tano
Tutajadili hali ya baadae ya uchumi katika muktadha wa deni la NJE, kwa kufanya tathmini ya mwenendo wa deni la nje.
Pamoja na mengineyo, tutajadili:
· Historia fupi ya deni la nje.
· Matumizi (kisekta) ya deni la nje.
· Athari (impact) ya mikopo ya nje katika maendeleo ya uchumi na jamii.
· Hatari (risk) iliyopo mbeleni ya nchi kuingia katika mgogoro mkubwa kiuchumi na hivyo kutoweza kukopesheka. Katika hili, tutafanya tathmini ya masuala makuu mawili:
- Kwanza ni tathimini ya Mapato ya kodi kwa kuangalia iwapo katika kipindi cha 2016-2021, mapato haya yatatosha kuiwezesha serikali kulipa madeni ya nje bila ya kuathiri majukumu ya serikali ya kutoa huduma mbalimbali kwa wananchi.
- Pili, ni tathmini ya Mapato ya Fedha za Kigeni kupitia mazao ya kibiashara nje ya nchi kwa kipindi cha 2016-2021, na kuangalia iwapo mapato haya yatatosha kuiwezesha serikali kulipa madeni ya nje bila ya kuathiri uwezo wake wa kuwajibika kwa wananchi.
Sehemu ya Sita
Sehemu ya Siita itakuwa ni hitimisho la mjadala.
Bandiko linalofuata litaanza na sehemu ya kwanza:
(1) Sura ya Bajeti ya Kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano (2016-17) na Mapendekezo ya Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano (2016/17-2020-2021).
(2) Tutajadili matarajio ya wananchi kwa undani juu ya yanayopaswa kuwa ‘Majukumu ya Serikali” katika Uchumi wa Taifa.