Tangu kuanza kwa mchakato wa uchaguzi 2010 nimekuwa nikifuatilia kwa makini sana uandishi wa habari kwenye magazeti yanayochapishwa hapa nchini ili kuona ni kiasi gani yamejikita katika kuandika habari zilizo balanced na bila upendeleo kwa wagombea au chama fulani (kama inavyotakiwa kitaaluma). Lakini nimebaini kuwa magazeti yafuatayo yamejidhihirisha wazi kuwa ni wakala wa chama tawala na yamekuwa yakitumiwa kikamilifu kama vyombo vya propaganda vya CCM. :violin:: Daily News/Sunday News, Habari Leo (magazeti ya serikali), Mtanzania, Rai (magazeti ya Rostam Aziz) Sauti Huru (gazeti la Subash Patel) , Tazama (linafadhiliwa na Lowassa). Katika kundi hili pia kuna stesheni za TV za Channel 10 na TBC1 ambazo zina uhusiano wa karibu sana na mafisadi. Ukifuatlia taarifa za vyombo hivi utagundua kwamba vimekuwa vikitumika kupotosha ukweli unaozungumzwa na vyama vya upinzani (hasa Chadema). Mfano ni jinsi walivyopotosha kile alichokisema Marando pale Jangwani wakati wa uzinduzi wa kampeni za Chadema kuhusu wizi wa EPA na kudai ni MATUSI na CHUKI, ingawa sisi tuliokuwepo Jangwani na wale waliomsikiliza Marando watakubaliana nami kwamba tamko lile linahitaji tu uthibitisho (Marando yupo tayari kuthibitisha) na kamwe sio tusi. Taaluma ya habari inataka chombo chochote kinachodhani kinaunga mkono chama fulani cha siasa katika uchaguzi kutangaza waziwazi msimamo wake ili wasomaji au wasikilizaji wajue mapema kuwa habari zitakazoandikwa au kutangazwa na chombo hicho zitakuwa ni za kuunga mkono upande fulani. Lakini hii ni kwa vyombo vilivyo independent na sio vyombo vya umma kama Daily News/Sunday News au TBC. Hawa wanapaswa kuwa impartial na sio vinginevyo. Sijui kama watendaji wa vyombo hivi wanatambua wajibu wao huo!