Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Mwanzoni kabisa tulionywa kuwa mafisadi wana nguvu kubwa na wakikamatwa tu, nchi itayumba. Akakamatwa Jeetu Patel na washiriki wenzake, nchi haikuyumba. Kafuatia Maranda na washiriki wenzake, nchi haikuyumba. Mramba na Yona wakapelekwa Keko, serikali hata haikutikisika. Kafuatia Liyumba na msaidizi wake, hata kutetereka serikali haikutetereka.
Mag3 bado ninasubiri kumwona hili lisilokamatika/hao wasiokamatika ambao wakiguswa tu serikali na nchi nzima ya TZ itawaka moto. Kama hii itatokea kesho, wiki ijayo, mwezi ujao au hata mwaka ujao, kama kawaida yao watanzania wengi naungana nao kuisubiri hii siku - siku ambayo tutatakiwa kujikunyata kwa hofu ya balaa itakayoishukia nchi yangu Tanzania.
Ni siku ambayo tutamfahamu mbaya wetu, tutamwona kwa sura yake halisi, tutamsikia anavyotema cheche kinywani na tutashuhudia atakavyowashukia wale wote waliothubutu kumnyooshea kidole. Siku hiyo zimwi letu linalotutafuna taratibu litajitokeza wazi wazi na masikini Mag3 na wenye mawazo kama yake watatakiwa kutafuta pa kujificha wasipaone.
Siku hiyo tutawatambua bila shaka wale wote waliojificha kivulini mwake na ambao wamemwezesha kulala mlango wazi bila wasiwasi wakimlinda 24/7. Wengine tunao humu humu na hawatakuwa na haja tena ya kuficha majina yao tena - watatembela vifua mbele wakitudhihaki kwa vijembe, tuliwaonya na hamkusikia, sasa mtaonja machungu ya jeuri yenu.
Pamoja na hayo yote naisubiri kwa hamu siku hiyo - kwa sababu licha ya nguvu za adui, ni siku wanyonge watajikomboa. Ni siku ghadhabu na hasira ambazo zimewajaa wazalendo hazitaweza kuzimwa hata kwa vifaru na tutasimama imara kutetea kilicho chetu. Silaha yetu kubwa itakuwa ni kiu ya haki na usawa, kiu ya maendeleo na kiu ya maisha bora - ole wao!!
Mag3 bado ninasubiri kumwona hili lisilokamatika/hao wasiokamatika ambao wakiguswa tu serikali na nchi nzima ya TZ itawaka moto. Kama hii itatokea kesho, wiki ijayo, mwezi ujao au hata mwaka ujao, kama kawaida yao watanzania wengi naungana nao kuisubiri hii siku - siku ambayo tutatakiwa kujikunyata kwa hofu ya balaa itakayoishukia nchi yangu Tanzania.
Ni siku ambayo tutamfahamu mbaya wetu, tutamwona kwa sura yake halisi, tutamsikia anavyotema cheche kinywani na tutashuhudia atakavyowashukia wale wote waliothubutu kumnyooshea kidole. Siku hiyo zimwi letu linalotutafuna taratibu litajitokeza wazi wazi na masikini Mag3 na wenye mawazo kama yake watatakiwa kutafuta pa kujificha wasipaone.
Siku hiyo tutawatambua bila shaka wale wote waliojificha kivulini mwake na ambao wamemwezesha kulala mlango wazi bila wasiwasi wakimlinda 24/7. Wengine tunao humu humu na hawatakuwa na haja tena ya kuficha majina yao tena - watatembela vifua mbele wakitudhihaki kwa vijembe, tuliwaonya na hamkusikia, sasa mtaonja machungu ya jeuri yenu.
Pamoja na hayo yote naisubiri kwa hamu siku hiyo - kwa sababu licha ya nguvu za adui, ni siku wanyonge watajikomboa. Ni siku ghadhabu na hasira ambazo zimewajaa wazalendo hazitaweza kuzimwa hata kwa vifaru na tutasimama imara kutetea kilicho chetu. Silaha yetu kubwa itakuwa ni kiu ya haki na usawa, kiu ya maendeleo na kiu ya maisha bora - ole wao!!