Around $60 a barrel
Dawa ni moja tu hapo. Kumchagua Lowassa
Safi IPI Mkuu,hapo hawatapunguza hata cent sana sana wataongeza hapo
Mungu jalia nasi tuwe na mafuta yetu wenyewe. Amen
Bei itapanda zaidi ya hapo kwa tanzania au mnajifanya hamjui mama baba riz na huyo riz ni wamiliki wa vituo vya mafuta
Sasa ikiwa mkuu wa kaya ndio muuza mafuta je unafikiri atasimamia kushuka kwa bei
Lowasa hoyeeeeee ukawa hoyeeeeee jamani Chonde Chonde dawa ni Kuwamwaga nnya hawa ccm
Halafu hii Ewura mkuu inakera sana eti gharama za uendeshaji wake tunakatwa kwenye bili za umeme kana kwamba wizara haina bajeti ya kuiendeshaEwura hapo macho yana gundi, yakipanda ni fastaaa kabla hata mtangazaji hajamaliza kutangaza...
Wanajamvi tuanze kupiga kelele.
Kukaa tu Kimya na kumtegemea Mungu katika mambo ambayo yapo katika uwezo wako huo ni ujinga ,vipi kwa wasio na imani hizo za kuja nao waseme vipi?.
Nishati ya mafuta ndio kila kitu katika uchumi hasa katika nchi kama yetu ambayo nishati hii inatumika sana kutokana na mahitaji yetu kutegemea huko kama magari/Meli/treni/et.c.
Hivi vyoote kama bei ya nishati hii ya mafuta itakuwa juu basi navyo vinageuka kuwa kama anasa vile ,nauli zitapanda na budhaa zote tunazozitumia zitapanda bei.
Wasomi wetu wameutumia usomi wao kuwagandamiza masikini tusio na elimu ,ni nani wa kutusemea au kututetea kwani CCM wameshashindwa kwa miaka 53 sasa.
Kama mfumo huu umeshindwa kutoa matokeo yaliyotarajiwa ni wa kuwekwa pembeni tulete mfumo mpya wenye fikra tofauti..
Ni kumtegemea Mungu tu ndo dawa, unaweza ukapiga kura vituo vyote vya Dar ila kama hakuna hofu ya Mungu ni bure kabisaOmbea maji yageuke petrol mkuu. Naona hujui maana ya uongozi na mfumo kandamizi. Nina uhakika hata kura wewe hupigi kwasababu unaamini haya yanayotokea yanahitaji maombi tu.
Poor you.