Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,744
mbona anaonekana ni kijana sana kastaafu vipi???? au changa la macho
nahisi kama wamemchakachua! ndo mwenyewe kweli?
mbona anaonekana ni kijana sana kastaafu vipi???? au changa la macho
Waungwana tuliambiwa hii Dowans ina wamiliki sita Andrew James Tice (Canadian), Gopalakrishnan Balachandran (Indian), Hon Sung Woo (Singapore), Guy Arthur Picard (Canadian), Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi (Oman) na Stanley Munai (Kenyan). Mbona huyu Sulaiman Mohammed Yahya Al Adawi (Oman) anajitambulisha kama vile yeye ni mmiliki pekee wa Dowans? Huyo Stanley Munai (Kenyan) ametambulishwa kama Director of Finance. Kulikoni hadi ajitambulishe kama yeye ni mmiliki pekee wa Dowans? Hao wamiliki wengine nao wana mpango wa kuja nchini ili kushiriki katika kudai malipo yao? au wameingia mitini baada ya kuona kasheshe inazidi kuwa ngumu?
Kuna mambo mengi yanayotia shaka katika ujio wa hyu anaejiita mmiliki wa Dowans.
- Imemchukua muda mrefu (takriban miaka mitano) kugundua kuwa yeye ndie mmiliki wa Dowans, baada ya kuikana alipohojiwa miaka iliyopita
- Kujikanganya kwenye maelezo yake kuhusu wamiliki wa kampuni. Anasema yeye ndie mmiliki pekee, wakati hati za usajili zinaonyesha sie pekee, na pidai kuwa major shareholder bila kutaja minor shareholders
- Aliwezaje kuwekeza pesa zote hizo na kukaa kimya mpaka mahakama iamuru alipwe?
- Nini kinachomfanya asitake kupigwa picha na wakati huo huo akijivunia preformance nzuri ya Dowans kwenye mradi huo wa uzalishaji umeme?
- Anategemea serikali (isiyomjua/isiyomfahamu) ifanyeje mazungumzo nae?
- Nini kinachompa nguvu ya kushughulikia na kufuatilia suala ambalo alishamkabidhi RA kulishughulikia kwa ukamilifu, wakati RA huyo huyo akidai haijui kampuni ya Dowans? Ni uwakilishi gani wa siri uliopo kati yao?
Ukiangalia kwa makini utaona kuna nia kuu ya kusafishana zaidi hata ya kudai kulipwa fidia husika. Ndio maana anadai yuko tayari kuipa TANESCO pungufu zuri la award.
Huo ni mtazamo wangu binafsi.
Haswaa... Sisi kweli vilaza...tena vilaza...wa wakutupa