Madiwani waliotimuliwa Chadema Arusha waomba radhi, Napendekeza wasamehewe

Sisiem na sera ya nguv mpya har mpya na kas mpy! ina maana watafkia maamuz ya kufunga viwanja vyote vya wazi coz of cdm?
 
Huyu Meya wa kuchonga, Gaudence Lyimo, akumbushwe kwamba siku zote MCHIMBA KABURI KWA WENGINE SIKU ZOTE huingia mwenyewe.

Hawezi akaamka tu na ulevi wa madaraka ya kuazimwa na kujiamulia tu eti anaufunga uwanja wa Unga Limitedi.

Kwa hili alilolianzisha limo siyo tu kwamba mji wa Arusha huenda kukawa pa moto kwake kuishi bali zaidi sintoshangaa kusikia kwamba Nguvu ya Umma imemg'oa hata hako ka-Umeya danganya toto hako.

Sakata la uwanja wa NMC kugeuzwa na kuwa hifadhi ya wamachinga imechukua sura mpya baada ya madiwani wa CCM kumgeuka meya gaudence lyimo na mkurugenzi kuwa ajenda ya kubadilisha matumizi ya uwanja huu haikufikiwa hitimisho.
Diwani mmoja wa kati ya maeneo ya mjini mjini amesema kuwa awali madiwani walikuwa wameridhia kuwa uwanja uliopo karibu na soko la kilombero utumike mahaliilipokuwa stendi ya semunge. Baadae kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa iliingiwa na hofu baada ya chadema kuubatiza uwanja huo kuwa ni uwanja wa ukombozi - chadema square na hivyo uamuzi wa kuuchukua uwanja huo ukafanyika kiholela holela kwa hamaki bila vikao vya maamuzi kukaa.

Diwani huyo amesema kuwa kiutaratibu uwanja wa wazi unapobadilishwa matumizi unatakiwa utangazwe kwa siku 21 na inapokuwa hauna pingamizi ndipo mkurugenzi anapotangaza mabadiliko ya uwanja wa wazi na matumizi mapya. Katika mazingira haya madiwani wa CCM wameonyesha kulalamika kwa vile vitu vidogo vidogo hivi vimekuwa vingi na vya kizembe na ndivyo vimekuwa vikiwapa chadema nguvu na hoja za kuonyesha ubabaishaji na udhaifu katika uendeshaji wa halmashauri ya arusha mjini kwa ujumla.
 
Nanyaro Ephata sio wala suala la kufanyia vikao tuu ni suala la kupanga mji unaendaje
Unawezaje kukaa na jiji halina uwanja wa wazio hata mmoja hata bustani ya jiji hakuna zaidi ya tu- round about na visehem kama pale ofisi ya mkuu wa mkoa au soweto pale kati kati ya makazi ya watu
Huyo mtu anayueeamua kuwa pale wawekwe machinga alifikiria nini na je haoni kuwa pale mbele ya uwanja kuna shule ya secondary
Huo usumbufu wanafunzi watauzoeaje au ndio mpango wa kuua kabisa ile shule isisikike tena

Nionavyo huu ni mpango kamili wa kuwagombanisha CHADEMA na wamachinga. Kama CHADEMA watapinga mpango huo wapinzani wao wataweza kujenga hoja hasi kuwa CDM hawawajali wamachinga.Hapa lazima kuwa makini sana.
 
Ni aibu kubwa SANA kwa CCM. Yaani ukisikia janga basi CCM ndio lenyewe.

Kwa sasa watanzania hatuna janga lolote la kututisha kwani haiwezekani kukawepo na janga kubwa kama hawa CCM.

Mh. Nanyaro, je kuna utaratibu gani wa kisheria na wa kijamii/kisiasa mnaweza kuuchukua dhidi ya huyo meya wa kichina, RC, na waharibifu wengine hapo Arusha?
 
wanajitekenya wanacheka wenyewe.
hii mipango ya ccm kila siku nivichekesho mara wahonge baadhi ya madaktari ili waombe msamaha kufurahisha nafsi zao.
mimi yangu macho na masikio na miguu.
 
Nionavyo huu ni mpango kamili wa kuwagombanisha CHADEMA na wamachinga. Kama CHADEMA watapinga mpango huo wapinzani wao wataweza kujenga hoja hasi kuwa CDM hawawajali wamachinga.Hapa lazima kuwa makini sana.

Kwa akili yao fupi hilo huenda ni kweli ndilo walilokusudia. Lakini wamachinga, kama watanzania wengine wanajua huo ni usanii wa CCM. Kwanu baada ya muda watawageuka na kujimilikisha wenyewe kisha kuwakodishia wamachinga kwa bei za kifisadi ili kuwafukuza.

Agghhhrrrr!!!! Hawa jamaa wanaudhi mno.
 
Nionavyo huu ni mpango kamili wa kuwagombanisha CHADEMA na wamachinga. Kama CHADEMA watapinga mpango huo wapinzani wao wataweza kujenga hoja hasi kuwa CDM hawawajali wamachinga.Hapa lazima kuwa makini sana.


Hilo nalo neno ila kwa watu makini Kama wa Rchuga wanapenda michezo na burudani wakiwemo hao hao machinga kimsingi machinga wataelewa Kama ndio msimamo wa CDM ila waboreshe zaidi nadhani mpango huo utakuwa hauna mashiko kwa Rchuga ni CDM's territory wako tayari kufa kwa ajili ya CDM japo wengine hawajui ata ilani ya CDM Yani wanaipenda natural na wanaamini na kuheshimu maamuzi ya CDM I'n fact Wana meru ni wanamapinduzi!
 
Hao madiwani wangeomba msamaha kabla ya kwenda Mahakamani wangesamehewa,lakini kwakua walishafika mahakamani na kukwama huko hawafai kabisa kubaki chamani watafute chama kingine,hii ni ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo wapo wengi,watakua wanafanya makusudi wakijua wataomba msamaha na watasamehewa.
 
Mimepita NMC SASA hivi uwanja umeburuzwa na catapila na tayari umezungushiwa nguzo labda by kesho utakukuwa na mabati. Wachezea ccm wewe?
 
Daudi mchambuzi;Wawe wanachama wa kawaida tu,wala la uongozi hapana hasa uyo Ngowi hatutaki hata kumuona

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums[/QUOTE]

NAUNGA HOJA MKONO!
 
Wanajamvini tusome maandiko matakafu. Msamehe mwenzio saba mara sabini. Wasamehewe.
 
Maamuzi haya ni ya KIWENDAWAZIMU,maana kwenye vikao hilo lilipingwa na wadau wengi kwa hoja kuwa kama ikitokea maafa yoyote Arusha hakuna uwanja mwingine wa wazi zaidi ya NMC.Pressure kubwa imetoka kwa Rc na kamati yake ya ulinzi na usalama kwa lengo la kuidhofisha CHADEMA Arusha,pamoja na ule mpango wake wa kuwatumia vijana kupita mtaani wakitukana viongozi wa CHADEMA
RC amekuwa ndio Meya,ndio Mkurugenzi ndie mipango miji

mpuuzi huyo
 
huyu ruben ngowi alikuwa diwani wetu,alivyofukuzwa uananchama alikosa sapoti ya marafiki akabaki mpweke,sisi hatuna diwani,hatuna mwenyekiti wa mtaa.hatuna mbunge.
 
waache wapambane na sijui mara haukufikiwa maamuzi
maana ya arusha ni mengi yanafanywa kiholela hata uuzwaji wa uwanja wa wazi ulio Kilombero pale ulifanywa bila maamuzi
Kila mtu Arusha hii anafanya kile ambacho anakiona cha maana au akishakuwa madarakani ana maamuzi yale ya kivyake na maamuzi ya pamoja ila mengi ni maamuzi ya mtu mmoja mmoja

Katika Manisipaaa nyingi hapa nchi Arusha inaongoza kwa wizi mkubwa na kuficha kichaka cha wala rushwa wengi kuna deals nyingi za ajabu sana pale.

Arusha City plan ni mbovu kupita maelezo ni kama vile kuna Mapapa au nyangumi wamekaaaaa tu na kujitizamia miradi yao inaendaje.

Hivinikiwaaambia maeneo ya matejeoo mbele ya ngarenaro ni bado kunadaiwa ni kijijini mtaamini? Au mfano mzurio tu huo ujenzi wa barabara unao endelea ulikuwa ni scandal WORLD BANK? mwanzoni mwa mwaka huu katika gazeti moja hapa nchini tena ilikuwa ni mwananchi waliandika World Bank yasitisha mikopo kwa manisipaa ya Arusha mjini kwa kile kuto kuona mahesabu ya pesa walizo pewa huko nyuma ndio watu kukurupuka na kuanza kujenga barabara, kweli mfano tu ile barabara ya njiro kwenda hadi kwa masister kule mwisho ilikuwa pia nayo ingojeee pesa za world Bank kweli Manisipaa ya Arusha ilikuwa inatutatania leo hii munayo yaona madudu pale ni kwaajili ya ulaji wa watu, Wakurugenzi wengi walisha hamishwa mkoa huo kwa ajili ya UFISADI. esp kwa ajili ya kile kiwanja cha Kilombero.

Cha kusikitisha sana Arusha ni kuna wafanyabiasha wajanja wajanja sana ambao wao walisha zoea kufanya biashara za kupiga deals tu hapa pale wakisikia mambo ya M4C wanaanza kuongea saaaaana huku wakija kwenye kodi wanakatwa sana na kuhonga wanahonga na deal wanapiga sasa siwaelewagi huwa wanataka kipi bora kwao?

Kuwa na uchahce wa mawazo kweli kuna changia sana kurudi nyuma kwa maendeleo ya nchi hii esp mkoa wa arusha mjini wakazi wake ndio wanachangia % kubwa mji huo kuto kukua, Hebu leo tizameni JIJI la mwanza kwa ukubwa sio kubwa kama Arusha lakini mji unatanuka kwa kasi sana na viwanja vinapimwa kila kukicha leo Arusha watu wanaenda nunua viwanja Gomba Estate ulizia njiro kwa msora kama utakuta viwanja vime pimwa? Nenda Mkorani Mwanza au nyegezi Buzuruga nyakato yaani utakuta kote viwanja vimepimwa, Kulikoni Arusha nini maisha ya deals mpaka leo,.

Tatizo lingine la Arusha ni tabia ya watu kuiga style moja ya biashara watu hawako creative na kwenda kwao kote Ulaya lakini wakija wote ni biasha ya nguo tuuuuu, wanabomoa nyumba za mjini kati wanaweka vibanda wakati huko nyuma tuliambiwa ukibomoa nyumba yako katikati ya mji ni upandishe Gorofa yako wapi sasa hebu pita mjini kuna renovation za kufa mtu na hakuna gorofa inapanda, Tizama mwanza inavyo panuka kwa kasi kubwa


 


na Grace Macha, Arusha


MADIWANI wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliotimuliwa kwa tuhuma za kukiuka taratibu za chama na kuingia muafaka wa kumaliza mgogoro wa umeya jijini Arusha wameuomba msamaha uongozi wa juu wa chama hicho.


Madiwani hao ni Ruben Ngowi wa Themi na Rehema Mohamed wa Viti Maalum ambao wameandika barua wakieleza namna walivyoamua baada ya kutafakari na kujiridhisha kwamba walikikosea chama chao.

Madiwani hao ni kati ya watano wa chama hicho waliotimuliwa mapema mwaka huu baada ya kukubali muafaka wa kumaliza mgogoro wa umeya na kugawana madaraka.


Madiwani wengine waliofukuzwa na kata zao kwenye mabano ni aliyekuwa Naibu Meya Estomih Mallah (Kimandolu), John Bayo (Elerai) na Charles Mpanda (Kaloleni).


Uamuzi wa madiwani hao umekuja baada ya juhudi za kumaliza suala lao kupitia vikao vya chama kushindikana hali iliyoilazimu Kamati Kuu ya chama hicho kuwafukuza.


Baada ya kufukuzwa madiwani wote hao walikimbilia mahakamani na kugonga mwamba pale Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Arusha kuitupa kesi yao kabla ya kufungua shauri jingine Mahakama Kuu ambalo hivi karibuni walilitoa mahakamani hapo.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima madiwani hao walikiri kuandika barua hizo ambapo Ngowi alisema haoni sababu ya kuendelea kulumbano na viongozi wa chama anachokipenda hivyo uamuzi wa kuomba radhi ni kutaka arudi kwenye chama.


Kwa upande wake Rehema hakutaka kueleza kwa kina sababu za kuomba radhi kwa madai kwamba yuko kwenye msiba.

“Kwa vile mimi nilijiunga na CHADEMA mwenyewe kwa ridhaa yangu na bila kushawishiwa na mtu ni mapenzi yangu mwenyewe ndiyo maana leo ninaomba radhi nirejeshewe uanachama wangu… sio kikundi.


“Ninaamini kila mmoja anaweza kuwa na makosa yake au upungufu wake hivyo baba Katibu Mkuu na viongozi wangu ninaomba msamaha na niko tayari kufuata yale yote mtakayonielekeza,” ilieleza sehemu ya barua iliyosainiwa na Rehema ambayo gazeti hili limefanikiwa kuiona nakala yake.

Katibu Mkuu wa CHADEMA Dk. Willibrod Slaa alikiri kupokea barua hizo na kusema mamlaka yenye uwezo wa kuwasamehe madiwani hao ni Kamati Kuu kwa vile ndiyo iliyowafutia uanachama wao.


 

Kweli kama Unakipenda CHAMA na Umefanya Makosa; Sio Mbaya kuomba Msamaha - Kosa ni kulirudia hilo kosa baada ya Kuomba

Msamaha... We R Human Beings We all Deserve a SECOND CHANCE!!!
 
Back
Top Bottom