Madhara ya kumuondoa Profesa Ndalichako Wizara ya Elimu yaanza kung'ata

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Elimu ni mojawapo ya wizara zilizoleta taharuki ya kuondolewa mawaziri wao kufuatia ladha za utendaji wao zilivyokuwa tamu kwa taifa (wananchi).

Wizara zingine ni Ardhi na Sheria & Katiba. Malalamiko ya ardhi yaliyokuwa yamepunguzwa sana na Mhe. Lukuvi sasa yameanza kurudi kwa kasi.

Prof. Kabudi aliboresha sekta ya Sheria na Idara ya Mahakama. Lakini pia alipokuwa Mambo ya Nje kwa kutumia uzalendo wake alitetea rasilimali za nchi zilizokamatwa ikiwa ni pamoja na kurejesha nyumbani wanafunzi wa Kitanzania walionasa nje ya JMT kwa lockdown ya Uviko-19 hasa China na India (wale wa vita ya Ukraine sijui wako wapi?).

Kiini cha wasilisho (post) hili ni elimu. Inawezekanaje mwanafunzi aliyehitimu kidato cha nne kwa ufaulu wa daraja la kwanza alama 8 (tena shule ya Junior Seminary) anapangiwa kwenda kusoma ualimu.

Binafsi sijasikia kama kuna mabadiliko ya sera wizara ya elimu yaliyoleta utaratibu huu mpya ambao hapo awali haukuwepo asilani.

Kama kuna mdau Mwalimu humu naomba taarifa ya kitaalam toka kwake kama mtaalam wa fani ya ualimu; ili nijuwe kama kuna mabadiliko ya sera chini ya Prof. Mkenda.


Watendaji wasio mahiri ndiyo walimponza Prof. Muhongo ambaye anajulikana kimataifa kwa umahiri wake, Dr. Kalemani alipopokea kijiti cha Prof. Muhongo ilibidi awe makini na watendaji na akawa na kasi kubwa ya kazi.

Mwl. Nyerere akihutubia katika hafla ya kubadili Chuo cha Itikadi Kivukoni kuwa taasisi ya kiserikali ya taaluma za jamii alisema kama atathibitika kufeli kwenye utawala wake basi wahusika ni watendaji aliowaweka na kama angeweza kurudi kutawala basi angepambana na watendaji zaidi kuliko watumishi wengine.
 
Yule mama ni vile tuu yale matokeo yaliyojirudia mwaka fulani yalimuangaza yeye na tv zote akapata jina. Ila hafai ata kua mjumbe wa nyumba kumi. Wizara ya elimu ilikua kubwa juu yake.
 
Kwakweli nimeshindwa kabisa kumalizia kusoma maana andiko lako limenisikitisha kwa kiwango kikubwa sana,,,,nikuulize kwanza unataka kweli mabadiliko katika elimu!?,,,,ok huo uwalimu ulitaka Nani akausomee!? Yaan kwa akili zako timamu kabisaa waliopata div 1 hawatakiwi kusoma uwalimu!? Anyway una umri gani kwanza maana naweza kuwa najibishana na mtoto ikawa sio kosa lako!!
 
Kwakweli nimeshindwa kabisa kumalizia kusoma maana andiko lako limenisikitisha kwa kiwango kikubwa sana,,,,nikuulize kwanza unataka kweli mabadiliko katika elimu!?,,,,ok huo uwalimu ulitaka Nani akausomee!? Yaan kwa akili zako timamu kabisaa waliopata div 1 hawatakiwi kusoma uwalimu!? Anyway una umri gani kwanza maana naweza kuwa najibishana na mtoto ikawa sio kosa lako!!
Tupe sera (nukuu utuwekee hapa tujiridhishe) inayosema kwamba Division One 8 points anaenda kusomea ualimu. Mtoto wa waziri aliyepata ufaulu huo anaweza kwenda kusoma ualimu? Mtoto wako je?

Nadhani tukiachana na siasa, ushabiki na hisia tutatenda haki na tutapata majibu stahiki.
 
Tupe sera (nukuu utuwekee hapa tujiridhishe) inayosema kwamba Division One 8 points anaenda kusomea ualimu. Mtoto wa waziri aliyepata ufaulu huo anaweza kwenda kusoma ualimu? Mtoto wako je?

Nadhani tukiachana na siasa, ushabiki na hisia tutatenda haki na tutapata majibu stahiki.
una shida kichwani sio siri...
 
nazani ingekuwa vyema turejeshe system ya UPE hawa waka somee ualimu...

nakumbuka juzi kuna Prof alikuwa ana zungumza katika kongamano la walimu dodoma, alisema ana shangaa kuona walio feli hesabu ndio wana enda kuwa walimu wa hesabu... walio feli kemia, fizikia nao hivyo hivyo... alafu una taka matokeo makubwa ktk elimu...

nae mtoa mada nae ni wale wale... hujafungwa kamba nenda kamsomeshe mwanao anachopenda iwe urubani hata udaktari, hacha kupiga kelele za kijinga... peleka mwanao unapo hisi anafiti kwa mustakhabari wa maisha yake

hakuna mbunge au mwanasiasa atakupelekea mwanao shule kama IST, FEZA etc hivyo ni jukumu lako mwenyewe. sasa kama wewe ndio mzazi unalialia, au unashindwa kufikiria na kuchukua hatua kutoka ktk tatizo ulilo nalo, utabaki kuwa kichekesho...
 
Prof Kabudi "alitetea raslimali za nchì zilipokamatwa"...Huna ujualo.
Rais Cyril Ramaphosa alitoka hapa nchini kwetu, baada ya kumaliza ziara yake halafu tena hapo hapo baada ya siku kadhaa tu eti Ndege yetu ikashikiliwa SA. Mimi nikashangaa kwamba ndege yetu ishikiliwe Afrika, tena SA? Under normal circumstances, it's practically impossible kwa ndege ya Tanzania kushikiliwa SA
 
👆 duh!

Bora wewe umetumia jicho la ziada na umakini, nahisi wewe ni mtaalam wa elimu.
Yani Mkuu,Ndalichako anafaa asiwe Waziri Tena,tayari ameshalitumikia Taifa hili Miaka mingi Sana yule mama,apumzishwe tu
Huyu kijana hoja yake ya kutaka Ndalichako abaki hapo W ya Elimu huenda ndio kile Nyerere alisema alikuwa anasukumwa abaki kuwa Rais na watu waliofaidika na yeye kuwa Rais
 
Back
Top Bottom