Madereva wa mikoani wasitisha mgomo wao!

Hapa ni kuzungushana tu; bado hatujafikia mahali pa litigations zinazowahusu wamiliki. Tumekuwa tukiwaadhibu madereva na watu wengine wa pembeni lakini hatujaanza kuwapa criminal hata civil liabilities kwa wamiliki.

a. Ni nani ana jukumu la kuajiri dereva mwenye uwezo, uzoefu na ujuzi wa kuendesha mabasi? Je, tunajua kama huyo dereva alikuwa ni competent? Je kuna standard yoyote ya uzoefu wa mabasi kabla mtu hajaajiriwa?

b. Basi likiwa bovu nani anajukumu la kusimamia matengenezo yake? Ni dereva au mmiliki? Je kuna utaratibu gani wa madereva kutoa taarifa za mabasi yao mabovu na haki yao ya kukataa kuendesha magari mabovu hadi yatengenezwe? Je akilazimishwa na mmiliki kuendelea na safari baada ya kutoa taarifa na ajali ikatokea na yeye akaonesha uthibitisho kuwa alitoa onyo hilo kwanini mmiliki naye asihusishwe?

Ninaamini njia mojawapo ya kuleta uangalifu na kupunguza ajali ni kuhakikisha kuwa wamiliki wa vyonmbo vya usafiri nao kwa namna moja wanabeba mzigo mkubwa wa lawama. Kwa mfano mwenye mabasi ya Mohammed Trans angelimwa faini ambayo ingemsababisha afilisike lingekuwa funzo kwa wenye mabasi kufikiria wao kama wamiliki wafanye nini wasijikute kwenye hali hiyo.

Kwa mtindo wa sasa tunajaribu kutibu dalili tu za tatizo ili kutuliza hisia zetu japo si akili zetu.

This fall under "Does SUMATRA have SAFETY MANAGEMENT SYSTEM? Does SUMATRA Act require any transporter or bus company to have such system?
 
Nadhani unafahamu kama hawa madereva wanakatazwa kuendesha gari kwa mwendo wa kasi!
Angalia nchi za nje,wao wanapangiwa kabisa speed wanayotakiwa waende kwa saa,na atakayekiuka kufanya hivyo adhabu kali hutolewa dhidi yake,na hiyo husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali kwenye nchi zao.
Tanzania isipochukua hatua mnalalamika,sasa mtu kachukuliwa hatua tena mnaanza tena kulalamika!!!Mtu gani wewe usiyekuwa na uelewa na kukubaliana na hali iliyotokea?!
Think twice before you say!
Mafisadi kama wameshindwa kufuatiliwa hiyo ni issue nyingine,here we are talking about madereva waliogoma..!

Wa MMOJA:

Nchi za nje madereva wazembe huwa hawafungwi miaka 10 au 30 na kwa kweli hakuna adhabu kali dhidi yao! watu huwa wanapewa pointi kwenye leseni na kufungiwa kuendesha kama miaka miwili au zaidi. Vifungo vya jela huwa miaka miwili hivi (inategemea na kosa pia).

Tatizo sisi hatuna bararara nzuri, mabasi/malori mengi hayakaguliwi kuangalia hali zake na pia mabasi kuendeshwa na utingo/makondakta amabao hawana ujuzi au wana leseni feki. Bila kusahau mishahara midogo ya trafiki polisi wetu ambayo inawafanya wajali tu maslahi yao!!
 
Last edited:
attachment.php


attachment.php


Kituo cha mabasi Ubungo kilivyo kuwa kinaonekana leo asubuhi.
 
Yah,it is nice kwa wao kugoma. Kwani hao wenyewe tu ndio wanasababisha ajali? je chenge atahukumiwa miaka mingapi?
 
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana. Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?

Madereva wanagoma kwani wengi wanatabia ya kuendesha kwa kasi na kutozingatia sheria za barabarani, wanaogopa wasikumbwe na mkasa wa mvua ya miaka. Mini naendeshaga mwenyewe kutoka Dar hadi Moshi. Lakini huko njiani kuna ukiukwaji sana wa sheria za barabarani. Utakuta mtu ana overtake kwenye kona, pasiporuhusiwa, wanapaki ovyo hasa malori, speed kali sana, penye speed 50km/h anaendesha mia

Mimi nadhani adhabu hii itakua fundisho kwa madereva wazembe na ninaiomba mahakama zetu hapa nchini zisicheleweshe kesi za namna hii. Mtu akiua halaiki ya watu namna hii haina tofauti sana na wanaojitolea mhana uko mashariki ya kati au mauajia ya jimbari, Darful n.k

Ungekua wewe ni mfiwa mmojawapo usingemtetea dereva hata kidogo. Umesababisha ajali kwa speed kali na kutofuata sheria za usalama barabarani then sheria ichukue mkondo wake.

Ila mimi nashangaa kwa nini mmiliki wa basi lile hajatiwa hatiani kwa makosa ya watendaji wake. Kifungu ni Skendo la Richmond amabapo Luwasa aliwajibishwa kutokana na Utendaji mbovu wa watendaji wake. Pia Mwinyi alijiuzuli akiwa waziri wa mambo ya ndani kutokana na utendaji wa askari wake.

Nawasilisha hoja
Just IMAGINE kwa speed ya 80km/hr unaenda Mbeya utafika saa ngapi?
Cha muhimu ni uzima/ubora wa matairi pamoja na gari na hapo sijaongelea ubovu wa mahandaki yetu wenyewe mwayaita mabarabara
 
Hizi sheria zetu za matabaka mawili nazo zinaudhi sana. Sheria za Vingunge na sheria za Makapuku. Huyo huyo Chenge anahusika pia kujipatia pesa kifisadi katika ununuzi wa rada lakini hadi leo hata kuchunguzwa na vyombo husika vya dola hakuna! bado anapeta tu uraiani bila hata kuguswa labda vile alivyonyunyiza ndani ya Bunge ndiyo vinafanya kazi yake.

Ungeulizwa yule dereva afungwe muda gani kwa kugonga na kuuwa? jibu lingekuwa MIAKA CHENGE??
 
Kwa barabara za Tanzania haziruhusu basi liendeshwe zaidi ya km 80 kwa saa. Ukifanya hivyo uko kwenye risk kwa sababu ya ufinyu wa barabara zenyewe, lakini mabasi mengi yanakwenda zaidi ya 100km/hr which more risky.

Wakuu ninaomba mnielimieshe, miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na suala la "spidi gavana" ambapo kila mmiliki wa basi alitakiwa kuweka ili kupunguza ajalli za barabarani. Hivi ziliishia wapi?
 
Hivi mtu akitaka kuwa dereva wa basi au lori la mizigo anatakiwa kuwa na ujuzi gani, ameupata wapi na unapimwaje ukiondoa kuwa na leseni. Yaani, ni sifa gani dereva wa basi anatakiwa kuwa nazo na ni nani anajukumu la kupima sifa hizo?
 
Hapa ni kuzungushana tu; bado hatujafikia mahali pa litigations zinazowahusu wamiliki. Tumekuwa tukiwaadhibu madereva na watu wengine wa pembeni lakini hatujaanza kuwapa criminal hata civil liabilities kwa wamiliki.

a. Ni nani ana jukumu la kuajiri dereva mwenye uwezo, uzoefu na ujuzi wa kuendesha mabasi? Je, tunajua kama huyo dereva alikuwa ni competent? Je kuna standard yoyote ya uzoefu wa mabasi kabla mtu hajaajiriwa?

b. Basi likiwa bovu nani anajukumu la kusimamia matengenezo yake? Ni dereva au mmiliki? Je kuna utaratibu gani wa madereva kutoa taarifa za mabasi yao mabovu na haki yao ya kukataa kuendesha magari mabovu hadi yatengenezwe? Je akilazimishwa na mmiliki kuendelea na safari baada ya kutoa taarifa na ajali ikatokea na yeye akaonesha uthibitisho kuwa alitoa onyo hilo kwanini mmiliki naye asihusishwe?

Ninaamini njia mojawapo ya kuleta uangalifu na kupunguza ajali ni kuhakikisha kuwa wamiliki wa vyonmbo vya usafiri nao kwa namna moja wanabeba mzigo mkubwa wa lawama. Kwa mfano mwenye mabasi ya Mohammed Trans angelimwa faini ambayo ingemsababisha afilisike lingekuwa funzo kwa wenye mabasi kufikiria wao kama wamiliki wafanye nini wasijikute kwenye hali hiyo.

Kwa mtindo wa sasa tunajaribu kutibu dalili tu za tatizo ili kutuliza hisia zetu japo si akili zetu.
Mwanakijiji,
Halafu umeacha kitu kikubwa zaidi, watu wanaojeruhiwa na kufariki/kufa, na ndugu vile vile hawana mwamko. I questioned a lot of such people who had such problems; wengi baada ya kujeruhiwa au kufa ndugu zao au watu wengine hawajawahi hata kudai insurance kwa ulemavu wao au kufa kwa ndugu zao. Insurance ingekuwa ni pigo mojawapo kwa mwenye gari na kampuni za insurance kuwa makini katika kuangalia usalama wa passengers. Inatia aibu kweli, watu wengi wanapuuza insurance kwa ulemavu wao na matibabu yao hata vifo vya ndugu zao.
 
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana. Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?

Madereva wanagoma kwani wengi wanatabia ya kuendesha kwa kasi na kutozingatia sheria za barabarani, wanaogopa wasikumbwe na mkasa wa mvua ya miaka. Mini naendeshaga mwenyewe kutoka Dar hadi Moshi. Lakini huko njiani kuna ukiukwaji sana wa sheria za barabarani. Utakuta mtu ana overtake kwenye kona, pasiporuhusiwa, wanapaki ovyo hasa malori, speed kali sana, penye speed 50km/h anaendesha mia

Mimi nadhani adhabu hii itakua fundisho kwa madereva wazembe na ninaiomba mahakama zetu hapa nchini zisicheleweshe kesi za namna hii. Mtu akiua halaiki ya watu namna hii haina tofauti sana na wanaojitolea mhana uko mashariki ya kati au mauajia ya jimbari, Darful n.k

Ungekua wewe ni mfiwa mmojawapo usingemtetea dereva hata kidogo. Umesababisha ajali kwa speed kali na kutofuata sheria za usalama barabarani then sheria ichukue mkondo wake.

Ila mimi nashangaa kwa nini mmiliki wa basi lile hajatiwa hatiani kwa makosa ya watendaji wake. Kifungu ni Skendo la Richmond amabapo Luwasa aliwajibishwa kutokana na Utendaji mbovu wa watendaji wake. Pia Mwinyi alijiuzuli akiwa waziri wa mambo ya ndani kutokana na utendaji wa askari wake.

Nawasilisha hoja

Sikubaliani na hoja yako, kwa sababu imeelemea kwenye ujumla kuliko kuangalia kosa kwa kosa.

Hilo Tairi la mbele linalopasuka ukiwa 80KM/hr kisha usipate msukosuko linapasukia wapi?
Pale Wami ?Kitonga,Katika kona fulani, au kwenye mteremko?

Hata baiskeli ikipasuka tairi lake liwe la nyuma au mbele unapata kashkash.

Mtu akifungwa miaka 30 ndo matairi yataacha kupasuka??
 
kinachochea ajali ni tabia za abiria na sio madereva

kabla ya kuwakomalia madereva inabidi tuanze na tabia za abiria
1.kama umeshawahi kwenda mikoani na kufika stendi abiria wanapenda basi linalokimbia na kufika haraka kule wanakokwenda.
2.hata ukiwa kwenye basi, mkiwa mnali overtake gari linalokwenda sehemu moja na nyie abiria wanafurahi kwa ajili wanaona wao wamechagua basi zuri.
3.siku zote mabasi yanayokimbia ndiyo ticket zake zinauzwa haraka.
4. kwa ajili wasafiri wanajirudia, mteja akipanda basi linalochelewa kufika safari ya kurudi halipandi tena lile basi atatafuta linalokimbia zaidi.
5. kama tabia ya abiria haita badilika basi mabasi yatakuwa yanakimbia siku zote.
kwa kifupi speed ya basi = wingi wa abiria
 
Mtu akifungwa miaka 30 ndo matairi yataacha kupasuka??

Hili swali ukiliangalia kwa haraka haraka ni rahisi kweli; ukilisogelea kwa karibu na kuweka chini ya mwangaza wa darubini kali utaona kuwa limejaa kila aina ya falsafa ya kuwajibika, ufahamu wa tatizo na mapendekezo ya kutatua matatizo hayo. Ni swali la wiki kwa kweli.
 
Wakuu ninaomba mnielimieshe, miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na suala la "spidi gavana" ambapo kila mmiliki wa basi alitakiwa kuweka ili kupunguza ajalli za barabarani. Hivi ziliishia wapi?

Speed governor/limiters zilikuwa ni mradi wa wakubwa fulani. Halafu ziligundulika kutokuwa effective kwa sababu zilikuwa zina legezwa garage na hivyo basi kwenda mwendo mdundo.
 
Hivi mtu akitaka kuwa dereva wa basi au lori la mizigo anatakiwa kuwa na ujuzi gani, ameupata wapi na unapimwaje ukiondoa kuwa na leseni. Yaani, ni sifa gani dereva wa basi anatakiwa kuwa nazo na ni nani anajukumu la kupima sifa hizo?

Kwa taratibu zilizopo kwanza, dereva wa basi ni lazima awe na umri kuanzia miaka 40 na kuendelea.

Pili, lazima awe na lesseni class C na uzoefu wa kuendesha magari yenye uwezo zaidi ya tani 7 kwa muda usiopungua miaka 5.

Tatu, lazima awe na cheti cha kuendesha magari makubwa kutoka VETA Dar es Salaam au National Institute of Transport (NIT) Dar es salaam.

Kinacho leta shida ni kwamba unaweza kuta mtu hana hata uzoefu lakini anachukua shs. 200,000 na anapata leseni kutoka traffic na inakuwa back-dated ili aonekane ana experiece, na hili ndo linatumaliza.

Cha mwisho ni magari mabovu.
 
Kwa taratibu zilizopo kwanza, dereva wa basi ni lazima awe na umri kuanzia miaka 40 na kuendelea.

Pili, lazima awe na lesseni class C na uzoefu wa kuendesha magari yenye uwezo zaidi ya tani 7 kwa muda usiopungua miaka 5.

Tatu, lazima awe na cheti cha kuendesha magari makubwa kutoka VETA Dar es Salaam au National Institute of Transport (NIT) Dar es salaam.

Kinacho leta shida ni kwamba unaweza kuta mtu hana hata uzoefu lakini anachukua shs. 200,000 na anapata leseni kutoka traffic na inakuwa back-dated ili aonekane ana experiece, na hili ndo linatumaliza.

Cha mwisho ni magari mabovu.

asante sana; jukumu la wamiliki ni nini katika kuhakikisha madereva wao wanatimiza matakwa hayo, na ni nini jukumu lao basi linaporipotiwa kuwa ni bovu na bado linapangiwa safari?
 
asante sana; jukumu la wamiliki ni nini katika kuhakikisha madereva wao wanatimiza matakwa hayo, na ni nini jukumu lao basi linaporipotiwa kuwa ni bovu na bado linapangiwa safari?

Kusema kweli kwa jinsi mimi navyoona na ukiangalia makampuni ya mabasi kama Abood pale morogoro, kweli wameajiri mtu anayehusika na kutest hao madereva na pia wakati mwingine wanampangia safari labda kwenda Dar kutoka moro, ila anakwenda na dereva mwingine pembeni kumwangalia anavyolimudu gari na barabara kwa ujumla, yule dereva mzoefu akiridhika anapeleka ripoti ofisini na mchezo umekwisha.

Sasa Mzee Mwanakijiji fikiria, kama huyu dereva mya akimpa hongo huyu anaye mtahini itakuwaje?? mimi sina jibu hapo.

Kuhusu ubovu wa gari, ukweli ni kwamba kuna udhaifu wa wataalamu kutoka Traffic police lakini pia kutoka SUMATRA. Mara nyingi traffic wanaangalia vioo kama vimepasuka, matairi kama yameisha n.k. lakini braking system hazichekiwi, kama tairi siyo geuine, utajuaje?? Hapa ndipo inatakiwa iwepo sheria kwamba ikigundulika gari ilikuwa mbovu ndo chanzo cha ajali basi mmiliki naye aadhibiwe, hili tunawaachia SUMATRA.
 
ni matokeo ya kukurupuka kwa rais.
kwa nini hakutoa amri na chenge ahukukumiwe fasta?
THEN DEREVA ALIYEFUNGWA ALIKUWA DEREVA MSAIDIZI ALIYEKUWA ANAENDESHA ALIFIA PALEPALE
 
ni matokeo ya kukurupuka kwa rais.
kwa nini hakutoa amri na chenge ahukukumiwe fasta?
THEN DEREVA ALIYEFUNGWA ALIKUWA DEREVA MSAIDIZI ALIYEKUWA ANAENDESHA ALIFIA PALEPALE

kama kweli aliyefungwa alikuwa haendeshi wakati huo, inamaana yeye dereva mzoefu alikaa pembeni akampa gari asiye na uzoefu.
 
Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?
kwani madhara ya UFISADI ni nini?.....
 
Kwa hakika nakubaliana na jamaa aliyesema kuwa msaliti wa utanzania hawezi kulinda mali za Tanzania. madereva walikuwa na haki/au sababu zakugoma maana wahenga walisema "ukiona mwenzio ananyolewa basi na wewe tia maji" hivyo madereva wana kila sababu ya kugoma maana wakati wowote yanaweza kuwatokea kama yaliyomtokea dereva mwenzao. Lakini kwa kawaida sisi tunaotokea kuwa abiri mara kwa mara huwa tunapenda kuwahi kufika tunaopokuwa safarini isipokuwa zinapotokea ajali ndio huwa wa kwanza kuwatuhumu madereva. Watanzania Maskini tutanyanyasika nchini kwetu hapa mpaka mwisho.
 
Back
Top Bottom