Madereva wa mikoani wasitisha mgomo wao!

Labda zimezidi mno. Utaratibu unaofaa ufuatwe. Madereva waliogoma wamekosea. Si abiria waliomhukumu huyo dereva. Kama hujui uzito wa hilo waulize wafiwa na mayatima waliokatishiwa ustawi wa maisha yao na ajali ile tena miaka zaidi ya 30 ya hukumu aliyopewa huyo dereva. Kama wanaodai wanampenda wana haki ya kukata rufaa kwenye mahakama za juu. Mashahidi wapo watasema waliona nini katika ajali hiyo. Alistahili hukumu hiyo kwa mujibu wa mwenendo wa kesi katika mahakama ile.
 
you guys are funny bana!HAWAJAGOMA HATA KIDOGO.wanafanya mkutano kujadili ajali nyingi za mfululizo za barabarani!

-chanzo
-namna ya kudhibiti

Watu bana!mnatoa wapi uzushi ninyi?
DAMN IT!

Si kama wanafunzi wa mlimani wanapoacha kuingia madarsani na kuenda NKURUMAH HALL kuzungumzia masuala yao kama vile boom n.k...huwa sio mgomo ule?

omarilyas
 
Hivi ingekuwaje kama mabasi ya mikoani yangekuwa ya SIRIKALI,2ngeona adhabu za mtindo huu,au wao wana device iitwayo accident removal so that kusingekuwa na ajali,Mbona kimya kuhusu Chenge?
 
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana. Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?

Madereva wanagoma kwani wengi wanatabia ya kuendesha kwa kasi na kutozingatia sheria za barabarani, wanaogopa wasikumbwe na mkasa wa mvua ya miaka. Mini naendeshaga mwenyewe kutoka Dar hadi Moshi. Lakini huko njiani kuna ukiukwaji sana wa sheria za barabarani. Utakuta mtu ana overtake kwenye kona, pasiporuhusiwa, wanapaki ovyo hasa malori, speed kali sana, penye speed 50km/h anaendesha mia

Mimi nadhani adhabu hii itakua fundisho kwa madereva wazembe na ninaiomba mahakama zetu hapa nchini zisicheleweshe kesi za namna hii. Mtu akiua halaiki ya watu namna hii haina tofauti sana na wanaojitolea mhana uko mashariki ya kati au mauajia ya jimbari, Darful n.k

Ungekua wewe ni mfiwa mmojawapo usingemtetea dereva hata kidogo. Umesababisha ajali kwa speed kali na kutofuata sheria za usalama barabarani then sheria ichukue mkondo wake.

Ila mimi nashangaa kwa nini mmiliki wa basi lile hajatiwa hatiani kwa makosa ya watendaji wake. Kifungu ni Skendo la Richmond amabapo Luwasa aliwajibishwa kutokana na Utendaji mbovu wa watendaji wake. Pia Mwinyi alijiuzuli akiwa waziri wa mambo ya ndani kutokana na utendaji wa askari wake.

Nawasilisha hoja

Napinga hoja yako. Umejenga maamuzi kutokana na assumptions ambazo huna uhakika nazo. Toa data. Sioni kwa nini mmiliki wa basi ahusishwe kwa makosa ya dereva wake. Mfano wako wa Lowassa wala hauleti maana yeyote.

Kwanza naona nchi hii kuna sheria ya uzembe kwa kazi za ngazi ya chini na ngazi za juu. Daktari akifanya uzembe ukasababisha kifo, utaona anashtakiwa tume/bodi ya madaktari, mara anasimamishwa kwa miezi kadhaa halafu baadaye anarudi kazini. Angalia kesi ya daktari yule wa Arusha aliyesababisha mja mzito afariki pamoja na mtoto wake. Vile vile ile kesi ya Muhimbili ya mgonjwa kufanyiwa operation ya kichwa badala ya mguu, and vice versa imeishia wapi. Kesi ya Chenge aliyesababisha ajali na kuua nayo ipo wapi? Mlinzi mzee anayetakiwa alinde kila siku, akilala lindoni halafu akaibiwa atashtakiwa kwa kosa la uzembe kazini na kuambulia mvua kadhaa jela.

Kifupi ni kwamba kwangu mimi naona hii adhabu ni excessive na ni imechukulia zaidi comments za wanasiasa kuliko hali halisi. Uzembe unaosababisha kifo uwe uzembe tu na hatua muhimu zichukuliwe bila kujali position ya mtu. Unapokuwa na seti mbili za sheria, kwa wanyonge na kwa wenye position, ntegemea vitu kama hivi kutokea kwani kunakuwa na hisia ya uonevu.

Naunga mkono madereva.
 
Naona makomredi waliosomea China wameona tufuate hata mfumo wao wa adhabu labda tutaheshimiana baada ya muda sio mrefu....yaani kuwe na mfululizo wa adhabu za kufa mtu;
-Aliyebaka: miaka 30
-Jambazi: miaka 30
-Aliyebaka mtoto mdogo: kifungo cha maisha (Nguza & sons)
-Dereva akisababisha ajali akaua: miaka 30 (Chenge nae yumo tunasubiria)
-Wanaoingiza madawa na vyakula feki: adhabu yao bado inatathminiwa (labda tutanyonga kama China)
-Mafisadi: adhabu yao bado inatathminiwa (labda nao tutanyonga kama China)
-Wauza madawa ya kulevya: Faini (nimesikia leo kwenye magazeti jamaa kapigwa faini ya milioni kumi baada ya kukiri kosa)...huyu ndio ilitakiwa anyongwe kabisa lakini kwa sababu ni biashara za vigogo wanapeana adhabu za kishkaji

Tatizo bongo mambo hayaeleweki-eleweki.....tatizo dogo adhabu kubwa.......tatizo kubwa adhabu ndogo!
 
Wakuu huyo dereva ni wa basi la Mhd trans wa hii ajali ya juzi juzi au ? kama ndivyo hukumu ina matatizo yahitaji uchunguzi huru wa mwenendo wa hiyo kesi,nijuavyo mimi kesi hizo upelelezi wake huchukua muda si chini ya miezi sita,iweje kwa muda mfupi hivi upelelezi umekamilika na dereva kahukumiwa.Ni kweli ajali zimezidi na kwa kiwango kikubwa kunakuwa na uzembe iwe ni kwa dereva au mmiliki. Kwa basi kupasuka tyre inaniwia vigumu kumhusisha derva na uzembe,labda uchunguzi wa kina ungefanyika kujua nani hasa mhusika wa uzembe huo,yaweza kuwa ni uzembe wa mamlaka zinazodhibiti uingizaji wa matairi ya magari nchini kuruhusu tairi za kiwango cha chini kuingizwa na kutumiwa kwenye mabasi ya abiria, lakini pia mmiliki wa gari anaweza kuwa ni mzembe kama ameacha tairi iendelee kutumika wakati muda wake au kilomita za matumizi yake zimekwisha (Matairi mengi ya sikuhizi yana kiwango cha kilomita ambacho kikitimia yabidi libadirishwe hata kama laonekana bado zima)
utetezi mwingine hauna maana....watu wote huwa wanaomba kesi zao ziende haraka, wewe unashangaa kwa nini wamefanya upelelezi haraka...!unajua mwaka huu pekee watu wangapi wamekufa kwa ajali za kizembe barabarani?mimi ni dereva,naendesha gari sana kwawastani wa km 150 hadi 200 kwa siku,hawa madereva wa malori na mabasi ni wa...nzi kweli kweli madereva watakubaliana na mimi...speed siku zote ndo zinaua sio kupasuka matairi...ukuwa speed 80km/h hutapindukapinduka tairi likipasuka....na hiyo ndo maximum allowable speed na unaruhusiwa sehemu iliyonyooka unaona mpaka mbali sana...sasa wao wanaovertake speed 120 kwenye kona.....
wakule mvua,na ningekuwa mmiliki wa mabasi ningeajiri wengine waadilifu na kuachana na hawa wanaogomea upuuzi
 
Nimesikitika sana na hiyo adhabu kwa dereva. Clearly something is wrong. Hata na hivyo mgomo wa madereva ni kiashiria tu cha hasira zao juu ya HAKI ambavyo haitendeki kwenye hii nchi. Mgono ndo the only way to talk to the gvt kama hii ya tanzania. Mnasema rufaaa? rufaa kitu gani watu si wale wale!!!
 
Hii kesi ni hii ya juzi au ni zile za awali?? Maana mtakumbuka Mohamed Trans walishasababisha ajali nyingine mbaya sana. Hapa mabasi yote ya Mohamed Trans yanakimbia sana, sijui tajiri pengine anawapa motisha kwa dereva anayekimbia na kuwahi!!! Wapo matajiri ambao wanafanya hivyo!!!

Kwa upande mwingine, kuondoa roho ya mtu haiwezi kulinganishwa na ufisadi hata kidogo. Imagine unakufa, mke au mume, mtoto, au ndugu wako wa damu!! ukiweza kuwaza hili utaona kuwa ni vema madereva wanaosababisha ajali kwa uzembe wafungwe not less than 30 years au maisha kabisa maana wamekusudia kuua kupitia tamaa na bangi zao.

Kwa wale ambao wanasababisha ajali za kawaida kwa uzembe, kuna tamko limetolewa kuwa watanyang'anywa leseni zao. Naona hii haitoshi, wapewe na kifungo badala ya faini ndogo ya sh. 20,000 halafu mwenye gari unaanza kupata joto la usumbufu na issurance companies. Ni lazima tufike mahali tukubali kufanya maamuzi ya kurekebisha tabia na kupunguza makosa katika jamii. Na serikali hapa ni lazima wawe na msimamo, hakuna kubadilisha hukumu hiyo katika appeal. Tena aongezewe viboko.
 
Safi sana madereva komaaeni mpaka wananchi wajue serikali yetu imeoza.
Sheria zinapindishwa pindishwa wanyonge tunachinjiwa mbali safi sana gomeni hata wiki nzima abiria nao washike adabu ili uchaguzi ujao wafanye right choise kwenye kura.
 
Hali ilivyo mpaka sasa
 

Attachments

  • DSC01930 small.JPG
    DSC01930 small.JPG
    36.2 KB · Views: 55
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana. Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?

Mkombozi sijakusoma. Hivi unadata za akina mama wangapi Tanzania katika saa moja wanakufa kwa kukosa huduma za matibabu wakati wa kujifungua? I suspect huna otherwise usingetofautisha vifo vya ajali na vifo vinavyosababishwa na ufisadi. Mafisadi na huyo dereva hawana tofauti unless mtu ameamua kwa makusudi kuupa likizo ubongo wake.
 
Mimi nadhani ukiwa katika speed ya kawaida 80Km/h tairi za mbele zikipasuka hakutakua na athari kubwa sana.

Mkuu sidhani kama unafahamu kwa uzuri ukubwa wa huo mwendo kasi ulioutaja. Fizikia ya ngazi ya sekondari inafundisha kitu kinachoitwa "momentum" ambacho kinatokana na kuzidisha uzito wa chombo na mwendo kasi wake. Katika ajali moja ya vitu vikubwa katika collision assessment ni hii momentum.

Kingine pia, usiunderestimate umuhimu wa matairi yako ya mbele. Haya nidyo yanayoongoza chongo cha usafiri. Kupasuka kwa tairi la mbele athari zake ni kubwa labda chombo cha usafiri kiwe kinakwenda 40 km/h au chini yake.

Binafsi nimeshapata front tyre burst miaka miwili iliyopita nikiwa chini ya 65 km/h na matokeo yake ni kwamba unapoteza steering geometry yote, gari linaangukia upande wa burst kwa mbele na kukuvuta upande huo. Heri yangu mimi nilikuwa katika barabara ya lami tambarare, kulikuwa hakuna magari, wanyama wala watumiaji wengine wa barabara, gari lilikuwa linaendeshwa na mzoefu wa miaka zaidi ya 30 barabarani na pia labda haikuwa siku yetu kufa. The stopping distance ilikuwa more than 100 metres na gari lilihama kutoka barabarani na kuvamia mashamba ya watu upande mwingine kabisa wa barabara.


Ila huyu jamaa inavyosadikika alikua kwenye speed kubwa sana. Pia hatuwezi kulinganisha kesi ya ufisadi na utoaji wa roho za watu, uizi na ubadilifu wa mali ya uma ni ufisadi ambapo vyote vinaweza kutafutwa ila roho ya mtu ikishapotea utaitafuta wapi?

Inaweza ikawa alikuwa katika mwendo mkubwa zaidi, inaweza ikawa alipatwa na mshtuko na kurreact irrationally, inaweza ikawa baada ya burst gari lilimshinda nguvu inaweza pia ikawa ilikuwa tu ni siku yake kupatwa na masahibu hayo. Kuhusu kulinganisha na mambo ya ufisadi, ndugu revisit ile concept ya "cost of alternatives forgone".


Ungekua wewe ni mfiwa mmojawapo usingemtetea dereva hata kidogo. Umesababisha ajali kwa speed kali na kutofuata sheria za usalama barabarani then sheria ichukue mkondo wake.

Mkuu inaelekea na wewe pia tayari umeshatoa hukumu ya kwamba chanzo cha ajali ilikuwa ni mwendo kasi na sio hitilafu za tairi.

Ila mimi nashangaa kwa nini mmiliki wa basi lile hajatiwa hatiani kwa makosa ya watendaji wake.

Ikithibitika ya kwamba zilikuwa ni hitilafu za tairi je hauni kama hiyo chain ya watuhumiwa inaweza kuwa ndefu sana na kuhusisha wauzaji wa matairi pamoja na watengenezaji?

hawa madereva wa malori na mabasi ni wa...nzi kweli kweli madereva watakubaliana na mimi...speed siku zote ndo zinaua sio kupasuka matairi...ukuwa speed 80km/h hutapindukapinduka tairi likipasuka....

Siafikiani na wewe. Mechanical defaults play a HUGE part in accidents.

na hiyo ndo maximum allowable speed na unaruhusiwa sehemu iliyonyooka unaona mpaka mbali sana...sasa wao wanaovertake speed 120 kwenye kona.....
wakule mvua,na ningekuwa mmiliki wa mabasi ningeajiri wengine waadilifu na kuachana na hawa wanaogomea upuuzi

Maximum speed ya haya mabasi mapya ni 120 kph. You work out the possibilities za kuovertake kwenye kona katika spidi hiyo.
 
Naomba hapa JF kuwe na mjadala huru ili tujue nini maana ya over speeding,naamini gari imeundwa kwa kuzingatia tafiti mabalimbali muhimu ili kuhakikisha zinaundwa na kuwekewa kiwango cha mwendo kasi ambacho hakitakiwi kusababisha ajari kama mazingira tarajiwa ya gari yatakuwepo,si kweli kwamba basi likiendeshwa kwa speed ya 120km/hr litapata ajali,ajali yaweza kutokea hata kama unaendesha kwa speed 60kms/hrs,lilio la muhimu inabidi tuangalie mazingira ya ajari kwa ukumla wake tukianzia na barabara na alama husika,ubora wa magari yenyewe na uwezo wa madereva.
Uzembe ni chanzo kikubwa cha ajali,wala kuendesha kwa speed kubwa hakuna uhusiano na uzembe,ni muhimu basi ajali inapotokea tuchunguze ni aina gani ya uzembe uliosabaisha ajali badala ya kukimbilia kuhukumu speed ya dereva. Huwezi ukaendesha gari Dar-Songea kwa 80kms/hr.labda kama abiria watakuwa na mkataba wa kudumu nawe,safari ni ndefu sana inafupishwa na speed inayotumiwa na madereva ambayo ndcho kivutio kwa abiria walio wengi.
Umakini wa madereva,wamiliki na mamlaka zinazohusika na miundo mbinu utaopunguza au kuoandoa ajali na si speed ya magari,speed itapunguza maafa lakini si kuondoa ajali


Kwa barabara za Tanzania haziruhusu basi liendeshwe zaidi ya km 80 kwa saa. Ukifanya hivyo uko kwenye risk kwa sababu ya ufinyu wa barabara zenyewe, lakini mabasi mengi yanakwenda zaidi ya 100km/hr which more risky.
 
Jambo la kushangaza zaidi ni pale vyombo vya usalama vilipotumwa kwenda kuangalia mgomo. Kulikuwa na gari mbili za nyuki na moja la upupu tazama picha hii.
 

Attachments

  • FFU.JPG
    FFU.JPG
    31.3 KB · Views: 58
Kwanza kama ingethibitika kwamba alikuwa ana overtake kwenye kona basi alistahili kifungo cha maisha
 
Tumesiokia mabasi yaendayo mikoani MADEREVA WAMEGOMA, kisa mwezao kafungwa miaka 30.Mh,Rais wa jamuhuri ya muungano ya Tanzania alitoa tamko MADEREVA WAZEMBE WAPEWE ADHABU KALI, WAKUTWAPO NA KOSA LA KUSABABISHA AJARI KWA UZEMBE. Je aliyefungwa miaka 30 kafanyauzembe au ajari haina kinga?
 
Mkuu sidhani kama unafahamu kwa uzuri ukubwa wa huo mwendo kasi ulioutaja. Fizikia ya ngazi ya sekondari inafundisha kitu kinachoitwa "momentum" ambacho kinatokana na kuzidisha uzito wa chombo na mwendo kasi wake. Katika ajali moja ya vitu vikubwa katika collision assessment ni hii momentum.

Kingine pia, usiunderestimate umuhimu wa matairi yako ya mbele. Haya nidyo yanayoongoza chongo cha usafiri. Kupasuka kwa tairi la mbele athari zake ni kubwa labda chombo cha usafiri kiwe kinakwenda 40 km/h au chini yake.

Binafsi nimeshapata front tyre burst miaka miwili iliyopita nikiwa chini ya 65 km/h na matokeo yake ni kwamba unapoteza steering geometry yote, gari linaangukia upande wa burst kwa mbele na kukuvuta upande huo. Heri yangu mimi nilikuwa katika barabara ya lami tambarare, kulikuwa hakuna magari, wanyama wala watumiaji wengine wa barabara, gari lilikuwa linaendeshwa na mzoefu wa miaka zaidi ya 30 barabarani na pia labda haikuwa siku yetu kufa. The stopping distance ilikuwa more than 100 metres na gari lilihama kutoka barabarani na kuvamia mashamba ya watu upande mwingine kabisa wa barabara.




Inaweza ikawa alikuwa katika mwendo mkubwa zaidi, inaweza ikawa alipatwa na mshtuko na kurreact irrationally, inaweza ikawa baada ya burst gari lilimshinda nguvu inaweza pia ikawa ilikuwa tu ni siku yake kupatwa na masahibu hayo. Kuhusu kulinganisha na mambo ya ufisadi, ndugu revisit ile concept ya "cost of alternatives forgone".




Mkuu inaelekea na wewe pia tayari umeshatoa hukumu ya kwamba chanzo cha ajali ilikuwa ni mwendo kasi na sio hitilafu za tairi.



Ikithibitika ya kwamba zilikuwa ni hitilafu za tairi je hauni kama hiyo chain ya watuhumiwa inaweza kuwa ndefu sana na kuhusisha wauzaji wa matairi pamoja na watengenezaji?



Siafikiani na wewe. Mechanical defaults play a HUGE part in accidents.



Maximum speed ya haya mabasi mapya ni 120 kph. You work out the possibilities za kuovertake kwenye kona katika spidi hiyo.

Hapana huyu ilikuwa ni unnecessary over speeding na ndo maana alipona. Wote ambao gari inamshinda huwa either anakufa au anajeruhiwa lakini huyu jamaa aliona kabisa kwamba kakosea ndo maana akaishia porini. Hicho kifungo ni halali yake ili wenzake wajifunze.
 
na hasa mabasi ya Mohamed trans yamezidi kwa speed kubwa, pamoja na bufalo. Mohamed trans anatoka mwanza saa 12 asubuhi na saa 2 usiku yupo DSM, hii ni hatari.
 
Back
Top Bottom