Madaktari hawakugoma ila wamebadili ofisi kutoka Muhimbili kwenda Agakhan,Kairuki,IMTU......

apolycaripto

JF-Expert Member
Feb 11, 2011
644
225
Huu mgomo kama unavyosemekana na undani wa madai yake "details" (haijajulikana kiasi gani wanataka) nadhani hautokwisha kirahisi. Nimezungukia Hospitali binafsi mbili hapa Jijini ama kweli kufa kufaana. Baadhi ya Madaktari wa Muhimbili wako huku wanapiga mzigo kama kawaida na fungu wanapata.Wangonjwa ni wengi na dau nahisi liko juu ama ni "peace of mind".

Tokea mgogoro huu uanze napata kizunguzungu hasa juu ya madai yao na kwanini Serikali imekuwa na kigugumizi. Kama alivyosema Pinda kuwa kwa anae anza kazi anadai alipwe 7,500,000 na wale nguri mpaka 17,000,000 du!.Hili mpaka sasa madaktari hawajakanusha hili binafsi naamini ni sehemu ya madai yao.

Kama ni hivi Serikali imeshikwa pabaya hapa bado polisi,walimu (wanadai isiwe chini ya 900,000 kwa graduate),na sekta binafsi ndio balaa tupu linakuja.

Kimsingi mgomo wa madaktari hautakwisha kama wanapo pa kushika na huko (private) kutokana na population ya wagonjwa kuongezeka bila shaka the law of marginal productivity ina apply (kwa maana ya pay as you earn).

Nashauri busara na uzalendo utumike kwa pande zote mbili katika kuokoa maisha ya sisi masikini (fast track inanyima haki kwa masikini). Binafsi niko skeptical na mgomo huu kwani hasara ni kwa sisi masikini .Tazama wenzetu wamesomeshwa kwa muda mwingi na kwa fedha zetu (100%), mioyo hii migumu wametoa wapi? je sisi wa 20% (kulipiwa na serikali inakuwaje)? .Ama ndio zile za bora punda afe (masikini) lakini mzigo ufike (maslahi).

Tumewapigia kelele Wabunge juu ya posho na hawa sasa inabidi tuwatizame kama wanachokidai in reality kinatekelezeka?. Kama kinatekelezeka basi Serikali iwajibike.
 
Kama Mbunge anapata kiasi hicho cha hela, tatizo liko wapi Madaktari wakilipwa kiasi kama hicho?

Uchaguzi ni rahisi tu, sielewi kwa nini wana take long kutoa ufumbuzi.

Acha niendelee kuisubiri Ijumaa kwa hamu, kuna kila dalili historia ikajitengeneza.
 
Mie naona kama siasa zinatawala hili suala au mahesabu yanasumbua watu hadi waziri wetu mkuu, hivi ni madaktari wote watakuwa call kila siku? ( mpaka awapigie mahesabu ya ten parcent kwa wote?), je ni madaktari wote watapewa hardship allowance? Kwa maana ya kuwa wataenda maeneo ambayo ni magumu kufanya kazi? Majibu hapo no hapana na hiyo tayari itaondoa asilimia hamsini ya hicho wanachokidai. Nina uhakika si chini ya madaktari hamsini wataenda mikoa itakayohitaji hardship allowsnce. Tusiwasaidie hawa viongozi wetu kupiga propaganda la tuwasaidie waelewe.
 
huu mgomo kama unavyosemekana na undani wa madai yake "details" (haijajulikana kiasi gani wanataka) nadhani hautokwisha kirahisi. Nimezungukia hospitali binafsi mbili hapa jijini ama kweli kufa kufaana. Baadhi ya madaktari wa muhimbili wako huku wanapiga mzigo kama kawaida na fungu wanapata.wangonjwa ni wengi na dau nahisi liko juu ama ni "peace of mind".

Tokea mgogoro huu uanze napata kizunguzungu hasa juu ya madai yao na kwanini serikali imekuwa na kigugumizi. Kama alivyosema pinda kuwa kwa anae anza kazi anadai alipwe 7,500,000 na wale nguri mpaka 17,000,000 du!.hili mpaka sasa madaktari hawajakanusha hili binafsi naamini ni sehemu ya madai yao.

Kama ni hivi serikali imeshikwa pabaya hapa bado polisi,walimu (wanadai isiwe chini ya 900,000 kwa graduate),na sekta binafsi ndio balaa tupu linakuja.

Kimsingi mgomo wa madaktari hautakwisha kama wanapo pa kushika na huko (private) kutokana na population ya wagonjwa kuongezeka bila shaka the law of marginal productivity ina apply (kwa maana ya pay as you earn).

Nashauri busara na uzalendo utumike kwa pande zote mbili katika kuokoa maisha ya sisi masikini (fast track inanyima haki kwa masikini). Binafsi niko skeptical na mgomo huu kwani hasara ni kwa sisi masikini .tazama wenzetu wamesomeshwa kwa muda mwingi na kwa fedha zetu (100%), mioyo hii migumu wametoa wapi? Je sisi wa 20% (kulipiwa na serikali inakuwaje)? .ama ndio zile za bora punda afe (masikini) lakini mzigo ufike (maslahi).

Tumewapigia kelele wabunge juu ya posho na hawa sasa inabidi tuwatizame kama wanachokidai in reality kinatekelezeka?. Kama kinatekelezeka basi serikali iwajibike.

tatizo bongo ni kila kuwa siasa.... Viongozi wakuu wanapotosha kuhusu madai a madaktari... Kiwango cha 7.5m hakiwahusu doctors wote... Eg...kumbuka si kila dr anatakiwa kulipwa call allowance, house allowance kwa kuwa wengine hawaitwi muda wa ziada wakati wengine wachache wamepewa nyumba... Hapa ni kupotosha ili wananchi wajue kuwa wanadai pesa nyingi.

Jaribu kujiuliza two qns:

1. Dr anaishi tegeta, amepigiwa simu kuja kazini kisha anatumia usafiri wake toka tegeta hadi muhimbili kisha analipwa 10,000/= alafu anaona mbunge anasaini 330,000/= kwa siku kwa kupiga meza au kulala kwenye kiti.... Hapa hakuna usawa hata kidogo. Cha msingi hapa ni keki kuigawa sawa. Dr aliyesoma 5yrs then 1 yr for intern kuomba 3.5m per month kwa serikali yetu ambayo mapato mengi yanapotea kwa ufisadi hili linawezekana kabisa tukiacha siasa.

2. Dactari anampokea dereva wa taasisi moja ya umma akiwa na green card ya bima ya afya (yenye kumuwezesha kupata huduma hata hospitali kubwa private hapa nchini)... Then yeye hapati hiyo card kisa mshahara mdogo kupata green card... Hapo ni fair?????? Wagome tu mpaka adabu ipatikane.



Nasupport mgomo ingawa tunapata mateso.
 
Mie naona kama siasa zinatawala hili suala au mahesabu yanasumbua watu hadi waziri wetu mkuu, hivi ni madaktari wote watakuwa call kila siku? ( mpaka awapigie mahesabu ya ten parcent kwa wote?), je ni madaktari wote watapewa hardship allowance? Kwa maana ya kuwa wataenda maeneo ambayo ni magumu kufanya kazi? Majibu hapo no hapana na hiyo tayari itaondoa asilimia hamsini ya hicho wanachokidai. Nina uhakika si chini ya madaktari hamsini wataenda mikoa itakayohitaji hardship allowsnce. Tusiwasaidie hawa viongozi wetu kupiga propaganda la tuwasaidie waelewe.
big up. Wewe kweli ni analyist. Umeanalyse balabala. Unajua wanasiasa wanapenda sana sympathy kutoka kwa wananchi wa kawaida kwa maana kwamba wanajua hawatakuwa na uwezo wa kutafiti na kupata data za kisayansi. Namuunga mkono aliyesema twende kindugai ndugai. Kufanyike upembuzi yakinifu idara zote siyo kuwalaumu walioona njia.
 
nadhani mleta mada ungjaribu kuchukua muda na kutafuta details za madai ya madaktari,upotoshaji unaofanya ndio umetufikisha wiki ya pili bila kutatua tatizo.punguza siasa,acha unafiki ......watu wanateseka sana.
 
Drs wamefunguka macho wakaona njia tunaomba watuongoze nasi tupite hiyohiyo mpaka tulikombowe taifa letu toka kwa hawa bongo lala
 
Back
Top Bottom