Coolhigh
JF-Expert Member
- Feb 5, 2011
- 1,338
- 1,221
Ndege zina iwezo wa kujirudisha nyuma kama ulivyoelezea, lakini watengeneza ndege hawashauri matumizi ya reverse thrusts kurudishia ndege nyuma kwa sababu ni hatari kwa usalama wa injini hasa hizi kubwa za jet zilizofungwa chini ya mabawa. Ni kawaida sana kwenye turbo props hasa ATRs kuona wakitumia kirudishia ndege nyuma na boeing C17 za kijeshi ambazo injini zake ziko juu kuliko kawaida.JE, NDEGE INARUDI NYUMA?
Ndege nyingi za sasa zina mfumo wa kurudi nyuma #reverse' ambao mara nyingi hutumika kupunguza kasi wakati ikitua (#Braking).
Kwa baadhi ya ndege za 'Mapangaboi' #Propeller hutumia panga zake kubadili umbile (#angle) hivyo badala ya kuvuta hewa kwenda nyuma inasukuma kuelekea mbele na kusababisha ndege kupunguza kasi yake pale inapotua.
Hali kadhalika na kwenye injini zenye mfumo wa #Jet huwa zinafungua injini katikati na kubadili uelekeo wa hewa inayosukumwa nyuma kuvuja na kulazimishwa kuelekea mbele.
Baadhi ya Injini za mfumo wa 'jet nyingine zinafungua vimilango vyake vidogo katikati au nyuma ya injini.
Ndege nyingi kubwa zina mifumo mitatu ya kupunguza mwendo #braking ikiwemo
1>#Reverse' ya Injini au #Reverse_Thrust
2>'Brake' za matairi na
3> #Ground_Spoilers au #Speedbrake' ambazo ni bapa zinazo nyanyuka juu ya mbawa.
Hivi vyote mara nyingi hufanya kazi kwa pamoja ili kupunguza kasi ya ndege inapotua ili kusimama haraka kwakuwa hutua na kasi kubwa sana.
Kasi ya kutua ndege kama #MD11 ikiwa imejaa mzigo hata Gari yako yenye speed 260km/h haifukuzi.
Brake zote za kukinzana na upepo {spoilers na reverse thrust} husaidia kutozipa mzigo mkubwa 'brake' za matairi ambazo huweza kupasua tairi, kuharibika, kuwaka moto au mda mwingine kuteleza kama barabara #Runway ikiwa imetuama maji endapo kama zitatumika pekee bila msaada wa #brake' nyengine.
Licha ya kukinzana na upepo juu ya mbawa, 'spoilers/speedbrake' pia husaidia kukandamiza ndege chini hivyo tairi kushika barabara vizuri wakati zinakamata 'brake kupunguza mwendo.
Sasa kwanini ndege haitumii 'Reverse' kujitoa kwenye Maegesho?
badala yake inasukumwa kurudi nyuma (#Pushback) na vigari maalumu #Tow_Truck/#Tug
1>Kuepuka kelele kali za 'reverse'
2>Kuepuka ulaji mafuta
3>Kuepuka hatari ya ndege kugongana na vitu vingine nyuma.
4>Kuepuka uharibifu wa injini kwa kunyonya taka na vumbi kwasababu upepo wa 'reverse' hutokea pembeni ya injini kwa kasi kubwa kuelekea mbele ya injini.
5> Reverse ni mfumo wa dharura ambao kiufundi haishauriwi kutumika hovyo kwasababu hewa yake inapitia sehemu za injini ambazo ni rahisi kupata uharibifu.
#Admin
Credit
#boldmethodView attachment 2620053
View: https://youtu.be/33pKd8pove0?si=vAk_XNrmhVKV0CrM
View: https://youtu.be/HEz7VjL6oPM?si=NzOxnQOECAsrYy7J